Jumanne, 20 Mei 2025

TANZIA: MTUMISHI WA MAHAKAMA LINDI AFARIKI DUNIA

 


Marehemu Andrea Hamisi Mpochele enzi za uhai wake.

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Mtumishi wake Bw. Andrea Hamisi Mpochele aliyekuwa akihudumu kama Afisa Hesabu Msaidizi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na   Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu MKazi Lindi Bi. Quip Godfrey Mbeyela amesema marehemu alifikwa na umauti jana tarehe 19 Mei, 2025 katika hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Benedict Ndanda iliyopo Mkoa wa Mtwara alipokuwa amelezwa akipatiwa matibabu.

Taarifa ya Mtendaji huyo imeeleza kuwa msiba upo nyumbani kwa Marehemu kijiji cha Lisekese wilayani Masasi Mkoa wa Mtwara, Aidha mazishi yatafanyika siku ya tarehe 21 Mei, 2025 muda wa saa 7:00 Mchana.

Marehemu  Andrea Hamisi Mpochele aliajiriwa na Mahakama ya Tanzania  tarehe 2 Aprili  mwaka 1990 kama  Masjala  Msaidizi wa Mahakama III katika Mahakama ya Wilaya ya Lindi na baada ya hapo alijiendeleza  katika fani ya uhasibu  na ilipofika tarehe 01 Oktoba 2021  alibadilishwa kada na kuwa  Msaidizi wa  Hesabu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi  mpaka umauti ulipomfika.

Mahakama ya Tanzania inaungana na Ndugu, Jamaa na Marafiki kuomboleza msiba huo wa kuondokewa na mpendwa wetu.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana lihimidiwe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni