Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam.
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya ametoa
rai kwa Viongozi wa Tume ya Taifa ya kuandaa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 kuweka
misingi bora ya kuimarisha utawala bora na utawala wa sheria, kwa kuweka bayana
misingi ya Demokrasia, uhuru wa kujieleza na haki za binadamu ili iweze
kujikita zaidi katika kuhimiza kulinda haki za binadamu.
Akizungumza na Ujumbe wa Tume hiyo uliyomtembelea ofisini
kwake jijini Dar es Salaam tarehe 18 Juni, 2024, kwa lengo la kupata maoni
yake kuhusu maeneo yanayopaswa kuzingatiwa wakati wa kuandaa Dira ya Maendeleo
ya Taifa 2050, Mhe Nkya aliainisha kuwa wakati wa kuandaa Dira ya Taifa ya Maendeleo
itakayo ishishia mwaka 2050 inapaswa kuzingatia mambo mbalimbali yanayolenga
ustawi wa Taifa, ikiwa ni pamoja na kulenge kuimiarisha ulinzi wa mazingira
pamoja na namna bora ya kukabili na mabadiliko ya tabia nchi.
’’Nitoe rai kwa Viongozi wa Tume ya Mipango ya kuona
namna bora ya kupata na kupokea maoni
ya Mhimili wa Mahakama kwa pamoja na siyo ya mtumishi mmoja mmoja,” alisistiza
Msajili Mkuu.
Aidha, Mhe. Nkya aliongeza kuwa, Dira
pia ilenge kuwa na Tanzania yenye Uchumi imara na Siasa safi (Economic, Social and Political Stability).
Na pia, Dira ilenge kuimarisha Tanzania ya kidijitali kwa kusisistiza matumizi
ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA). Vilevile Dira ilenge kutengeneza
mazingira ya namna bora ya kutumia maliasili zinazopatikana nchini kwa masilahi
mapana ya nchi.
Vilevile,
Mhe. Nkya alisema, Diara iangazie Mikakati mbalimbali ya namna ya kufikia
maeneo ya kuwekeza zaidi kwenye rasilimali watu na kuwa na elimu bora zaidi, na
pia kuwa na mikakati bora ya kutumia maliasili za nchi mfano, kuvua au kuvuna
Samaki wanaopatikana kwenye kina kirefu cha bahari (deep sea) pamoja na namna ya kutumia rasilimali za asili kama
vile madini, gesi asili kwa maendeleo ya Taifa.
Msajili
Mkuu alihimiza Dira kuimarisha Sekta binafsi na kuwa na miundombinu
inayowezesha kuyafikia masoko kwa urahisi. Kuhakikisha mipango ya Mahakama ya
kuzogeza huduma ya utoaji wa haki kwa wananchi kwa wakati na kwa gharama nafuu
inatekelezwa.
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Tume ya Taifa ya kuandaa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 wakati walipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam kufanya mazungumzo naye tarehe 18 Juni, 2024, wa tatu kutoka kulia ni Msajili wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. George Hillary Herbert.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni