Na. Ally Ally Ramadhani – Mahakama, Katavi
Kiongozi wa Msafara wa Benki ya Dunia Bi. Christine Owuor, amepongeza kasi
ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Mkoa wa
Katavi.
Ameyasema hayo jana tarehe 03 Septemba, 2025 wakati wa ziara ya hiyo
iliyokuwa na lengo la kukagua mradi wa ujenzi jengo hilo la kisasa la Mahakama
ya Tanzania ya litakalo tumika kutoa haki kwa wananchi wa Mkoa huo.
Akitoa taarifa ya maendeleo ya mradi wa ujenzi wa jengo la hilo
mkoani hapo Mhandisi Victor Vedasto ambaye
ni mwakilishi wa Mkandarasi kampuni ya AZHAR Construction Co. Ltd, alisema
mradi huo umefikia asilimia 76.1 za utekelezaji wake na kuongeza kuwa tayari
kazi za umaliziaji wa jengo zinaendelea.
Aidha, Mhandisi huyo aliongeza kuwa, mradi huo unahusisha sehemu tatu
ambazo ni jengo Kuu, eneo la nje (uzio, mgahawa, chumba cha ulinzi) pamoja na
Manzari (Landscaping).
Vilevile, akieleza kuhusu mradi huo, Mhandisi na mtaalam wa manunuzi Bw. Fedrick
Nkya kutoka Benki ya Dunia alishauri kuzingatia uwepo wa mfumo wa mifereji ya
kupitisha maji nje ya jengo ili kuzuia maji kuingia eneo la jengo hasa kipindi
cha mvua za masika.
Naye, Mkuu wa Kitengo cha Maboresho ambaye pia ni Jaji wa Mahakama Kuu ya
Tanzania Mhe. Dkt. Angelo Rumisha akiwa kwenye ziara ya Benki ya Dunia ya
kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo la
Mahakama, alisema jengo hilo linalojengwa na Kampuni ya AZHAR Construction Co.
Ltd. linatarajiwa kukamilika Mwezi Novemba, 2025.
Jaji Rumisha aliongeza kuwa, ”tumepokea pongezi hili linatupa nguvu ya
kuendelea kuongeza kasi kwa kushirikiana na timu nzima ili ifikapo mwezi
Novemba 2025 mradi wetu uwe umekamilika kama tulivyo kubaliana na kampuni
inayojenga jengo letu la IJC – Katavi”.
Mkuu wa Kitengo cha Maboresho ya Mahakama aliongeza kuwa, nguzo ya pili ya
Mpango Mkakakati wa miaka mitano wa Mahakama ya Tanzania inasisitiza Utoaji
Haki kwa wakati. Mahakama ya Tanzania inatekeleza mpango huu kwa kuboresha
mazingira ya utoaji haki na kusogeza huduma za utoaji haki karibu zaidi na
wananchi kwa kujenga miundombinu bora na wezeshi itakayochangia ufanisi mzuri
wa utekelezaji wa nguzo hiyo.
Kiongozi wa msafara wa Benki ya Dunia Bi. Christine Owuor, (wa kwanza mbele) akikagua ujenzi wa IJC KATAVI.
Mhandisi Victor Vedasto,
akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya mradi wa ujenzi wa jengo la Kituo Jumuishi
cha Utoaji Haki Katavi kwa kiongozi wa msafara wa Benki ya Dunia Bi. Christine
Owuor.
Msanifu Linda
Kasilima, mshauri wa mradi kutoka kampuni ya Crystal Consultant akielezea
maendeleo ya Mradi wa ujenzi IJC KATAVI kwa timu ya msafara wa Benki ya Dunia.
Jaji wa Mahakama
Kuu ya Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maboresho Mhe. Dkt. Angelo Rumisha
akitoa maelezo kwa kiongozi wa Msafara wa Benki ya Dunia wakati wa ziara ya
ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa IJC Katavi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni