Na. ALLY RAMADHANI - Mahakama, Katavi
Mtendaji
Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel Jana tarehe 16
Desemba, 2025 alitembelea na kukagua Mradi wa Ujenzi wa Kituo Jumuishi cha
utoaji Haki (IJC) Katavi kwa lengo kufuatilia maendeleo ya Mradi huo.
Akitoa
taarifa ya maendeleo ya mradi wa ujenzi wa jengo hilo Mhandisi Victor
Vedasto ambaye ni mwakilishi wa Mkandarasi kampuni ya AZHAR Construction Co.
Ltd, alisema “Mradi mzima wa Kituo cha IJC Katavi ambao unajumuisha sehemu tatu
yani Jengo Kuu, Eneo la nje (Mgahawa, uzio na chumba cha walinzi) pamoja na
Manzari (Land scaping) umefikia asilimia 92, huku Jengo Kuu likiwa limefikia
asilimia 95 na kuongeza kuwa tayari kazi za umaliziaji wa jengo unaendelea.
Aidha,
akitoa maelekezo kwa Mwakilishi wa mkandarasi wa mradi huo, Prof. Ole Gabriel
alisisitiza kuwa ni muhimu mpaka kufikia tarehe 31 Desemba, 2025 Mradi uwe
umekamilika. Vilevile alisema kuwa, Mahakama “Lazima tuzingatie matumizi mazuri
ya muda kwa kasi ninayoiona naomba iendane na ubora ulio unaokubalika ili
tupate jengo nzuri,”
Aidha,
Mtendaji Mkuu akiwa katika eneo la mradi wa ujenzi wa Kituo hicho, alipata wasaa
wa kusalimiana na watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Katavi.
Moja
ya nguzo katika Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania ni Utoaji Haki kwa
wakati mapema ipasavyo. Mahakama inatekeleza Mpango huo kwa kuboresha mazingira
ya utoaji haki na kusogeza huduma za utoaji haki kwa wananchi kwa kujenga
miundombinu bora na wezeshi itakayochangia ufanisi mzuri wa utekelezaji wa
azimio hilo.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof.
Elisante Ole Gabriel, akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Mahakama Mkoa
wa Katavi, wakati wa ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa IJC Katavi.
Mhandisi Victor Vedasto, akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya mradi wa ujenzi wa jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Katavi kwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama Prof. Elisante Ole Gabriel.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof.
Elisante Ole Gabriel akitoa maelekezo kwa mwakilishi wa mkandarasi wa
mradi, wakati wa ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa IJC Katavi.
.jpg)
.jpg)
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni