- Watoka na maazimio kadhaa kuboresha utendaji
Na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Mwanza
Kikao cha Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania, Kanda na Divisheni, kilichokuwa kinafanyika jijini hapa
kimehitimishwa leo tarehe 19 Machi, 2025, huku Viongozi hao wakitoka na maazimio
kadhaa yanayolenga kuboresha huduma za utoaji haki kwa Wananchi.
Kabla ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania,
Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, ambaye alikuwa Mwenyekiti, kuhitimisha Kikao
hicho, Majaji Wafawidhi walipokea mada tatu zilizowasilishwa na wataalam wa
ndani ya Mahakama.
Mada ya kwanza iliwasilishwa na Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Manyara, Mhe. John Kahyoza kuhusu matumizi
ya Mifumo katika kutekeleza majukumu ya Jaji Mfawidhi.
Mkurugenzi wa Usimamizi na Ukaguzi wa Huduma za
Kimahakama, Mrejesho kwa Umma na Maadili wa Mahakama ya Tanzania, ambaye pia ni
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Maira Kasonde, aliwasilisha
taarifa ya ukaguzi wa Mahakama.
Kadhalika, Jaji Mfawidhi wa Kituo Jumuishi cha Masuala
ya Familia, Mhe. Mwanabaraka Mnyukwa alitoa uzoefu kuhusu usimamizi wa mashauri
ya mirathi baada ya uteuzi wa msimamizi.
Katika maazimio hayo, Majaji hao wamehimiza changamoto
zinazozitokeza kwenye matumizi ya Mfumo wa Tafsiri na Unukuzi Pamoja na Mifumo
mingine ziendelee kuibuliwa na kutafutiwa ufumbuzi ili kuboresha ufanizi.
Majaji hao pia wameazimia kuwa Maafisa wote wa
Mahakama wapatiwe kompyuta mpakato kama sehemu ya kitendea kazi, kwa kuwa sasa Mahakama
hatumii karatasi.
Kadhalika, Majaji Wafawidhi wameazimia kuwa kuwepo na progamu
za unasihi kwa Maafisa wa Mahakama katika kila Kanda na Divisheni za Mahakama
Kuu kama inavyoelekezwa katika Mwongozo wa Malezi ya Kitaalam ya Maofisa wa Mahakam
awa mwaka 2025. 
Baadhi ya Viongozi wa Mahakama wanaohudhuria Kikao
hicho ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Msajili wa Mahakama ya Rufani,
Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mtendaji wa Mahakama Kuu-Kanda, Mtendaji
wa Mahakama Kuu-Divisheni, Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu, Wakurugenzi
mbalimbali, Naibu Wasajili na wengine.
Mbali na kujadili masuala
mbalimbali yanayohusu utendaji wa Mahakama, Kikao hicho pia kilitoa fursa ya
kujipima na kujitathmini kuhusu utendaji kazi, sambamba na utekelezaji wa
Mpango Mkakati, Dira na Dhima ya Mahakama.
Aidha, Majaji walipata fursa muhimu ya kubadilishana uzoefu kwenye utendaji wa kazi za Mahakama, pamoja na kutambua na kujadili changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika Mahakama Kuu na Mahakama za chini yake na hivyo kutafuta majibu kwa changamoto hizo.
Jaji Mfawidhi wa Majakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile akichangia mada kwenye Kikao hicho.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Zahra Maruma naye hakuwa nyuma kuchangia mada zilizowasilishwa.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mwanza, Mhe. Dkt. Ntemi Kilekamajenga akichangia mada hizo.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tabora, Mhe. Dkt. Adam Mambi akichangia mada zilizowasilishwa.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Shinyanga, Mhe. Frank Mahimbali naye hakubaki nyuma.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Joachim Tiganga akichangia mada hizo.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Arusha, Mhe. Ilvin Mugeta akichangia mada zilizowasilishwa.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni