Na ARAPHA RUSHEKE-Mahakama Kuu, Dodoma
Watumishi watatu wa Mahakama ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma, ambao wamestaafu kazi kwa mujibu wa sheria, wameagwa rasmi.
Hafla ya kuwaaga Watumishi wao ilifanyika jana
tarehe 8 Aprili, 2025 katika ukumbi uliopo Rafiki Hoteli jijini Dodoma na
kuhudhuriwa na Viongozi pamoja na Watumishi wakiongozwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama
Kuu Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani.
Katika hafla hiyo, Watumishi hao walipatiwa zawadi
mbalimbali ikiwa ni ishara ya kuenzi mchango wao katika kuitumikia Mahakama ya Tanzania
kwa uadilifu na uchapakazi uliotukuka.
Wastaafu hao ni Bi. Scholastica Njiwa ambaye
ni Mwandishi Mwendesha Ofisi, Bw. Hemed Hemed na Bw. Issa Rajab Kabandika.
Watumishi hao walipata fursa ya kushiriki
katika shughuli mbalimbali ikiwemo tukio la kukata keki pamoja na burudani,
hali iliyoleta furaha na kumbukumbu nzuri, huku wakikumbushana mambo ya zamani
waliyokutana nayo pamoja na chamngamoto katika utumishi wao.
Walitumia hao pia walipata
nafasi ya kueleza jinsi walivyoweza kuvuka vikwazo na kufanya kazi kwa
ushirikiano ili kufanikisha malengo ya Mahakama na kuwasihi wanaobaki waendelee
kufanya kazi kwa bidii pamoja na kujituma.
Akitoa neno la
shukrani kwa niaba ya wenzake, Bi. Scholastika Njiwa aliwashukuru Viongozi na Watumishi
kwa kuwafanyia sherehe pamoja na kuwapatia zawadi.
Watumishi wastaafu wa Masjala Kuu wakiwa katika picha ya
pamoja wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Rafiki Hoteli jijini Dodoma.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Morogoro.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni