Na Fredrick Mahava- Mahakama, Sumbawanga
Watumishi
wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya
Sumbawanga wamepata mafunzo juu ugonjwa
wa Mpox
ili kuwajengea uwezo na njia sahihi za kujikinga na maambukizi ya
ugonjwa huo baada ya Serikali kutoa taarifa juu ya uwepo wa ugongwa huo nchini.
Mafunzo
hayo yalifunguliwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya
Sumbawanga Mhe. Fredrick Manyanda jana tarehe 27 Machi, 2025 na yalifanyika
katika Ukumbi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga.
Akizungumza
wakati wa kufungua mafunzo hayo Mhe. Manyanda alisema kwa kuwa taarifa ya Serikali
kuhusu uwepo wa ugonjwa huo nchini haikusema wagonjwa wamegundulika sehemu gani
kama watumishi wa Mahakama shughuli za utoaji haki zimekuwa na mwingiliano
mkubwa sana na watu hivyo ni lazima tahadhali ichukuliwe na kuwaita wataalamu
wa afya waje kutoa elimu namna ya kujikinga na ugonjwa huo.
Aidha,
Mtaalum wa Afya kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dkt. Maingu
Matoke alitoa elimu kwa watumishi wa Mahakama kuhusu historia ya ugonjwa huo wa
mpox tangu umegunduliwa, jinsi ugonjwa huo unavyonea, dalili zake, matibabu
yake, watu gani wapo hatarini kuambukizwa, namna ya kujikinga na ugonjwa huo na
pia alitoa takwimu za ugonjwa huo kwa Mkoa wa Rukwa.
Naye,
Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba aliwaomba watumishi
kuendelea kuchukua tahadhari na kuzingatia elimu iliyotolewa na mtaalamu wa
afya hasa namna ya kujikinga na ugonjwa huo wa Mpox.
Wakati
wa mafunzo hayo, watumishi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga walipata wasaa
wa kuuliza maswali kwa mtaalamu wa afya na kupewa majibu ambayo yaliwasidia
kuelewa zaidi kuhusu ugonjwa wa Mpox.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Fredrick Manyanda
akifungua Mafunzo kwa Watumishi wa Mahakama Kanda hiyo kuhusu Ugonjwa wa Mpox.
Mtaalam
wa Afya kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa ya Rukwa Dkt. Maingu Matoke akitoa
Mafunzo kwa Watumishi wa Mahakama, Kanda ya Sumbawanga.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba akizungumza wakati wa
Mafunzo hayo.
(Habari Hii Imehariri na Innocent Kansha - Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni