Na. Muksini Nakuvamba – Mhakama, Mbeya
Kaimu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya, Mhe. Said Kalunde amengoza
kikao cha menejimenti mkoa wa Mbeya kilichofanyika jana tarehe 09 Oktoba 2025 katika
ukumbi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya.
Akiwasilishwa taarifa ya utendaji kazi kwa
kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2025/2026 Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya
Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya ambaye pia alikuwa Katibu katika kikao
hicho Bi. Mervis Miti alitoa taarifa ya rasilimali watu ambapo ilieleza kuhusu hali ya watumishi
wa Mahakama Mkoa wa Mbeya, upimaji wa watumishi na motisha za watumishi.
Aidha,
taarifa hiyo ilieleza kuhusu taarifa ya usimamizi wa rasilimali fedha, vyombo
vya usafiri, taarifa ya mashauri, taarifa ya matumizi ya TEHAMA na
ushughulikiaji wa malalamiko na mapendekezo, utoaji wa elimu kwa umma na hali
ya majengo mbalimbali ya Mahakama mkoa wa Mbeya.
Vilevile,
taarifa hiyo ilifafanua juu ya mafanikio kadhaa ikiwemo kupokea watumishi 18 wa
ajira mpya, ukarabati na uboreshaji wa baadhi ya majengo ya Mahakama, kusimamia
nidhamu ya watumishi, matengenezo ya magari ya ofisi na kupokea na kuanza
kutumika kwa Majengo mapya matatu yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.
Kwa
upande mwingine, taarifa hiyo ilieleza changamoto kadhaa ikiwemo uchakavu wa
magari na majengo ya ofisi kama majengo ya Mahakama za mwanzo na nyumba ya
kuishi Jaji Mfawidhi hali inayopelekea kupanga nyumba mtaani kwa gharama kubwa.
Changamoto
zingine ni usajili wa mashauri kwa jina moja la wadaawa au washitakiwa kwa
mashauri ambayo yana washitakiwa zaidi ya mmoja, sambamba na hilo pia kumekuwa
na changamoto ya uwepo wa vielelezo vya muda mrefu katika mahakani, alisema Mtendaji
huyo.
Taarifa
hiyo pia ilifafanua juu ya mikakati kadhaa ya kuimarisha mifumo ya TEHAMA kwa
kuhakikisha upatikanaji wa nishati na mtandao, kutenga fedha kwa ajili ya
ukarabati wa majengo na kuendelea kulipa mirathi kwa wakati.
Aidha,
iliwasilishwa taarifa ya mashauri kwa Mahakama zote za mkoa wa Mbeya na
Mahakama Kuu, Kanda ya mbeya, taarifa hiyo iliwasilishwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi
wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya Mhe. Tedy Mlimba.
“Baki
ya mashauri hadi mwezi juni ni 639 na yaliyofunguliwa kuanzia julai hadi
septemba ni 2481, yaliyomalizika kati ya julai hadi septemba ni 2501 na mashauri
yaliyobaki hadi kufikia Septemba ni mashauri 619,” alisema Mhe. Mlimba.
Aidha,
kikao kilijadili taarifa za Mirathi kwa Mahakama zote za Wilaya Mkoa wa Mbeya ambapo
Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama zote waliwasilisha taarifa zao.
Mtendaji
hiyo wa Mahakama aliwasilisha taarifa ya mirathi inayowataka kushirikiana
katika kufanya tathimini ya fedha zote zilizopo kwenye akaunti ya mirathi kwa Mahakama
zote na kuzilipa kwa haraka na kutuma taarifa ya utekelezaji wa jambo hilo
kabla ya tarehe 05 novemba, 2025.
Kaimu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya ambaye ni mwenyekiti katika kikao
hicho akifuatilia mawasilisho.
Sehemu
ya wajumbe wa kikao
Hakimu
mkazi mfawidhi mahakama ya wilaya Rungwe Mhe. Jackson Banobi (aliyesimama) akiwasilisha
taarifa ya mirathi mahakama ya wilaya Rungwe
Afisa
Hesabu Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Bi. Nancy Rwebembela (aliyesimama) Akichangia
Hoja katika kikao hicho
Hakimu
Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya Mhe. Tedy Mlimba (kulia) akiwasilisha
taarifa ya mashauri na mirathi kwa Mahakama za Mkoa wa Mbeya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni