Jumatano, 26 Februari 2025

MAHAKAMA MBEYA YASHIRIKI MAMA SAMIA LEGAL AID KAMPENI

Na Daniel Sichula-Mahakama, Mbeya

Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya tarehe 24 Februari, 2025 imeungana na Taasisi zingine za kisheria mkoani Mbeya kwenye uzindua wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika viwanja vya Stendi ya Daladala Kabwe na kushiriki kikamilifu katika utoaji wa elimu na msaada wa kisheria.

Katika banda la Mahakama Mkoa wa Mbeya limejikita katika kutoa elimu ya kisheria kwa wananchi hususan katika masuala ya ukatili wa kijinsia, migogoro ya ardhi, mirathi, usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala.

Aidha, akizungumzia kampeni hiyo Mtaalam kutoka Wizara ya Katiba na Sheria alifafanua kwamba, lengo la kuanzishwa kwa Kampeni hiyo ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia ni kulinda na kukuza upatikanaji wa haki kwa wote kupitia huduma ya msaada wa kisheria nchini na kampeni hiyo ilianzishwa mwaka 2023 na itaendelea hadi 2026 kwa nchi nzima.

Vilevile, katika kampeni hiyo, wananchi wa Mbeya wamejitokeza kwa wingi katika mabanda ya Taasisi mbalimbali ili kupata msaada wa kisheria na imepelekea kampeni hiyo kuongeza uelewa wa kisheria na haki za binadamu kwa jamii hususani haki za wanawake na watoto, ukatili wa kijinsia, masuala ya haki na wajibu na misingi ya utawala bora.

Aidha, toka Kampeni hiyo imeanza katika mikoa mbalimbali nchini imekua ikigusa moja kwa moja mambo mbalimbali ya kisheria ya wananchi katika kupata msaada wa kisheria kwa kushirikiana na Wizara na Taasisi za Serikali, Asasi za Kiraia, Wanazuoni na Wadau wa Maendeleo.

Watumishi wa Mahakama Wakitoa Elimu ya Sheria kwa Wananchi waliofika Kwenye Banda la Mahakama Kuu Mkoa wa Mbeya

Wananchi wakipata huduma kwenye Banda la Rita

Wananchi wakipata Elimu ya Sheria kwenye Banda la Wizara ya Katiba na Sheria


Wananchi wakipata Elimu ya Sheria kwenye Banda la Wizara ya Katiba na Sheria

Wananchi wakipata Elimu ya Sheria kwenye Banda la Wizara ya Katiba na Sheria



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni