Alhamisi, 10 Septemba 2026

JAJI MWENEMPAZI AMUAPISHA OFISA USULUHISHI NA UAMUZI

Na SHARIFU MOKIWA - Mahakama Sumbawanga

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Sumbawanga Mhe. Thadeo Mwenempazi, amemuapisha Bw. Ayubu Joseph Mniko kuwa Msuluhishi na Muamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) Mkoa wa Rukwa.

Uapisho huo umefanyika tarehe 9 Septemba, 2026, katika Ofisi ya Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Sumbawanga na kuhudhuriwa na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Sumbawanga, Mhe. Pamela Mazengo, pamoja na Afisa Mfawidhi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Mkoa wa Rukwa Bi. Salome Kamwela.

Akizungumza baada ya kumuapisha Bw. Mniko, Mhe. Mwenempazi amesema anatarajia kwamba, katika utekelezaji wa majukumu yake atatenda haki bila upendeleo na kuhakikisha haki inatolewa kwa wakati mapema ipasavyo.

Mhe. Mwenempazi amemtaka Bw. Mniko kujipanga na kuwa tayari katika kutekeleza majukumu yake, akisisitiza umuhimu wa kuwa na utayari wa kuwaelewesha wananchi pale wanapokuwa hawajaelewa masuala mbalimbali yanayohusu majukumu yake ili kuepusha malalamiko na minong’ono inayoweza kujitokeza kutokana na kutokuelewana kwa wadaawa.

“Anatakiwa kutenda haki, kutokuwa na upendeleo na kutoa haki kwa wakati. Pia anatakiwa kujipanga na kuwa tayari kwa kuwa wakati mwingine watu hawajui, hivyo asione shida kumuelewesha mtu ili kuepusha minong’ono,” amesema Mhe. Mwenempazi.

Kwa upande wake, Bw. Mniko amesema kipaumbele chake katika kutekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo ni kuhakikisha anatimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria na kutenda haki.

“Nitahakikisha natimiza majukumu yangu kama sheria inavyonitaka na kutenda haki,” amesema Bw. Mniko.

Uapisho huo ni sehemu ya taratibu za kumuwezesha Bw. Mniko kuanza kutekeleza majukumu yake katika nafasi ya Msuluhishi na Muamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) Mkoa wa Rukwa, kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazotawala utekelezaji wa majukumu hayo.





Jumatano, 9 Septemba 2026

JAJI MFAWIDHI SINGIDA AWAHIMIZA WATUMISHI KUISHI KWA UPENDO, USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO

·       Awataka Watumishi kutooneana wivu, kuinuana na kupendana

Na EVA LESHANGE & AMIRI BAKARI, Mahakama - Singida

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda amewataka Watumishi wa Mahakama mkoani humo kutooneana wivu na kufanyiana hujuma badala yake wadumishe ushirikiano, upendo na mshikamano mahali pa kazi ili kuongeza ufanisi katika utoaji haki kwa wananchi.

Mhe. Mwenda aliyasema hayo tarehe 07 Septemba, 2026 alipokuwa wilayani Manyoni katika ziara yake ya ukaguzi wa shughuli za Mahakama kwa robo ya kwanza mkoani Singida. Ziara hiyo ilianzia katika Mahakama za Mwanzo za Mwamagembe, Rungwa na Mgandu zilizopo Wilaya ya Manyoni na kumalizia kwenye Mahakama ya Wilaya Manyoni.

Akizungumzia msingi wa utendaji kazi mwema, Jaji Mwenda alisema kuwa, ushirikiano wa dhati na kupendana ndiyo nguzo kuu inayowafanya watumishi kufanya makubwa hata pale wanapokuwa wachache.

"Acheni kuoneana wivu, ombeaneni mema, pendaneni na hamasishaneni na msifanyiane hujuma. Kila mmoja amsapoti mwenzake," alisisitiza Jaji Mfawidhi huyo.

Mhe. Mwenda aliongeza kuwa, mshikamano huo unapaswa kuonekana baina ya ngazi zote za Uongozi na Watumishi wa kawaida, na kusisitiza kwa kusema, "tusaidiane, wa chini amsaidie bosi wake azidi kupanda, na bosi pia awasaidie wa chini yake wazidi kupanda."

Akitoa pongezi kwa watumishi wa Mahakama alizotembelea, Jaji Mfawidhi huyo alisema, "nichukue nafasi hii kuwapongeza Mahakimu na Watumishi wote kwa kufanya kazi kwa ushirikiano bila kujali uchache wenu. Pamoja na uchache wenu, ni vema tukafanya kazi kwa weledi, kujituma, kuwajibika na kuhakikisha haki inapatikana kwa wananchi mapema ipasavyo kwani ndio lengo kuu la Mahakama."

Katika ziara hiyo, Mhe. Mwenda alieleza kwamba, kipimo halisi cha utendaji kazi mzuri kinatokana na mrejesho (feedback) kutoka kwa Wadau wa Mahakama, hususan Jeshi la Magereza (Wafungwa na Mahabusu) pamoja na Mkuu wa Wilaya. Alieleza kuwa, alipita kwa Mkuu wa Wilaya ya Manyoni na kupata mrejesho chanya kuhusu utendaji kazi wa Mahakama hizo.

Ili kuendelea kuimarisha imani ya wananchi kwa Mahakama, Jaji Mwenda aliwataka watumishi hao kuongeza kasi ya usikilizaji wa mashauri bila kuvunja sheria na miongozo, na kuweka mikakati thabiti ya kuondoa mlundikano wa mashauri (case backlog).

Mbali na kuzungumza na watumishi, Mhe. Mwenda alitembelea Mradi wa Ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Rungwa unaoendelea tangu mwaka 2024 ambapo alipata wasaa wa kuzungumza na Mkandarasi Emmanuel Mchaki na kubaini changamoto zinazochelewesha mradi huo kuwa, ni pamoja na upatikanaji wa vifaa, na nguvu kazi.

Mkandarasi wa Mradi huo alisema kuwa, ameshafikia zaidi ya asilimia 40 ya ujenzi huo na ameahidi kumaliza ujenzi huo kwani kwa kiwango kikubwa vifaa (materials) tayari vipo eneo la mradi huo.

Jaji Mwenda alimshauri Mkandarasi kutumia nguvu kazi kutoka maeneo ya jirani na mradi ili kuimarisha uhusiano mwema kati ya jamii na Mahakama.

Ziara hiyo ya ukaguzi inatarajiwa kuendelea katika Mahakama za Wilaya za Iramba, Mkalama pamoja na Mahakama zake za Mwanzo na Mahakama ya Wilaya Singida pamoja na Mahakama zake za Mwanzo pamoja na Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda akipokelewa na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni alipowasili katika Mahakama hiyo tarehe 07 Septemba, 2026 kwa ziara ya kikazi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (katikati) akizungumza na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni (hawapo katika picha) alipokuwa katika ziara ya kikazi. Kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Jasmine Abdul na kushoto ni Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Manyoni, Mhe. Alisile Mwankejela.

Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni wakifuatilia kikao kilichokuwa kikiendelea kwenye Ukumbi wa Mahakama ya Wilaya ya Manyoni tarehe 07 Septemba, 2026.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni mara baada ya kufanya Ukaguzi katika Mahakama hiyo. Wa kwanza kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Bw. Filbert Matotay, wa pili kushoto ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Jasmine Abdul na wa kwanza kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Manyoni, Mhe. Alisile Mwankejela.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (aliyevaa tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Haki Jinai alioambatana nao kukagua Gereza la Mahakama ya Wilaya Singida.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (wa kwanza kushoto) akiongoza ukaguzi Mradi wa Ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Rungwa. Wa pili kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Bw. Filbert Matotay, akifuatiwa na Mkandarasi wa Mradi huo pamoja na Viongozi wengine walioambatana na Jaji Mfawidhi wakati wa ukaguzi wa Mradi huo.

 Muonekano wa Jengo la Mahakama ya Mwanzo Rungwa lililopo katika Wilaya ya Manyoni linaloendelea na ujenzi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda akitoa ushauri kwa mkandarasi katika mradi wa mahakama ya mwanzo  Rungwa katika wilaya ya Manyoni.

  Picha ya baada ya ukaguzi. Wa nne kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Ayoub Mwenda, wa nne kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Mhe. Jasmine Abdul, wa tatu kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Singida, Bw. Filbert Matotay, wa pili kushoto ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni, Mhe. Alisile Mwankejela, wa pili kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mwanzo Rungwa, Mhe. David Deogratias, wa kwanza kulia ni Mkandarasi wa Jengo la Mahakama ya Mwanzo Rungwa, Mhandisi Emmanuel Mchaki,  wa tatu kulia ni Katibu wa Jaji, Mhe. Mariam Hamis, wa kwanza kushoto ni Ofisa Utumishi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni, Bi. Anna Kisambale. 


(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)

 

 

 

 


 





 


 

TANZANIA JUDICIARY JUDGES, LABOUR JUSTICE STAKEHOLDERS IN SOUTH AFRICA FOR BENCHMARKING

  • To exchange judicial experiences, strengthen collective commitment in labour justice administration

By FAUSTINE KAPAMA-Judiciary, monitoring from Dodoma

THIRTEEN members of Judiciary of Tanzania and Labour Justice Stakeholders are in South Africa for benchmarking visit aimed at exchanging judicial experiences and strengthening collective commitment to the administration of labour justice, the rule of law and the protection of the rights and dignity of those who seek justice.

Justice of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. Dr. Yose Mlyambina, is leading the delegation, which also comprises the Principal Judge of the High Court of Tanzania, Hon. Dr. Mustapher Mohamed Siyani and three judges from the High Court of Tanzania, Labour Division, among others.

In his address on official benchmark visit, Justice Mlyambina told Judge President of the Labour Court and Labour Appeal Court, Hon. Mogomotsi Edwin Molahlehi, and other officials that the diplomatic and historical relations between the United Republic of Tanzania and the Republic of South Africa are deeply rooted.

He explained that the diplomatic and historical relations were founded and nurtured by the two countries’ founding fathers, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere and Nelson Rolihlahla Mandela.

“Under the leadership of Mwalimu Nyerere, Tanzania opened its doors to freedom fighters and hosted the offices of liberation movements, including the African National Congress and the Pan Africanist Congress, following our independence in the 1960s,” Dr. Mlyambina said.

In doing so, he said, Tanzania helped to cement a relationship between the two countries founded upon shared values of freedom, justice, human dignity and solidarity.

According to him, Mwalimu Nyerere understood that Tanzania's independence could not be complete while other African nations remained under colonial rule or apartheid and that, that spirit of solidarity helped to lay a foundation upon which the two countries have continued to build.

“Today, we are privileged to continue that noble tradition not on the battlefield of liberation, but through the rule of law, the administration of justice and the strengthening of our respective Judiciaries,” he said.

Justice Mlyambina explained further that the Tanzania delegation decided to have the benchmarking visit in order to understand how South Africa legal framework has evolved through the jurisprudence of Courts and judicial interpretation and how legislation and institutions have responded to changing times and emerging challenges in labour relations.

He said that as Member States of the Southern African Development Community (SADC), their engagement was of particular importance as the shared aspiration is to promote greater coherence and, where appropriate, harmonisation of labour laws consistent with International Labour Organization standards and guidelines.

Such cooperation, Dr. Mlyambina said, can facilitate trade and investment, promote decent work, uphold the dignity of workers and strengthen social justice throughout our region.

“We are particularly keen to learn from South Africa's experience in addressing emerging forms of employment and the changing world of work, including the rapidly developing field of the platform economy…

“The growth of digital labour platforms, app-based work and other non-traditional forms of employment presents new challenges concerning employment status, minimum labour standards, social protection, collective bargaining, occupational safety and health and access to labour justice,” he said.

He said that they would, therefore, be particularly interested in understanding how South Africa has responded, both legislatively and judicially, to the emerging forms of work and how questions of employee or worker status have been determined.

The delegations would also want to know whether platform workers have been afforded protection under existing labour legislation and how the Courts and the CCMA have balanced technological innovation and business flexibility with the constitutional and statutory imperatives of decent work, fair labour practices and social justice.

“These are matters of growing importance not only to the United Republic of Tanzania, but also to the wider SADC region. Your experience will therefore be invaluable as we consider how our own legal and institutional framework should respond to the future of work,” said Justice Mlyambina.

During the session, the head of delegation also conveyed the warmest judicial and diplomatic greetings of the Chief Justice of the United Republic of Tanzania, His Lordship George Masaju, to the Judge President of the Industrial Court and Labour Appeals Court of Republic of South Africa.

“His Lordship has asked me to convey his sincere regards and his profound appreciation for the cordial and longstanding relations between our two Judiciaries…

“He attaches great importance to the continued strengthening of judicial cooperation between the United Republic of Tanzania and the Republic of South Africa and regards the exchange of judicial knowledge and experience as an important means through which our institutions can learn from one another and collectively strengthen the administration of justice,” Dr. Mlyambina said.

Other members of the Tanzania delegation to the benchmarking visit to to the Labour Appeal Court, Labour Court and Commission for Conciliation Mediation and Arbitration of South Africa (CCMA), includes Presiding Judge-in-Charge of the High Court of Tanzania, Labour Division, Hon. Dr. Ntemi Kilekamajenga and two other Judges from the same court, Dr. Modesta Opiyo and Nehemia Mandia.

The rest are Deputy Registrar of the High Court of Tanzania Labour Division, Hon. Cassian Matembele, Deputy Registrar of the High Court of Tanzania, Hon. Mussa Ahmed Hamza, Court Administrator of the High Court of Tanzania, Labour Division, Ms. Joyce Mulugu and the Director of the Commission for Mediation and Arbitration (CMA) of Tanzania, Hon. Usekelege Mpullah.

In the same boat are two Tanzanian labour justice stakeholders, Mr. Christian Chiduga, Litigation Services Manager at the Tanzania Ports Authority and Ms. Comfort Laizer, who is Senior Legal Officer at the Tanzania Ports Authority. The delegation is accompanied by two Protocol Officers: Mr. Fadhili Mgutta and Ms. Janeth Makopolo.

As a gesture of appreciation and friendship, and as a token of the warm regards of His Lordship Chief Justice George Masaju, Justice Mlyambina presented on his behalf, a gift to the Judge President, as a symbol of gratitude, friendship and the enduring bonds between two Judiciaries.


Justice of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. Dr. Yose Mlyambina, stressing a point at a meeting duing the benchmarking visit in South Africa Judiciary.

Other members of the Tanzania delegation during the meeting. From right in above and below pictures is the Judge in Charge of the High Court Labourt Division, Hon. Dr. Ntemi Kilekamajenga, the Principal Judge of the High Court of Tanzania, Hon. Dr. Mustapher Mohamed Siyani and Justice of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. Dr. Yose Mlyambina. Extreme right in the above picture is Deputy Registrar of the High Court Labour Division, Hon. Cassian Matembele.



Judges of the High Court of Tanzania, Labour Division, Hon. Dr. Modesta Opiyo (above) and Hon. Nehemia Mandia (below) noting important points during the meeting.


Other members of the Tanzania delegation (above and two below pictures) following proceedings of the meeting.





The meeting is on.

Justice of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. Dr. Yose Mlyambina (left) and Principal Judge of the High Court of Tanzania, Hon. Dr. Mustapher Mohamed Siyani (right) present a gift to Judge President of the Labour Court and Labour Appeal Court, Hon. Mogomotsi Edwin Molahlehi on behalf of the Chief Justice of the United Republic of Tanzania, His Lordship George Masaju.


Two memorable pictures (above and below) comprising the Tanzania delegation and officials of the Judiciary of South Africa.


Picture by a Correspondent in South Africa.

 

 

Jumanne, 8 Septemba 2026

JAJI RWIZILE AMUAPISHA MUAMUZI WA 'CMA' KIGOMA

  •  Amsisitiza kuzingatia Maadili, Weledi 

Na AIDAN ROBERT,Mahakama-Kigoma

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile leo tarehe 08 Septemba, 2026,  amemuapisha Bw. Machumu Chirya kuwa Muamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) wa mkoani humo.

Uapisho wa Muamuzi huyo uliofanyika ofisini kwa Jaji Mfawidhi unamuwezesha rasmi Bw.  Chirya, kutekeleza majukumu yake ya kisheria ya uamzi wa migogoro ya kikazi na ajira, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kuimarisha upatikanaji haki kwa wote mapema ipasavyo ili kupunguza mlundikano wa mashauri ya migogoro ya kazi mkoani humo.

Aidha, Mhe. Rwizile ametumia nafasi hiyo kutoa nasaha kwa Muamuzi huyo, ambapo amemkumbusha kuzingatia misingi ya maadili, weledi wa hali ya juu na kujituma katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku. 

Aidha, Jaji Rwizile amemsisitiza Muamuzi huyo kuwa uaminifu na kufuata sheria kwakuwa ni nguzo kuu katika kutatua migogoro ya kikazi kwa haki, maslahi ya pande zote mbili (Waajiri na Wafanyakazi) jambo litakalochochea amani na utulivu mahali pa kazi mkoani Kigoma.

“CMA inaendelea kuwa nguzo muhimu katika usuluhishi na uamuzi wa migogoro ya kistaarabu na nje ya Mahakama za kawaida, jambo linalochochea ustawi wa uchumi na usalama mahali pa kazi, tunakutakia kila la heri katika kutekeleza majukumu yako mapya ya kulijenga Taifa lenye amani na usawa mahali pa kazi,” amesema Jaji Mfawidhi huyo.

Tukio la Uapisho huo limehudhuriwa na Naibu Masajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Yusufu Kasuka pamoja Wasaidizi wa Sheria wa Majaji wa Mahakama Kuu Kigoma.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile (aliyesimama mbele) akimuapisha Bw. Machumu Chirya kuwa Muamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA). Aliyesimama kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa na Watumishi wengine wakifuatilia kiapo hicho.


Bw. Machumu Chirya akila kiapo mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile cha kuwa Muamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA). Uapisho huo umefanyika leo tarehe 08 Septemba, 2026 ofisini kwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kigoma .

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile (kushoto) akimkabidhi hati ya kiapo chake Muamzi, Bw. Machumu  Chirya mara baada ya kula kiapo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile akitoa neno baada ya kumuapisha Bw. Machumu  Chirya kuwa Muamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile (aliyeketi mbele) akizungumza mara baada ya kumuapisha Muamuzi mpya wa CMA, Bw. Machumu Chirya (wa kwanza kulia).

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo, Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Muamuzi mpya wa CMA , Bw. Machumu Chirya (kulia) aliyeapa leo tarehe 08 Septemba, 2026. Wengine ni Viongozi wengine wa Mahakama Kuu Kigoma walioshuhudia uapisho wa Muamuzi huyo.


(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)



 

 

Jumatatu, 7 Septemba 2026

BALOZI MDOGO WA BURUNDI MKOANI KIGOMA AFANYA ZIARA MAHAKAMA KUU KIGOMA

Na AIDAN ROBERT,Mahakama-Kigoma.

Balozi mdogo wa Jamhuri ya Burundi nchini Tanzania anayehudumia Mkoa wa Kigoma, Bw. Kekenwa Jeremia, hivi karibuni alifanya ziara Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Kigoma na kufanya mazungumzo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. Augustine Rwizile.

Lengo kuu la ziara hiyo ya Kiofisi iliyofanyika tarehe 04 Septemba, 2026 lilikuwa ni kujitambulisha upya na kutoa taarifa rasmi kwa Jaji Mfawidhi kuwa ameongezewa muda wa kuhudumu katika nafasi yake ya ubalozi mdogo nchini Tanzania. Hatua hiyo, inatajwa kuwa chachu kubwa ya ushirikiano wa karibu katika kutoa huduma za haki kwa raia wa Burundi.

Aidha, Balozi huyo alitumia fursa hiyo kufikisha salamu maalum za Serikali ya Jamhuri ya Burundi kwa Mahakama Kigoma, huku akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi katika nyanja za sheria, haki, na usalama wa wananchi wa nchi hizo mbili Tanzania na Burundi ambao wamekuwa wakiishi kwa amani na udugu wa karibu mkoani Kigoma.

Vile vile alimjulisha Mhe. Rwizile kuwa, Rais wa Jamhuri ya Burundi amependa kumuongezea muda wa kuendelea kufanya kazi katika nafasi hiyo ya Balozi ili kuhudumu katika ubalozi mdogo hapa nchini, uamuzi unaolenga kuendeleza kazi.

“Naleta salamu maalum kutoka Serikali ya Jamhuri ya Burundi kwa lengo la kuendeleza na kuimarisha uhusiano mwema na ushirikiano wa kitaasisi baina yetu, hasa katika masuala yanayohusu huduma za kisheria na kijamii mkoani Kigoma, mahusiano haya thabiti yanazidi kuchochea amani, usalama na ushirikiano mzuri kwa wananchi wetu wanaoishi na kufanya shughuli zao mkoani Kigoma,” alisema Balozi huyo.

Kwa upande wake, Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. Augustine Rwizile alimkaribisha na kumpongeza Balozi huyo kwa kuongezewa muda wa kazi, akibainisha utayari wa Mahakama Kuu Kigoma kuendelea kushirikiana ki-taasisi ili kuhakikisha haki inatendeka na ustawi wa jamii unalindwa.

“Ziara hii inazidi kuimarisha daraja la kidiplomasia na udugu uliopo kati ya Tanzania na Burundi, ikithibitisha dhamira ya dhati ya Viongozi wa nchi hizi katika kudumisha amani na maendeleo endelevu,” alisema Jaji Rwizile.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile (kulia) akiwa katika mazungumzo Balozi Mdogo wa Jamhuri ya Burundi, Bw. Kekenwa Jeremia alipotembelewa na Balozi huyo ofisini kwake Mahakama Kuu Kigoma tarehe 04 Septemba, 2026.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na mgeni wake Balozi Mdogo wa Jamhuri ya Burundi, Bw. Kekenwa Jeremia (hayupo katika picha).


Mazungumzo yakiendelea. Kulia ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile (kulia), wa pili kulia ni Balozi Mdogo wa Jamhuri ya Burundi nchini Tanzania mkoani Kigoma, Bw. Kekenwa Jeremia, wa kwanza kushoto ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa, wa pili kushoto ni Msaidizi wa Balozi Mdogo wa Burundi Mkoani Kigoma, Bw. Nininahazwe Adalbert.

Picha ya Balozi Mdogo wa Jamhuri ya Burundi nchini Tanzania Mkoani Kigoma, Bw. Kekenwa Jeremia (katikati). Kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Kigoma, Mhe. Fadhili  Mbelwa na kushoto ni Msaidizi wa Balozi Mdogo wa Burundi Mkoani Kigoma, Bw. Nininahazwe Adalbert.


(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)

 

 

 

 

 

 

JAJI MFAWIDHI MBEYA AANZA ZIARA YA UKAGUZI WA SHUGHULI ZA MAHAKAMA

Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya, ameanza ziara ya ukaguzi katika maeneo mbalimbali ya Masjala hiyo kwa lengo la kutathmini utendaji wa kazi ili kubaini mafanikio na changamoto katika utoaji wa huduma, mazingira ya kazi na miundombinu ya Mahakama.

Ziara hiyo iliyoanza tarehe 03 Septemba 2026 ni sehemu ya utekelezaji wa Mahakama kusogeza huduma za haki karibu na wananchi, ambapo Mhe. Mtulya anatembelea Mahakama zinazotoa huduma pamoja na maeneo ambayo kwa sasa hayatoi huduma kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo uchakavu wa miundombinu, ukosefu wa majengo ya kutolea huduma na maeneo ambayo tayari yametengwa na Serikali za vijiji kwa kushirikiana na wananchi kwa ajili ya uanzishwaji wa huduma za Mahakama.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mtulya ametembelea Mahakama ya Wilaya ya Kyela pamoja na Mahakama za Mwanzo Busale, Ndobo, Ikolo na Kyela Mjini, ambapo amekagua hali ya utendaji, mazingira ya kazi na miundombinu ya Mahakama hizo.

Aidha, Mhe. Mtulya ametembelea maeneo ya Lema, Ipande, Mwaya na Kajunjumele, ambayo kwa sasa hayatoi huduma za Mahakama, huku baadhi ya maeneo hayo yakiwa na viwanja vilivyotengwa na Serikali za Vijiji kwa kushirikiana na wananchi kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Mtulya ameeleza kuwa kutembelea maeneo yenye viwanja vilivyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama ni muhimu katika kuhakikisha maeneo hayo yanalindwa na kutumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa.

“Katika kutekeleza mkakati wa Mahakama wa kusogeza huduma za Mahakama karibu na wananchi, ndiyo maana sisi tumekuja kutekeleza ziara hii ili kufanikisha mkakati huo,” amesema Mhe. Mtulya.

Katika kuhakikisha maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama yanalindwa, Mhe. Mtulya amewaelekeza viongozi wa maeneo husika kufuatilia upatikanaji wa hati za umiliki na kuweka alama za utambuzi katika kingo za viwanja hivyo ili kuvilinda dhidi ya uvamizi na matumizi yasiyokusudiwa.

Vilevile, amesisitiza umuhimu wa kutunza miundombinu ya Mahakama iliyopo na kuboresha mazingira ya kazi, ikiwa ni pamoja na usafi wa mazingira, upandaji na utunzaji wa miti na kuhakikisha majengo pamoja na maeneo ya Mahakama yanatunzwa ipasavyo.

Katika eneo la utoaji wa haki mapema ipasavyo, Mhe. Mtulya ameelekeza kuendelea kuweka mkazo katika usikilizaji na utatuzi wa mashauri ya vipaumbele, hususan mashauri ya mirathi na ndoa, ili kupunguza muda wa wananchi kusubiri haki na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za Mahakama.

Viongozi wengine walioshiriki ziara hiyo ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Benard Mpepo, pamoja na Mtendaji wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Ndobo. Viongozi wengine alioambatana nao (wanne kushoto) ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya, Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo (wanne kulia) na watatu kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Kyela Mhe. Rosta Mofuga.



Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akiwa katika ukaguzi wa viwanja mbalimbali vya mahakama katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akiwa katika ukaguzi wa viwanja mbalimbali vya mahakama katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akiwa katika ukaguzi wa viwanja mbalimbali vya mahakama katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akiwa katika ukaguzi wa viwanja mbalimbali vya mahakama katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya, akipokelewa Mahakama na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Kyela.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Ipande katika uwanja wa Mahakama uliotengwa na Serikali ya Kijiji cha Ipande, (wanne kulia) ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Ipande Bw. Lugano Mwabulanga na (watano kushoto) ni Afisa Ugani Kata ya Ipande Bw. Hamadi Mussa Kassim.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Lema katika eneo wa lililotengwa na Serikali ya Kijiji cha Lema, wanne kulia ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Lema Bw. Charles Emily Mwakabulufu, wanne kushoto ni Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Lema Bi. Joice Mkumbwa Kaminyoge.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiongoza kikao cha pamoja na watumishi (hawapo pichani) wa Mahakama ya Wilaya Kyela, kulia ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya na Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na Viongozi wengine alioambatana nao wakiwa kwenye picha ya Pamoja na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Kyela.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Mwanzo Kyela Mjini Mhe, Nassir Alfred Msafiri akiwasilisha taarifa, kwa Viongozi hao waliowasili katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya, akipokelewa Mahakama ya Mwanzo Ndobo.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)

Jumapili, 6 Septemba 2026

WATUMISHI MAHAKAMA NJOMBE WAFUNDISHWA MBINU ZA KUJIKINGA NA MAJANGA YA MOTO

Na ABDALLAH SALUM, Mahakama-Njombe

Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Njombe, wamepatiwa mafunzo ya siku moja kuhusu namna ya kujikinga na majanga ya moto pamoja na kuchukua tahadhali dhidi ya moto mahali pa kazi na nyumbani.

Mafunzo hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu Njombe yalifunguliwa na ASF. Bw. Bahati Mkutani tarehe 03 Septemba, 2026 na kuhudhuriwa na Viongozi pamoja na Watumishi wa Mahakama hiyo.

Akitoa mafunzo hayo, Ofisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, ZMK-FC Bi. Blandina Kayuya, alieleza kuhusu vifaa vya awali vya kuzimia moto, ikiwemo (portable fire extinguishers) za aina mbalimbali kama vile poda, povu na gesi ya kaboni dioksidi, pamoja na (fire blanket).

Bi. Kayuya alisema kuwa, miongoni mwa mambo yanayoweza kumfanya mtu ashindwe kukabiliana na moto katika hatua za awali ni uwoga na kutokuwa na vifaa sahihi vya kuzimia moto.

Alisisitiza umuhimu wa kuchukua tahadhali na kuwa na uelewa wa namna sahihi ya kutumia vifaa vya kuzimia moto ili kuhakikisha usalama wa watu na majengo dhidi ya majanga ya moto.

Akieleza hatua za kuchukua mtu anapogundua moto, Bi. Kayuya alisema; “moto unapotokea mtu hushindwa kuukabili kutokana na uwoga, unatakiwa ufanye yafuatayo pindi unapogundua moto: piga king’ora na yowe, piga simu ya bure Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kupitia namba 114, watu wasiojiweza wapewe kipaumbele kutoka eneo hatarishi, na jaribu kuzima moto bila kuhatarisha usalama wako na watu wengine.”

Aidha, alieleza kuwa vyanzo vikuu vinavyoweza kusababisha majanga ya moto ni pamoja na hitilafu za umeme, uzembe jikoni, uvutaji wa sigara, hujuma na uhalifu, pamoja na matukio ya asili kama vile radi.

Kwa upande wake, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Njombe, Mhe. Victoria Nongwa, baada ya kushiriki mafunzo ya nadharia na vitendo kuhusu namna ya kuzima moto, alilishukuru Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kutoa mafunzo katika Mahakama hiyo.

Mhe. Nongwa aliwaalika tena Maofisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kufika katika Mahakama hiyo kutoa mafunzo zaidi watakapopata nafasi, huku akiwashukuru Viongozi na Watumishi wote walioshiriki katika mafunzo hayo.

Mafunzo hayo, yaliyotolewa kwa ushirikiano na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Njombe, yalihusisha vipindi vya nadharia na vitendo. 

Mafunzo hayo yaliwajengea watumishi uelewa kuhusu matumizi sahihi ya vifaa vya kuzimia moto, namna ya kukabiliana na moto ukiwa katika hatua za awali, kutambua aina mbalimbali za moto na njia sahihi za kuukabili, pamoja na mbinu za kujiokoa pindi moto unapotokea.

Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Njombe, wakishiriki mafunzo ya vitendo kuhusu namna ya kuzima moto na kujikinga na majanga ya moto. Mafunzo hayo yalifanyika tarehe 03 Septemba, 2026.

Maofisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Njombe wakiwafundisha Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Njombe namna ya kujikinga na kukabiliana na majanga ya moto. Kutoka kushoto ni ZMK Bi. Blandina Kayuya, akifuatiwa na ZMM Bw. Msiwa Iddi, ASF Bw. Bahati Mkutani, na ZMM Bw. Kelvin Ngonyani. Mafunzo hayo yalifanyika tarehe 03 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa Mahakama hiyo.

Ofisa Hesabu Mahakama Kuu Njombe, Bw. Juma Nyenzi akiuliza swali kwa Maofisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati wa mafunzo huku baadhi ya watumishi wa Mahakama Kuu wakisikiliza kwa umakini.


Ofisa Utumishi, Bi. Happy Merere akijifunza kwa vitendo namna ya kutumia kifaa cha kuzimia moto, huku watumishi wengine wakifuatilia kwa karibu.

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)