Na NAUMI SHEKILINDI, Mahakama-Simiyu
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga, Mhe. John Rugalema Kahyoza
amefungua mafunzo kwa watumishi wapya wa Mahakama wa kada mbalimbali walioajiriwa
hivi karibuni lengo likiwa ni kuwajenga
watumishi hao waweze kuwa bora wakiwa katika utumishi wao kwa kuwa waadilifu,
wawajibikaji, wafanisi na wenye bidii ya kazi.
Mafunzo
hayo yaliyofunguliwa jana tarehe 13 Novemba, 20254 yameandaliwa na Ofisi ya
Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu yakiongozwa na Mtendaji wa Mahakama
ya Hakimu Mkazi Simiyu, Bw. Gasto Kanyairita.
Aidha,
Mhe. Kahyoza alionesha kufurahishwa na maandalizi ya mafunzo hayo na kusema
kuwa, yatawafanya watumishi wa ajira mpya wawe bora zaidi wakati wa utekelezaji
wa majukumu yao.
Jaji
Mfawidhi huyo alitoa mada kuhusu (non-Judicial Staff na Judicial Officers) kwa
kueleza namna muundo ulivyoanzishwa na sababu za kuanzishwa kwake na mwisho alisisitiza
kwamba watumishi wote wanajenga nyumba moja ambayo ni Mahakama ya Tanzania.
Kadhalika,
watumishi hao wamefundishwa namna ya kujipatia kipato cha ziada bila kuathiri
utendaji wao wa kazi.
Mafunzo
hayo yalitolewa na wakufunzi mbalimbali ambao ni Maafisa Tawala/Utumishi na
Wahasibu kutoka Wilaya mbalimbali ndani ya Mkoa wa Simiyu ambao wamewahimiza
watumishi hao kuwa waadilifu, wawajibikaji, wafanisi, wenye bidii ya kazi na
tabia njema.
Mfanzo
hayo yalifungwa na Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu, Bw. Gasto
Kanyairita ambaye aliwaasa watumishi hao Kwenda kuyaishi yale yote
waliofundishwa.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni