Jumatatu, 15 Desemba 2025

WAJUMBE WA TAASISI YA MAFUNZO YA UANASHERIA KWA VITENDO WAKUTANA NA JAJI MKUU

  • Wajadiliana juu ya utoaji wa elimu bora ya Sheria

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 15 Desemba, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Wajumbe wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST), waliomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania Jijini Dodoma.

Mazungumzo hayo yamelenga kuhakikisha utoaji wa elimu bora ya sheria, upatikanaji wa mikopo na upatikanaji wa fursa kwa vijana kusoma Shule ya Sheria kwa vitendo.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. George Masaju (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya wajumbe wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika leo tarehe 15 Desemba, 2025, ofisini kwa Jaji Mkuu jijini Dodoma.
 
Sehemu nyingine ya wajumbe wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) wakiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (wa nne kulia) mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika ofisini kwa Jaji Mkuu jijini Dodoma.  Wa tatu kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Kuu, Mhe. Abdi Kagomba, wa nne kushoto ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Samweli Maneno (kushoto)  na wa kwanza kulia ni Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. George Herbert. 

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) akipokea nakala ya kitabu kutoka kwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Samweli Maneno (kushoto). Kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Kuu, Mhe. Abdi Kagomba.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akizungumza jambo wakati wa mazungumzo kati yake na Wajumbe wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo yaliyofanyika leo tarehe 15 Desemba, 2025 ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.


Sehemu ya wajumbe wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo wakisikiliza kwa makini hoja zilizokuwa zikitolewa wakati wa mazungumzo kati ya Wajumbe wa Taasisi hiyo na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju yaliyofanyika leo tarehe 15 Desemba, 2025 kwenye Ofisi ya Jaji Mkuu jijini Dodoma.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akimsikiliza kwa makini Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Abdi Kagomba alipokuwa akichangia hoja wakati wa kikao cha mazungumzo na Wajumbe wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo yaliyofanyika Ofisini kwa Jaji Mkuu Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.

(Picha na HABIBA MBARUKU & JEREMIA LUBANGO, Mahakama)


 

 

 

 

 



 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni