Alhamisi, 3 Julai 2025

JAJI MFAWIDHI KANDA IRINGA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI MKOANI NJOMBE

  • Atembelea Mradi wa Mahakama ya Mwanzo Lupembe 

Na ABDALLAH SALUM, Mahakama-Njombe

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru ameanza ziara ya ukaguzi wa Mahakama za Mkoa wa Njombe kwa kufanya ukaguzi wa Mahakama za Wilaya za Njombe na Wanging’ombe.

Mbali na Mahakama hizo, Mhe. Ndunguru alifanya pia ziara ya ukaguzi katika Mahakama za Mwanzo Wilaya kuanzia tarehe 01 Julai, 2025.

Akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Mhe.Ndunguru alipokea taarifa ya jumla ya Mkoa mzima juu ya uendeshaji wa mashauri pamoja na miundombinu ya   Mahakama ya Mkoa Njombe pamoja na  Mahakama zake za Mwanzo za Wilaya zilizopo katika Mkoa huo.

Akiwasilisha taarifa ya Mahakama katika Mkoa huo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Mhe. Liadi Chamshama alidokeza kuhusu hali ya usikilizwaji wa mashauri kwa Mkoa mzima pamoja  na   utekelezaji wa Nguzo namba moja (1) katika Mpango Mkakati wa Mahakama utawala bora uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali.

Mhe. Chamshama alibainisha mafanikio mbalimbali  yaliyopatikana katika Mahakama hiyo kuwa, ni pamoja na   kufanya marekebisho ya jengo la Mahakama ya Mwanzo Makambako Mjini ambalo lilikuwa halipo kwenye hali nzuri licha ya ufinyu wa bajeti.

Aidha, baada ya kupokea taarifa hiyo Mhe.Ndunguru alijibu hoja mbalimbli zilizojitokeza kwenye taarifa hiyo huku akisisitiza kuhusu matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa kupandisha vielelezo na hati za mashtaka   kwenye mfumo wa usimamizi wa mashauri Mahakamani (e-CMS) hasa kwa mashauri yaliyokatiwa rufaa kwenda Mahakama ya juu.

Sanjari na hilo Mhe. Ndunguru alizungumza na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Wanging’ombe ambapo alitoa  pongezi juu ya utendaji kazi wa Mahakama hiyo.

Baada ya hapo Mhe,Ndunguru alienda kukagua jengo la Mahakama ya mwanzo Mdandu ambalo lipo chini ya Mahakama ya Wilaya Wangingombe ambalo kulikuwa na jengo la zamani la kihistoria lillilojengwa na wakoloni kwa shunghuli za kiMahakama

Mhe. Ndunguru alitembelea pia jengo la kale la Mahakama ya Mwanzo Mdandu lililojengwa na wakoloni na kujionea majalada ya zamani waliokuwa wanatumia machifu kuhamua mashauri pamoja na kuona makabati yaliyokuwa yanatunza majalada hayo.

Kadhalika Mhe.Ndunguru alifanya ukaguzi Mahakama ya Mwanzo Njombe Mjini ambapo alizungumza na watumishi na kusomewa taarifa fupi ya  Mahakama hiyo.

Kwa upande wake, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Mhe.Bernazitha Maziku alisisitiza juu ya kusajiLi mashauri yote yanayoingia mahakamani ili kuweka sawa kumbukumbu pamoja na  kuhuhisha mashauri hayo kwa kila Hakimu na kuwa rafiki na mifumo inayosimamia haki kwa wananchi  kwani bila kufanya hivyo ni ukiukwaji wa misingi ya haki.

Aidha, Jaji Mfawidhi huyo pamoja na alioambatana nao walifanya ukaguzi katika Mradi wa Ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Lupembe ambayo  inaendelea kujengwa na sasa umefikia asilimia 90 ili ukamilike. Hata hivyo, Mhe. Ndunguru amemtaka Mkandarasi wa Mradi huo kukamilisha ujenzi huo ndani ya muda aliomba kuongezewa.

