Jumatano, 24 Februari 2021

JAJI MKUU PROF JUMA AONGOZA KUAGA MWILI WA JAJI MSTAAFU WILLIAM MAINA

  • ·       Ibada ya kuaga mwili yafanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Oysterbay
  • ·       Mwili wake wazikwa katika Makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam
  • ·       Jaji Maina atakumbukwa kwa Uadilifu, uchapakazi na uzalendo

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Marehemu Jaji William Maina. Ibada ya kuaga mwili huo imefanyika leo Februari 24, 2021 katika kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Jaji Mstaafu Maina.
 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Lameck mlacha akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Jaji Maina.


Baadhi ya ndugu wakiaga mwili wa mpendwa wao.

Sehemu ya ndugu wa marehemu wakiwa katika ibada ya kuaga mwili wa mpendwa wao.

Mapadri wakiongoza ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Jaji Mstaafu William Maina.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma pamoja na baadhi ya Waheshimiwa Majaji wakifuatilia ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Jaji William Maina, katikati ni Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi na kushoto ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Lameck Mlacha na wawili waliopo nyuma ni Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Viongozi na Maafisa mbalimbali wa Mahakama wakiwa katika ibada hiyo.

Mhe. Jaji Mkuu akitoa risala yake mara baada ya ibada kukamilika, katika salaam zake za rambirambi, Mhe. Jaji Mkuu amesema kuwa Marehemu Jaji Mstaafu Maina alikuwa mchapakazi, muadilifu na mwenye kupenda ushirikiano katika kazi.

Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi akitoa salaam za rambirambi kwa familia, marehemu Jaji Maina aliwahi pia kufanya kazi Sekretariat ya Maadili.

(Picha na Mary Gwera, Mahakama)

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni