Na FRANCISCA SWAI – Mahakama, Musoma.
Chama cha Majaji na
Mahakimu (TMJA) Kanda ya Musoma, kilifanya mkutano wake tarehe 10 Aprili, 2026 kujadiliana
masuala ya kiutendaji na kuweka mikakati mbalimbali kuhakikisha suala la utoaji
wa haki linatekelezwa kama inavyokusudiwa bila mkwamo.
Akizungumza wakati wa
ufunguzi wa mkutano huo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya
Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya, alisistiza umuhimu wa Mahakimu kuhudhuria mikutano,
kwani ndio sehemu pekee wanapopata nafasi ya kukutana kwa wingi na kujadiliana
mambo mbalimbali.
“Kanda inavyo vikao
mbalimbali ikiwemo cha menejimenti, kusukuma mashauri, vikao vya Mawakili na Madalali
na vingine vingi, ila huko kote Mahakimu hawaingii kwa pamoja, isipokuwa katika
mkutano wa TMJA ambao ndio jukwaa pekee linalowawezesha Mahakimu kwa umoja wao kukukutana
na kujadili masuala yanayowahusu,” alisema Mhe. Mtulya.
Pamoja na kuwasisitiza
umuhimu wa mkutano huo, Jaji Mfawidhi aliwahimiza kuzingatia na kutekeleza
maelekezo ya Viongozi mbalimbali, ikiwemo kusimamia utekelezaji wa malengo
yanapangwa na Menejimenti ya Kanda, kwani yanasaidia kuboresha utendaji wa kazi
na kuwezesha Kanda ya Musoma kushika nafasi ya pili kitaifa kwa kasi nzuri ya
usikilizaji wa mashauri.
Aidha, katika mkutano huo
mada mbalimbali zilizijadiliwa ikiwa ni pamoja na ushughulikiwaji wa mashauri
ya mirathi. Wajumbe wa mkutano huo walikumbushana maelekezo mbalimbali ya Viongozi
kuhusu utekelezaji wa masuala ya mirathi, changamoto wanazokutana nazo katika
kushughulikia masuala hayo pamoja na namna bora ya kuyashughulikia.
Vilevile, wajumbe wa mkutano huo kwa pamoja walishiriki mafunzo yaliyotolewa kwa njia ya mtandao kuhusu matumizi ya Sheria ya Kiislam katika Mahakama za Mwanzo. Mafunzo hayo yaliyotolewa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania.
Mwenyekiti wa Chama cha
Majaji na Mahakimu (TMJA), Kanda ya Musoma, Mhe. Hadija Masala (aliyesimama)
akitoa neno la utangulizi wakati wa mkutano wa Chama cha Majaji na Mahakimu
(TMJA) Kanda ya Musoma.
Wajumbe wa mkutano wa
Chama cha Majaji na Mahakimu (TMJA) Kanda ya Musoma wakiwa wamesimama kwa ajili
ya kutoa heshima zao na kuwakumbuka watumishi wa Kanda ya Musoma waliofariki
katika kipindi cha mwaka 2025/2026, akiwemo aliyekuwa Hakimu Mahakama ya Mwanzo
Bunda Mjini, Mhe. Patrick Masenge na aliyekuwa Dereva Mahakama ya Wilaya Bunda,
Bw. Abriel Lazaro.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya (aliyesimama) akitoa neno
la ufunguzi wakati wa mkutano wa Chama cha Majaji na Mahakimu (TMJA) Kanda ya
Musoma.
Mjumbe wa mkutano wa
Chama cha Majaji na Mahakimu (TMJA) Kanda ya Musom,a Mhe. Oscar Lyimo
(aliyesimama) akiwasilisha mada kuhusu ushughulikiwaji wa mashauri ya mirathi
wakati wa mkutano huo.
Naibu Msajili wa Mahakama
Kuu Musoma, Mhe. Monica Ndyekobora (wa pili kushoto), akisisitiza jambo wakati
wa mkutano huo.
Wajumbe wa mkutano wa
Chama cha Majaji na Mahakimu (TMJA) Kanda ya Musoma, ambao pia ni Majaji wa
Mahakama Kuu Musoma, wakifurahia jambo wakati wa mkutano huo, wa kwanza kushoto
ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu
Mtulya, katikati ni Jaji wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Marline Komba na wa kwanza
kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Kamazima Kafanabo.
Wajumbe wa mkutano wa
Chama cha Majaji na Mahakimu (TMJA) Kanda ya Musoma wakifuatilia kwa makini
mafunzo yaliyotolewa kwa njia ya mtandao kuhusu matumizi ya Sheria ya Kiislam
katika Mahakama za Mwanzo.
Sehemu
ya
wajumbe wa mkutano wa Chama cha Majaji na Mahakimu (TMJA) Kanda ya Musoma
wakiwa katika picha ya pamoja.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni