Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Emilian Matata Ezekiel Mushi, kilichotokea tarehe 24 Januari, 2026 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Marehemu Mushi aliajiriwa na Mahakama ya Tanzania
tarehe 7 Aprili, 1976 kama Hakimu Mkazi na kuhudumu katika vituo mbalimbali
hadi tarehe 11 Juni, 2002 alipoteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na
kuhudumu katika Kanda mbalimbali.
Enzi za uhai wake, Mhe. Mushi alihudumu pia katika
nafasi ya Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto [IJA] kwa vipindi viwili
tofauti, yaani mwaka 2000 hadi 2002, na mwaka 2004 hadi 2010 alipohamishwa
kwenda Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ambapo aliendelea na kazi mpaka
mwaka 2012 alipostaafu kazi kwa mujibu wa sheria.
Marehemu anatarajiwa kuzikwa tarehe 29 Januari, 2026
Kibaha Mwendapole, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani.
Mahakama ya Tanzania inaungana na ndugu, jamaa na
marafiki kuomboleza msiba huu mkubwa wa kuondokewa na mpendwa wetu
BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA JINA LA BWANA
LIHIMIDIWE
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni