Ijumaa, 10 Oktoba 2025

JAJI DINGO’HI AFANYA ZIARA YA UKAGUZI MKOANI LINDI


  • ·Apongeza kasi ya uondashaji wa Mashauri Mahakamani
  • ·Awaasa watendaji kukaza buti kwenye matumizi ya TEHAMA
  • ·Asisitiza kufanya kazi kwa uadilifu

Na. Hilary Lorry – Mahakama, Lindi

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara, Mhe. Saidi Dingo’hi amefanya ziara ya ukaguzi katika Mkoa wa Lindi na kukagua Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi, Mahakama za Wilaya tano (5) za Mkoa wa Lindi, Mahakama ya Wilaya ya Lindi, Kilwa, Liwale, Ruangwa, Nachingwea na Mahakama za mwanzo zilizopo katika Mkoa huo.

Akizungumza na watumishi wa Mahakama kwa nyakati tofauti wakati wa ziara hiyo Mhe. Dingo’hi alisema nimeshuhudia kazi nzuri mnayofanya alipokuwa akikagua Mahakama za Wilaya hizo na kuwakumbusha watumishi kufanya kazi kwa bidii na kwa uadilifu wa hali ya juu.

Aidha, Mhe. Dingo’hi aliwapongeza watumishi katika mkoa huo kwa kuchukua jitihada za makusudi  katika ufanyaji wa  kazi kwa bidii hasa Mahakimu kwa  kusikiliza mashauri kwa wakati  bila kuzalisha mashauri ya muda mrefu (mashauri ya Mlundikano)  na kutokuwa na mashauri mengi yanayoendelea mahakamani (pending cases) hiyo ni kutokana na kasi ya usikilizaji na umalizaji wa mashauri kwa wakati.

“Nawapongeza Mahakimu wote  kwa kutekeleza jukumu lenu la  msingi la usikilizaji na uondoshaji wa Mashauri kwa wakati lakini pia niwatake mtekeleze jukumu hilo kwa uadilifu ili haki isionekene tu bali ionekane ikitendeka hii itarejesha imani ya jamii kwa Mahakama” alisisitiza Jaji Dingo’hi.

Aidha, Mhe. Dingo’hi aliwaasa watumishi katika mkoa huu kuachana kabisa na matumizi ya karatasi na kujikita zaidi  katika matumizi  ya Mifumo ya TEHAMA, pamoja na mifumo ya uratibu wa Mashauri na Mifumo Mingene yote iliyoanzishwa au kutumiwa na Mahakama ya Tanzania  kwani lengo ni  kurahisishia utekelezaji wa majukumu ya kila siku.

Vilevile, Mhe. Dingo’hi aliwataka watumishi kuwachukulia wateja wote kwa usawa  bila kujali vyeo vyao, hadhi  zao hili kuwachukulia kwa usawa Mawakili wa Serikali na Mawakili wakujitegemea vyivyo hivyo.

Aidha, Jaji Dingo’hi aliwataka watumishi kuendelea kuleana kielimu (Mentorship) ikiwa ni mwendelezo wa utekelezaji wa agizo la Jaji Mfawidhi Kanda ya Mtwara Mhe.Edwin Kakolaki.

Mhe.Dingo’hi pia alitembelea na kukagua Mradi wa Ujenzi wa Kituo Jumuishi (IJC) Lindi pamoja na gereza la Wilaya ya Lindi.

Kwa upande wao viongozi wengine walioambatana na Jaji Dingo’hi katika ziara hiyo ya ukaguzi ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara Mhe. Seraphina Nsana, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Lindi Mhe. Consolata Peter Singano, Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara Bw. Yusuph Msawanga na Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi.Quip Mbeyela  kwa nyakati tofauti wakati wa ziara hiyo waliwataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kwa nidhamu.

Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara Mhe.Saidi Dingo’hi (katikati) akiteta Jambo na watumishi (hawapo kwenye picha) wakati wa ziara ya ukaguzi.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe.Consolata Peter Singano akisoma taarifa ya Mahakama ya Mkoa wa Lindi Mbele ya Mhe.Jaji Dingo’hi.

Mtendaji wa Mahakama Kuu kanda ya Mtwara Bw. Yusuph Msawanga akiteteta jambo na watumishi katika ziara hiyo ya ukaguzi.

Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi.Quip Godfrey Mbeyela akieleza jambo wakati wa ukaguzi.





Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara Mhe. Saidi Dingo’hi akipanda Mti wa Kumbukizi alipotembelea Mahakama ya Mwanzo Mandawa iliyopo Wilaya ya Ruangwa.

Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi wakiwa katika Picha ya pamoja na Jaji wa mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Saidi Dingo’hi (aliyesimama katikati).

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara Mhe Saidi Dingo’hi na Jopo lake wakionyeshwa mwenendo wa Ujenzi wa Mradi wa chumba cha Mahakama Mtandao kinajojengwa Gereza kuu Lindi.


Picha ikionyesha zoezi la ukaguzi wa mradi wa Ujenzi wa kituo Jumuishi (IJC) Lindi.

Watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Ruangwa wakiwa katika Picha ya pamoja na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Saidi Dingo’hi wakati wa ziara yake ya ukaguzu wilaya ya Ruangwa.

Picha ikionyesha zoezi la ukaguzi wa mradi wa Ujenzi wa kituo Jumuishi (IJC) Lindi.

Picha ikionyesha zoezi la ukaguzi wa mradi wa Ujenzi wa kituo Jumuishi (IJC) Lindi.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni