Na. CHRISTOPHER MSAGATI- Mahakama, Manyara
Wanafunzi
wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka kilichopo Moshi mkoani Kilimanjaro
wamefanya ziara ya kujifunza taratibu mbalimbali za kimahakama katika katika
uendeshaji wa mashauri yanayohusu uendeshaji wa mashauri yanayohusu wanyamapori.
Mafunzo
hayo yanaendeshwa katika ukumbi namba Tatu wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara
ambao unatumiwa na Mahakama ya Wilaya ya Babati katika kuendesha shughuli za
Mahakama.
Katika
ziara hiyo, jumla ya wanafunzi Hamsini na nane (58) kutoka Chuo hicho
waliambatana na walimu wao wanne (4) kwa lengo la kujifunza taratibu na masuala
mbalimbali yanayotokea mahakamani kwa njia ya vitendo mtandao ili ziweze
kuwasaidia katika elimu yao wanayojifunza chuoni.
Akizungumza
wakati wa kufungua mafunzo hayo, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo
ya Manyara Mhe. Charles Mnzava, aliwasihi wanafunzi hao kuzingatia yale yote
ambayo watafundishwa na wataalamu wa masuala ya kisheria ili yaweze kuwasaidia
katika masomo yao ya chuoni na hata katika maisha ya baada ya chuo pale ambapo
watakuwa wameajiriwa au kujiajiri katika maeneo mbalimbali.
“Chuoni
mnasoma zaidi kwa nadharia, nawapongeza kwa kuja leo na kushuhudia namna
mashauri haya yanayohusu wanyamapori na nyara za Serikali yanavyoendeshwa mahakamani.
Mafunzo haya yatawaongeza tija na uelewa wenu zaidi katika hayo mnayojifunza
chuoni na hata baadae mtakapokuwa katika ajira zenu” alisema Mhe. Mnzava.
Katika
hatua nyingine, Mhe. Mnzava alitumia nafasi hiyo kuwafundisha wanafunzi hao juu
ya Muundo wa Mahakama Tanzania ulivyo. “Mahakama zetu hapa nchini, kuanzia
Mahakama ya Mwanzo, Mahakama za Wilaya na Mahakama za Hakimu Mkazi, Mahakama
Kuu Pamoja na Mahakama ya Rufani zina taratibu zake za usikilizwaji wa mashauri
kulingana na uzito wa mashauri husika hivyo ni vema mkafahamu kuwa hata haya
mashauri ya Wanyamapori mathalani hayawezi kusikilizwa katika ngazi za Mahakama
za Mwanzo”.
Aidha,
wanafunzi wa chuo hicho cha Mweka waliweza kuhoji na kujibiwa maswali
mbalimbali kwa wawezeshaji wa Mafunzo hayo ambao walikuwa ambaye Hakimu Mkazi
Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Babati, Mhe. Victor Joseph Kimaro pamoja na
Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Mhe. Martin Massao.
Akishukuru
baada ya mafunzo hayo Mwakilishi wa Walimu waliombatana na wanafunzi hao Mwalimu
Melckezedeck Tarimo alishukuru uongozi wa Mahakama Kuu Manyara kwa kuwapokea
vema na kuwapa Elimu waliyokuwa wakiihitaji.
“Tunashukuru
sana Uongozi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara kwa kutupokea na kwa
ushirikiano mliotupa, tuaamini kuwa elimu hii itatusaidia sana na tutaendelea
kuja hapa kwa ajili ya mafunzo mengine,” alisema Mwalimu Tarimo.
Mahakama
Kuu Masjala Ndogo ya Manyara imeendelea na utaratibu wa kutoa elimu kwa
wananchi wanaofika mahakamani kila wakati lakini pia kwa kupitia vyombo vya
Habari vilivyopo hapa mkoani kwa lengo la kutimiza mahusiano bora kati ya
Mahakama na wadau wanaosaidia utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Mahakama.
Walimu
na wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori, Mweka wakiwa katika picha ya
pamoja na watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara walipohudhuria
mafunzo katika Mahakama ya Wilaya ya Babati.
Sehemu
ya wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori, Mweka wakaifuatilia mada
zilizokuwa zinafundishwa wakati wa mafunzo yaliyokuwa yakitolewa kwa wanafunzi
wao kutoka kwa Mahakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Babati.
Mmoja
wa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori, Mweka akichangia mada wakati
wa mafunzo yaliyokuwa yakitolewa kwa wanafunzi wao kutoka kwa Mahakimu wa
Mahakama ya Wilaya ya Babati.
Walimu
wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori, Mweka (waliosimama) wakifuatilia mafunzo
yaliyokuwa yakitolewa kwa wanafunzi wao kutoka kwa Mahakimu wa Mahakama ya
Wilaya ya Babati.
Hakimu
Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Babati Mhe. Martin Massao akiendelea na mafunzo
kwa Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori, Mweka waliofika katika
Mahakama ya Wilaya ya Babati kwa ajili ya Mafunzo.
Hakimu
Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Babati Mhe. Victor Kimario (mwenye suti
ya rangi ya buluu) akiendelea na mafunzo kwa Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa
Wanyamapori, Mweka waliofika katika Mahakama ya Wilaya ya Babati kwa ajili ya
Mafunzo.
Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava (aliyevaa
suti nyeusi) akitoa Neno la Ukaribisho kwa Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa
Wanyamapori, Mweka waliofika katika Mahakama ya Wilaya ya Babati kwa ajili ya
Mafunzo.


















