Jumatatu, 2 Septemba 2024

BALOZI MNDOLWA ATOA ELIMU YA ITIFAKI KWA MAJAJI WA MAHAKAMA YA RUFANI

Na Innocent Kansha- Mahakama

Mkuu wa Idara ya Itifaki Kitaifa Mhe. Balozi Yusuph Mndolwa amesema kuwa itifaki ni suala mtambuka la utaratibu unaokubalika wa kufanya mambo kwa heshima na tabia njema jambo ambalo linapaswa kuanzia ngazi ya familia, jamii ya watu wastarabu, taasisi, mihimili na hata kitaifa katika misingi inayoheshimisha utu na hadhi za viongozi.

Akizungumza katika kikao kazi cha kujadili masuala ya itifaki kilichowahusisha Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania kilichofanyika jijini Dar es salaam leo tarehe 02 Septemba, 2024 Balozi Mndolwa amesema kuwa kuna baadhi ya taratibu zimekuwa zinafuatwa na zingine kufuatwa katika misingi isiyo ya ukamilifu wa kiitifaki.

Mhe. Balozi Mndolwa amewakumbusha Majaji hao juu ya mambo kadhaa ya kiitifaki kwa kuzingatia utaratibu unaokubalika bila kumkwaza aliyealikwa na aliyealika mambo hayo ni pamoja na mavazi ya staha, ukaaji na mpangilio wa nani aanze na nani afuate, kuzingatia vyeo, tabia za mezani pamoja na mawasiliano mbalimbali, mambo hayo ndiyo msingi wa tabia njema za kiitifaki.

“Mavazi ya staha na rangi kwa watumishi wa umma ni vitu vinavyotambulisha watu wa fani fulani kama Majaji na watu wa kanda mbalimbali za watumishi wa umma, mfano kwa upande wa wanaume tuepuke sana kuvaa tai nyekundu kwani rangi nyekundu inamaanisha mamlaka,” amesema Mhe. Balozi.

Mhe. Balozi Mndolwa akagusia itifaki ya ukaaji kwa Waheshimiwa Majaji na Watendaji wa Mahakama wakati wamealikwa kwenye hafla na dhifa mbalimbali za mhimili na zingine za kitaifa na serikali. Amesema kwamba eneo hilo lina

changamoto sana na linahitaji kufanyiwa mkakati mahususi wa kuondoa mtanziko huo. Njia moja wapo ni sekretarieti inayoandaa dhifa kushirikiana na viongozi wa mihimili mingine kushauriana namna ya ukaaji wa kufuata hadhi za wageni walioalikwa.

“Changamoto nyingine ya kiitifaki ni namna ya ukaaji kwenye picha, kuna picha nyingine ukiiangalia tu inakueleza kuwa hapa mpangilio hakufuata itifaki. Picha ni historia hivyo ni lazima itifaki kuzingatiwa ili kulinda historia,” ameongeza Mhe. Mndolwa.

Mhe. Balozi Mndolwa akizungumzia matumizi ya simu za mikononi, ametoa rai kuwa wakati wote mgeni anapaswa kuzingatia mahali alipo na watu aliokuwa nao. Mtu anapokuwa kwenye hafla au dhifa ya aina yoyote ile itifaki inashauri kuweka simu kwenye sauti ndogo ama mtetemo ili kuondoa usumbufu.

Mhe, Balozi Mndolwa akizungumzia eneo la utoaji wa mialiko ya dhifa mbalimbali za serikali na kitaifa amesema kumekuwa na changamoto ya watu kutothibitisha ushiriki wao kwa maandishi ili kuwawezesha waandaaji kuratibu shughuli husika kwa ufasha kuanzia mapokezi, ukaaji kwa kuzingatia uthibitisho wa wageni husika. Itifaki inashauri kuwa mwalikwa anapaswa kutoa uthibitisho wa kushiriki katika muda uliokusudiwa ili kurahisisha shughuli nzima ya itifaki.

Kuhusu matumizi ya pasi za kusafiria zenye hadhi ya kibalozi, Balozi Mndolwa amesema Majaji na watendaji wa Mahakama na wenza wao wanaruhusiwa kisheria kutumia pasi hizo za kusafiria. Lakini wakati mwingine wahusika wamekuwa wamekuwa wakitumia hadhi hiyo kinyume na utaratibu

Kwa upande wake Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Augustine Gherabast Mwarija akifungua kikao kazi hicho amewataka Majaji hao kusikiliza Balozi huyo kwa umakini ili waweze kutoa michango mizuri hasa ya kuuliza maswali kwenye maeneo mbalimbali yanayotokana na changamoto za itifaki.

Mkuu wa Itifaki na Adabu Kitaifa Mhe. Balozi Yusuph Mndolwa (aliyenyoosha mkono) akifafanua jambo wakati wa kikao kazi cha kujadili masuala ya itifaki na ustarabu kilichowahusisha Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania kilichofanyika Mahakama ya Rufani jijini Dar es salaam leo tarehe 02 Septemba, 2024

Mkuu wa Itifaki na Adabu Kitaifa Mhe. Balozi Yusuph Mndolwa (aliyenyoosha mikono) akifafanua jambo wakati wa kikao kazi cha kujadili masuala ya itifaki na ustarabu kilichowahusisha Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania kilichofanyika Mahakama ya Rufani jijini Dar es salaam leo tarehe 02 Septemba, 2024

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania ambaye pia ni mlezi wa Majaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Augustine Gherabast Mwarija (katikati) akifungua kikao kazi hicho kilichowahusisha Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania.

Sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania walioshiriki kikao kazi hicho wakisikiliza kwa umakini hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa kikao hicho.

Sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania walioshiriki kikao kazi hicho wakisikiliza kwa umakini hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa kikao hicho.

Sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania walioshiriki kikao kazi hicho wakifuatilia kwa umakini hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa kikao hicho.


Sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania walioshiriki kikao kazi hicho wakifuatilia kwa umakini hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa kikao hicho.


Mkuu wa Itifaki na Adabu Kitaifa Mhe. Balozi Yusuph Mndolwa (aliyenyoosha mikono) akifafanua jambo wakati wa kikao kazi cha kujadili masuala ya itifaki na ustarabu kilichowahusisha Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania kilichofanyika Mahakama ya Rufani jijini Dar es salaam leo tarehe 02 Septemba, 2024

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Rehema Kerefu akichangia hoja wakati wa kikao hicho.
 
Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Lugano Samson Mwandambo akichangia hoja wakati wa kikao hicho.
 

Sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania walioshiriki kikao kazi hicho wakifuatilia kwa umakini hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa kikao hicho.

Picha na Innocent Kansha- Mahakama

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni