Jumanne, 10 Desemba 2019

MTENDAJI MKUU-MAHAKAMA AFANYA ZIARA YA KWANZA KIKAZI MANYARA


  Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Bw. Mathias Kabunduguru (mwenye shati la bluu bahari) akionyeshwa chumba cha mahabusu ndani ya jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara alipofanya ukaguzi wa jengo hilo mwishoni mwa wiki iliyopita. Hii ni ziara yake ya kwanza kikazi baada ya kuteuliwa na Mhe. Rais hivi karibuni. Aidha, Mtendaji Mkuu huyo amepongeza hatua ambazo jengo hilo limefikiwa na kusisitiza kuwa limalizike haraka kwa ajili ya kuruhusu shughuli za Mahakama ziendelee ipasavyo. 

   Mtendaji Mkuu wa Mahakama akiendelea na ukaguzi wa jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara. Wengine ni baadhi ya Maafisa wa Mahakama alioambatana nao katika ziara yake.

Sehemu ya mbele ya jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara.
      Mtendaji Mkuu wa Mahakama akiendelea na ukaguzi wa jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara.

   Mtendaji wa Mahakama ya Mkoa wa Manyara, Bw. Jacob Swalle akimsomea Mtendaji Mkuu wa Mahakama (kulia) historia ya jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara. Hata hivyo, Mtendaji Mkuu amewasisitiza Viongozi wa Mahakama katika mkoa huo kushughulikia upatikanaji wa hati za majengo na viwanja vya Mahakama (kwa maeneo ambayo hayajapata) ili kuweza kuwa na huduma za mahakama katika maeneo ambayo hayana huduma hizo katika Mkoa huo.

(Picha na Christopher Msagati, Mahakama-Manyara)



 



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni