Na Mwinga Mpoli – Mahakama, Mbeya
Jumla
ya mashauri 24 ya mauaji yanatarajiwa kusikilizwa mfululizo na kuyatolewa uamuzi
katika kipindi cha mwezi mmoja cha kusikiliza mashauri hayo yatakayoendeshwa na
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya na kufanya jumla ya vikao hiyo kufikia
5 kwa mwaka 2024.
Akitoa taarifa ya ufunguzi wa vikao hivyo hivi karibuni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, alisema kuwa, vikao viwili vitafanyika ndani ya Wilaya ya Mbeya na kikao kimoja kitafanyikia wilayani Rungwe ambapo jumla ya mashauri 24 ya mauaji yanatarajiwa kushughulikiwa katika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia tarehe 20 Mei, 2024.
Mhe.
Temu ameongeza kuwa, mashauri 10 yanatoka Mkoa wa Songwe, mashauri 14 yanatoka
Mkoa wa Mbeya. Aidha amewaambia wadau kwamba matarajio ya Mahakama ni
kuhakikisha mashauri hayo yanakamilika kwa asilimia 100 kama yalivyopangwa.
“Mashauri
yote yamepangwa kwa kuzingatia umri wake toka kusajiliwa mahakamani kwa
kitaalamu tumetumia mfumo wa ‘FIFO’ na kesi hizo zinatoka katika Mikoa ya Songwe
na Mbeya kwa kuwa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya inaundwa na Mikoa ya Mbeya na
Songwe. Hivyo katika mashauri yaliyopangwa kusikilizwa, mashauri 10 yanatoka
Mkoa wa Songwe na mashauri 14 yanatoka mkoa wa Mbeya,” alisisitiza Mhe. Temu.
Mhe. Temu amebainisha kuwa mashauri tajwa hayahusishi mashauri yanayosubiri washtakiwa kusomewa kwa mara ya kwanza (plea taking).
Kwa
upande wake, Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Dunstan
Ndunguru amewashukuru wadau kwa ushirikiano waliouonesha na kuomba kuendeleza
ushirikiano huo hasa katika ushiriki wa vikao kama hivyo.
“Vikao
kama hivi vimekuwa vikifanikiwa kwa kiasi kikubwa na hutumika katika kujenga
ushirikiano mzuri na utatuzi wa mashauri ya mlundikano na yale yenye viashiria
vya kuwa mlundikano. Ndiyo vikao pekee ambavyo vinaleta ufanisi mkubwa katika
umalizaji wa mashauri yanayokua yamepangwa kusikilizwa kwa mfululizo
(sessions),” alisema Jaji Mfawidhi
Aidha,
Mhe. Ndunguru amewapongeza wadau kwa ushirikiano ambayo wamekuwa wakiuonesha
katika kufanikisha usikilizwaji wa mashauri na kuendelea kuwasisitiza Mawakili
na Wadau kutumia utaalamu wao kwa kusoma majalada vizuri na kuongea na wateja
wao mapema angalau wiki moja kabla ya kuanza kusikilizwa kwa mashauri yao.
Vilevile amewasisitiza Magereza kuhakikisha Mahabusu ambao wako mbali kuwa
wanafikishwa mapema angalau wiki moja kabla ya kikao kuanza ili waweze kupata
muda wa kutosha kuzungumza na Mawakili wao.
Sambamba
na hayo, Wadau kwa pamoja wamehaidi kuendelea kutoa ushirikiano mkubwa na
kusema kwamba wao wamejipanga vizuri hasa Ofisi ya Mashtaka katika kuhakikisha
mashahidi wao wanapatikana kwa wakati wanaokua wameitwa mahakamani.
Wameipongeza Mahakama kwa kuandaa vikao kama hivyo vyenye kuleta tija katika
dhana nzima ya utoaji haki kwa wakati.
Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Dunstan Ndunguru (katikati) akieleza jambo wakati wa kikao kazi na wadau cha maandalizi ya kusikiliza mashauri ya mauaji. Wengine ni
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni