Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Jaji
Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani
amewaongoza mamia ya waombolezaji katika ibada ya kumuaga na kumsindikiza katika nyumba yake ya milele Jaji
Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Marehemu Mhe. Kakusulo Mwakipome Mbutolwe
Sambo aliyefariki Dunia mnamo 26 Julai, 2026 jijini Dar es Salaam.
Ibada
hiyo ya kumuaga Marehemu Jaji Sambo ili kumpumzisha kwenye nyumba yake ya
milele imefanyika leo tarehe 31 Julai, 2026 nyumbani kwa marehemu kitongoji cha
Masebe wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya.
Akitoa
salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa, majirani na marafiki Mhe. Dkt. Siyani
amesema kuwa, maisha ya marehemu Jaji Sambo ni maisha ya mfano kwa aliowaacha
kwani aliyaishi maisha yake kama sehemu ya maandalizi ya maisha ambayo sasa
ameyaanza.
Jaji
Kiongozi amesema kwa wale wanaomjua marehemu Jaji Sambo alikuwa mtu muadilifu
mwenye hekima na imani ya Mwenyezi Mungu, na ndiyo maana Majaji na watu kutoka
sehemu mbalimbali wakiwemo aliofanya nao kazi na alioshirikiana nao katika
shughuli mbalimbali za kijamii wamesafiri kuja kumuaga na kumpumzisha katika
nyumba yake ya milele, hali hiyo inaonesha jinsi gani aliweza kuishi na watu
vizuri.
Aidha,
Mhe. Dkt. Siyani amesema kuwa, kwa upande wa Mahakama na tasnia ya Sheria kwa
ujumla, Mhe. Sambo alichangia kwa kiasi kikubwa katika kutafsiri sheria kupitia
maamuzi mbalimbali ambayo yataendelea kuwepo hata baada ya kuwa yeye
amepumzika.
Aliongeza
kuwa, maamuzi ambayo aliyatoa yameleta mchango ambao umewasaidia wengi kufahamu
haki na namna ambavyo wanaweza kuziendea mahakamani. Mhe Sambo alikuwa na
mchango mkubwa katika kuendeleza taaluma za wengine.
Mhe.
Dkt.Siyani alirejea salamu za rambirambi kutoka kwa mmoja wa wahadhiri wa chuo
kikuu cha Dar Es Salaam na kueleza namna ambavyo alimsaidia mhadhiri huyo
kukamilisha tafiti yake. Jambo hilo linaonesha namna ambavyo alifundisha wengi
na wengi wataendelea kumkumbuka.
Aidha,
Mhe. Dkt. Siyani amesema kwamba, pamoja na hadhi yake ya Ujaji, Mhe. Sambo
aliendelea kushikilia imani yake kwa Mungu na kushiriki katika shughuli
mbalimbali za kijamii wakati wa utumishi wake na hata baada ya kustaafu
utumishi alijishughulisha na kilimo na ufugaji akiwa Sumbawanga na hata mkoani Arusha.
“Madaraka
tunayopewa ni makoti na majoho, Maisha yetu rasmi yapo katika Jamii
inayotuzunguka hivyo hatupaswi kujitenga nayo,” alisema Jaji Kiongozi,
akisisitiza juu ya mafunzo yapatikanayo katika maisha ya Marehemu Jaji Kakusulo
Sambo.
“Nimepata
funzo kupitia maisha ya Jaji Sambo hakuwabagua watu waliomzunguka, alikuwa
anafikika na watu wote, alikwa tayari kupokea ushauri kutoka kwa mtu yoyote
hata walioko chini yake na aliwaunganisha watu akiwa hai lakini leo pia katika
kumuaga ametuunganisha pamoja watu wa imani tofauti,” amesisitiza Mhe. Dkt.
Siyani.
Jaji
Kiongozi alihitimisha kwa kusema kuwa, wanapata faraja wakiyakumbuka maneno ya
Mungu yasemayo, “Heri wafu wafao katika Bwana maana watapata kupumzika la
milele,”
Kwa
upande wake, Mchungaji Michael Bureta aliyeongoza Misa takatifu ya Ibada ya
maziko ya Marehemu Jaji Sambo alisema, “Ndugu yetu amelala katika kristo na ni
njia mbayo kila mmoja wetu atapita. Tuiombee familia ili iangalie jambo hili
katika imani na waendelee kumkumbuka kwa imani na sala wakati wote.”
Mchungaji
Bureta aliongeza kuwa, Marehemu alikuwa na mchango mkubwa sana katika Kanisa
alinunua vifaa mbalimbali vya Kanisa, kuwezesha safari za kikanisa ndani na nje
ya nchi na alikuwa Mfadhili wa Kwaya ya Kanisa hadi kuteuliwa mnamo mwaka 2023
kuwa Mwenyekiti wa kwaya ya “Nuru Angaza” kanisani kwake alipokuwa mkoani Arusha.
Naye,
Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mashtaka
Mkoa wa Mbeya alisema kuwa, msiba wa kuondokewa na Jaji Mstaafu, Marehemu Mhe. Sambo
umeacha pengo kubwa kwa watu ambao mpaka sasa walikuwa wanategemea huduma
kutoka kwake.
Marehemu Jaji Kakusulo Mwakipome Mbutolwe Sambo ameacha mjane mmoja, Watoto watano na Wajukuu 11 “BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE” AMEN.
Jaji
Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani akiaga
mwili wa marehemu Jaji Mstaafu Kakusulo Mwakipome Mbutolwe Sambo mara baada ya Ibada
Takatifu ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwa marehemu kitongoji cha Masebe wilayani
Rungwe Mkoa wa Mbeya, leo tarehe 31 Julai, 2026.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Ferdinand
Leons Katipwa Wambali akiaga mwili wa marehemu Jaji Mstaafu Kakusulo Mwakipome Mbutolwe
Sambo.
Jaji
Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (katikati),
akiwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Ferdinand
Leons Katipwa Wambali (wapili kushoto), na Majaji wengine wa Mahakama Kuu ya
Tanzania wakiwa kwenye mazishi ya marehemu Jaji Sambo. Walioketi
mbele (wa kwanza kushoto) ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala
Ndogo ya Iringa Mhe. Dustun Beda Ndunguru, Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu
Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Angaza Mwipopo (wa pili kulia) na (wa kwanza kulia)
ni Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Sumbawanga Mhe. Thadeo
Marco Mwenempazi.
Jaji
Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani akihutubia
waombolezaji katika mazishi hayo.
Msajili
wa Mahakama Kuu ya Tanzania kutoka Masjala Kuu Makao Makuu ya Mahakama Mhe.
Chiganga Mashauri Tengwa akifanya utambulisho wa Viongozi walioshiriki katika
mazishi hayo.
Sehemu ya Viongozi wa Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya
Rungwe wakiwa katika mazishi hayo
Kwaya ya Angaza nuru ikitumbuiza katika mazishi hayo,
kwaya ambayo Marehemu Jaji Sambo alikuwa Mwenyekiti wake.
Mwili wa Marehemu Jaji Mstaafu Sambo ukipumzishwa katika Nyumba
yake ya milele.
Sehemu ya mamia ya waombolezaji katika mazishi hayo.
Sehemu ya mamia ya waombolezaji katika mazishi hayo
Sehemu ya mamia ya waombolezaji katika mazishi hayo.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Ferdinand
Leons Katipwa Wambali akisaini Kitabu cha waombolezaji nyumbani kwa marehemu Jaji Mstaafu Kakusulo Mwakipome Mbutolwe
Sambo.
Sehemu ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania walioshiriki msiba huo wakiaga Mwili wa Marehemu Jaji Mstaafu Kakusulo Mwakipome Mbutolwe Sambo mara baada ya Ibada Takatifu ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwa marehemu kitongoji cha Masebe wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
.png)

.png)
.png)

.jpg)
.jpg)

.jpg)
.jpg)







