Ijumaa, 18 Septemba 2026

MHE. TARIMO AWAPONGEZA WADAU WA HAKI JINAI KUPUNGUZA MALALAMIKO YA MAHABUSU, WAFUNGWA MAGEREZANI

Na AIDAN ROBERT, Mahakama-Kigoma

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mhe. Aristida Tarimo amewapongeza Wadau wa Haki Jinai mkoani humo kwa ushirikiano wao na kutimiza wajibu katika kutatua malalamiko kwa mahabusu na wafungwa hatua iliyowezesha kupunguza malalamiko yaliyokuwepo awali.

Mhe. Tarimo ametoa pongezi hizo leo tarehe 18 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma katika kikao maalum kilichowakutanisha wadau mbalimbali wa mnyororo wa haki jinai wa mkoani humo kwa lengo la kuimarisha ushirikiano, kuboresha utendaji kazi na kuharakisha utoaji wa haki kwa wananchi mapema ipasavyo.

“Nawapongeza sana wadau wote kwa ushirikiano wenu na kutimiza wajibu wetu katika kutatua malalamiko kwa mahabusu, na wafungwa kwani katika ukaguzi wa Magereza nimeona ushughulikiaji wa changamoto zao ni kwa kiwango cha juu, hivyo twendelee na juhudi hizo ili kuodoa kabsa Malalamiko katika Mahakama zetu.” amesema Mhe. Tarimo.

Aidha, kikao hicho kimejadili mafanikio ya kuendesha mashauri kwa njia ya mtandao (Video Conferencing), jambo ambalo limepunguza kwa kiasi kikubwa gharama na hatari za kusafirisha Mahabusu kutoka Magereza ya mbali na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika Magereza  ili  kuongeza ziara za pamoja za Mahakama, Waendesha Mashtaka na Polisi ili kubaini Mahabusu waliokaa muda mrefu bila mashauri yao kutajwa au kusikilizwa, na hatimaye kuchukua hatua za haraka.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (NPS), Bw. Nestory Kuyula amewahakikishia wajumbe kuwa, ofisi hiyo itaendelea kutoa ushirikiano kwa wadau wote ili kuisaidia Mahakama kusikiliza mashauri kwa wakati.

Kikao hicho kimelenga kutathmini mafanikio, kubaini changamoto sugu na kuweka mikakati ya pamoja ya kuondoa vikwazo vinavyochelewesha upatikanaji haki mapema ipasavyo, huku akiwasisitiza wadau kuhusu  matumizi ya Teknolojia na Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Kikao hicho cha Wadau wa Haki Jinai Kigoma kimehudhuriwa na Wajumbe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Magereza, Polisi, TAKUKURU, Uhamiaji, Ofisi ya Upelelezi Mkoa, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (NPS), Ustawi wa Jamii, Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Idara ya Marekebisho ya Tabia, na Ofisi ya Uangalizi Mkoa wa Kigoma.


Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mhe. Aristida Tarimo akisikiliza kwa makini mjadala uliokuwa ukiendelea katika Kikao cha Wadau wa Haki Jinai Mkoa wa Kigoma kilichofanyika leo tarehe 18 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu Kigoma.

Sehemu ya wajumbe wa Kikao cha Wadau wa Haki Jinai Mkoa wa Kigoma wakisikiliza kwa makini mjadala unaoendelea kwenye kikao kilichofanyika leo tarehe 18 Septemba, 2026 Mahakama Kuu Kigoma.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kibondo, Mhe. Maira Makonya akisoma kwa makini nyaraka za kikao cha Wadau wa Haki Jinai wa Mkoa wa Kigoma kilichofanyika leo tarehe 18 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma.
Sehemu ya wajumbe wa Kikao cha Wadau wa Haki Jinai Mkoa wa Kigoma wakisikiliza kwa makini mjadala unaoendelea kwenye kikao kilichofanyika leo tarehe 18 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kakonko, Mhe. Ambilike Kyamba (kushoto) pamoja na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Uvinza Mhe. Misana Majura (kulia) wakifuatilia mjadala uliokuwa ukiendelea wakati wa Kikao cha Wadau wa Haki Jinai wa Mkoani Kigoma.

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)

 

 


 

 

 

 

 

 

 

 


JAJI MTULYA AHITIMISHA ZIARA YA UKAGUZI WA MAHAKAMA ZA CHINI

Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya amekamilisha ziara ya siku 14 ya kukagua na utambuzi wa Mahakama za Wilaya na Mwanzo kwa lengo la kutathmini utendaji kazi, kubaini mafanikio, changamoto katika utoaji wa huduma za haki pamoja na kuangalia hali ya miundombinu na mazingira ya kazi.

Ziara hiyo iliyoanza tarehe 03 Septemba, 2026 na kuhitimishwa tarehe 16 Septemba, 2026 imehusisha kutembelea vituo vya Mahakama vilivyopo katika Wilaya za Kyela, Rungwe, Mbarali, Chunya na Mbeya, ambapo jumla ya vituo 48 vilitembelewa, vikiwemo vinavyotoa huduma na vile ambavyo kwa sababu mbalimbali havitoi huduma kwa sasa.

Katika ziara hiyo, Viongozi hao walifanya ukaguzi wa majengo, viwanja, mali za ofisi, mazingira ya kazi na upatikanaji wa huduma za Mahakama, pia walitembelea maeneo mbalimbali yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Mahakama.

Aidha, ukaguzi huo umewezesha kubaini hali halisi ya vituo mbalimbali, ikiwemo baadhi ya majengo chakavu, vituo ambavyo majengo yake hayatumiki au yameharibika, pamoja na maeneo yenye viwanja pekee bila majengo ya Mahakama.

Ziara imebaini hatua mbalimbali zinazochangia kuboresha utoaji wa huduma za haki ikiwemo usikilizwaji wa mashauri kwa wakati, matumizi ya mfumo wa ‘Primary Court App’ katika Mahakama za Mwanzo, upatikanaji wa viwanja kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu, ukarabati mdogo wa majengo na vifaa vya Ofisi, pamoja na kuimarika kwa ushirikiano kati ya Mahakama na wadau mbalimbali.

Katika baadhi ya vituo, ziara imebaini mafanikio katika kufunga mirathi kwa wakati, utoaji wa nakala za hukumu na mienendo kwa wakati, utoaji wa elimu kwa umma, pamoja na kuendelea kwa jitihada za kuimarisha mazingira ya utoaji wa huduma za haki.

Hata hivyo, ukaguzi umebaini changamoto zinazohitaji hatua za kimkakati, zikiwemo uchakavu wa baadhi ya majengo yanayotumika kutoa huduma za kimahakama, upungufu wa watumishi, ukosefu wa huduma muhimu kama maji katika baadhi ya vituo, upungufu wa Samani za ofisi, pamoja na baadhi ya viwanja vya Mahakama kutokuwa na hati miliki na alama za kudumu za mipaka.

Viongozi hao kupitia ziara hiyo, walitoa maelekezo mbalimbali kwa uongozi wa vituo husika, yakilenga kuharakisha hatua za upatikanaji wa hati na alama za mipaka ya viwanja, kuboresha miundombinu, kuongeza kasi ya usikilizwaji na ukamilishaji wa mashauri, kutoa nakala za hukumu kwa wakati, pamoja na kuimarisha usimamizi wa karibu wa utendaji kazi wa Mahakama.

Aidha, katika vituo ambavyo huduma za Mahakama hazipatikani, viongozi walifanya tathmini ya sababu za kutokuwepo kwa huduma hizo na kutoa maelekezo yanayolenga kuweka mazingira wezeshi ya kurejesha au kuimarisha huduma, ikiwemo kuhamasisha ushirikiano na Serikali za Vijiji na wadau wengine katika ujenzi wa majengo ya Mahakama.

Uongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya utaendelea kufuatilia utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa katika vituo mbalimbali, kwa lengo la kuhakikisha maboresho yaliyobainika yanatekelezwa na huduma za haki zinaendelea kutolewa kwa ufanisi, kwa wakati na katika mazingira yanayokidhi mahitaji ya wananchi na watumishi wa Mahakama.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati), na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wadau na Watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Madibira alipotembelea Mahakama hiyo alipokuwa ziarani wilayani Mbarali.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Watoto Mbeya.


Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akiwa ndani ya Ofisi ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Rungwe, alipotembelea alipokuwa katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kulia), akikagua miundombinu ya TEHAMA katika Chumba cha TEHAMA Mahakama ya Mwanzo Madibira.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati), na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakipokelewa na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Chunya na Mahakama ya Mwanzo Chunya Mjini. 

Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Chunya na Mahakama ya Mwanzo Chunya Mjini wakimsikiliza Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (hayupo pichani), ndani ya ukumbi wa Mahakama ya Wilaya Chunya.


Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wengine alioambatana nao na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Rungwe alipotembelea Mahakama hiyo  

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakikagua viwanja na maeneo mbalimbali ya yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahakama za mwanzo katika wilaya mbalimbali walizotembelea katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakikagua viwanja na maeneo mbalimbali ya yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahakama za mwanzo katika wilaya mbalimbali walizotembelea katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakikagua viwanja na maeneo mbalimbali ya yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahakama za mwanzo katika wilaya mbalimbali walizotembelea katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo wakikagua viwanja na maeneo mbalimbali ya yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahakama za mwanzo katika wilaya mbalimbali walizotembelea katika ziara hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati), na viongozi wengine alioambatana nao katika ziara hiyo pamoja na viongozi wa Mahakama ya Wilaya Chunya na Diwani wa Kata ya Makongorosi (watatu kushoto) wakiwa mbele ya jengo la Mahakama ya Mwanzo Mkongorosi linalojengwa na nguvu ya Wananchi na wadau mbalimbali wakiongozwa na Diwani wa Kata hiyo.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)


JAJI AWAMU MBAGWA AFANYA UKAGUZI MAHAKAMA KIBAHA

Na EUNICE LUGIANA, Mahakama-Kibaha

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe Awamu Mbagwa amefanya ukaguzi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha na Mahakama ya Wilaya Kibaha ili kuangalia mwenendo wa mashauri na masuala ya utawala.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo tarehe 17 Septemba, 2026, Mhe. Mbagwa alisema ukaguzi huo ni wa kawaida unaofanyika kila baada ya robo mwaka.

Akitoa taarifa ya utekelezaji ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha-Pwani, Naibu Msajili na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Pwani, Mhe. Joyce Mkhoi alisema Mahakama mkoani humo ina jumla ya Mahakama za Wilaya saba na Mahakama za Mwanzo 40.

Amesema, katika utekelezaji wa maagizo ya Viongozi Wakuu wa Mahakama Mkoa wa Pwani umejitahidi kupanga mashauri kwa kuzingatia muda, pia uondoshaji wa mashauri ya mlundikano inaridhisha kwa kuzingatia maelekezo, wananchi wanapata huduma katika Mhakama ya Hakimu Mkazi kulingana na taratibu.

“Wananchi wanapata huduma katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kulingana na taratibu zilizopangwa na pia usikilizwaji wa mashauri kupitia Mahakama Mtandao (Virtual Court) unaendelea kuzingatiwa kipindi cha Julai-Septemba, 2026 yamesikilizwa mashauri saba kwa njia ya mtandao (VC)” amesema Mhe. Mkhoi.

Akizungumzia kuhusu uelewa wa watumishi juu ya Mpango Mkakati  na Programu ya Maboresho ya Mahakama, Naibu Msajili huyo amesema  elimu inatolewa kupitia  vikao vya kila wiki ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya kazi zillizofanyika ndani ya wiki na kuelimishana.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mahakama ya Wilaya Kibaha, naye Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kibaha, Mhe. Emmael Lukumai amesema Mahakama pamoja na Wadau wa Haki wamekuwa na vikao vya mara kwa mara vya kujadiliana namna bora ya uendeshaji wa mashauri na kuondokana na mashauri ya mlundikano ambapo wameweza kuondoa mlundikano wa mashauri mahakamani na vikao hivyo vimekuwa vikizaa matunda.

Mhe Lukumai amesema pia, elimu kwa umma imekuwa ikitolewa kwa ajili ya ufafanuzi wa taratibu za Mahakama na sheria mbalimbali, ambapo Mahakama ya Wilaya Kibaha na Mahakama zake za Mwanzo wametenga muda wa siku moja kwa juma muda wa nusu saa kabla ya kuanza kwa mashauri  kwa kuweka ratiba maalum ambayo kila Idara ndani ya Mahakama inakuwa na siku ambayo inatoa elimu kwa wananchi.

Kadhalika, Mfawidhi huyo ameeleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi ya Julai mpaka Septemba ambapo ni pamoja na kutoa huduma kwa wakati na kutoa nakala za hukumu mara baada ya kumaliza kusikiliza shauri, kumaliza na kuzuia mashauri mlundikano, kutoa elimu na mengine.

Katika ziara hiyo, Jaji Mhe. Mbagwa aliambatana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Hussein Mushi, Msaidizi wa Sheria wa Jaji, Mhe. Bitulo Magafu na Ofisa Utumishi wa Kanda hiyo, Bi. Winifrida Shirima.


Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Awamu Mbagwa akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Pwani tarehe 17 Septemba, 2026 kwa lengo la kufanya ukaguzi wa Mahakama hiyo.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Awamu Mbagwa (aliyeketi mbele) akiwa katika Kikao pamoja na Viongozi wengine wa Mahakama ya Hakimu Mkazi na Wilaya Kibaha wakati wa ukaguzi wa Mahakama uliofanyika tarehe 17 Septemba, 2026.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Hussein Mushi akitambulisha msafara wa Jaji Awamu Mbagwa baada ya kuwasili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Pwani na Mahakama ya Wilaya Kibaha kwa ajili ya ukaguzi. Aliyeketi kulia ni Msaidizi wa Sheria, Mhe. Bitulo Magafu.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kibaha, Mhe. Emmael Lukumai akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mahakama hiyo mbele ya Jaji Awamu Mbagwa (hayupo katika picha). Aliyeketi kulia ni Naibu Msajili na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Pwani, Mhe. Joyce Mkhoi.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Awamu Mbagwa akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Hussein Mushi (kushoto), Naibu Msajili na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha-Pwana, Mhe. Joyce Mkhoi (kulia). Waliosimama nyuma, wa kwanza kushoto ni Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha-Pwani, Bw. Nestory Mujunangoma, wa kwanza kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kibaha Mhe. Emmael Lukumai, wa pili kushoto ni Msaidizi wa Sheria wa Jaji, Mhe Bitulo Magafu na wa pili kulia ni Ofisa Utumishi wa Mahakama Kuu ya  Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Bi.Winifrida Shirima.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Awamu Mbagwa (wa pili kushoto) akiagana na Mtendaji wa Mahakama Pwani, Bw. Nestory Mujunangoma (wa kwanza kushoto) baada ya kumaliza ziara ya ukaguzi Mahakamani hapo. Wanaoshuhudia wa kwanza kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha-Pwani ambaye pia ni Naibu Msajili, Mhe. Joyce Mkhoi na wa pili kulia ni Msaidizi wa Sheria wa Jaji, Mhe. Bitulo Magafu.

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)


 


 


 


 


 


 

 

JUDICIAL COMMUNICATION ROUNDTABLE PARTICIPANTS DEPART CAPE TOWN WITH COMMON UNDERSTANDING

By FAUSTINE KAPAMA-Dar es Salaam, just back from Cape Town

The African Judicial Exchange Network Roundtable, which was organized by CEELI Institute at Pullman Hotel City Centre in Cape Town, South Africa, was concluded yesterday dated September 17, 2026.

Such roundtable brought participants from Tanzania, Ghana, North Macedonia and Namibia, Uganda, Gambia, The Netherlands, Malawi, Botswana, Kenya, Nigeria, France, Czech Republic, United States of America and the host country, South Africa.

The participants described the roundtable as successful, as the topics presented contains important matters enabling them to understand the proper person, who is supposed tom speak for the Judiciary.

They could not prefer the Chief Justice to be in a fore front to avoid embarrassments as happened in one case, where the Head of the Judiciary issued a statement concerning demonstration, which was later misinterpreted. The Chief Justice had to come back to the media to clarify what he meant.

Before the conclusion of the three-day roundtable, which started on September 15, 2026, the participants were take through Artificial Intelligence (AI) in judicial communication and digitalization.

During the session, District Judge from United States, Hon. John Tunheim talked about Federal Judicial Centre’s AI toolkit and Judge from Poland, Hon. Greg Borkowski explained about European Judicial Training Strategy 2025-2023.

On her part, Advocate Lynn Coleridge from South Africa explained about perspectives on AI from a judicial training institute.

Thereafter, the participants were taken through plans for dissemination of the guidelines, next year activities and final remarks were given, before allowing judges to hold the Africa Judicial Network Core Group Meeting.

During the three-day conference, the participants were engaged in a cross-regional dialogue on key challenges facing contemporary judicial systems. They also discussed various issues relating to judicial communication, independence, rule of law and public trust.

The roundtable also touched upon the growing role of digitalization and artificial intelligence in judicial systems, examining the potential to enhance efficiency while considering the ethical, legal and regulatory challenges they raise.

In parallel, sessions on judicial communication explored how courts can effectively with the public, address complex or sensitive issues and maintain public confidence, including discussions on the scope and limits of judges’ freedom of expression.

Judge in Charge of the High Court of Tanzania, Morogoro Sub-Registry, Hon. Rose Ebrahim in a smiling mood on the last day of the African Judicial Exchange Network Roundtable. Picture below are other participants to the roundtable.


Coordinators of the African Judicial Exchange Network Roundtable, Mr Marek Svoboda (left) and Ms Monique Kamies. Picture below are other participants to the roundtable.



Another section of participants to the African Judicial Exchange Network Roundtable (two pictures above and belw) following what was going on on the last day.




 

JAJI MTULYA AKUTANA NA MKUU WA MKOA MBEYA

    .Asisitiza Ushirikiano katika kuimarisha utendaji kazi

Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya amefanya ziara ya kikazi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha ushirikiano na uhusiano baina ya Mahakama na Ofisi hiyo ili kuwezesha utendaji bora wa shughuli za kimahakama.

Ziara hiyo imelenga pia kujitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa pamoja na kujadili changamoto mbalimbali za kiutawala zinazohusiana na utendaji wa Mahakama katika Masjala hiyo, hususan masuala yanayohitaji ushirikiano na mamlaka za Serikali ya Mkoa, Halmashauri, Kata na Vijiji.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mhe. Mtulya, alieleza kuwa baadhi ya maeneo na miundombinu ya Mahakama katika Mkoa wa Mbeya yamekuwa yakiingiliwa na mamlaka nyingine bila ushirikishwaji wa Mahakama, hali ambayo inaweza kuathiri matumizi na ulinzi wa mali na maeneo ya Mahakama.

Katika ziara hiyo, Jaji Mfawidhi pia alitoa pongezi kwa Diwani wa Kata ya Makongolosi kwa jitihada za kuwashirikisha wananchi na wadau mbalimbali katika ujenzi wa jengo jipya la Mahakama ya Mwanzo Makongolosi, baada ya jengo la awali kuharibiwa wakati wa ghasia zilizotokea kipindi cha uchaguzi Mkuu mwishoni mwa mwezi Oktoba 2025.

Akizungumzia utekelezaji wa Nguzo ya Tatu ya Mpango Mkakati wa Mahakama, inayolenga kuimarisha imani ya wananchi kwa Mahakama na ushirikishwaji wa wadau, Jaji Mfawidhi alibainisha kuwa Mahakama Kuu Mbeya imeendelea kuwa na ushirikiano mzuri na wadau mbalimbali wa haki, wakiwemo Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, TAKUKURU na taasisi nyingine zinazohusika katika mfumo wa utoaji haki.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini, amemshukuru Jaji Mfawidhi kwa ziara hiyo na kusisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya Ofisi yake na Mahakama.

Mhe. Sagini amesema ziara hiyo imempa fursa ya kupata taarifa na uelewa zaidi kuhusu baadhi ya changamoto zinazoikabili Mahakama katika Mkoa wa Mbeya na kwamba Ofisi yake iko tayari kushirikiana na Mahakama katika kuzitafutia ufumbuzi.

“Nashukuru kwa ujio wenu na kunifungua macho katika baadhi ya mambo ambayo sikuyafahamu katika mkoa wangu na kunipa mwanga wa namna ya kuyafanyia kazi. Naahidi ushirikiano mkubwa kwa Mahakama na pale uonapo masuala yangu ya kiutawala yanakwamisha utendaji wa shughuli za kimahakama, milango iko wazi, nakukaribisha wakati wowote kuweza kurekebisha hilo,” alisema Mhe. Sagini.

Mkuu wa Mkoa pia ameeleza kuwa Serikali ya Mkoa itafuatilia migogoro na changamoto zilizobainishwa, huku akimuagiza Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya, kuwasilisha taarifa rasmi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inayoainisha maeneo yenye changamoto za kiutawala katika Mkoa wa Mbeya, ili kuwezesha hatua stahiki kuchukuliwa katika kuzitatua.

Hatua hiyo imetia msisitizo wa kuendelea kujenga ushirikiano wa karibu, mawasiliano na mahusiano ya kikazi kati ya Mahakama na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, hatua inayotarajiwa kuchangia katika kuondoa vikwazo vya kiutawala na kuweka mazingira bora kwa Mahakama kutekeleza jukumu lake la msingi la utoaji wa haki kwa wananchi.

