Na Mohamed Kimungu, Mahakama-Mbeya
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Rose Ebrahim amewaasa
Mahakimu wa Mkoa huo kuzingatia mambo manne katika utekelezaji wa majukumu yao
kwa kufanya kazi kwa pamoja (team work), bidii katika utendaji kazi, nidhamu, weledi
na kuwataka kulinda na kudumisha uhuru wa Mahakama.
Akizungumza hivi karibuni wakati akifungua Kongamano la Chama cha Majaji na Mahakimu (JMAT) tawi la Mbeya, Mhe. Rose aliwataka pia Maafisa hao wa Mahakama kuzingatia kanuni za maadili kwa maafisa wa Mahakama “Code of Conduct for Judicial Officers of Tanzania’ ili wasiende kinyume na miongozo ya utendaji kazi ya Mhimili huo.
“Ni vyema pia muendelee kujielimisha kwa kusoma mabadiliko ya Sheria mbalimbali pamoja na kusoma uamuzi wa Mahakama za juu, (Courts of records)” alisema Mhe. Rose.
Katika
Kongamano hilo, lililobeba maudhui ya ‘timu moja, Lengo moja- pamoja kufikia
mafanikio’ Mada mbalimbali zilitolewa kwa Wanachama lengo likiwa kuwajengea
uwezo na kukumbashana masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha jukumu la
utoaji haki.
Aidha;
katika kongamano hilo lilihitimishwa kwa Chama hicho kufanya uchaguzi Mkuu na wajumbe
mbali mbali waliteuliwa ambapo Mhe.
Andrew Scout aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa JMAT Mbeya, Mhe Ayubu Shellimo
aliteuliwa kuwa Katibu, Mhe Angela Byera aliteuliwa kuwa Muweka Hazina na Mhe Tedy Mlimba kuwa Mwakilishi wa JMAT Taifa.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Rose Ebrahim akifungua Kongamano la Chama cha Majaji na Mahakimu tawi Mbeya. Kongamano hilo lilifanyika katika katika ukumbi wa 'Matema beach' jijini Mbeya.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni