Ijumaa, 8 Januari 2021

KAMATI YA NIDHAMU YA MAAFISA WA MAHAKAMA YAKUTANA

Na Mwandishi Wetu- Mahakama

Kamati ya nidhamu ya Maafisa wa Mahakama imekutana na kuwaachia huru  Maafisa watatu wa Mahakama waliofikishwa mbele ya kamati hiyo wakituhumiwa kwa makosa mbalimbali ya ukiukwaji wa maadili kazini.

Kwa mujibu wa Katibu wa kamati hiyo ambaye pia ni Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Sharmilla Sarwatt, kamati hiyo ilikutana jijini Dar es salaam kuanzia Desemba 12 hadi 14, 2020 ili kusikiliza mashauri 13 yaliyowasilishwa.

Aidha, kati ya mashauri 13 yalisikilizwa kwenye kikao cha kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi, ni mashauri matatu 3 tu ndiyo yaliyomalizika na kutolewa uamuzi ambapo washitakiwa wote watatu hawakutiwa hatiani

Mashauri mengine 10 bado yanaendelea kusikilizwa na kamati hiyo.

Kwa mujibu wa Sheria ya Uendeshaji wa Mahakama namba 4 ya mwaka 2011, Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania ndiye Mwenyekiti wa kamati hiyo na Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania ni Katibu wa kamati hiyo.




 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni