Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya amewaongoza Watumishi
wa Masjala hiyo kufanya ziara ya kujifunza katika Kituo cha kupooza na
kusambaza umeme cha Mtera, kilichopo Bwawa la Mtera mkoani Iringa kwa lengo
kuwajengea watumishi uelewa wa masuala ya uzalishaji wa nishati ya umeme kwa
njia ya maji.
Watumishi
hao, walipata elimu ya kina kuhusu mchakato wa uzalishaji wa umeme, kuanzia
hatua za awali za uzalishaji hadi umeme unapofikia hatua ya mwisho ya
kumwezesha mtumiaji kupata huduma hiyo.
Aidha,
elimu hiyo iliambatana na uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi, hususan
katika matumizi ya majumbani na kwenye vyombo vya usafiri, huku watumishi
wakifafanuliwa namna matumizi ya nishati safi yanavyoweza kuwa na mchango
mkubwa katika kupunguza athari za kimazingira na kuboresha maisha na ustawi wa
jamii.
Matumizi
ya nishati safi yana manufaa mathalani kuokoa muda, kupunguza gharama, kutunza
mazingira na kulinda afya za watumiaji, hivyo ni wito kwa jamii kuendelea
kuhamasishwa na kuelimishwa kuhusu fursa na manufaa yanayotokana na matumizi ya
nishati hiyo.
Watumishi
hao wameaswa kuendelea kuwa mabalozi wazuri katika kutunza miundombinu ya umeme
kwani umeme unachagiza maaendeleo ya Taifa, huku wataalum hao wakitoa wito kwa
Majaji na Mahakimu kuchukulia kwa uzito wa aina yake suala uendeshaji wa
mashauri yanayo husu uharibifu wa miundo mbinu ya umeme.
Ziara
hiyo pia ilitoa fursa kwa watumishi hao kutembelea Mahakama Kuu Masjala Ndogo
ya Iringa, ambapo walikutana na kufanya mazungumzo na viongozi pamoja na
watumishi wa Mahakama Kuu Masjala hiyo.
Mazungumzo
ambayo yaliweka msisitizo katika umuhimu wa kuendelea kujenga ushirikiano,
mshikamano na kubadilishana uzoefu miongoni mwa watumishi wa Mahakama katika
Masjala hizo, kwa lengo la kuimarisha utendaji na kuongeza ufanisi katika
utoaji wa huduma.
Sehemu
ya watumishi na viongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya wakipewa
maelezo na elimu mbalimbali juu ya namna umeme unavyochakatwa katika ziara hiyo.
Sehemu
ya watumishi na viongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya wakipewa
maelezo na elimu mbalimbali juu ya namna umeme unavyochakatwa katika ziara hiyo.
Sehemu
ya matukio mbalimbali ya watumishi wakiwa katika kituo cha Mtera
Sehemu
ya watumishi na viongozi wakiwa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Iringa ikiwa sehemu
ya ziara hiyo.
Kaimu
Meneja wa Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Mtera Mhandisi William
Modesti akiwapa elimu na kutoa historia ya kituo hicho na maendeleo yake kwa
watumishi wa Mahakama Mbeya waliotembelea katika kituo hicho.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya akitoa utambulisho na
kuzungumza machache katika ziara hiyo wakiwa Mtera.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kushoto), akipewa
Zawadi ya jiko la umeme la kupikia “Electrical pressure cooker” wakati
walipotembelea katika kituo cha kupooza na kusambaza umeme cha Mtera..jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)









.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)























