Jumatano, 21 Oktoba 2020

JAJI KIONGOZI AKAGUA SHUGHULI ZA MAHAKAMA WILAYANI UKEREWE

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi ameendelea na ziara yake katika Kanda ya Mwanza ambapo jana alikagua shughuli za Mahakama katika wilaya ya Ukerewe. Pichani akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na watumishi wa Mahakama ya wilaya ya Ukerewe. Kushoto ni Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Mwanza Mhe. Sam Rumanyika. 
Watumishi wa Mahakama ya wilaya ya Ukerewe wakimsikiliza Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi alipokuwa akizungumza nao. Amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa uadilifu na kuw na utayari wa kujiendeleza kitaaluma. Jaji Kiongozi pia amesisitiza umuhimu wa matumizi ya Tehama katika kazi za Mahakama. 
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi  akizungumza alipokuwa ofisini kwa Mkuu wa wilaya ya Ukerewe, Cornel Magembe alipomtembelea jana. 
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa wilaya ya Ukerewe, Cornel Magembe (wa pili kushoto) pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo na Watumishi wa Mahakama.
Mkuu wa wilaya ya Ukerewe, Cornel Magembe akimsikiliza Jaji Kiongozi alipomtembelea ofisini kwake jana.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya wilaya ya Ukerewe. Wa tatu kushoto wliokaa ni Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Mwanza Mhe. Sam Rumanyika na wengine waliokaa ni Viongozi wa Mahakama wakiwemo Naibu Wasajili, Mtendaji na Mahakimu.
Jengo la Mahakama ya wilaya ya Bunda likiendelea kujengwa. jengo hili linatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Disemba mwaka huu.Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akisaliamiana na Spika Mstaafu wa Bunge la Tanzania Mhe. Pius Msekwa alipofika nyumbani kwake Nansio Ukerewe kumsalimia.Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi na Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Mwanza Mhe. Sam Rumanyika wakiwa katika picha ya pamoja na Spika Mstaafu wa Bunge la Tanzania Mhe. Pius Msekwa walipofika nyumbani kwake Nansio Ukerewe kumsalimia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni