Ijumaa, 19 Desemba 2025

TANZIA; JAJI MSTAAFU WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA AFARIKI DUNIA

 


TANZIA

 Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Julius Benedicto Mallaba enzi za uhai wake.

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Julius Benedicto Mallaba kilichotokea leo tarehe 19 Desemba, 2025, saa 10 alfajiri, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu kwa ugonjwa wa sukari na shinikizo la damu.

Marehemu Jaji Mallaba alizaliwa tarehe 12 Machi, 1960. Aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania tarehe 25 Julai, 2015 na kustaafu rasmi mnamo tarehe 12 Machi, 2020.

Kwa Mujibu wa Msemaji wa Familia, msiba upo nyumbani kwake Mbweni jijini Dar es Salaam. Taratibu nyingine za mazishi zitatolewa na Familia.

Mahakama ya Tanzania inaungana na ndugu, jamaa na marafiki kuomboleza msiba huu wa kuondokewa na mpendwa wetu.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

    


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni