Alhamisi, 2 Mei 2019

JAJI MAKARAMBA ASTAAFU RASMI- AWASHUKURU VIONGOZI NA WATUMISHI WA MAHAKAMA KWA USHIRIKIANO


Na Rajabu Singana, Mahakama Kuu Mbeya

Aliyekuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Robert V. Makaramba amestaafu rasmi baada ya kufikisha umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria.

Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya ofisi kati yake na Jaji Mfawidhi mpya wa Kanda hiyo, Mhe. Dkt. John Utamwa iliyofanyika Aprili 30, 2019, Mhe. Jaji Mstaafu Makaramba  aliwashukuru viongozi na watumishi wote wa Kanda ya Mbeya kwa ushirikiano na upendo mkubwa waliompatia tangu alipowasili katika Kanda hiyo na kuwaomba kuhamishia nguvu hiyo kwa Jaji Mfawidhi mpya.

Naye Jaji Mfawidhi mpya, Mhe. Dkt. Utamwa aliwataka viongozi na watumishi wote kumpa ushirikiano kwa kuwa kila mtumishi ana mchango mkubwa katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku. 

“Ili kuifikia Dira ya Mahakama isemayo Haki Sawa kwa Wote na kwa Wakati  kila mtumishi ana nafasi yake bila kujali cheo au wadhifa alionao,” alisisitiza Mhe. Jaji Utamwa.

Hafla hiyo fupi ilihudhuriwa na Wahe. Majaji waliohamishimiwa katika Kanda hiyo ambao ni Mhe. Dkt. Adam J. Mambi, Mhe. Dunstan B. Ndunguru na Mhe. Dkt. Lilian M. Mongella. 
  Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambaye pia alikuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya akisoma taarifa ya makabidhiano ya Ofisi mbele ya viongozi mbalimbali wa Mahakama Kanda ya Mbeya.
 Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya, Mhe. Dkt. John Utamwa (kushoto) akisimkiliza Mhe. Jaji Mstaafu Makaramba alipokuwa akiwasilisha taarifa ya makabidhiano ya ofisi.

Sehemu ya Watumishi wa Mahakama Kanda ya Mbeya wakifuatilia kwa makini taarifa kutoka kwa Jaji Mfawidhi Mstaafu (hayupo pichani).

Jaji Mstaafu, Mhe. Robert V. Makaramba  (kulia) akikabidhi shada la ua kwa Jaji Mfawidhi mpya Mhe. Dkt. John H. K. Utamwa kama ishara ya ukaribisho katika Ofisi ya Jaji Mfawidhi.
 
 








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni