Na DOTTO NKAJA – Mahakama, Geita
Timu
ya Mpira wa Miguu ya Mahakama Kuu Kanda ya
Geita, hivi karibuni ilimenyana vikali na Timu ya Polisi
Mkoa wa Geita katika mchezo uliovutia hisia za mashabiki wengi, licha ya kupoteza kwa mabao 4-2.
Mchezo
huo wa
kirafiki ulifanyika
katika uwanja wa Shule ya Msingi Waja uliopo
eneo la
Magogo, mkoani Geita. Kuanzia
dakika za mwanzo, timu ya Mahakama ilionyesha kiwango cha juu cha mchezo kwa
kushambulia kwa kasi na nidhamu kubwa.
Kipindi cha kwanza
kilitawaliwa na Mahakama ambapo walifanikiwa kufunga magoli mawili safi
yaliyoamsha shangwe kwa mashabiki wao. Ushirikiano mzuri kati ya safu ya kiungo
na ushambuliaji uliwapa nafasi nyingi za kufunga, huku safu ya ulinzi
ikidhibiti vyema mashambulizi ya wapinzani.
Hata hivyo, kipindi cha
pili kilileta ushindani mpya baada ya Polisi Mkoa wa Geita kurejea uwanjani
wakiwa na ari na mikakati mipya. Walifanikiwa kusawazisha kwa kufunga magoli
mawili ya haraka na kurejesha matumaini yao. Baada ya kusawazisha, waliendelea
kushambulia kwa nguvu na kuongeza magoli mengine mawili, na kufanya jumla ya
magoli yao kufikia manne.
Mchezo huo ulimalizika
kwa Polisi Mkoa wa Geita kuibuka na ushindi wa magoli 4–2 dhidi ya Mahakama Kuu
Kanda ya Geita. Licha ya matokeo hayo, Mahakama Kuu Kanda ya Geita wanastahili
pongezi kwa kiwango bora walichoonesha hasa katika kipindi cha kwanza, wakidhihirisha
ushindani na umoja mkubwa.
Baada ya mashindano hayo,
watumishi na wadau wote walikutana kwa ajili ya kufungua mwaka. Waliohudhuria
ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Geita, Mhe. Kevin Mhina na Jaji wa
Mahakama Kuu Geita, Mhe. Giffin Mwakapeje.
Wengine ni Mawakili wa
Serikali, Mawakili wa Kujitegemea, Waendesha Mashtaka wa Mkoa wa Geita pamoja
na Polisi Mkoa wa Geita, wakiongozwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Safia
Jongo.
Naibu Msajili wa Mahakama
Kuu,
Kanda ya
Geita, Mhe. Fredrick Lukuna akitoa maelekezo
kwa wachezaji katika Timu ya Mahakama Kanda ya Geita.
Wachezaji
kutoka Polisi Geita wakijiandaa kuanza mashindano na Timu ya Mahakama
Geita.
Timu ya Mahakama Kanda ya
Geita ikiwa katika
picha ya pamoja kabla ya kuanza mchuano na Timu ya Polisi Geita.
Innocent Mwandoje wa Timu ya Mahakama akichuana na mchezaji kutoka Polisi Mkoa Geita.
Kiungo
mshambuliaji wa Timu ya Mahakama Abel
Lucas Bunzali akiwa kasi kuelekea lango la Police Geita.
Naibu Msajili Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Fredrick Lukuna akiwakilibisha wageni.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Kevin Mhina, akiwahimiza wadau wa Mahakama kuongeza umoja na mshikamano ili kuongeza kasi ya kutoa haki mapema ipasavyo.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Morogoro.






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni