Na Arapha Rusheke –Mahakama, Dodoma
Chama
cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) Dodoma na Morogoro wamepongeza
Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Latifa Alhinai Mansoor baada ya
kuapishwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia
Suluhu Hassan katika hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ya Chamwino Mkoani
Dodoma leo tarehe 22 Januari, 2025.
Mhe
Jaji Mansoor aliteuliwa tarehe 10 Januari, 2025 na Mhe. Rais Samia kuwa Jaji wa
Mahakama hiyo. Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mansoor alikuwa Jaji Mfawidhi, Kituo
Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC), Morogoro.
Akizungumza
na wanachama wa TAWJA kwa Mkoa wa Dodoma na Morogoro Mhe. Jaji Mansoor amewashukuru wanachama hao kwa upendo na
ushirikiano wao waliouonesha kwake.
“Namshukuru
Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema kwa neema yake ya kunifanya nimetambuliwa na
kunifanya niwe hivi nilivyo leo, sijui tamaduni za kule lakini ninaahidi nitafanya
kazi kwa bidii kubwa ninamuomba Mwenyezi Mungu anipe afya ya kutosha ili niweze
kutimiza majukumu yangu ipasavyo hasa kusimamia ukuaji, uboreshaji na utendaji
kazi wa Mahakimu,” amesema Mhe. Jaji Mansoor.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo
fupi Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana
Masabo amempongeza Mhe. Mansoor na kumtakia kila lakheri katika majukumu yake,
na kumuomba apokee zawadi ambayo ameandaliwa na wanachama wa TAWJA wa Mkoa wa
Dodoma.
Akizungumza kwa niaba ya TAWJA
Morogoro pamoja na watumishi wa Morogoro Naibu Msajili wa Kituo Jumuishi cha
Utoaji Haki (IJC), Morogoro Mhe. Susan Kihawa amempongeza Mhe. Jaji Mansoor kwa
kuteuliwa kushika nafasi hiyo na kuahidi wataendeleza yale mazuri ambayo
amewaachia.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na baadhi ya
watumishi kutoka Dodoma na Morogoro.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzani,a
Mhe.Latifa Alhinai Mansoor (katikati ) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi
ya wanachama wa TAWJA wakati ya hafla ya kumpongeza iliyofanywa na
wanachama wa TAWJA Mkoa wa Dodoma na Morogoro iliyofanyika Kituo Jumuishi cha
Utoaji Haki(IJC), Dodoma.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Latifa Alhinai Mansoor (aliyeshika ua) akiwasili katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC), Dodoma mara baada ya uapisho.
Jaji wa
Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Latifa Alhinai Mansoor (wa kwanza kushoto) akipokea
zawadi kutoka kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma.
Mhe. Dkt.Juliana Masabo wakati ya hafla ya kumpongeza iliyofanywa na wanachama
wa TAWJA Dodoma na Morogoro iliyofanyika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC)
Dodoma.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe.Latifa Alhinai Mansoor (aliyevalia Joho) akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Msajili wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki(IJC) Morogoro Mhe.Susan Kihawa wakati ya hafla ya kumpongeza iliyofanywa na wanachama wa TAWJA Dodoma na Morogoro iliyofanyika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki(IJC), Dodoma.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni