- Viongozi wamiminika kwenye Banda la Mahakama
Na FAUSTINE
KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam
Viongozi mbalimbali wa
Mahakama na Serikali leo tarehe 8 Julai, 2025 wametembelea Banda la Mahakama ya
Tanzania kwenye Maonesho ya Kibiashara ya Kimataifa, Saba Saba, kujionea zoezi
la utoaji elimu kwa wananchi katika masuala mbalimbali ya kisheria.
Banda la Mahakama lipo katika
Maonesho hayo kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Temeke Jijini Dar es Salaam
likiwa limesheheni watalaam waliobobea kwenye sekta ya sheria, Teknolojia ya
Habari na Mawasiliano-TEHAMA, uboreshaji wa miundombinu ya majengo na maeneo
mengine mbalimbali muhimu.
Viongozi hao ni Naibu
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini na Majaji wanne wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, akiwemo Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania,
Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina.
Wengine ni Jaji Mfawidhi
wa Mahakama Kuu ya Tanzania, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Masoko na
Mitaji, Mhe. Dkt. Ntemi Kilekamajenga, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania, Divisheni ya Biashara, Mhe. Cyprian Mkeha na Jaji Mfawidhi wa Kituo
Jumushi cha Masuala ya Familia Temeke, Mhe. Mwanabaraka Mnyukwa.
Viongozi hao wamejionea
jinsi watalaam wa Mahakama na Wadau walivyojipanga kushiriki kwenye zoezi la
utoaji elimu kwenye masuala mbalimbali ya kisheria na kwa wakati tofauti wameelezea
kufurahishwa na maandalizi ambayo yamefanyika.
Jana tarehe 7 Julai,
2025, Viongozi wengine, wakiwemo Majaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe.
Winfrida Korosso, Mhe. Dkt. Mary Levira na Mhe. Gerson Mdemu walitembelea Banda
la Mahakama na kushuhudia jinsi wananchi kutoka viunga mbalimbali ya jiji la
Dar es Salaam wakinufaika na zoezi la utoaji elimu ya sheria.
Alikuwepo pia Katibu Mkuu
wa Wizara ya Katiba na Sheria, Mhe. Eliakim Maswi na Jaji wa Mahakama Kuu ya
Tanzania katika Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke, Mhe. Sharmillah
Sarwatt.
Banda la Mahakama ya
Tanzania linajumusha watalaam kutoka Kurugenzi ya Menejimenti ya Mashauri, Kurugenzi
ya Ujenzi na Usimamizi wa Majengo, Kurugenzi ya Mipango, Kurugenzi ya TEHAMA, Huduma
kwa Mteja na Kurugenzi ya Huduma za Mahakama, Ukaguzi, Mrejesho kwa Umma na
Maadili.
Wapo pia watalaam kutoka Kituo
Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke, Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya
Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Biashara, Mahakama
ya Rufani na Masjala Kuu ya Mahakama Kuu na Mahakama ya Watoto.
Kadhalika, Banda la
Mahakama limesheheni watalaam kutoka Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka, Idara ya
Huduma za Maktaba, Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi, Mahakama Kuu ya
Tanzania Divisheni ya Ardhi na Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi.
Kuna Wadau wanaoshirikiana
na Mahakama katika zoezi la utoaji elimu, wakiwemo Chama cha Majaji na Mahakimu
Tanzania-TAWJA, Tume ya Utumishi wa Mahakama, Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto-IJA
na Wakili Mkuu wa Serikali.
Wadau wengine ni Chama
cha Madalali wa Mahakama na Wasambaza Nyaraka Tanzania, Kituo cha Sheria na
Haki za Binadamu-LHRC na Chama cha Mawakili Tanganyika-TLS.
(Picha na INNOCENT KANSHA- Mahakama 77)

.jpeg)
.jpeg)








Hakuna maoni:
Chapisha Maoni