Jumatatu, 3 Aprili 2017

JAJI KIONGOZI AWATAKA MAJAJI KUSHIRIKIANA KUWAHUDUMIA WANANCHI

Na Lydia Churi-MAHAKAMA, ARUSHA
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mheshimiwa Ferdinand Wambali amewataka Majaji wa Mahakama Kuu nchini kufanya kazi zao kwa kuzingatia Maadili, kuwa waaaminifu na kushirikiana katika kuwahudumia wananchi ili kesi zimalizike kwa haraka katika Mahakama mbalimbali.  

Akifungua Mafunzo ya siku tano ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tazania kuhusu Uongozi katika shughuli za Mahakama  leo jijini Arusha, Jaji Kiongozi amesema lengo la Mafunzo hayo ni kujadiliana kwa kina nini kifanyike ili kesi zimalizike mapema kwenye mahakama mbalimbali nchini.

Jaji  Wambali alisema katika mkutano huo, Majaji watapata nafasi ya kujifunza Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa Mahakama ya Tanzania wenye nguzo tatu ambazo ni pamoja na masuala ya Utawala, Upatikanaji wa haki kwa wakati na imani ya wananchi kwa Mahakama na ushirikishwaji wa wadau katika shughuli za Mahakama.

Katika Mafunzo hayo pia Majaji watajadiliana ni nini kilifanyika mwaka jana katika umalizwaji wa mashauri, changamoto zilizojitokeza na nini kifanyike ili kutatua changamoto zinazojitokeza katika utendaji wao wa kazi wa kila siku.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali akifungua Mafunzo ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania katika Ukumbi wa AICC leo jijini Arusha. Mahakama inaendesha Mafunzo kwa Majaji wote wa Tanzania ambapo Majaji wa Mahakama ya Rufani wanahudhuria Mafunzo kuhusu namna ya kutoa maamuzi ya Mahakama katika usikilizwaji wa kesi ngazi ya Rufaa, Majaji Wafawidhi kuhusu Usimamizi wa uendeshaji wa kesi wakati Majaji wengine wanapatiwa mafunzo kuhusu uongozi na usimamizi wa kuleta mabadiliko.

Naye Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mheshimiwa Katarina Revokati akizungumza na Waandishi wa habari kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo  alisema  yamegawanyika katika makundi matatu ambapo kundi la kwanza ni la Majaji wa Mahakama ya Rufani, kundi la pili ni la Majaji  Wafawidhi  wa Kanda 14 za Mahakama Kuu ya Tanzania na  kundi la Tatu ni la Majaji wengine wote.

Alisema Majai wa Mahakama ya Rufani watapatiwa Mafunzo kuhusu namna ya kutoa maamuzi ya Mahakama katika usikilizwaji wa kesi ngazi ya Rufaa, ambapo Majaji Wafawidhi watapewa mafunzo kuhusu Usimamizi wa uendeshaji wa kesi wakati Majaji wengine watapatiwa mafunzo kuhusu uongozi na usimamizi wa kuleta mabadiliko.

Mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Benki ya Dunia ni Utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Miaka mitano wa Mahakama ya Tanzania na yanalenga katika kuboresha utendaji kazi na kuleta mabadiliko ndani ya Mahakama.
 Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma (wa pili kushoto) akiwasili katika ukumbi wa AICC jijini Arusha kuhudhuria Mafunzo ya Majaji yaliyoanza leo. Kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali.
  Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma (wa pili kushoto) akiwasili katika ukumbi wa AICC jijini Arusha kuhudhuria Mafunzo ya Majaji yaliyoanza leo. Kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali. Kushoto kwa Jaji Mkuu ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Katarina Revokati na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Mahakama Bibi Wanyenda Kutta.
 Waheshimuiwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakiwa kwenye ufunguzi wa Mafunzo yao yaliyoanza leo jijini Arusha.
 Baadhi ya Waheshimuiwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakiwa kwenye ufunguzi wa Mafunzo yao yaliyoanza leo jijini Arusha. Katikati ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Noel Chocha, kushoto ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi Mhe. Aisha Nyerere na kulia ni Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Mwanza Mhe. Robert Makaramba.
 Waheshimuiwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakiwa kwenye ufunguzi wa Mafunzo yao yaliyoanza leo jijini Arusha.
 Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma(waliokaaa -katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani mara baada ya ufunguzi wa Mafunzo yao leo jijini Arusha.
 Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma(waliokaaa -katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Wasajili na wanasheria wa Mahakama Mahakama ya Rufani mara baada ya ufunguzi wa Mafunzo ya Majaji leo jijini Arusha.
  Waheshimuiwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wakiwa kwenye Mafunzo  yao yaliyoanza leo jijini Arusha.
 Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania mara baada ya kufungua Mafunzo yao leo katika Ukumbi wa AICC leo jijini Arusha.
 Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma(kushoto) akiwa katika katika Mafunzo ya siku tano ya Majaji wa Mahakama ya Rufani kuhusu namna ya kutoa Maamuzi ya Mahakama katika usikilizwaji wa kesi ngazi ya Rufaa, yaliyoanza leo jijini Arusha.
 Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani wakiwa kwenye Mafunzo ya siku tano ya Majaji wa Mahakama ya Rufani kuhusu namna ya kutoa Maamuzi ya Mahakama katika usikilizwaji wa kesi ngazi ya Rufaa, yaliyoanza leo jijini Arusha.
 Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Katarina Revokati akiwa kwenye Mafunzo ya Majaji wa Mahakama ya Rufani leo jijini Arusha.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni