Na DHILLON UISSO-Mahakama, Dar es Salaam
Kituo Jumuishi cha Masuala ya FamiliaTemeke tarehe 28 Machi, 2026 kiliendesha
mafunzo maalum kwa wajane wa Wilaya ya Temeke kwa lengo la kuwajengea uelewa kwenye haki zao za kisheria, hususan katika
masuala ya urithi na mirathi.
Halikadhalika,
washiriki wa mafunzo hayo walipatiwa elimu ya kisheria
itakayowasaidia kulinda
haki zao na za watoto wao, kusimamia
mali za marehemu kwa mujibu wa sheria
na kuepuka
migogoro ya mirathi katika familia na jamii
Mafunzo hayo yalifunguliwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kituo Jumuishi Temeke,
Mhe. Mwanabaraka
Mnyukwa, ambaye alisisitiza umuhimu wa wajane kufahamu haki zao, kufungua
mirathi kwa wakati
na kutumia mifumo ya kisheria ili kuepusha migogoro ya kifamilia.
Mtandao wa Mashirika
yanayotoa Msaada wa Sheria Tanzania (TANLAP), uliowakilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa TANLAP, Wakili
Fransisca Silaya, ndiyo
uliofadhili mafunzo hayo.
Wakili
Silaya, akizungumza wakati wa mafunzo hayo, alionesha dhamira ya Taasisi hiyo kuendelea kuunga mkono
juhudi za utoaji wa elimu ya kisheria kwa makundi maalum katika jamii.
Mafunzo hayo yalijumuisha mada kuu nne
zilizowasilishwa na wakufunzi wenye uzoefu,
ikiwemo Urithi
na Mirathi na Sheria
za Urithi Tanzania zilizowasilishwa na Mhe. Magdalena Malaba.
Nyingine
ni Kufungua
Mirathi na Nyaraka Muhimu na Wosia
na Ulinzi wa Haki zilizowasilishwa na Mhe. Edna Mollel.
Katika mada hizo, washiriki walipata uelewa wa kina
kuhusu taratibu za mirathi, haki zao za kisheria, umuhimu wa nyaraka sahihi pamoja na namna ya kuandika wosia na
kulinda haki zao.
Mafunzo yalihusisha
wajane kutoka maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Temeke, wakiwemo wanachama wa
vikundi vya kijamii,
hususan kikundi cha VIWOTA Women Group.
Washiriki
walionesha hamasa kubwa ya kujifunza na kuchangia mijadala.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu Kituo Jumuishi Temeke, Bw. Samson Mashalla, alifunga mafunzo
hayo na kuwasihi washiriki wote kutumia maarifa waliyoyapata maarifa kwenye
maisha yao na kuwafikishia wengine elimu hiyo kwani ni nyenzo ya kujikomboa
dhidi ya dhuluma na kuhakikisha haki inatendeka.
“Napenda
pia kuwakumbusha kuwa taasisi zetu za haki, ikiwemo Kituo Jumuishi Temeke, zipo
kwa ajili yenu. Msisite kufika pale mnapohitaji msaada wa kisheria au ushauri,”
alisema.
Bw.
Mashalla alitumia fursa hiyo kuushukuru Mtandao wa Asasi za Msaada wa Sheria
Tanzania (TANLAP) kwa mchango wao katika kufanikisha mafunzo hayo, kwani mchango
wao umeleta mabadiliko chanya katika maisha ya washiriki.
Aliwashukuru pia wakufunzi kwa kujitolea kutoa maarifa na kwa uvumilivu wao katika kuhakikisha kila mshiriki anaelewa mada zilizowasilishwa. “Mafunzo haya yamekuwa ya manufaa makubwa na yamegusa moja kwa moja maisha yetu ya kila siku,” alisema.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia
Temeke, Mhe. Mwanabaraka Mnyukwa, akizungumza wakati anafungua mafunzo hayo (Picha na Maktaba).
Kaimu
Mkurugenzi wa Mtandao wa Asasi za Msaada wa Sheria Tanzania (TANLAP), Bi.
Fransisca Silaya.
Hakimu
Mkazi wa Mahakama ya Wilaya kwenye Kituo Jumuishi Temeke, Mhe. Magdalena Malaba,
akiwsilisha mada kwenye mafunzo hayo.
Hakimu
Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo kwenye Kituo Jumuishi Temeke, Mhe. Moleli, akiwasilisha
mada kwenye mafunzo hayo.
Washiriki
wa mafunzo wakifuatilia kilichokuwa kinajiri.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu Kituo Jumuishi Temeke, Bw. Samson Mashalla, akizungumza wakati
anahitimisha mafunzo hayo.
Picha
ya pamoja ya washiriki wakati wa mafunzo hayo.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.
















.jpg)



