Na Mwinga Mpoli – Mahakama, Mbeya
Mahakimu
waajiriwa wapya mkoani Mbeya wamekabidhiwa vitendea kazi ikiwemo Vipakatalishi (laptops)
na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles
Tiganga, makabidhiano hayo yamefanyika leo tarehe 14 Machi, 2025 katika ofisi
ya Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo.
Akiongea
na Mahakimu hao wakati wa kuwakabidhi vifaa kazi hivyo Mhe. Tiganga amewaasa
Mahakimu hao juu ya matumizi sahihi ya vifaa hivyo vya kazi, vilevile
aliwakumbusha kwenda kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya maadili, weledi,
kujituma na kusimamia viapo vyao vya uhakimu.
“Leo
tutawakabidhi komputa mpakato (laptops) mpya za kisasa kama moja ya nyenzo za
kazi na Mahakama yetu kwa sasa ni ya kidigitali hivyo mmewezeshwa na mwajiri
ili kurahisisha kutenda kazi zenu kidigitali. Tunategemea mtafanya kazi zenu
vizuri mkitimiza lengo la umalizaji wa mashauri 260 kwa mwaka kama ilivyo lengo
la upimaji utendaji kazi kwa Mahakama za Mwanzo. Nasisistiza mkafanye kazi kwa
weledi, kujituma na kuwajibika huku mkisimamia viapo vyenu vya uhakimu,”
alisema Jaji Tiganga
Aidha,
Mhe. Tiganga akatoa rai kwa Mahakimu hao kuanza kukimbizana na kazi ya
kusikiliza na kuamua mashauri ili waende sambamba na Mahakimu wenzao, na pia
kuhakikisha wanaandika maamuzi ambayo yana hoja zilizojadiliwa kwa
kina na kushirikiana na wenzao katika vituo vyao vya kazi na kuheshimu nafasi
ya kila mtumishi.
“Tuna
matarajio makubwa kutoka kwenu hivyo ninyi kama vijana tumieni nguvu zenu,
akili na maarifa kufanya kazi zenu,” aliongeza Mhe. Tiganga
Mahakimu
waliokabidhiwa vifaa kazi hivyo ni Mhe. Franco Deogratius Isuja, Mhe. Gift
Isack Massawe na Mhe. Joseph George Singano.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga
akimkabidhi vitendea kazi Hakimu Mpya Mhe. Franco Deogratius Isuja.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga
akimkabidhi vitendea kazi Hakimu Mpya Mhe. Joseph George Singano.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga
akimkabidhi vitendea kazi Hakimu Mpya Mhe. Gift Isack Massawe.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga (katikati) akiongea wakati wa makabidhiano ya vitendea kazi hivyo.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga (katikati)
akiwa kwenye picha ya pamoja na Mahakimu Wapya waliokabidhiwa Vipakatalishi leo tarehe 14 Machi, 2025 wa pili kutoka kushoto ni Naibu Msajili
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Emily Temu.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni