Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu
Mtulya, ameongoza mafunzo ya rasimu ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania
wa mwaka 2026/27–2030/31 kwa watumishi wa Mahakama Kuu kwa lengo la kuwajengea
uelewa wa pamoja ili kila mtumishi aweze kutekeleza wajibu wake kwa ufanisi na
kuchangia katika kufikia malengo ya Taasisi.
Mafunzo
hayo yamefanyika jana Agosti 20, 2026 katika ukumbi wa Mahakama Kuu, Masjala
Ndogo ya Mbeya, yakijumuisha watumishi wa Mahakama kutoka Masjala Ndogo ya Mbeya
na sehemu ya watumishi hao walishiriki mafunzo hayo kwa njia ya mkutano mtandao.
Akifungua
mafunzo hayo, Mhe. Mtulya, alisisitiza umuhimu wa kila mtumishi kuuelewa kwa
kina Mpango Mkakati wa Mahakama, akieleza kuwa, uelewa huo ni msingi muhimu wa
utekelezaji wa majukumu ya kila siku.
“Kila
mtumishi wa Mahakama kwa ngazi zote anatakiwa afahamu kwa kina juu ya Mpango
Mkakati wa Mahakama ili kufanikisha malengo ya Taasisi, kwani kwa kufanya hivyo
itatujengea ufanisi wa kutekeleza majukumu ili kulifikia lengo mama la Mahakama
ya Tanzania la kutoa haki kwa wakati mapema ipasavyo,” alisema Mhe. Mtulya.
Jaji
Mtulya ameongeza kuwa, uwasilishaji wa rasimu hiyo kwa watumishi wote unalenga
kujenga uelewa wa pamoja kuhusu mwelekeo wa Mahakama katika kipindi kijacho,
hasa kutokana na changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa Mpango Mkakati
uliopita wa mwaka 2021/22-2024/25, ambapo watumishi wengi hawakuwa na uelewa wa
kutosha kuhusu Mpango Mkakati huo.
Watumishi
hao walipitishwa kwenye utekelezaji wa Mpango Mkakati uliopita, ikiwa ni pamoja
na mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza pamoja na mafunzo
yaliyopatikana yanayopaswa kuzingatiwa katika kuandaa na kutekeleza Mpango Mkakati
mpya.
Akifafanua
umuhimu wa kuweka vipaumbele vinavyotekelezeka na vyenye tija, Mhe. Mtulya alisema:
“Tunatakiwa kuwa na vipaumbele muhimu na vyenye tija na kuhakikisha bajeti
iliyopo inaendana na vipaumbele vyetu,”
Amesisitiza
kuwa, utekelezaji wenye mafanikio wa Mpango Mkakati wa Mahakama hautategemea
mpango huo pekee, bali pia utayari, uwajibikaji na ushiriki wa kila mtumishi
katika kutekeleza jukumu lake kwa kuzingatia mwelekeo na vipaumbele vya
Taasisi.
Aidha,
Jaji Mtulya alieleza kwa kina nguzo za kimkakati na maeneo ya msingi ya matokeo
yaliyoainishwa katika rasimu hiyo, akifafanua namna malengo ya Taasisi
yanavyoweza kufikiwa kupitia utekelezaji madhubuti wa majukumu ya kila
mtumishi.
Kwa
upande wake, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya,
alisisitiza umuhimu wa kuwa na Mpango Mkakati ambao siyo kwa Taasisi pekee bali
hata katika maisha ya mtu mmoja mmoja, akihusianisha umuhimu wa kupanga, kuweka
malengo kuyafanyia kazi na utekelezaji wake.
Naye, Naibu
Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi Laizer, alitoa shukrani kwa
Jaji Mfawidhi kwa uwezeshaji wa mafunzo hayo, huku akisisitiza umuhimu wa kila
mtumishi kutekeleza wajibu wake kwa kuzingatia nguzo za kimkakati za Mahakama.
“Wote
tunahusika katika kuhakikisha kuwa, nguzo hizo za kimkakati zinakuwa msingi wa
utekelezaji wa majukumu yetu,” alisema Mhe. Laizer.
Katika
hatua nyingine, watumishi walipata fursa ya kutoa maoni, ushauri na mapendekezo
kuhusu maboresho ya vipengele mbalimbali vya rasimu hiyo, hatua iliyolenga
kuhakikisha kuwa maoni ya watumishi yanazingatiwa katika kuboresha rasimu kabla
ya kukamilishwa.
Jaji
Mfawidhi, aliwashukuru watumishi kwa kushiriki katika mafunzo hayo na kuwataka
kutambua thamani ya nafasi waliyonayo kama watumishi wa umma. Aidha,
amewasisitiza kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na kuzingatia misingi ya
utumishi wa umma katika kutekeleza majukumu yao.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (Katikati), akiwasilisha
rasimu ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania kwa watumishi ya mwaka
2026/27–2030/31, Kulia ni Naibu Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi
Laizer na (kushoto) ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo
Chonya.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya (aliyesimama)
akizungumzia rasimu pendekezwa ya Mpango Mkakati wa Mahakama katika kikao
hicho.
Sehemu
ya Watumishi kutoka Mahakama mbalimbali Masjala Ndogo ya Mbeya walioshiriki na
kupata mafunzo juu ya rasimu mpya ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania ya Mwaka
2026/27–2030/31 katika mafunzo hayo.
Sehemu
ya Watumishi kutoka Mahakama mbalimbali Masjala Ndogo ya Mbeya walioshiriki na
kupata mafunzo juu ya rasimu mpya ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania ya Mwaka
2026/27–2030/31 katika mafunzo hayo.
Sehemu
ya Watumishi kutoka Mahakama mbalimbali Masjala Ndogo ya Mbeya walioshiriki na
kupata mafunzo juu ya rasimu mpya ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania ya Mwaka
2026/27–2030/31 katika mafunzo hayo.
Sehemu
ya Watumishi kutoka Mahakama mbalimbali Masjala Ndogo ya Mbeya walioshiriki na
kupata mafunzo juu ya rasimu mpya ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania ya Mwaka
2026/27–2030/31 katika mafunzo hayo.
Sehemu
ya Watumishi kutoka Mahakama mbalimbali Masjala Ndogo ya Mbeya walioshiriki na
kupata mafunzo juu ya rasimu mpya ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania ya Mwaka
2026/27–2030/31 katika mafunzo hayo.
Hakimu
Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe. Paul Dandi Ntumo akitoa maoni
yake ya kuboresha katika rasimu ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania ya Mwaka 2026/27–2030/31.
Hakimu
Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbeya Mhe. Tedy Mlimba (katikati) akichangia jambo
katika Mafunzo hayo ya watumishi wa Masjala Ndogo ya Mbeya.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
.jpg)
.jpg)
%20(1).jpg)
%20(1).jpg)
.jpg)
%20(1).jpg)












.jpg)
.jpg)
.jpg)