- Atembelea Mradi wa Mahakama ya Mwanzo Lupembe
Na ABDALLAH SALUM, Mahakama-Njombe
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru ameanza
ziara ya ukaguzi wa Mahakama za Mkoa wa Njombe kwa kufanya ukaguzi wa Mahakama za
Wilaya za Njombe na Wanging’ombe.
Mbali na Mahakama hizo, Mhe. Ndunguru alifanya
pia ziara ya ukaguzi katika Mahakama za Mwanzo Wilaya kuanzia tarehe 01 Julai, 2025.
Akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Mhe.Ndunguru
alipokea taarifa ya jumla ya Mkoa mzima juu ya uendeshaji wa mashauri pamoja na
miundombinu ya Mahakama ya Mkoa Njombe pamoja na Mahakama zake za Mwanzo za Wilaya zilizopo
katika Mkoa huo.
Akiwasilisha
taarifa ya Mahakama katika Mkoa huo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya
Hakimu Mkazi Njombe, Mhe. Liadi Chamshama alidokeza kuhusu hali ya usikilizwaji
wa mashauri kwa Mkoa mzima pamoja
na utekelezaji wa Nguzo namba moja (1) katika
Mpango Mkakati wa Mahakama utawala bora uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali.
Mhe.
Chamshama alibainisha mafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika Mahakama hiyo kuwa, ni pamoja
na kufanya marekebisho ya jengo la Mahakama ya Mwanzo
Makambako Mjini ambalo lilikuwa halipo kwenye hali nzuri licha ya ufinyu wa
bajeti.
Aidha,
baada ya kupokea taarifa hiyo Mhe.Ndunguru alijibu hoja mbalimbli
zilizojitokeza kwenye taarifa hiyo huku akisisitiza kuhusu matumizi ya Teknolojia
ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa kupandisha vielelezo na hati za
mashtaka kwenye mfumo wa usimamizi wa
mashauri Mahakamani (e-CMS) hasa kwa mashauri
yaliyokatiwa rufaa kwenda Mahakama ya juu.
Sanjari
na hilo Mhe. Ndunguru alizungumza na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Wanging’ombe
ambapo alitoa pongezi juu ya utendaji
kazi wa Mahakama hiyo.
Baada ya hapo Mhe,Ndunguru alienda kukagua jengo la Mahakama ya mwanzo Mdandu ambalo lipo chini ya Mahakama ya Wilaya Wangingombe ambalo kulikuwa na jengo la zamani la kihistoria lillilojengwa na wakoloni kwa shunghuli za kiMahakama
Mhe. Ndunguru
alitembelea pia jengo la kale la Mahakama ya Mwanzo Mdandu lililojengwa na
wakoloni na kujionea majalada ya zamani waliokuwa wanatumia machifu kuhamua
mashauri pamoja na kuona makabati yaliyokuwa yanatunza majalada hayo.
Kadhalika
Mhe.Ndunguru alifanya ukaguzi Mahakama ya Mwanzo Njombe Mjini ambapo alizungumza
na watumishi na kusomewa taarifa fupi ya
Mahakama hiyo.
Kwa upande wake, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Mhe.Bernazitha Maziku alisisitiza juu ya kusajiLi mashauri yote yanayoingia mahakamani ili kuweka sawa kumbukumbu pamoja na kuhuhisha mashauri hayo kwa kila Hakimu na kuwa rafiki na mifumo inayosimamia haki kwa wananchi kwani bila kufanya hivyo ni ukiukwaji wa misingi ya haki.
Aidha, Jaji Mfawidhi huyo pamoja na alioambatana nao walifanya ukaguzi katika Mradi wa Ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Lupembe ambayo inaendelea kujengwa na sasa umefikia asilimia 90 ili ukamilike. Hata hivyo, Mhe. Ndunguru amemtaka Mkandarasi wa Mradi huo kukamilisha ujenzi huo ndani ya muda aliomba kuongezewa.
Katika
ziara hiyo Jaji Mfawidhi huyo ameambatana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa,
Mhe. Bernazitha Maziku, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Bi.Melea
Mkogwa, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Njombe, Mhe. Liadi Chamshama pamoja na
Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru (aliyeketi mbele) akisikiliza taarifa iliyokuwa ikiwasilishwa kwake na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Mhe. Liadi Chamshama (aliyeketi wa kwanza kulia kwa Jaji Mfawidhi). Wengine ni Viongozi walioambatana na Jaji Mfawidhi katika ziara hiyo.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru (kushoto) akifuatilia taarifa ya Mashauri ya Mahakama ya Wilaya Wangingombe iliyokuwa ikisomwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. James Muhoni (aliyesimama). Walioketi wa kwanza kulia ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Bi. Melea Mkongwa, anayefuata ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Bernazitha Maziku.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru akipanda mti wa mparachichi nje ya jengo la Mahakama ya Wilaya Wangingombe. Waliosimama kutoka kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Bi.Melea Mkongwa, anayefuata ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Mhe. Bernazitha Maziku anayefuata ni Afisa Utumishi wa Mahakama yaHakimu Mkazi Njombe, Bi. Happy Merere, anayefuata ni Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Bw. Richard Mbambe na wa kwanza kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Wanging’ombe, Mhe.James Muhoni kwa pamoja wakishuhudia zoezi la upandaji mti.
Viongozi kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Iringa akiwemo Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo, Mhe. Dunstan Ndunguru (wa pili kushoto) wakizungumza na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Wanging’ombe walipotembelea Mahakama hiyo wakati wa ziara ya ukaguzi.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya Wanging’ombe. Wa pili kushoto ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Mhe. Bernazitha Maziku, wa kwanza kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Bi. Melea Mkongwa, wa kwanza kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Mhe.Liadi Chamshama na wa pili kulia ni Afisa Utumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Bi.Happy Merere.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru akisoma moja ya jalada la zamani ndani ya jengo la zamani la Mahakama ya mwanzo mdandu ambalo ni la kihistoria lililojengwa na Wakoloni lililotumiwa na Machifu kuendeshea Mashauri mahakamani.
Makabati ya kihistoria ya kikoloni ambayo yalikuwa yanatumika kutunzia majalada ya mashauri yaliyokuwa yanaendeshwa na machifu enzi hizo. Makabati hayo yapo Mahakama ya zamani Mdandu.
Muonekano wa nje wa Jengo la kihistoria lililojengwa na wakoloni ambalo machifu walitumia kuamua mashauri kwenye jengo hilo la zamani la Mahakama ya Mwanzo Mdandu.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania ,kanda ya Iringa, Mhe. Dunstan Ndunguru akiwa katika picha pamoja na Viongozi wa Mahakama ya Mkoa Njombe.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dar es Salaam)