Katika ziara hiyo Jaji Mfawidhi huyo ameambatana na  Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Mhe. Bernazitha Maziku, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Bi.Melea Mkogwa, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Njombe, Mhe. Liadi Chamshama pamoja na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru (aliyeketi mbele) akisikiliza taarifa iliyokuwa ikiwasilishwa kwake na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi  Njombe, Mhe. Liadi Chamshama (aliyeketi wa kwanza kulia kwa Jaji Mfawidhi). Wengine ni Viongozi walioambatana na Jaji Mfawidhi katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru (kushoto) akifuatilia taarifa ya Mashauri ya  Mahakama ya Wilaya Wangingombe iliyokuwa ikisomwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. James Muhoni (aliyesimama). Walioketi wa kwanza kulia ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Bi. Melea Mkongwa, anayefuata ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya  Iringa, Mhe. Bernazitha Maziku.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru  akipanda mti wa mparachichi nje ya jengo la Mahakama ya Wilaya Wangingombe. Waliosimama kutoka kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Bi.Melea Mkongwa, anayefuata ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya  Iringa, Mhe. Bernazitha Maziku anayefuata ni Afisa Utumishi wa Mahakama yaHakimu Mkazi Njombe, Bi. Happy Merere, anayefuata ni Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Bw. Richard Mbambe na wa kwanza kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Wanging’ombe, Mhe.James Muhoni kwa pamoja wakishuhudia zoezi la upandaji mti.

Viongozi kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Iringa akiwemo  Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo, Mhe. Dunstan Ndunguru (wa pili kushoto) wakizungumza na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Wanging’ombe walipotembelea Mahakama hiyo wakati wa ziara ya ukaguzi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama  ya Hakimu Mkazi wilaya Wanging’ombe. Wa pili kushoto ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Mhe. Bernazitha Maziku, wa kwanza kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Bi. Melea Mkongwa, wa kwanza kulia  ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi  Njombe, Mhe.Liadi Chamshama na wa pili kulia ni Afisa Utumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Bi.Happy Merere.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru akisoma moja ya jalada la zamani ndani ya jengo la zamani la Mahakama ya mwanzo mdandu ambalo ni la kihistoria lililojengwa na Wakoloni lililotumiwa na Machifu kuendeshea Mashauri mahakamani.

Makabati ya kihistoria ya kikoloni ambayo yalikuwa yanatumika kutunzia majalada ya mashauri yaliyokuwa yanaendeshwa na machifu enzi hizo. Makabati hayo yapo Mahakama ya zamani Mdandu.

Muonekano wa nje wa Jengo la kihistoria lililojengwa na wakoloni ambalo machifu walitumia kuamua mashauri kwenye jengo hilo la zamani la Mahakama ya Mwanzo Mdandu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania ,kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru akikagua maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Jengo  la Mahakama ya Mwanzo lupembe ambalo lipo kwenye hatua za mwisho za kukamilika kwake.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania ,kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru akiwa katika picha pamoja na Viongozi wa Mahakama ya Mkoa Njombe.

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dar es Salaam)

 

 

 

MAHAKAMA DODOMA YAZINDUA HAKI HEMA

Na ARAPHA RUSHEKE-Mahakama Kuu, Dodoma

Mahakama ya Tanzania, Kanda ya Dodoma imezindua hema maalum litakalokuwa linatumika kutoa huduma za haki kwenye mashauri ya familia, ikiwemo ndoa, mirathi na talaka katika ngazi ya Mahakama ya Mwanzo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt Juliana Masabo ndiye aliyekuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa hema hili-Hema Haki-uliohudhuriwa na mamia ya Wananchi wa Dodoma na viunga vyake.

Uzinduzi huo ulifanyika tarehe 1 Julai, 2025 katika eneo la Mahakama ya Mwanzo ya zamani ya Dodoma mjini  iliyopo relini, Dodoma.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi, Mhe. Dkt. Masabo alisema, “ni jambo lisilopingika kuwa, migogoro ya kifamilia imeongezeka kwa kasi, na imekuwa chanzo kikubwa cha maumivu ya kijamii.

‘..Kumekuwa na utitiri wa migogoro inayotokana na mizozo ya ndoa, talaka zisizo na mwongozo wa kisheria, malezi ya watoto, hasa pale wazazi wanapokuwa wametengana, usimamizi na ugawaji wa mali za marehemu (mirathi), pamoja na mambo mengine mengi yanayokosa utatuzi na hivyo kuleta migogoro ya kifamilia na kijamii,’alisema.

Alieleza kuwa hali hiyo imekuwa chanzo cha mateso kwa watu wengi na hivyo kuhitaji mfumo rahisi, wa haraka, na wa haki na Haki Hema ni mojawapo ya majibu ya changamoto hizo.

Jaji Mfawidhi alibainisha kuwa takwimu za mashauri katika Mahakama za Mwanzo zinaonesha kuwa kwa kipindi cha mwaka 2023 hadi Juni 2025, Mahakama tatu za Mwanzo zilizopo mjini Dodoma, yaani: Mahakama ya Mwanzo Dodoma Mjini (iliyopo katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki- maarufu IJC), Mahakama ya Mwanzo Makole na Mahakama ya Mwanzo Chamwino Mjini, zilipokea na kusajili jumla ya mashauri 12,267.

Kati ya hayo, Mashauri 4,627 (sawa na asilimia 37.7) ni ya ndoa, talaka na mirathi. Kwa Mahakama ya Mwanzo Makole pekee, mashauri ya familia (ndoa, talaka na mirathi) yaliyopokelewa katika kipindi hicho ni 1,492, sawa na asilimia 38.9 ya mashauri 3,838 yaliyopokelewa na kusajiliwa katika mahakama hii.

Akitoa salam za pongezi katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Mhe. Alhaji Jabir Shekimweri aliipongeza Mahakama kwa hatua nzuri iliyoichukua ya kusogeza huduma hiyo ya Mahakama karibu na Wananchi.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Majaji kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Wadau mbalimbali wa haki, watumishi wa Mahakama, Viongozi wa Dini, wawakilishi wa serikali na wananchi wa Dodoma ambao walipokea hatua hiyo kwa furaha na matumaini makubwa katika kuboresha haki nchini.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo akizungumza wakati wa halfla ya uzinduzi wa Huduma ya Mahakama katika Haki Hema.

Mkuu wa Wilaya wa Dodoma, Mhe Jabiri Shekimweri akitoa salamu wakati wa hafla hiyo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo-wa pili kutoka kulia-akikata utepe  wakati wa halfla ya uzinduzi  wa Huduma ya Mahakama katika Haki Hema.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo akisaini kitabu ch wageni mara baada ya uzinduzi huo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi.

Baadhi ya Viongozi wa Mahakama waliohudhuria uzinduzi huo.

Mwananchi akisema neno la shukrani kwa niaba ya Wananchi wenzake.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wananchi wa Dodoma kutoka sehemu mbalimbali  wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma

JAJI MKUU MASAJU ASISITIZA MAADILI, UADILIFU KWA MAWAKILI WAPYA

Na FAUSTINE KAPAMA na ARAPHA RUSHEKE-Mahakama, Dodoma

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju amewahimiza Mawakili wapya kuzingatia maadili, uadilifu na weledi na kuishi viapo vyao wanapotekeleza majukumu yao katika muktadha mzima wa utoaji haki kwa Wananchi.

Mhe. Masaju, ambaye ni Jaji Mkuu wa tisa wa Tanzania na Jaji Mkuu wa saba Mtanzania, ametoa wito huo leo tarehe 3 Julai, 2025 baada ya kuwapokea na kuwakubali waombaji 449 kuwa Mawakili wa Kujitegemea.

Hili ni tukio lake la kwanza tangu alipoapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu tarehe 15 Juni, 2025, kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

Katika hotuba yake kwenye sherehe hiyo ya uapisho iliyofanyika katika ukumbi wa Jiji Mtumba Jijini Dodoma, Jaji Mkuu Masaju amewakumbusha Mawakili kuwa taaluma ya sheria ni wito wa kuhudumia wananchi kwa haki na sio njia ya kujinufaisha binafsi.

“Mnaingia kwenye taaluma nyeti inayogusa maisha ya watu. Haki ya mwananchi inaweza kupatikana au kupotea kupitia maneno yenu. Kuweni waadilifu, wenye maadili, na waaminifu kwa wito wenu,” amesema Mhe. Masaju kwa msisitizo.

Ameongeza kuwa Mawakili wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kutetea haki za wanyonge, kulinda Katiba na kushiriki kikamilifu katika mageuzi ya kimahakama yanayoendelea nchini.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Viongozi wa Mahakama, wakiwemo Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu ya Tanzania. Alikuwepo pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wakili Mkuu wa Serikali.

Wengine ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, mwakilishi wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), familia za Mawakili wapya na Wadau mbalimbali wa sekta ya sheria.

Uapisho huo unaashiria mwanzo mpya kwa Mawakili hao katika kujenga jamii yenye haki, usawa na utawala bora wa sheria.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju-juu na chini-akizungumza kwenye sherehe ya kuwapokea na kuwakubali Mawakili wa Kujitegemea wapya 449 leo tarehe 3 Julai, 2025 jijini Dodoma.


Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya akitoa utambulisho wa wageni mbalimbali.
Sehemu ya Mawakili wapya-juu na chini-wakifuatilia kilichokuwa kinajiri wakati wa sherehe hiyo.


Viongozi mbalimbali, wakiwemo Majaji Wastaafu wakiwa kwenye sherehe hiyo. Picha chini ni wageni mbalimbali wakifuatilia kilichokuwa kinajiri.


Meza Kuu inayoongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju.

Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu ya Tanzania-juu na chini-wakiwa kwenye sherehe hizo.


Viongozi Waandamizi wa Mahakama ya Tanzania wakifuatilia kilichokuwa kinajiri wakati wa sherehe hiyo. Kushoto ni Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa na kulia ni Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Sundi Fimbo.


 

TUKIO LA KWANZA LA JAJI MKUU MASAJU

  • Awapokea, awakubali Mawakili wapya zaidi ya 400

Na FAUSTINE KAPAMA na ARAPHA RUSHEKE- Mahakama, Dodoma

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju leo tarehe 3 Julai, 2025 amewapokea na kuwakubali waombaji 449, wakiwemo wanaume 252 na wanawake 197, kuwa Mawakili wapya wa Kujitegeme.

Hili ni tukio kubwa la kwanza kwa Mhe. Masaju kulifanya tangu alipoapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 15 Juni, 2025, kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Sherehe hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Jiji uliopo Mtumba katika Ofisi za Serikali na kuhudhuriwa na Majaji wa Mahakama ya Rufani, Majaji wa Mahakama Kuu na Viongozi wengine wa Mahakama.

Walikuwepo pia Viongozi wengine, akiwemo Mwanasheria Mkuu wa Serikali, mwakilishi wa Mkurugenzi wa Mashtaka, Wakili Mkuu wa Serikali, Viongozi wa Baraza la Elimu ya Sheria na Wananchi kwa ujumla.

Miongoni mwa Mawakili hao wapya, 81 ni wale waliopata msamaha wa kutohudhuria Shule ya Sheria kwa Vitendo baada ya kuhudumu katika masuala ya kisheria kwa muda mrefu.

Yupo pia mmoja aliyefaulu mtihani wakuwa Wakili na wengine 367 waliofaulu katika Shule ya Sheria kwa Vitendo.

“Kwa mamlaka niliyopewa na Sheria ya Mawakili Sura 341, Kifungu cha 16 (4) natamka kwamba wale wote ambao majina yao yamesomwa hapa wamekubaliwa kuwa Mawakili na wameingizwa rasmi kwenye daftari la Mawakili kuanzia leo tarehe 3 Julai, 2025," amesikika Jaji Mkuu akitangaza mara baada ya kuwakubali na kuwapokea Mawakili hao wapya.

Tukio hilo la kuwapokea na kuwakubali Mawakili hao wapya 449 lililofanywa na Jaji Mkuu linafĂ nya idadi ya Mawakili nchini kuongezeka na kufikia 13,446.

Baada ya kukubaliwa, Jaji Mkuu wa Tanzania aliwatunuku vyeti vya uwakili na kusema, “Kwa mamlaka niliyopewa na Sheria ya Mawakili Sura 341, Kifungu cha 16 (4), nawatunuku vyeti vya uwakili nyinyi wote Mawakili mliopokelewa na kukubaliwa kuwa Mawakili.”

Kisha Mawakili hao walikula kiapo cha uadilifu mbele ya Msaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa. Msajili wa Mahakama Kuu amewakumbusha Mawakili ambao bado ni watumishi wa umma kujiepusha na vitendo vya kuanza kutetea wateja hadi hapo watakapofika ukomo katika utumishi wao.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju-kushoto-akiwapokea na kuwakubali Mawakili wapya 449 leo tarehe 3 Julai, 2025 jijini Dodoma. Picha chini, Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa akiratibu zoezi hilo.

Mawakili wapya-juu na picha mbili chini-wakitoa heshima kwa Jaji Mkuu baada ya kupokelewa na kukubaliwa kuwa Mawakili wa Kujitegemea.

Majaji wa Mahakama ya Rufani, wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mchecha Masaju-katikati- na Mahakama Kuu ya Tanzania-juu na chini-wakipokea heshima kutoka kwa Mawakili wapya.

Jopo linaloongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari-katikati likipokea heshima kutoka kwa Mawakili hao wapya. Picha chini ni Viongozi wa Baraza la Elimu ya Sheria.

Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa-kushoto-akiwaongoza Mawakili wapya kula kiapo.

Jumatano, 2 Julai 2025

MAONESHO YA 49 YA BIASHARA YA KIMATAIFA SABASABA 2025 MAHAKAMA IPO

 MAHAKAMA YA TANZANIA IKIWAHUDUMIA WADAU KATIKA MAONESHO YA 49 YA BIASHARA YA KIMATAIFA SABASABA 2025

Wananchi mbalimbali wanaendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.
Wananchi mbalimbali wanaendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.
Wananchi mbalimbali wanaendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.


Wananchi mbalimbali wanaendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.







Wananchi mbalimbali wanaendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.

Wananchi mbalimbali wanaendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.


Wananchi mbalimbali wanaendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.

(Picha na Innocent Kansha - Mahakama)