Jumapili, 16 Februari 2020

JAJI WA MAHAKAMA KUU ZANZABAR MHE. SEPETU AFARIKI DUNIA LEO


Jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar Mhe. Mkusa Isaac Sepetu amefariki Dunia leo Asubuhi, Zanzibar.

Pichani ni Jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar Marehemu Mkusa Isaac Sepetu. 

HISTORIA YA MAREHEMU MKUSA ISAAC SEPETU
(JAJI WA MAHAKAMA KUU ZANZIBAR)
KUZALIWA
Marehemu Jaji Mkusa Sepetu alizaliwa 12/3/1974 Zanzibar
ELIMU
Alipata Elimu yake ya Msingi na Sekondari nchini Russia mwaka 1982-1992
Alisoma Shahada ya kwanza ya Sheria (LLB) mwaka 1993-1997 nchini Russia
AJIRA
Mwaka 2001-2002 – Marehemu aliajiriwa kama Afisa Sheria wa wizara ya Fedha na Uchumi Zanzibar.
Mwaka 2002-2004 - Aliteuliwa kuwa Hakimu wa Mkoa katika Mahakama ya Mkoa wa Vuga.
Mwaka 2004-2006- Aliteuliwa kuwa Hakimu wa Mkoa Dhamana katika Mahakama ya Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Mwaka 2006-2009- Aliendelea kuwa Hakimu wa Mkoa Dhamana wa Mahakama ya Mkoa wa Kusini Unguja (Mwera)
Mwaka 2009-2010 Aliendelea kuwa Hakimu Dhamana wa Mahakama ya Mkoa wa Vuga
2010-2020 Aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar.

NYADHIFA NYINGINE ZA UTEUZI

2014-2020 Aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Zanzibar
10/12/2014- 20/1/2015 Aliteuliwa kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Zanzibar
1/12/2016 -16/1/2017 Aliteuliwa kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Zanzibar

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni