Alhamisi, 2 Julai 2026

JUSTICE MLYAMBINA VISITS ILO COUNTRY DIRECTOR DAR ES SALAAM OFFICE

  • Expresses appreciation for technical, financial support to Labour Court Division
  • Congratulates ILO for Economy Convention adoption

From FAUSTINE KAPAMA-Judiciary, Singida

The outgoing Judge in-Charge of the High Court Labour Division and incumbent Justice of Appeal. Hon. Dr. Yose Mlyambina, has expressed gratitude to the International Labour Organization (ILO) for remarkable partnership, friendship and support extended throughout his tenure.

Hon. Dr. Mlyambina voiced out such appreciation on Monday dated July 1, 2026, when he paid a courtesy visit to the ILO Country Director, Dar es Salaam Office, Madam Caroline Mugalla.

“The partnership between the International Labour Organization and the Labour Court has existed for many years and has consistently contributed to the advancement of labour justice in Tanzania.,” he said.

Justice Mlyambina made particular reference to the period between January 2023 and May 2026, during which their cooperation reached remarkable heights.  During such relatively short period, the ILO extended generous technical and financial support that has left a lasting institutional legacy.

He pointed out one of the most significant achievements was the sponsorship of the first publication of the Court of Appeal Labour Cases Report, 2023.

He said that such important publication was followed by the publication of the Compilation of Principal and Subsidiary Labour Laws, and subsequently the publication of the High Court Labour Cases Report, 2025, comprising two comprehensive volumes.

“These publications represent much more than collections of judicial decisions and statutes. They are indispensable tools in the administration of labour justice,” said Justice Mlyambina.

According to him, another notable achievement for which they remain deeply grateful is the generous donation by the ILO of a substantial collection of labour law textbooks and reference materials to the High Court Labour Division Library.

These books, he said, have greatly enriched our legal resources and strengthened legal research within the Division.

“Although the world is progressively transitioning towards digital libraries and electronic legal databases, the reality in developing countries such as Tanzania is that printed legal materials continue to play an indispensable role,” he said.

He also congratulated the Organization at the global level for another historic milestone reached on June 12, 2026, during the 114th Session of the International Labour Conference in Geneva, with the adoption of the Decent Work in the Platform Economy Convention, No. 193 of 2026.

“This Convention demonstrates once again the ILO's leadership in responding to the changing nature of work across the world,” Justice Mlyambina told the ILO Country Director.

He pointed out that the rapid expansion of digital labour platforms has created enormous employment opportunities, while simultaneously presenting new legal and policy challenges relating to workers' rights, social protection, occupational safety and health, fair remuneration and effective access to justice.

According to him, the Convention provides a timely international framework for balancing innovation with social justice.

Hon. Dr. Mlyambina said that for countries such as Tanzania, where the platform economy continues to expand, the Convention offers valuable guidance in developing legal and policy frameworks that protect workers while encouraging entrepreneurship, innovation and investment.

He told the Country Director that the Convention No. 193 comes at an opportune moment, thus providing an international framework within which Member States can respond to emerging challenges, while fostering innovation and sustainable economic growth. 

“It is also noteworthy that the platform economy is steadily blurring the traditional distinction between an employee and an independent contractor, a distinction upon which much of our labour legislation has historically been built,” Justice Mlyambina said.

He pointed out further that Convention No. 193 provides an important normative framework to guide that evolution while respecting national legal systems. The Convention will only attain its intended impact when it is ratified and effectively implemented by ILO Member States, including Tanzania.

“We therefore look forward to the ILO continuing to support the United Republic of Tanzania including the Judiciary of Tanzania, through technical assistance, legislative advisory services, capacity building and institutional strengthening,” he said.

Justice Mlyambina added that such an undertaking would ensure that the aspirations embodied in Convention No. 193 are translated into meaningful improvements in the world of work, while simultaneously fostering innovation, entrepreneurship and sustainable economic development.

During the visit, Justice Mlyambina was accompanied by other senior judicial official, including his successor, High Court Judge, Hon. Dr. Ntemi Kilekamajenga, who has assumed the responsibility of Judge In-Charge of the High Court Labour Division since on June 22, 2 2026.

He took such opportunity to introduce him to the ILO Country Director and expressed his confidence that under his capable leadership, the Division will continue to grow from strength to strength.

Justice Mlyambina request that the excellent cooperation and partnership that has existed between the International Labour Organization and the High Court Labour Division continues under his stewardship.

Other judicial official in attendance during the visit were Deputy Registrar In-Charge of the High Court Labour Division, Hon. Cassian Enock Matembele, Deputy Registrar of the High Court Labour Division, Hon. Mary Mrio, another Deputy Registrar of the High Court Labour Division, Hon. Ritha Tarimo, Judge’s Law Assistant of the High Court Labour Division, Hon. Jane Masua and Acting Court Administrator of the High Court Labour Division, Ms. Joyce Mulugu.

The outgoing Judge in-Charge of the High Court Labour Division and incumbent Justice of Appeal. Hon. Dr. Yose Mlyambina,presents a gift to Internatioanl Labour Organization Country Director, Dar es Salaam Office, Madam Caroline Mugalla. The picture below, the duo is in a group picture.



The host and visiting judicial officials sharing information.

The ILO Country Director, Dar es Salaam Office, Madam Caroline Mugalla (right) in a group picture with Judge In-Charge of the High Court Labour Division, Hon. Dr. Ntemi Kilekamajenga.

A group photo of three officials. Middle if the outgoing Judge in-Charge of the High Court Labour Division and incumbent Justice of Appeal. Hon. Dr. Yose Mlyambina, left is Judge in Charge of the High Court Labour Division, Hon. Dr. Ntemi Kilekamajenga and right if ILO Country Director, Dar es Salaam Office, Madam Caroline Mugalla. The picture below comprises other judicial officials who were part of the visit.



 

MASJALA NDOGO MBEYA YAWAKARIBISHA VIONGOZI WAPYA

Na. MUKSINI NAKUVAMBA –Mahakama, Mbeya

Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya wamekutana katika ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu kwa ajili ya hafla ya kuwakaribisha na kuwatambulisha viongozi wapya waliohamia kuhudumu katika kanda hiyo.

Viongozi waliokaribishwa katika hafla hiyo ni Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo na Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bw. Festo Chonya.

Hafla hiyo, iliongozwa na Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Said Kalunde na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Mahakama Kuu, Mahakimu wakiongozwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, Mhe. Teddy Mlimba, pamoja na watumishi wa Mahakama Kuu, Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mahakama za Wilaya na Mahakama za Mwanzo zilizopo Jijini Mbeya.

Akizungumza katika kikao hicho, Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo alisisitiza umuhimu wa kujenga ushirikiano mzuri kati ya viongozi na watumishi ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi. .

Aidha, aliwahimiza watumishi kuendelea kuendana na maboresho yanayoendelea kufanywa na Mahakama ya Tanzania, hususan katika matumizi ya mifumo ya TEHAMA, ambayo imekuwa nyenzo muhimu katika kuboresha utoaji wa huduma za haki.

Kwa upande wake, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya, aliwahimiza watumishi kuendelea kudumisha upendo, kuheshimiana na kushirikiana katika kutekeleza majukumu yao.

Pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, kuhakikisha usafi na usalama wa miundombinu ya Mahakama, kutumia mifumo ya TEHAMA kwa usahihi na kuwajibika kikamilifu katika maeneo yao ya kazi.

Hafla hiyo pia, ilitoa fursa kwa wawakilishi wa watumishi kutoka katika kila Mahakama kutoa salamu za ukaribisho kwa viongozi hao wapya na kuahidi ushirikiano katika kutekeleza majukumu ya Mahakama.

Aidha, hafla hiyo ya utambulisho na ukaribisho wa viongozi wapya ni hatua muhimu katika kuimarisha mshikamano, kujenga uhusiano mzuri wa kikazi na kuweka msingi wa ushirikiano kati ya viongozi na watumishi.

Vilevile, hutoa fursa ya kuelekeza matarajio ya utendaji, kuimarisha uwajibikaji na kuongeza ari ya pamoja katika kuboresha utoaji wa huduma za haki kwa wananchi kwa kuzingatia maadili, ueledi na matumizi bora ya mifumo ya kisasa ya Mahakama.

Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Said Kalunde (aliyesimama) akizungumza katika kikao hicho cha kuwakaribisha Viongozi, kulia ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya Bw. Festo Chonya, na kushoto ni Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo.

Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo akizungumza na watumishi katika kikao hicho. (hawapo pichani) kulia ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya Bw. Festo Chonya.

Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bw. Festo Chonya, akizungumza na watumishi wa kanda ya Mbeya katika kikao hicho. (hawapo pichani)

Sehemu ya watumishi walioshiriki katika hafla fupi ya kuwakaribisha Viongozi wapya wa Masjala Ndogo ya Mbeya wakifuatilia kwa makini shughuli zilizokuwa zikiendelea katika kikao hicho.

 

Sehemu ya watumishi walioshiriki katika hafla fupi ya kuwakaribisha Viongozi wapya wa Masjala Ndogo ya Mbeya wakifuatilia kwa makini shughuli zilizokuwa zikiendelea katika kikao hicho.

Sehemu ya watumishi walioshiriki katika hafla fupi ya kuwakaribisha Viongozi wapya wa Masjala Ndogo ya Mbeya wakifuatilia kwa makini shughuli zilizokuwa zikiendelea katika kikao hicho

Hakimu Mkazi Mahakama ya Wilaya Mbeya Mhe. Happines Chuwa (aliyesimama) akitoa neno la shukurani katika kikao hicho kwa niaba ya watumishi.


Afisa Utumishi Mahakama Kuu na Mahakama ya Watoto Mbeya Bw. Ibrahim Mgallah (aliyesimama) akitoa neno la ukaribisho katika kikao hicho.






 

“OSHA ENDELEENI KUFANYA UKAGUZI WA MIUNDOMBINU MAHALI PA KAZI; NI TAKWA LA KISHERIA”

Na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju ametoa rai kwa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kuendelea kufanya ukaguzi katika miundombinu yote ya maeneo ya kazi ili kuhakikisha usalama mahali pa kazi sambamba na kutekeleza takwa la Sheria ya Afya na Usalama Kazini.

Mhe. Masaju ametoa rai hiyo leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma alipokuwa akifungua Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania.

“Ushauri wangu kwenu ni kwamba endeleeni kufanya ukaguzi katika miundombinu yote kama ilivyotajwa katika Sheria ya Afya na Usalama Kazini, na ikiwemo miundombinu ya Mahakama. Sababu hii ya kwenu sio utashi, ni maelekezo ya sheria. Sheria lazima itekelezwe tu," amesema Jaji Mkuu na kuongeza:

"Na Mwalimu Nyerere aliwahi kusema mwaka 1988, alipokuwa anafunga mkutano wa ALAT, alisema hivi, 'Serikali ni Sheria.' Hakuna kitu kinaitwa Serikali bila sheria, na sheria zikishatungwa lazima zifuatwe.”

Mhe. Masaju aliongezea, “Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaweka msingi wa Utawala wa Sheria na inamtaka kila mtu kuitii Katiba hii na Sheria za Jamhuri ya Muungano, na kwamba kila mtu ana haki ya kuchukua hatua kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa kuhakikisha hifadhi ya Katiba na Sheria za Nchi.”

Katika hatua nyingine, Jaji Mkuu ameipongeza OSHA, chini ya Mtendaji Mkuu Bi. Khadija Mwenda, kwa kwenda mbali zaidi ya kusimamia Sheria, kufanya mafunzo na kutoa vitendea kazi vinavyozingatia mifumo ya kiorganomia (ergonomics) ili kuwakinga watumishi na magonjwa yatokanayo na mazingira ya kazi.

Ameongeza kuwa, haki ya kuishi imewekwa katika ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nayo inasema hivi, "Kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata kutoka katika jamii hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa sheria." Amesema Sheria ya Afya na Usalama Kazini, msingi wake ni huo: watu kuishi. “Kazi hizi zisifanye tukafa, ndio maana inasisitiza... sasa ukishakufa una maana gani? Na... ukishakufa unaishia pale.”

Amesema, msingi mwingine wa Sheria ya Afya na Usalama Kazini ni Ibara ya 12 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, inayosema kwamba kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake. 

“Na sasa sisi Taifa hili lina kaulimbiu inayosema, "Kazi na Utu". Tufanye hizi kazi lakini tukiwa tumezingatia utu ikiwa ni pamoja na kuzingatia ustawi wetu, kwamba hizi kazi zisifanye tukafa mapema halafu kuwepo kwetu kukawa hakuna maana yoyote,” amesema Jaji Mkuu.

Amesema, suala hilo limehusishwa moja kwa moja na Ibara ya 14 ya Katiba inayofafanua haki ya kuishi, pamoja na Ibara ya 12 inayosisitiza heshima na utu wa binadamu, ikizingatiwa Kaulimbiu ya sasa ya Taifa ya "Kazi na Utu."

"Maendeleo yanapangwa na binadamu na ni kwa ajili yao; hayawezi kupangwa na mashine wala wanyama. Ndio maana uwekezaji katika afya zao ni muhimu. Kadri mtu anavyofanikiwa, ndivyo anavyotaka kuendelea kuishi ili atoe mchango kwa Taifa lake," amesisitiza Mhe. Masaju huku akiongeza kuwa mafunzo hayo yanaendana na Nguzo ya Pili ya Dira ya Taifa ya Maendeleo, 2050 inayolenga kujenga nguvu kazi yenye ujuzi, motisha na ubunifu na Kipaumbele cha kwanza cha Dira hiyo kinachohusu Utawala Bora na Haki.

Jaji Mkuu ameeleza kuwa, Taifa hili linastahili ustawi wa binadamu wote, wakiwemo Wakulima kwa wafanyakazi na wafanyabiashara na kila mmoja. Amesema, “Na sisi tunaofanya kazi, wawe Mahakimu au Waamuzi kama tulivyo sisi, na kila mmoja wetu anahitaji ustawi. Mafunzo haya pia yanatupeleka kwenye utekelezwaji wa hiyo Dira kwenye ustawi, lakini imeandamana na kitu cha msingi sana: haki, hivyo Mahakama itaendelea kusimamia utoaji haki ipasavyo.”

Ameongeza kuwa, Taifa jumuishi lenye ustawi ni Taifa ambalo halimwachi mtu nyuma, huku akirejea na kupongeza mafunzo ambayo OSHA wameshatoa kwa makundi mbalimbali ya watu. 

Katika hatua nyingine; Jaji Mkuu amemshukuru Rais Samia kwa Uteuzi wa Majaji tisa wa Mahakama ya Rufani kwa jitihada zake za makusudi za kuendelea kuimarisha Mhimili huo kupitia rasilimali watu na vitendeakazi.

“Ninamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha Mhimili huu wa Mahakama kwa rasilimaliwatu, vitendeakazi na rasilimali nyingine ili Mhimili huu uweze kuendelea kutekeleza jukumu lake la utoaji haki kwa ufanisi zaidi. Na kwa sababu hiyo, ninamshukuru kwa uteuzi huu alioufanya mwezi uliopita na akawaapisha hawa Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani tisa kwa wakati mmoja; hilo ni kazi kubwa sana amefanya. Mheshimiwa Rais namshukuru sana sio kazi ndogo,” amesema Mhe. Masaju.

Ameongeza kuwa, “Unapomteua Jaji, umeteua watu wengine tisa nyuma yake, kwa uchache. Kwa hiyo, anapoteua ni kwamba amedhamiria kwa dhati kabisa. Na hii inaonesha utayari wake wa kuendelea kuimarisha Mhimili huu kuweza kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ipasavyo ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ninamshukuru sana.”

Jaji Mkuu amesema, uamuzi wa hivi karibuni wa Mkuu wa Nchi wa kuteua na kuwaapisha Majaji tisa wa Mahakama ya Rufani kwa wakati mmoja umetajwa kama uthibitisho wa utayari wake wa dhati wa kuhakikisha haki inatendeka kwa ufanisi mkubwa nchini. 

Aidha, Jaji Mkuu amewapongeza Majaji walioteuliwa hivi karibuni, ambapo amesema, “Ninakutana nanyi mara ya kwanza katika tukio hili rasmi. Niwapongeze sana kwa mwenendo wenu mwema, kuwa na sifa za kuweza kuteuliwa hata kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani. Na Mwenyezi Mungu aendelee kuwabariki sana katika maisha yenu, katika utumishi wenu, na katika shughuli zenu.”

Kadhalika Mhe. Masaju amempongeza Jaji Mlyambina aliyekuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama kwa kuwa na ushirikiano mzuri na Wadau wa Haki Kazi ambapo umeiwezesha Mahakama kunufaika na mambo mengi ikiwemo mafunzo kwa Watumishi wake wakiwemo Majaji, Naibu Wasajili, Mahakimu, Madereva na kadhalika.

Viongozi wengine wakuu waliohudhuria tukio hilo ni pamoja na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) Lushoto, Mhe.Dkt. Paul Faustine Kihwelo, Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Amir Mruma, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu, baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Mahakama ya Tanzania, Watumishi wa OSHA, watumishi wengine wa Mahakama.

Wengine waliohudhuria ni pamoja na Wataalamu Wabobezi/Madaktari na Wauguzi kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Chuo Kikuu cha Tiba na Afya Muhimbili (MUHAS) na Taasisi ya Mifupa (MOI).

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju akifungua Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Sehemu ya Majaji na Viongozi wengine wa Mahakama na OSHA wakimsikiliza Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju alipokuwa akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.


Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina akitoa neno wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda akitoa neno wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu (kushoto) pamoja na Mtendaji wa Mahakama ya Rufani, Bw. Victor Kategere wakiwa katika hafla ya ufunguzi wa Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu-Mahakama ya Tanzania, Bi. Beatrice Patrick (kulia) pamoja na Mtendaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Bw. Victor Kategere wakifuatilia kinachojiri katika hafla ya ufunguzi wa mafunzo hayo.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju akimpatia zawadi ya saa Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda baada ya hafla ufunguzi wa Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda (kulia) akimpatia zawadi Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju ya Vifaa tiba vya huduma ya kwanza (First Aid Tool Box) baada ya hafla ufunguzi wa Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) yanayotolewa kwa Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 02 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Majaji wapya Mahakama ya Rufani (waliosimama) wanaopatiwa mafunzo ya Usalama na Afya mahali pa Kazi yanayotolewa na OSHA. Aliyeketi kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda.

Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Amir Mruma (aliyesimama). Aliyeketi kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda.

Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Mahakama ya Tanzania (waliosimama). Aliyeketi kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda.

Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa OSHA (waliosimama). Aliyeketi kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda.

Meza Kuu katika picha ya pamoja na Wataalamu wa Afya kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili na MOI.

Meza Kuu katika picha ya pamoja na Wawezeshaji wa Mafunzo ya Usalama na Afya mahali pa Kazi yanayotolewa na Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani. Aliyeketi kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Mlyambina na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda.

(Picha na MARY GWERA & JEREMIA LUBANGO, Mahakama)

Jumatano, 1 Julai 2026

KITUO JUMUISHI TEMEKE, MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI WABADILISHANA UZOEFU

  • Waweka mikakati kuboresha utoaji haki kwenye mashauri ya mirathi, madai ya fidia

Na MWANDISHI WETU-Mahakama, Temeke

Mahakama Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke hivi karibuni kilishiriki mafunzo ya kubadilishana uzoefu na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ili kuongeza ufanisi katika kuwahudumia wananchi, hasa katika utoaji wa haki zinazohusu fidia katika mashauri ya mirathi.

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Destiny Hall ulioko Kibaha katika Mkoa wa Pwani yalifunguliwa rasmi Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Temeke, Mhe. Mwanabaraka Mnyukwa.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Mhe. Mwanabaraka alisisitiza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kutatua changamoto za ucheleweshaji wa haki kwa warithi na kuimarisha ushirikiano wa kiutendaji kati ya Taasisi hizo mbili. 

Katika Kikao hicho, mada ziliwasilishwa kuhusu Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi, Taratibu na changamoto za madai ya fidia kwa wafanyakazi pamoja na taratibu za ufunguaji na uendeshaji wa mashauri ya mirathi.

Bw. Deo Victor Ngowi kutoka Idara ya Huduma za Sheria WCF, akiwasilisha mada kuhusu sheria inayoongoza fidia kazini, alitoa ufafanuzi kuwa fidia hutolewa na WCF kutokana na ajali au vifo kazini na hivyo haiwezi kudaiwa kama sehemu ya mirathi na wasimamizi wa mirathi.

Alieleza pia kuwa fedha hizo hazilipwi kwenye akaunti ya mirathi, bali huenda moja kwa moja kwenye akaunti binafsi za wanufaika sahihi.  Bw. Ngowi alichambua makundi muhimu yanayolipwa na WCF ambayo ni wenza na watoto wenye umri chini ya miaka 18.

Aidha, alieleza kuwa madai yote ya fidia ni lazima yawasilishwe WCF ndani ya miezi 12 tangu kutokea kwa ajali au kifo kwa mnufaika wa WCF.

Bw. Ngowi aliwaelimisha washiriki pia juu ya nani hufaa kuwa wanafaika wa WCF kwa kusema kuwa, “WCF haihusiki na wafanyakazi wa sekta isiyo rasmi kama mikataba ya chini ya siku 30, wafanyakazi wa kujitolea, pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama.”

Meneja Msimamizi wa Ulipaji Fidia, Bi. Rehema Mwakabongo, alipokuwa akiwasilisha mada, alieleza faida mbalimbali zitolewazo na mfuko huo, ikiwemo gharama za matibabu ya ulemavu wa muda au wa kudumu, msaada wa matibabu nje ya nchi, na fao la mazishi.

Alieleza changamoto zinazojitokeza katika ulipaji wa fidia kama udanganyifu kutoka kwa wanufaika, ikiwemo uwepo wa nyaraka zaidi ya moja ya cheti cha kifo, changamoto ya utofauti wa majina ya walipwaji, hivyo kusababisha uwepo wa ‘deed poll’ za udanganyifu.

Bi. Rehema alielezea pia changamoto ya waajiri na waajiriwa kuchelewa kuwasilisha nyaraka muhimu kwa ajili ya malipo ya fidia kwa wakati, hivyo kuomba ushirikiano mkubwa na Mahakama pale inapohitajika.

Katika kikao hicho, mada kuhusu utaratibu wa ufunguaji mashauri ya mirathi, uendeshaji hadi kufungwa zilitolewa na  Mahakimu, Mhe. Stephanie Kagaruki Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Mwanzo, kwa kushirikiana na Mhe. Mhangwa Yunge, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya.

Mahakimu hao walifafanua mada juu ya taratibu za ufunguaji na uendeshaji wa mashauri ya  mirathi, taratibu na mamlaka za Mahakama kulingana na ngazi zake.

Mahakama za Mwanzo husikiliza mirathi ya kiislamu na ile ya mila na desturi, Mahakama za Wilaya na Mahakama Kuu husikiliza mirathi ya kikristo na asili ya kiasia.

Pia watoa mada walieleza juu ya nyaraka zinazoweza kutumika ili WCF itoe malipo, nyaraka za Mahakama kama vile fomu namba 80 kwa Mahakama Kuu na Wilaya pamoja na Fomu No.5 kwa Mhakama ya Mwanzo zinazoonyesha orodha ya mali za marehemu.

Fomu No.81 kwa Mahakama Kuu na Wilaya pamoja na Fomu No. 6 kwa Mahakama ya Mwanzo zinazoonyesha hesabu za mali ya marehemu ikiwaonyesha wanufaika na walichopewa.

Watoa mada walisema muhtasari wa kikao cha familia sio takwa la kisheria bali hutumika kama utaratibu wa kujiridhisha. Walieleza pia hukumu inaweza kuwa nyaraka muhimu, lakini sio inayowataja warithi halisi, hivyo ni muhimu kuthibitisha wanaostahili kulipwa.

Watoa mada walieleza kuwa hakuna haja ya msimamizi wa mirathi kuagizwa hati ya kiapo cha uthibitisho kwa kuwa hati ya usimamizi wa mirathi kutoka mahakamani ni uthibitisho tosha kuwa ameteuliwa na Mahakama.

Washiriki wa mafunzo hayo walipata nafasi ya kujadili juu ya mada zilizowasilishwa na kuibua maswali muhimu kama vile stahiki za watoto waliozidi miaka 18 wenye changamoto maalumu za kuwafanya kuwa chini ya uangalizi wa wazazi wao.

Mfuko wa WCF uliahidi kuifanyia kazi changamoto hiyo kwa kuwa kwa sasa watoto wa kuanzio umri huo sio wanufaika wa mfuko.

Kuhusu maboresho ya sheria, washiriki waliishauri WCF kuona namna ya kurahisisha michakato, ikiwemo kuheshimu nyaraka za Mahakama bila kuweka ulazima mkubwa wa cheti cha kifo pale ambapo Mahakama imeshathibitisha vifo hivyo.

Kikao kazi hicho kilifungwa na Jaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Gladys Barthy, ambaye aliishukuru WCF kwa fursa hiyo ya kujengeana uwezo. Ili kuhakikisha makubaliano hayo yanafanyiwa kazi kwa vitendo, Mahakama imeahidi kuteua mtu maalum (focal person) atakayekuwa kiunganishi cha haraka kati ya Mahakama Kituo Jumuishi Temeke na WCF ili kuharakisha huduma kwa wananchi.

Jaji Mfawidhiwa Mahakama Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke, Mhe. Mwanabaraka Mnyukwa, akifungua mafunzo ya kubadilishana ujuzi katika ukumbi wa Destiny Hall Kibaha Pwani.

Washiriki wa mafunzo hayo wakisikiliza hotuba kutoka kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Wa WCF, Bw. Abrahamu Siyovelwa.

Majaji Kutoka Mahakama Kuu Kituo Jumuishi Temeke walioshiriki katika kikao mafunzo wakifuatilia mada zilizokuwa zinawasilishwa.

Hakimu Mkazi Mwandamizi, Mhe. Mhe. Stephani Kagaruki,  akitoa mada juu ya taratibu za ufunguaji wa mirathi Mahakama za Mwanzo  katika kutoa haki kwa wananchi.

Hakimu Mkazi Mwandamizi, Mhe. Mhangwa Yunge, akitoa ufafanuzi juu ya mada za Usimamizi wa mashauri ya mirathi katika Mahakama ya Wilaya na Mahakama Kuu Temeke.

Meneja Malipo toka WCF, Bi Rehema Kabongo, akitoa mada kuhusu taratibu za fidia kwa wafanyakazi.

Jaji wa Mahakama Kuu Kituo Jumuishi Temeke, Mhe. Gladies Barthy akihitimisha rasmi mafunzo hayo.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Singida.


WADAU WA HAKI JINAI SONGWE WAKUTANA KUPANGA MIKAKATI YA UONDOSHAJI MASHAURI

Na. ELIUD KIWANGA – Mahakama, Songwe

Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe, hivi karibuni ilifanya kikao cha kusukuma Mashauri ya Jinai, kikilenga kutathimni na kuimarisha usimamizi na ufanisi wa utoaji wa haki katika Masjala ya Songwe.

Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe na kuongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Malata, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Joyce Minde na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Abubakar Mrisha na kuhudhuriwa na wadau wa Haki Jinai kutoka Taasisi mbalimbali Mkoa wa Songwe.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Joyce Minde alisoma taarifa ya mwenendo wa Mashauri ya Haki Jinai Masjala ya Songwe kuanzia tarehe 30, Machi, 2026 mpaka tarehe 26 Juni, 2026 kwa kuainisha mashauri yote yaliyofunguliwa, mashauri yaliyomalizika na mashauri yaliyoendelea kusikilizwa.

Mhe. Minde aliaainisha changamoto zinazoathiri usikilizwa wa mashauri ya jinai na baadae zilipatiwa ufumbuzi. “Tunaomba ushirikiano wa wenu kwa Mahakama na sisi tunajitahidi kadri tunavyoweza ili kuhakikisha mashauri aliyosalia yanamalizika kwa wakati,” alisistiza.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Malata alisisitiza kwamba, kikao hicho kinajikita katika mikakati ya kuhakikisha mashauri ya jinai kwa ngazi ya Mahakama Kuu yanasikilizwa haraka ili kuepuka mlundikano wa Mashauri huku tukiendelea kuwahimiza wadau kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake katika mnyororo wa haki jinai ili kusaidia Mahakama kutekeleza jukumu lake la msingi ipasavyo.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Tawi la Songwe, Bw. Moses Mwampashi amesema, idadi ya Mawakili mkoani Songwe haitoshi ukilinganisha na uhitaji wa wananchi katika uwakilishi wa Mawakili mahakamani Songwe, aliendelea kubainisha kuwa uhitaji wa Mawakili ni mkubwa ukilinganisha na idadi ya mashauri yaliyopo mkoani humo.

Wakili huyo, ameliomba jukwaa la Haki Jinai Mkoa wa Songwe kusaidia ongezeko la Mawakili ili kutoa huduma ya kisheria na uwakilishi mzuri wa wananchi mahakamani kwa wakati, hatua hiyo itaiwezesha Mahakama kumaliza mashauri mapema ipasavyo.

Katika kikao hicho, Wadau wa Haki Jinai pamoja Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe waliazimia kuwa Wafungwa na Mahabusu wafikishwe kwa wakati, Mawakili wa Serikali na wa Kujitegemea wafike mahakamani saa moja kabla ya muda ulioandikwa kwenye Summons, kujiridhisha kwa kina juu ya mashahidi wanaofika kutoa ushahidi mahakamani.

Vilevile, wadau waliazimia kwamba, ikiwa wakili atashindwa kuendelea kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake arudishe doc brief ili wakili mwingine aweze kupangiwa shauri hilo, pia uongozi wa TLS uwakumbushe mawakili majukumu yao kisheria ikiwemo kuwatembelea mahabusu kabla ya kuletwa mahakamani, Mawakili wa Serikali na wa kujitegemea kujiandaa ipasavyo kabla ya kuingia mahakamani. Vyombo vya haki jinai kuzingatia taratibu za kisheria zinazosimamia masuala yote ya haki jinai.

Mhe. Malata aliwashukuru wadau wote waliofika katika kikao hicho na kuwasisitiza kutimiza na kutekeleza maazimio yote waliyokubaliana kwa kuzingatia sheria za haki jinai zinavyotaka, aliomba ushirikiano ili kuboresha utoaji wa haki jinai kwa wananchi.

Kikao hicho cha Wadau wa Haki Jinai Songwe kilihudhuriwa na wajumbe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Magereza, Polisi, Ofisi ya Upelelezi Mkoa, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (NPS), Ustawi wa Jamii, Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Ofisi ya Uangalizi Mkoa wa Songwe na Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe.

Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala, Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (katikati), Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Abubakar Mrisha (kushoto) na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Joyce Minde (kulia) wakiwa kwenye kikao cha kusukuma mashauri ya jinai.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe Mhe. Stephano Minja akifuatilia kikao hicho.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (katikati), Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Abubakar Mrisha (kushoto) na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Joyce Minde (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Wadau wa Mahakama mara baada ya kuhitimisha kikao cha kusukuma mashauri ya jinai.

Sehemu ya wawakilishi wa baadhi ya Taasisi zilizoalikwa za haki jinai mkoani Songwe.

Kaimu Mtendaji wa Mahakama ya Tanzania Masjala Ndogo ya Songwe Bw. Mohamed Kimungu Rajabu akifuatilia kikao hicho.

Sehemu ya Wadau wa Mahakama waliohudhuria kikao hicho akiwemo Bi.Tea Mshana, Bi. Maria Sanga kutoka NPS-Songwe pamoja na Bi. Geladina Theobard kutoka Ofisi ya Uangalizi-Songwe.