Alhamisi, 10 Aprili 2025

MLUNDIKANO WA MASHAURI WAPUNGUA MAHAKAMANI

Na ARAPHA RUSHEKE –Mahakama, Dodoma

Mahakama, katika kutekeleza jukumu lake la kikatiba la utoaji haki kwa mwaka 2024, imefanikiwa kupunguza mlundikano wa mashauri hadi kufikia asilimia 4 katika miaka minne mfululizo .

Mafanikio hayo yamebainishwa leo tarehe 10 April,2025 na Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya alipokuwa anawasilisha taarifa yake kwenye Kikao cha Baraza la Wafanyakzi Kitaifa linalofanyika katika ukumbi wa PSSF Jijini Dodoma.

Msajili Mkuu amebainisha pia kuwa, mlundikano wa mashauri umeshuka toka asilimia 11 kwa mwaka 2021 hadi asilimia 4 kwa mwaka 2024.

Wastani wa jumla wa mzigo wa kazi ulipungua kutoka mashauri 234 hadi 227. Aliongezea kuwa wastani huo pia ulipungua katika ngazi zote za Mahakama isipokuwa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani.

Ameeleza kuwa katika kufanikisha mafanikio hayo,  Mahakama ilifanya vikao maalumu vya kuondoa na kuzuia mlundikano wa mashauri katika ngazi zote za Mahakama isipokuwa Mahakama za Mwanzo.

“Ufunguaji  wa mashauri  Mahakama Kuuuliongezeka kwa silimia 11 na kupungua kwa Mahakama ya Hakimu Mkazi kwa silimia 24, Mahakama za Wilaya kwa asilimia 6, Mahakama za Watoto kwa asilimia 9 na Mahakama za Mwanzo kwa asilimia 36,’’alisema Msajili Mkuu.

Aliongezea kuwa umalizaji wa mashauri uliongezeka kwa Mahakama Kuu kwa asilimia 14 na Mahakama za Watoto kwa sailimia 3 na kupungua kwa Mahakama za Hakimu mkazi kwa silimia 21, Mahakama za Wilaya kwa asilimia 3 na Mahakama za Mwanzo kwa asilimia 2.

Mhe. Nkya ameeleza kuwa utendaji mzuri wa Watumishi wa Mahakama, wakiwemo Majaji na Mahakimu umesababisha kupungua kwa kiasi kikubwa malalamiko ya Wananchi na kuongeza Imani katika utoaji haki.

Alimaliza kwa kusema kuwa wataendelea kuongeza ufanisi wa mifumo ili kuongeza kasi ya usikilizaji wa mashauri, kuendelea kuchambua kanuni zinazohitaji marekebisho, kusimamia utekelezaji wa vigezo vya upimaji utendaji na kufuatilia maendeleo ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 ambayo italeta taswira ya Mpango Mkakati wa Mahakama unaokuja.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe .Eva Nkya akiwasilisha taarifa yake katika Kikao cha Baraza la Wafanayakazi linalofanyika Jijini Dodoma katika ukumbi wa PSSSF.

Katibu wa TUGHE Mahakama, Bw. Alquine Masubo akiwasilisha hoja mbalimbali za Wafanyakazi.


Sehemu ya Wajumbe wa Baraza-juu na chini- wakifuatilia kilichokuwa kinajiri kwenye Kikao hicho.


Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto.

Meza Kuu inayoongozwa na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya wajumbe ambao ni wanachama wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati walio kaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi kutoka TUGHE.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.


 

 

 

 

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni