EVA LESHANGE & AMIRI BAKARI, Mahakama – Singida
Maofisa Magereza wanaohusika na Mifumo ya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano (TEHAMA) mkoani Singida wamepatiwa mafunzo ya Mifumbo mbalimbali ya Kielektroni ya Mahakama lengo likiwa ni kuwajengea uelewa Maofisa hao juu
ya mifumo mbalimbali ya kimahakama ikiwemo Mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi
wa Mashauri (e-Case Management System), Mahakama Mtandao (Virtual Court) na Mfumo
wa Taarifa za Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania (TanzLII).
Akifungua
mafunzo hayo jana tarehe 17 Agosti, 2026 kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu Singida, Naibu Msajili Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Jasmin Abdul aliwasisitiza washiriki kuongeza
ufanisi katika kutoa huduma na kuwa wabunifu ili kutoa Haki kwa wakati.Aidha
mafunzo haya yalihusisha maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Magereza Mkoa wa
Singida,Maafisa kutoka Magereza ya Wilaya Singida, Iramba,Ushora na Manyoni.
“Watumishi
wenzangu napenda kuwajulisha kuwa Mahakama ya Tanzania kwa sasa inatumia mifumo
ya TEHAMA katika kuendesha shughuli zake za kila siku hususan za utoaji haki na
Magereza ni miongoni mwa Wadau muhimu wa Mahakama, ni matarajio yangu kuwa
katika mafunzo haya mtajifunza kwa vitendo, mtabadilishana uzoefu na mwisho
kubaini changamoto na kuzitafutia suluhu hivyo muwe wazi na tayari kujifunza,”
alisema Naibu Msajili huyo.
Aidha, aliwasisitiza kufanya kazi kwa ushirikiano wanapopata changamoto za kimfumo kuziwasilisha kwa haraka na kwamba mafunzo hayo yatakuwa endelevu kwa kadri mabadiliko kimifumo yanayotokea.
Mada
za mafunzo hayo ya TEHAMA ziliwasilishwa na Ofisa TEHAMA Mahakama Kuu Masjala
Ndogo Singida, Bi.Valentina Nkullanga ambapo katika uwasilishaji wake
aliwaeleza Maofisa Magereza kuwa matumizi ya mifumo hiyo katika uendeshaji wa
shughuli za Mahakama umeleta manufaa makubwa kwa Mahakama na Wadau kwani
imeongeza ufanisi katika usimamizi wa mashauri, imepunguza matumizi ya karatasi.
Manufaa
mengine ni kupunguza ucheleweshwaji wa mashauri, kuimarika kwa usalama,
kupunguza gharama za usafirishwaji wa Mahabusu na kuongezeka kwa upatikanaji wa
haki mapema ipasavyo.
Katika
mafunzo, walijifunza pia kwa vitendo hatua zote kuanzia shauri linavyosajiliwa
hadi kukatiwa rufaa na waliona maandalizi ya awali katika kuandaa mashauri
yanayosikilizwa kwa njia ya mtandao namna ya kuandaa vitendea kazi, kuviunganisha
na mtandao.
Kadhalika,
walielekezwa namna ya kuingia katika mfumo wa TanzLII kwa ajili ya kupata
nakala za hukumu za wafungwa wao na kupata rejea mbalimbali kwa ajili ya
kujifunza.
Akihitimisha mafunzo hayo Naibu Msajili wa Mahakama, Mhe. Allu Nzowa aliwasisitiza washiriki kufanya kazi kama timu na kuyachukulia mabadiliko hayo katika mtazamo chanya ili kuleta ufanisi zaidi.
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Jasmin Abdul akizungumza jambo na Washiriki wa Mafunzo ya Mifumo ya Kielektroni ya Mahakama (hawapo katika picha) wakati wa ufunguzi wa Mafunzo kwa Maofisa Magereza tarehe 17 Agosti, 2026.
Ofisa TEHAMA wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Bi Valentina
Nkullanga (aliyesimama) akitoa mada kwa washiriki wa Mafunzo hao (hawapo katika picha) wakati wa mafunzo na Maofisa Magereza.
CPL
Yondani Kibuti kutoka Gereza la Wilaya Singida akichangia jambo wakati wa
mafunzo hayo.
Meza Kuu ikiongozwa na Naibu Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, Mhe. Allu Nzowa (aliyeketi katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo kutoka Gereza la Wilaya Manyoni. Aliyeketi kulia ni Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Singida na Mwenyekiti Kamati ya Elimu Kanda, Mhe. Aloyce Masua na kushoto ni Afisa Utumishi Mahakama Kuu Singida, Bi.Eva Leshange.
Meza Kuu ikiongozwa na Naibu
Msajili wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, Mhe. Allu Nzowa (aliyeketi katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Washiriki kutoka Gereza la Wilaya Iramba. Aliyeketi kulia ni Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Singida na Mwenyekiti Kamati ya Elimu Kanda, Mhe. Aloyce Masua na kushoto ni Afisa Utumishi Mahakama Kuu Singida, Bi.Eva Leshange.
Meza Kuu ikiongozwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, Mhe. Allu Nzowa (aliyeketi katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki kutoka Gereza la Wilaya Singida. Aliyeketi kulia ni Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Singida na Mwenyekiti Kamati ya Elimu Kanda, Mhe. Aloyce Masua na kushoto ni Afisa Utumishi Mahakama Kuu Singida, Bi.Eva Leshange.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)



























