Alhamisi, 27 Februari 2025

JOPO LA MAJAJI WA RUFANI MBEYA LASIKILIZA, KUAMUA MASHAURI ASILIMIA 96

Na Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Winifrida B. Korosso ameongoza kikao cha tathmini ya vikao vya vya Mahakama ya Rufani Tanzania Mbeya vilivyoanza mnamo wa tarehe 10 February, 2025 hadi tarehe 28 February, 2025 ikiwa mashauri 25 kati ya 26 yamesikilizwa na kuamuriwa na shauri 1 limehairishwa na kufika malengo kwa asilimia 96 ya mashauri yaliyopangwa.

Aidha, Mhe. Korosso ambaye alikuwa Mwenyekiti wa jopo la Majaji wa Mahakama ya Rufani waliosikiliza wa mashauri hayo kwa kushirikiana na Majaji wengine wa Mahakama hiyo ambao ni Mhe. Panterine M. Kente na Mhe. Leila E. Mgonya kwa pamoja walisikiliza mashauri ya Jinai 16 na Mashauri ya Madai 10 na mashauri 12 yametolewa hukumu na mashauri 13 yatatolewa uamuzi tarehe 28 February, 2025.

Akieleza sababu moja wapo ya mafanikio hayo, Mhe. Korosso aliwashukuru Jeshi la Magereza jijini Mbeya kwa kuwawaisha wafungwa mapema Mahakamani na Mawakili kwa ujumla kufika mapema kumewarahisishia wao kufanya kazi kwa urahisi na kumaliza mashauri mapema.

“Niwapongeze Jeshi la Magereza, Mawakilia wa Serikali na wa kujitegemea, Ofisi ya Waendesha Mashtaka na Wadawaa wengine kwa kufika kwao mapema Mahakamani kwa wakati wote wa usikilizaji wa mashauri hayo, naweza kusema mafanikio haya yamechangiwa nanyi kwa kujitoa kwa wakati wote,” alisema Mhe. Korosso

Wakati huohuo, Jopo la Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Kanda ya Mbeya walieleza changamoto zilizojitokea kwa upande wa Magereza na kwa Mawakili katika suala la uchelewashaji wa kuleta sababu za nyongeza katika mashauri ya Rufani pamoja na vitabu vya Rufani kuwa na sababu nyingi za Rufaa zisizokua na mashiko na kupelekea baadhi ya mashauri kuchelewa kufanyiwa maamuzi, vielelezo kutosamana na hukumu zinazotolewa hasa kwa Mahakama za Mwanzo.

Kwa upande wake Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa kwa niaba ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya aliwapongeza Majaji wa Mahakama ya Rufani kwa mafanikio waliyopata kwa kipindi chote cha usikilizaji wa mashauri hayo yaliyokuwa yamepangwa kusikilizwa.

“Tuna ahidi kwenu kwamba tutaendelea kutembelea Gereza la Ruanda lililopo Mbeya kutoa elimu ya sheria ili wafungwa waweze kuendelee kuboresha sababu zao za Rufaa wanazoleta Mahakamani,” alisema Jaji Nongwa.

Naye, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu na  Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bi. Mavis Miti pamoja na Mahakimu wa Mahakama Mkoa wa Mbeya, Jeshi la Mageleza, Polisi, Mawakili wa Serikali, Mawakili wa kujitegemea, Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali kwa nyakati tofauti walilishukuru Jopo hilo la Majaji wa Mahakama ya Rufani kwa kuendesha mashauri ya Rufani kwa haki, kusaidia kujifunza mambo mengi katika utekelezaji wa sheria na utoaji haki kwa wananchi kwa wakati.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Winifrida Korosso akifungua Kikao cha tathmini ya uendeshaji wa mashauri ya rufaa ya Mahakama ya Rufani jopo lililoketi Mahakama Kuu Mbeya, kushoto ni Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Judith Lyimo.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Panterine M. Kente (kulia) na Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Leila E. Mgonya (kushoto) wakifuatilia kikao cha tathmini.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa akisema jambo wakati wa kikao hicho.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu na  Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bi. Mavis Miti nao walikuwepo kwenye kikao
Mahakimu wa Mahakama Mkoa wa Mbeya, Jeshi la Mageleza, Polisi, Mawakili wa Serikali, Mawakili wa kujitegemea, Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali wote walishiriki kikao hicho.

Mahakimu wa Mahakama Mkoa wa Mbeya, Jeshi la Mageleza, Polisi, Mawakili wa Serikali, Mawakili wa kujitegemea, Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali wote walishiriki kikao hicho.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni