Ijumaa, 10 Oktoba 2025

SHEREHE ZA KUWAAGA WASTAAFU KANDA YA MTWARA YAFANA

Na. Hilary Lorry – Mahakama, Lindi

Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara ikijumuisha na Mikoa ya Lindi na Mtwara, imefanya sherehe ya kuwaaga watumishi waliostaafu utumishi wa umma kufikia October 2025,

Sherehe hiyo iliyofanyika ndani ya Hoteli ya Sea View Beach Resort iliyoko wilayani Lindi ikiwakutanisha viongozi mbalimbali wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara akiwemo Jaji Mfawidhi Mhe.Edwin Kakolaki, Jaji Saidi Ding’ohi,Jaji Martha Mpaze ,Naibu Msajili Mhe. Seraphine Nsana, Hakimu Mkazi Mfawidhi Lindi Mhe. Consolata Singano, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mtwara Mhe. Charles Mnzava ambaye pia ndiye aliekuwa Mshereheshaji wa shughuli hiyo.

Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Mtwara Mhe. Edwin Kakolaki katika sherehe hiyo aliwapongeza watumishi waliostaafu kwa utumishi wao uliotukuka katika kutoa huduma kwa wananchi kwa kipindi chote walichotumikia muhimili wa Mahakama.

“Kuna msemo unaosema “Life begins at forty” kwa maana Maisha yanaanza ukiwa na miaka arobaini. Lakini hiyo inatuhusu sisi tulio kazini. Ila kwa nyinyi wastaafu tunasema “Life begins at sixty” hivyo kwenu nyie Maisha ndo kwanza yameanza.” alisisitiza Mhe. Jaji Kakolaki.

Kwa nyakati tofauti Watendaji wa Mahakama Kuu Mtwara Bw. Yusuph Msawanga na Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi.Quip Mbeyela waliwashukuru sana watumishi waliostaafu kwa utumishi wenye nidhamu kwa kipindi chote cha utumishi wao.

Aidha, amewaomba watumishi waliopo kazini kudumisha nidhamu mahala pa kazi na kuchapa kazi kwa bidii kwani ni moja kati ya misingi ya ufanisi kazini.

Wastaafu walioagwa walishukuru uongozi wa Mahakama Kanda ya Mtwara ukiongozwa na Mhe. Jaji Kakolaki kwa kuwaandalia sherehe hiyo ambayo hawakutarajia ingefana kwa kiasi hicho.

Pongezi nyingi zilielekezwa kwa Mwenyekiti wa maandalizi ya sherehe hiyo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi. Mhe. Consolata Singano   Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi. Quip Mbeyela na kamati nzima ya maandalizi ya Sherehe hiyo.

Sherehe hiyo pia ilihudhuriwa na Watendaji wa Mahakama ya Lindi na Mtwara, Mahakimu Wafawidhi wa Wilaya zote, Mahakimu Mahakama za Mwanzo na Maafisa wengine wa Mahakama Kanda ya Mtwara.

Wastaafu wakiwa ukumbini tayari kwa kuagwa

Wabobezi katika zoezi la ufunguzi wa Shampeni wakitekeleza jukumu hilo kwa umaridadi  mkubwa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwini Kakolaki (wa pili kushoto) akiwa na, Jaji Saidi Ding’oi, wakiingia uwanjani kusakata rhumba.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwini Kakolaki (wa pili kushoto) akitoa zawadi kwa mmoja wa wastaafu katika sherehe hiyo

Wastaafu wakikata keki katika sherehe hiyo 

Bango lenye ujumbe wa kuwaaga wastaafu wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara na wakati huo Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwini Kakolaki  akiwahutubia waalikwa wote katika sherehe hiyo.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Mhe. Edwini Kakolaki akigonga glass na Wastaafu kutakiana afya njema.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mtwara Mhe. Edwini Kakolaki (wa tatu kulia) wakigonga glass kutakiana afya njema katika sherehe hiyo.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya sherehe ya kuwaaga wastaafu Kanda ya Mtwara Mhe. Consolata Singano (aliyesimama mbele) akitoa taarifa fupi ya sherehe hiyo.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Lindi Mhe. Subilaga Mwakalobo (kushoto) akiwa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya wilaya ya Lindi Mhe. Khalfan O. Khalfan wakifuatilia sherehe hiyo.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni