Jumatatu, 14 Septemba 2026

JAJI FERDINAND WAMBALI MWENYEKITI MPYA TMJA TAWI LA MAHAKAMA YA RUFANI

Na HABIBA MBARUKU, Mahakama-Dodoma

Wajumbe wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) Tawi la Mahakama ya Rufani wamemchagua Mhe. Ferdinand Wambali Jaji wa Mahakama ya Rufani kuwa Mwenyekiti wa Tawi hilo kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Tawi hilo, Mhe. Shaaban Lila.

Uchaguzi huo uliosimamiwa na Mlezi wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Augustine Mwarija umefanyika leo tarehe 14 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania ambapo wajumbe wa Tawi hilo walikutana ili kujadili mambo mbalimbali yanayohusu Tawi lao.

Mapema kabla ya uchaguzi kufanyika wajumbe walipendekeza majina ya wagombea wawili wa kiti hicho ambao ni Mhe. Dkt. Yose Mlyambina, Jaji wa Mahakama ya Rufani pamoja na Mhe. Ferdinand Wambali kisha majina hayo kupigiwa kura na wajumbe.

Matokeo ya uchaguzi wa Mwenyekiti mpya wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani yalipatikana baada ya wajumbe waliohudhuria kikao hicho kupiga kura ya siri ambapo jumla ya wapiga kura 53 walipiga kura, kura halali zilikuwa 53, na hakukuwa na kura zilizoharibika.

Baada ya zoezi la kupiga kura ya siri na kuhesabu kura kukamilika, Mlezi wa Tawi hilo Mhe. Augustine Mwarija alimtangaza Mhe. Ferdinand Wambali kuwa Mwenyekiti mpya wa Tawi hilo baada ya kupata kura 31 sawa na asilimia    58.5 ya kura halali zilizopigwa dhidi ya mgombea mwenza Mhe. Dkt. Yose Mlyambina ambaye alipata jumla ya kura 22 sawa na asilimia   41.51 ya kura zote zilizopigwa.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Wambali amesema kuwa, ni vema wanachama wote wa tawi hilo kushirikiana ili kufika mbali na kuendelea kulifanya tawi hilo kuwa mfano kwa matawi mengine ya TMJA kama ilivyo sasa, huku akiwahakikishia wajumbe na wananchama wa Tawi hilo, kupata ushirikiano wake katika kila hatua.

Kwa upande wake, aliyekuwa Mgombea Mwenza katika kinyang’anyiro cha kumpata Mwenyekiti mpya wa Tawi hilo, Mhe. Dkt. Mlyambina amempongeza Mhe. Wambali kwa ushindi alioupata.

Kabla ya zoezi la kupiga kura na kumpata Mwenyekiti Mpya wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, kikao kiliongozwa na Mlezi wa Tawi hilo Mhe. Augustine Mwarija kama Mwenyekiti akiwa pamoja na Makamu Mwenyekiti wa TMJA Tawi hilo, Mhe. Charles Magesa pamoja na Katibu wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Adelina Nyamizi.

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na Mwenyekiti mpya wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Ferdinand Wambali akitoa neno mara baada ya kuchaguliwa kushika kiti hicho leo tarehe 14 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Wa pili kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mlezi wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Augustine Mwarija, wa kwanza kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Charles Magesa na wa kwanza kulia ni Katibu wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Adelina Nyamizi.

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na Mwenyekiti mpya wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Ferdinand Wambali akitoa neno mara baada ya kuchaguliwa kushika kiti hicho leo tarehe 14 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.


Sehemu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ambao ni Wanachama wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) Tawi la Mahakama hiyo wakifuatilia yanayojiri katika kikao chao kilichofanyika leo tarehe 14 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Katibu wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Adelina Nyamizi akiwasilisha taarifa wakati wa kikao kilichofanyika leo tarehe 14 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Sehemu ya Wasajili/ Naibu Wasajili na Wasaidizi wa Sheria wa Majaji wa Mahakama ya Rufani ambao ni Wanachama wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) Tawi la Mahakama ya Rufani wakifuatilia yanayojiri katika kikao cha Chama hicho kilichofanyika leo tarehe 14 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Makamu Mwenyekiti wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Charles Magesa akizungumza jambo wakati wa kikao cha TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani kilichofanyika leo tarehe 14 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na Mwenyekiti mpya wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Ferdinand Wambali (wa pili kulia) akiongoza kikao cha tawi hilo kilichofanyika leo tarehe 14 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Wa pili kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mlezi wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Augustine Mwarija, wa kwanza kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Charles Magesa na wa kwanza kulia ni Katibu wa TMJA Tawi la Mahakama ya Rufani, Mhe. Adelina Nyamizi.


(Picha na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)









MAHAKAMA KIGOMA YAKUTANA NA WADAU KUWEKA MIKAKATI YA KUMALIZA MASHAURI YA MAUAJI

Na AIDAN ROBERT, Mahakama-Kigoma

Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma imefanya kikao maalum cha maandalizi (pre-session) kilichoongozwa na Jaji wa Kanda hiyo, Mhe. John Francis Nkwabi kwa lengo la kuweka mikakati madhubuti ya kumaliza mashauri nane ya mauaji yaliyopangwa kusikilizwa Wilayani Kasulu mkoani humo tarehe 21 Septemba, 2026.

Katika kikao hicho kilichofanyika tarehe 11 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu Kigoma kiliwaunganisha wajumbe wa haki jinai kwa njia Mahakama Mtandao (Virtual Court) ambapo Mhe. Nkwabi aliwakumbusha wadau wote kutimiza wajibu wao kwa uadilifu mkubwa ili wananchi waweze kuona na kupata haki kwa mapema ipasavyo.

Jaji Nkwabi alisema, hatua hiyo itasaidia kuimarisha amani na usalama katika jamii, na kueleza kuwa, ratiba maalum ya usikilizwaji wa mashauri hayo nane imepangwa kwa umakini ili kuzuia kuahirishwa kwa mashauri bila sababu za msingi.

Naye Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa aliwashukuru Wadau kwa ushiriki wao na ushirikiano mkubwa waliotoa kwa Mahakama ili kuendelea kutimiza majukumu yake ya kusikiliza mashauri.

Kwa upande wake Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Bw. Yusufu Kasuka ameahidi juu ya uwepo wa vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa ajili ya kurahisisha usikilizwaji wa mashauri hayo ikiwa ni sambamba na kutoa uwezesho kwa watumishi na Mawakili upande wa utetezi katika mashauri hayo.

Aidha, Wadau walikubaliana kuimarisha mawasiliano na ushirikiano wa karibu na Mahakama, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na upande wa utetezi ili kuhakikisha ushahidi na vielelezo vinawasilishwa kwa wakati.

Kikao kilisisitiza kuhusu umuhimu wa kutumia kikamilifu vikao vya maandalizi ili kupunguza muda unaotumika mahakamani na kuharakisha usikilizwaji wa mashauri ya jinai, hasa ya mauaji.

Kikao hicho kilichowahusisha Waendesha Mashtaka wa Serikali, Mawakili wa utetezi na Maofisa Magereza na Polisi kililenga kuondoa vikwazo vyote vya kiutawala na kiufundi vinavyoweza kuchelewesha mwenendo wa mashauri hayo, na hivyo kuhakikisha haki inatendeka mapema ipasavyo.

 


Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. John Nkwabi (katikati) akiongoza kikao cha pamoja na Wadau wa Mahakama Kigoma. Aliyeketi kushoto ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa, kulia ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Bw. Yusufu Kasuka, wakifuatilia kwa makini hoja za wadau walizokuwa wakitoa kupitia Mahakama Mtandao wakati wa kikao kilichofanyika tarehe 11 Septemba, 2026.


Wajumbe wa Kikao  cha Tathmini ya maandalizi ya kikao cha mashauri ya mauaji waliojiunga kwenye kikao kwa njia ya Mahakama Mtandao wakiwa katika Taasisi zao. Kikao hicho kilifanyika tarehe 11 Septemba, 2026.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. John Francis Nkwabi akisikiliza kwa makini Mdau wa Haki Jinai alipokuwa akiwasilisha mchango wake kwenye kikao cha tathmini ya maandalizi ya kikao cha mashauri ya mauaji kilichofanyika tarehe 11 Septemba, 2026.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa akifafanua jambo wakati wa kikao cha tathmini ya maandalizi ya kikao cha mashauri ya mauaji mkoani humo.

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Bw. Yusufu Kasuka akifuatilia kwa makini mjadala uliokuwa ukiendelea kwenye kikao cha tathmini ya maandalizi ya kikao cha mashauri ya mauaji.


(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)



 

 

Ijumaa, 11 Septemba 2026

JAJI KAKOLAKI ASISITIZA UMUHIMU WA MAZOEZI KWA WATUMISHI

Na FRANCISCA SWAI – Mahakama, Musoma

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Musoma, Mhe. Edwin Kakolaki, amezindua rasmi utaratibu wa mazoezi kwa watumishi wa Mahakama Musoma kwa kuwasisitiza kuzingatia utaratibu wa mazoezi ya mara kwa mara, kwani mazoezi ni afya, ajira, furaha na ushirikiano.

Katika uzinduzi huo, Mhe. Kakolak, amewashukuru viongozi wa Mahakama Sports Club Musoma kwa kuonesha umahiri wao katika kusisitiza na kufuatilia suala hili.

Aidha, ametoa rai kwa viongozi na watumishi kuhakikisha utaratibu huu wa mazoezi haupotei, bali uwe endelevu kwa ajili ya  kuimarisha afya za watumishi ili waweze kufanya kazi zao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji.

Aidha, viongozi wa Mahakama Sports Cub Musoma waliwasilisha taarifa yao iliyowashukuru viongozi chini ya mlezi wao, ambaye ni Mtendaji wa Mahakama Musoma Bw. Leonard Maufi, kwa kuwaunga mkono kutafuta Mwalimu wa Mazoezi na kusisitiza utaratibu huu wa mazoezi kwa watumishi kuwa endelevu.

Pamoja na shukrani hizo, walieleza mikakati mbalimbali ya michezo waliyojiwekea ikiwa ni pamoja na kuandaa bonanza la michezo litakalohusisha Mahakama za jirani pamoja na wadau mbalimbali wa Mahakama.

Uzinduzi wa program hii ya mazoezi umefanyika baada ya kuona faida za mazoezi kwa watumishi wa Mahakama Kuu Musoma ambao wamekuwa wakifanya mazoezi ya pamoja kila siku ya Jumanne na Alhamisi jioni.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Musoma, Mhe. Edwin Kakolaki (mwenye kofia), na mbele yake ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Musoma, Bw. Leonard Maufi, wakiwa katika mazoezi yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mahakama Kuu Musoma.

Watumishi wa Mahakama wakiendelea na mazoezi yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mahakama Kuu Musoma.

Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Tarime wakiwa katika mazoezi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Musoma, Mhe. Edwin Kakolaki (katikati), akiwa pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Marlin Komba (kulia) na Mhe. Kamazima Idd (kushoto) wakati akiongea na watumishi (hawapo pichani) waliohudhuria uzinduzi rasmi wa mazoezi.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam.

GEREZA KONGWE LA NGWALA SONGWE LAPOKEA VIFAA VYA TEHAMA

Na IMAN MZUMBWE - Mahakama, Songwe

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Songwe Mhe. Abubakar Amin Mrisha amefanya ziara ya ukaguzi katika Gereza la Ngwala lililopo katika Wilaya ya Songwe mkoani Songwe.

Ziara hiyo iliambatana na tukio la kukabidhi vifaa vya TEHAMA kama vile Televisheni na Kamera kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa huduma za Mahakama Mtandao ili kurahishisha upatikanaji wa haki kwa wakati mapema ipasavyo kwa Wafungwa na Mahabusu wanaohifadhiwa mahala hapo.

Aidha, Ukaguzi huo unatokana na utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Malata alipofanya ziara katika Gereza hilo miezi miwili iliyopita na kubaini changamoto ya usafiri kwa wafungwa na mahabusu kutoka gerezani kwenda mahakamani kwa ajili ya usikilizwaji wa mashauri yao.

“Tumekuja kukabidhi vifaa vitavyosaidia kuweza kutatua changamoto ya usafiri kwa wafungwa na mahabusu kutoka gerezani kwenda mahakamani kupitia matumizi ya vifaa vya TEHAMA maarufu kama Mahakama mtandao,” alisema Mhe. Mrisha.

Mhe. Mrisha alisema kuwa, matumizi ya Mahakama mtandao ni hatua muhimu katika kuboresha utoaji huduma kwa wakati kwani teknolojia hiyo itawezesha baadhi ya taratibu za kimahakama kufanyika kwa njia ya mtandao bila ulazima wa wafungwa na mahabusu kusafirishwa kila mara kutoka gerezani kwenda mahakamani.

Kwa upande, Afisa wa Magereza SP Kassim Akalama alisema kwamba, vifaa hivyo vitasaidia kwa kiasi kikubwa usikilizwaji wa mashauri ya wafungwa na mahabusu pamoja na gharama zingine zinazotumika katika kuwasafirisha kutoka gerezani kwenda mahakamani. 

SP Akalama alisema kwamba, Jeshi la Magereza limepokea vifaa hivyo TEHAMA na vitatumika kama ilivyokusudiwa, hatua hii ni muhimu kwani itasaidia kuboresha huduma za utoaji haki kwa wafungwa na mahabusu na kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati mapema ipasavyo alisema afisa huyo wa magereza.

Ziara hiyo ya kutembele na kukagua gereza hilo ni mwendelezo wa juhudi za Mahakama ya Tanzania katika kuimarisha utendaji kazi wa Jeshi la Magereza, huku matumizi ya TEHAMA yakitarajiwa kuwa nyenzo muhimu katika kupunguza changamoto za utoaji haki kwa wafungwa na mahabusu.



WATUMISHI MAHAKAMA MANYARA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO GEITA

Na DOTTO NKAJA-Mahakama, Geita

Katika kuendelea kuimarisha ufanisi wa utendaji kazi na kuboresha utoaji wa haki nchini, watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Manyara, wamefanya ziara ya mafunzo na kubadilishana uzoefu katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Geita.

Ziara hiyo iliyofanyika Septemba 7 na 8, 2026, imelenga kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika uratibu na uendeshaji wa mashauri, pamoja na shughuli za kiutawala.

Ujumbe wa Mahakama Manyara uliongozwa na Jaji Mfawidhi, Mhe. Dkt. Adam Mambi na ulihusisha Naibu Wasajili, Mtendaji, Hakimu, Maafisa Rasilimali Watu na Utawala, Mkaguzi wa Ndani, Madereva pamoja na watumishi wengine kutoka vituo mbalimbali vya Masjala hiyo.

Akizungumza wakati wa kuupokea ujumbe huo katika Ukumbi wa Mafunzo wa Mahakama Kuu Geita, Jaji Mfawidhi, Mhe. Projestus Kahyoza, aliwakaribisha na kuwapongeza viongozi na watumishi wa Manyara kwa kuichagua Geita kuwa kituo cha kujifunza na kubadilishana uzoefu.

“Tunawakaribisha sana ndugu zetu kutoka Manyara. Hapa ni mahali sahihi kwenu kujifunza. Tumekuwa tukiwezesha Mahakama kutoka maeneo mbalimbali kupata mafunzo na kubadilishana uzoefu katika masuala ya TEHAMA kwa lengo la kuboresha utoaji wa haki. Nanyi mtajifunza kutoka kwetu na sisi pia tutajifunza kutoka kwenu,” alisema Mhe. Kahyoza.

Kwa upande wake, Mhe. Dkt. Mambi aliipongeza Mahakama Kuu Geita kwa mapokezi mazuri na kueleza kuwa mafanikio yaliyopatikana katika matumizi ya TEHAMA ndiyo yaliyowavutia kufanya ziara hiyo.

“Tumesikia mambo mazuri ambayo Wanageita mnayafanya katika mapinduzi ya matumizi ya TEHAMA. Hivyo, tukaona ni vema tufike tujifunze kutoka kwenu na pia tushirikiane uzoefu wa Masjala zetu ili tuboreshe utendaji wetu wa kila siku,” alisema Mhe. Dkt. Mambi.

Katika ziara hiyo, watumishi wa Mahakama Kuu Geita, waliwasilisha mada mbalimbali kuhusu matumizi ya TEHAMA katika shughuli za kimahakama na kiutawala.

Miongoni mwa mada zilizowasilishwa ni matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa mashauri, unaowezesha uendeshaji wa mashauri kwa njia ya kielektroniki bila kutegemea matumizi ya karatasi. Mada hiyo iliwasilishwa na Naibu Msajili wa Masjala Ndogo Geita, Mhe. Fredrick Lukuna.

Washiriki pia walijifunza namna Mahakama za Wilaya zinavyotumia mifumo ya TEHAMA katika kutekeleza shughuli za kimahakama na kiutawala, pamoja na hatua zinazochukuliwa na Mahakama za Mwanzo katika kupunguza matumizi ya karatasi, kupitia mfumo wa Mahakama za Mwanzo Electronic Register.

Aidha, washiriki walipata fursa ya kujifunza namna huduma ya Kiosk inavyofanya kazi kwa kuwasaidia wananchi ambao hawana uelewa wa kutosha kuhusu matumizi ya TEHAMA ili waweze kupata huduma za kimahakama kwa urahisi. Mada hiyo iliwasilishwa na Afisa Kumbukumbu, Bi. Winfrida Warsha.

Kwa upande wa shughuli za kiutawala, Mtendaji wa Mahakama Geita, Bi. Masalu Kisasila, aliwasilisha mada kuhusu namna Mahakama hiyo ilivyopunguza na kuachana na matumizi ya karatasi katika shughuli mbalimbali za kiutawala kupitia matumizi ya mifumo ya kielektroniki.

Naye Afisa TEHAMA, Bw. Dotto Nkaja, aliwasilisha mifumo mbalimbali iliyobuniwa na Mahakama Geita kwa lengo la kurahisisha upatikanaji, uhifadhi na matumizi ya taarifa za kimahakama. Mifumo hiyo ni pamoja na Geita Repository Database, Geita Electronic Visitors na Geita Legal Decisions.

Katika kuendeleza mafunzo hayo, Septemba 8, 2026, Mhe. Dkt. Mambi, aliwasilisha mada kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa, ikiwemo Akili Bandia (Artificial Intelligence – AI), katika kufanya tafiti za kimahakama pamoja na maadili yanayopaswa kuzingatiwa katika matumizi ya AI wakati wa tafiti na uratibu wa mashauri mahakamani.

Mada hiyo iliwapa washiriki fursa ya kutafakari namna teknolojia mpya zinavyoweza kutumika kuongeza ufanisi katika shughuli za Mahakama, huku wakizingatia misingi ya maadili na utoaji wa haki.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya ujumbe huo, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Manyara, Mhe. Charles Mnzava, aliwapongeza watumishi wa Geita kwa bidii na weledi wao, akieleza kuwa juhudi hizo zimechangia kuboresha utendaji kazi na kupunguza mlundikano wa mashauri.

“Kwa kweli tumeona jitihada zenu katika usikilizwaji wa mashauri ya kila siku, lakini pia katika usimamizi wa rasilimali. Tunaahidi kutumia elimu tuliyoipata katika kuboresha utendaji wetu tutakaporejea Manyara,” alisema Mhe. Mnzava.

Ziara hiyo imehitimishwa kwa viongozi wa Masjala hizo mbili kuweka mikakati ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati yao, ikiwemo kuanzisha utaratibu wa kuwa Kanda Rafiki katika masuala ya kikazi, kijamii na kiutawala.

Aidha, Uongozi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Geita, umeahidi kufanya ziara ya kimafunzo katika Mkoa wa Manyara hivi karibuni. Hatua hiyo inatarajiwa kuendeleza na kuimarisha utamaduni wa kujifunza, kushirikishana uzoefu na kubadilishana mbinu bora za utendaji kazi ndani ya Mahakama.

Ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika Mahakama na kuhakikisha teknolojia inatumika ipasavyo katika kuongeza ufanisi, kurahisisha upatikanaji wa huduma za haki na kuboresha utoaji wa haki kwa wananchi.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Geita, Mhe. Projestus Kahyoza, akiwakaribisha wageni kutoka Masjala Ndogo Manyara.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Manyara, Mhe. Dkt. Adam Mambi, akitoa elimu kwa watumishi waliohudhuria mafunzo katika Ukumbi wa Mafunzo wa Mahakama Kuu Geita, huku wengine wakishiriki kwa njia ya mtandao (Video Conference), kuhusu matumizi ya Kanuni za Ushahidi wa Kielektroniki pamoja na sheria zinazohusu matumizi sahihi ya Akili Mnemba (Artificial Intelligence – AI).



Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Geita, Mhe. Fredrick Lukuna, akieleza namna Mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi wa Mashauri unavyorahisisha usikilizaji na uendeshaji wa mashauri, pamoja na kupunguza matumizi ya karatasi mahakamani.

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Geita, Bi. Masalu Kisasila, akielezea namna matumizi ya TEHAMA yanavyorahisisha na kuboresha utekelezaji wa shughuli za kiutawala Mahakamani.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Manyara, Mhe. Charles Mnzava, akitoa shukrani baada ya kukamilika kwa mafunzo.

Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Geita, Mhe. Projestus Kahyoza (kulia) na Mhe. Griffin Mwakapeje (kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Manyara, Mhe. Dkt. Adam Mambi.


Picha ya pamoja ya viongozi na watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo za Geita na Manyara, katika Jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Geita.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam.

Alhamisi, 10 Septemba 2026

JAJI MWENEMPAZI AMUAPISHA OFISA USULUHISHI NA UAMUZI

Na SHARIFU MOKIWA - Mahakama Sumbawanga

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Sumbawanga Mhe. Thadeo Mwenempazi, amemuapisha Bw. Ayubu Joseph Mniko kuwa Msuluhishi na Muamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) Mkoa wa Rukwa.

Uapisho huo umefanyika tarehe 9 Septemba, 2026, katika Ofisi ya Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Sumbawanga na kuhudhuriwa na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Sumbawanga, Mhe. Pamela Mazengo, pamoja na Afisa Mfawidhi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Mkoa wa Rukwa Bi. Salome Kamwela.

Akizungumza baada ya kumuapisha Bw. Mniko, Mhe. Mwenempazi amesema anatarajia kwamba, katika utekelezaji wa majukumu yake atatenda haki bila upendeleo na kuhakikisha haki inatolewa kwa wakati mapema ipasavyo.

Mhe. Mwenempazi amemtaka Bw. Mniko kujipanga na kuwa tayari katika kutekeleza majukumu yake, akisisitiza umuhimu wa kuwa na utayari wa kuwaelewesha wananchi pale wanapokuwa hawajaelewa masuala mbalimbali yanayohusu majukumu yake ili kuepusha malalamiko na minong’ono inayoweza kujitokeza kutokana na kutokuelewana kwa wadaawa.

“Anatakiwa kutenda haki, kutokuwa na upendeleo na kutoa haki kwa wakati. Pia anatakiwa kujipanga na kuwa tayari kwa kuwa wakati mwingine watu hawajui, hivyo asione shida kumuelewesha mtu ili kuepusha minong’ono,” amesema Mhe. Mwenempazi.

Kwa upande wake, Bw. Mniko amesema kipaumbele chake katika kutekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo ni kuhakikisha anatimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria na kutenda haki.

“Nitahakikisha natimiza majukumu yangu kama sheria inavyonitaka na kutenda haki,” amesema Bw. Mniko.

Uapisho huo ni sehemu ya taratibu za kumuwezesha Bw. Mniko kuanza kutekeleza majukumu yake katika nafasi ya Msuluhishi na Muamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) Mkoa wa Rukwa, kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazotawala utekelezaji wa majukumu hayo.






Jumatano, 9 Septemba 2026

JAJI MFAWIDHI SINGIDA AWAHIMIZA WATUMISHI KUISHI KWA UPENDO, USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO

·       Awataka Watumishi kutooneana wivu, kuinuana na kupendana

Na EVA LESHANGE & AMIRI BAKARI, Mahakama - Singida

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda amewataka Watumishi wa Mahakama mkoani humo kutooneana wivu na kufanyiana hujuma badala yake wadumishe ushirikiano, upendo na mshikamano mahali pa kazi ili kuongeza ufanisi katika utoaji haki kwa wananchi.

Mhe. Mwenda aliyasema hayo tarehe 07 Septemba, 2026 alipokuwa wilayani Manyoni katika ziara yake ya ukaguzi wa shughuli za Mahakama kwa robo ya kwanza mkoani Singida. Ziara hiyo ilianzia katika Mahakama za Mwanzo za Mwamagembe, Rungwa na Mgandu zilizopo Wilaya ya Manyoni na kumalizia kwenye Mahakama ya Wilaya Manyoni.

Akizungumzia msingi wa utendaji kazi mwema, Jaji Mwenda alisema kuwa, ushirikiano wa dhati na kupendana ndiyo nguzo kuu inayowafanya watumishi kufanya makubwa hata pale wanapokuwa wachache.

"Acheni kuoneana wivu, ombeaneni mema, pendaneni na hamasishaneni na msifanyiane hujuma. Kila mmoja amsapoti mwenzake," alisisitiza Jaji Mfawidhi huyo.

Mhe. Mwenda aliongeza kuwa, mshikamano huo unapaswa kuonekana baina ya ngazi zote za Uongozi na Watumishi wa kawaida, na kusisitiza kwa kusema, "tusaidiane, wa chini amsaidie bosi wake azidi kupanda, na bosi pia awasaidie wa chini yake wazidi kupanda."

Akitoa pongezi kwa watumishi wa Mahakama alizotembelea, Jaji Mfawidhi huyo alisema, "nichukue nafasi hii kuwapongeza Mahakimu na Watumishi wote kwa kufanya kazi kwa ushirikiano bila kujali uchache wenu. Pamoja na uchache wenu, ni vema tukafanya kazi kwa weledi, kujituma, kuwajibika na kuhakikisha haki inapatikana kwa wananchi mapema ipasavyo kwani ndio lengo kuu la Mahakama."

Katika ziara hiyo, Mhe. Mwenda alieleza kwamba, kipimo halisi cha utendaji kazi mzuri kinatokana na mrejesho (feedback) kutoka kwa Wadau wa Mahakama, hususan Jeshi la Magereza (Wafungwa na Mahabusu) pamoja na Mkuu wa Wilaya. Alieleza kuwa, alipita kwa Mkuu wa Wilaya ya Manyoni na kupata mrejesho chanya kuhusu utendaji kazi wa Mahakama hizo.

Ili kuendelea kuimarisha imani ya wananchi kwa Mahakama, Jaji Mwenda aliwataka watumishi hao kuongeza kasi ya usikilizaji wa mashauri bila kuvunja sheria na miongozo, na kuweka mikakati thabiti ya kuondoa mlundikano wa mashauri (case backlog).

Mbali na kuzungumza na watumishi, Mhe. Mwenda alitembelea Mradi wa Ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Rungwa unaoendelea tangu mwaka 2024 ambapo alipata wasaa wa kuzungumza na Mkandarasi Emmanuel Mchaki na kubaini changamoto zinazochelewesha mradi huo kuwa, ni pamoja na upatikanaji wa vifaa, na nguvu kazi.

Mkandarasi wa Mradi huo alisema kuwa, ameshafikia zaidi ya asilimia 40 ya ujenzi huo na ameahidi kumaliza ujenzi huo kwani kwa kiwango kikubwa vifaa (materials) tayari vipo eneo la mradi huo.

Jaji Mwenda alimshauri Mkandarasi kutumia nguvu kazi kutoka maeneo ya jirani na mradi ili kuimarisha uhusiano mwema kati ya jamii na Mahakama.

Ziara hiyo ya ukaguzi inatarajiwa kuendelea katika Mahakama za Wilaya za Iramba, Mkalama pamoja na Mahakama zake za Mwanzo na Mahakama ya Wilaya Singida pamoja na Mahakama zake za Mwanzo pamoja na Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda akipokelewa na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni alipowasili katika Mahakama hiyo tarehe 07 Septemba, 2026 kwa ziara ya kikazi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (katikati) akizungumza na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni (hawapo katika picha) alipokuwa katika ziara ya kikazi. Kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Jasmine Abdul na kushoto ni Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Manyoni, Mhe. Alisile Mwankejela.

Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni wakifuatilia kikao kilichokuwa kikiendelea kwenye Ukumbi wa Mahakama ya Wilaya ya Manyoni tarehe 07 Septemba, 2026.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni mara baada ya kufanya Ukaguzi katika Mahakama hiyo. Wa kwanza kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Bw. Filbert Matotay, wa pili kushoto ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Jasmine Abdul na wa kwanza kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Manyoni, Mhe. Alisile Mwankejela.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (aliyevaa tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Haki Jinai alioambatana nao kukagua Gereza la Mahakama ya Wilaya Singida.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (wa kwanza kushoto) akiongoza ukaguzi Mradi wa Ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Rungwa. Wa pili kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Bw. Filbert Matotay, akifuatiwa na Mkandarasi wa Mradi huo pamoja na Viongozi wengine walioambatana na Jaji Mfawidhi wakati wa ukaguzi wa Mradi huo.

 Muonekano wa Jengo la Mahakama ya Mwanzo Rungwa lililopo katika Wilaya ya Manyoni linaloendelea na ujenzi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda akitoa ushauri kwa mkandarasi katika mradi wa mahakama ya mwanzo  Rungwa katika wilaya ya Manyoni.

  Picha ya baada ya ukaguzi. Wa nne kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda, wa nne kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Jasmine Abdul, wa tatu kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Bw. Filbert Matotay, wa pili kushoto ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni, Mhe. Alisile Mwankejela, wa pili kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mwanzo Rungwa, Mhe. David Deogratias, wa kwanza kulia ni Mkandarasi wa Jengo la Mahakama ya Mwanzo Rungwa, Mhandisi Emmanuel Mchaki,  wa tatu kulia ni Katibu wa Jaji, Mhe. Mariam Hamis, wa kwanza kushoto ni Ofisa Utumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni, Bi. Anna Kisambale. 


(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)

 

 

 

 


 





 


 

TANZANIA JUDICIARY JUDGES, LABOUR JUSTICE STAKEHOLDERS IN SOUTH AFRICA FOR BENCHMARKING

  • To exchange judicial experiences, strengthen collective commitment in labour justice administration

By FAUSTINE KAPAMA-Judiciary, monitoring from Dodoma

THIRTEEN members of Judiciary of Tanzania and Labour Justice Stakeholders are in South Africa for benchmarking visit aimed at exchanging judicial experiences and strengthening collective commitment to the administration of labour justice, the rule of law and the protection of the rights and dignity of those who seek justice.

Justice of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. Dr. Yose Mlyambina, is leading the delegation, which also comprises the Principal Judge of the High Court of Tanzania, Hon. Dr. Mustapher Mohamed Siyani and three judges from the High Court of Tanzania, Labour Division, among others.

In his address on official benchmark visit, Justice Mlyambina told Judge President of the Labour Court and Labour Appeal Court, Hon. Mogomotsi Edwin Molahlehi, and other officials that the diplomatic and historical relations between the United Republic of Tanzania and the Republic of South Africa are deeply rooted.

He explained that the diplomatic and historical relations were founded and nurtured by the two countries’ founding fathers, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere and Nelson Rolihlahla Mandela.

“Under the leadership of Mwalimu Nyerere, Tanzania opened its doors to freedom fighters and hosted the offices of liberation movements, including the African National Congress and the Pan Africanist Congress, following our independence in the 1960s,” Dr. Mlyambina said.

In doing so, he said, Tanzania helped to cement a relationship between the two countries founded upon shared values of freedom, justice, human dignity and solidarity.

According to him, Mwalimu Nyerere understood that Tanzania's independence could not be complete while other African nations remained under colonial rule or apartheid and that, that spirit of solidarity helped to lay a foundation upon which the two countries have continued to build.

“Today, we are privileged to continue that noble tradition not on the battlefield of liberation, but through the rule of law, the administration of justice and the strengthening of our respective Judiciaries,” he said.

Justice Mlyambina explained further that the Tanzania delegation decided to have the benchmarking visit in order to understand how South Africa legal framework has evolved through the jurisprudence of Courts and judicial interpretation and how legislation and institutions have responded to changing times and emerging challenges in labour relations.

He said that as Member States of the Southern African Development Community (SADC), their engagement was of particular importance as the shared aspiration is to promote greater coherence and, where appropriate, harmonisation of labour laws consistent with International Labour Organization standards and guidelines.

Such cooperation, Dr. Mlyambina said, can facilitate trade and investment, promote decent work, uphold the dignity of workers and strengthen social justice throughout our region.

“We are particularly keen to learn from South Africa's experience in addressing emerging forms of employment and the changing world of work, including the rapidly developing field of the platform economy…

“The growth of digital labour platforms, app-based work and other non-traditional forms of employment presents new challenges concerning employment status, minimum labour standards, social protection, collective bargaining, occupational safety and health and access to labour justice,” he said.

He said that they would, therefore, be particularly interested in understanding how South Africa has responded, both legislatively and judicially, to the emerging forms of work and how questions of employee or worker status have been determined.

The delegations would also want to know whether platform workers have been afforded protection under existing labour legislation and how the Courts and the CCMA have balanced technological innovation and business flexibility with the constitutional and statutory imperatives of decent work, fair labour practices and social justice.

“These are matters of growing importance not only to the United Republic of Tanzania, but also to the wider SADC region. Your experience will therefore be invaluable as we consider how our own legal and institutional framework should respond to the future of work,” said Justice Mlyambina.

During the session, the head of delegation also conveyed the warmest judicial and diplomatic greetings of the Chief Justice of the United Republic of Tanzania, His Lordship George Masaju, to the Judge President of the Industrial Court and Labour Appeals Court of Republic of South Africa.

“His Lordship has asked me to convey his sincere regards and his profound appreciation for the cordial and longstanding relations between our two Judiciaries…

“He attaches great importance to the continued strengthening of judicial cooperation between the United Republic of Tanzania and the Republic of South Africa and regards the exchange of judicial knowledge and experience as an important means through which our institutions can learn from one another and collectively strengthen the administration of justice,” Dr. Mlyambina said.

Other members of the Tanzania delegation to the benchmarking visit to to the Labour Appeal Court, Labour Court and Commission for Conciliation Mediation and Arbitration of South Africa (CCMA), includes Presiding Judge-in-Charge of the High Court of Tanzania, Labour Division, Hon. Dr. Ntemi Kilekamajenga and two other Judges from the same court, Dr. Modesta Opiyo and Nehemia Mandia.

The rest are Deputy Registrar of the High Court of Tanzania Labour Division, Hon. Cassian Matembele, Deputy Registrar of the High Court of Tanzania, Hon. Mussa Ahmed Hamza, Court Administrator of the High Court of Tanzania, Labour Division, Ms. Joyce Mulugu and the Director of the Commission for Mediation and Arbitration (CMA) of Tanzania, Hon. Usekelege Mpullah.

In the same boat are two Tanzanian labour justice stakeholders, Mr. Christian Chiduga, Litigation Services Manager at the Tanzania Ports Authority and Ms. Comfort Laizer, who is Senior Legal Officer at the Tanzania Ports Authority. The delegation is accompanied by two Protocol Officers: Mr. Fadhili Mgutta and Ms. Janeth Makopolo.

As a gesture of appreciation and friendship, and as a token of the warm regards of His Lordship Chief Justice George Masaju, Justice Mlyambina presented on his behalf, a gift to the Judge President, as a symbol of gratitude, friendship and the enduring bonds between two Judiciaries.


Justice of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. Dr. Yose Mlyambina, stressing a point at a meeting duing the benchmarking visit in South Africa Judiciary.

Other members of the Tanzania delegation during the meeting. From right in above and below pictures is the Judge in Charge of the High Court Labourt Division, Hon. Dr. Ntemi Kilekamajenga, the Principal Judge of the High Court of Tanzania, Hon. Dr. Mustapher Mohamed Siyani and Justice of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. Dr. Yose Mlyambina. Extreme right in the above picture is Deputy Registrar of the High Court Labour Division, Hon. Cassian Matembele.



Judges of the High Court of Tanzania, Labour Division, Hon. Dr. Modesta Opiyo (above) and Hon. Nehemia Mandia (below) noting important points during the meeting.


Other members of the Tanzania delegation (above and two below pictures) following proceedings of the meeting.





The meeting is on.

Justice of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. Dr. Yose Mlyambina (left) and Principal Judge of the High Court of Tanzania, Hon. Dr. Mustapher Mohamed Siyani (right) present a gift to Judge President of the Labour Court and Labour Appeal Court, Hon. Mogomotsi Edwin Molahlehi on behalf of the Chief Justice of the United Republic of Tanzania, His Lordship George Masaju.


Two memorable pictures (above and below) comprising the Tanzania delegation and officials of the Judiciary of South Africa.


Picture by a Correspondent in South Africa.