Viongozi wengine walioambatana na Mhe. Mtulya, katika ziara hiyo ni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Benard Mpepo, Naibu Msajili wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi Laizer, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya, Afisa Utumishi Mwandamizi wa Mahakama Kuu Mbeya, Bw. Alintula Ngalile na Msaidizi wa Sheria wa Jaji Mfawidhi Mhe. Jane Mwaitumile.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini (kulia) akisalimiana na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kushoto) alipowasili ofisini kwake jijini Mbeya.
Sehemu ya Viongozi mbalimbali wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya wakifuatilia mazungumzo kati ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Sigini na Jaji Mfawidhi Mhe. Mtulya walipotembelea ofisini kwake 

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini (wanne kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya walipotembelea ofisini kwake wakiongozwa na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (wanne kushoto).


Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bw. Festo Chonya, (aliyesimama) akijitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini, Kulia ni Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo.

Naibu Msajili wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi Laizer akijitambulisha Mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini (hayupo pichani)

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini akiwa ofisini kwake akiwasikiliza Viongozi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya (hawapo pichani) walipotembelea ofisini kwake.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya, akiwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mbeya. 

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akitia sahihi kitabu cha wageni wakati alipowasili ofisini ya Mkuu wa Mkoa Mbeya.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)

HAKI JINAI SI MALI YA TAASISI MOJA; JAJI MKUU

Na HABIBA MBARUKU, Mahakama-Dodoma

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju amesema kuwa, Haki Jinai si mali ya Taasisi moja bali ni mfumo wenye Taasisi nyingi, wenye lengo la kuhakikisha haki inapatikana mapema ipasavyo kwa usawa, uadilifu na kwa kuzingatia Katiba na Sheria za nchi huku akieleza kuwa wadau wote wanapaswa kushirikiana kwa pamoja ili kuhakikisha haki haicheleweshwi bila sababu za msingi.

Mhe. Masaju ameyasema hayo wakati wa kufunga Mkutano wa Mahakama na Wadau wa Haki Kuhusu Ushirikiano na Mahusiano katika Utekelezaji Majukumu ya Utoaji Haki Mahakamani leo tarehe 17 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

“Haki jinai ni mfumo mmoja wenye taasisi nyingi lakini wenye lengo moja, yaani kuhakikisha kuwa haki inapatikana mapema ipasavyo tunapaswa kuzungumza kuhusu mfumo mzima kwa sababu udhaifu wa kiungo kimoja katika mnyororo wa haki jinai unaweza kuchelewesha haki kwa mfumo mzima,” amesema Jaji Mkuu.

Mhe. Masaju ametoa mfano wa Mtume Paulo anapozungumza kuhusu kanisa ambapo amesema, “ni kama mwili wa binadamu, kama ambavyo kuna mikono, macho, miguu, lakini hivyo vyote ndiyo vinakamilisha mwili. Yaani macho hayawezi kujifanya yenyewe ni bora kuliko mguu na vile viungo vilivyoonekana kama ni dhaifu, hivyo Mungu alivifanya kuwa vya maana zaidi lakini ukweli hapa wote hakuna kiungo dhaifu, hizi Taasisi zote ni muhimu.”

Ameongeza kuwa, jukumu la kwanza la sheria duniani kote ni kusimamia utawala wa sheria, amani na usalama katika jamii na jukumu la pili ni kukusanya kodi kwa ajili ya maendeleo mbalimbali na kuongeza kuwa hata Mwenyezi Mungu huko mbinguni aliweka sheria, na aliyekwenda kinyume na sheria aliwajibika kama ambavyo Lucifer alivyowajibika.

“Kwa hiyo, mkishakuwa zaidi ya mtu mmoja tu lazima mjiwekee sheria namna ya kufanya mambo yenu na kwetu Tanzania utawala wa sheria unapatikana katika Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mfumo wowote lazima uwe unaongozwa na utawala wa sheria, hata Mwenyezi Mungu kule mbinguni aliweka sheria, na bwana mkubwa yule akiitwa Lucifer alipoasi akawajibika” amesema Mhe. Masaju.

Katika hatua nyingine Jaji Mkuu amefafanua kuwa, Dira ya Taifa ya Maendeleo, 2050 inasisitiza juu ya amani, usalama na utulivu, ulinzi wa haki, uhuru wa msingi, uimara wa Taasisi na utawala wa sheria ambao ni kipengele muhimu cha utawala bora kinachosaidia kujenga jamii yenye usawa, uwajibikaji, haki na kuaminiana.

Aidha, ameeleza kuwa, mashauri ya jinai hayaanzii mahakamani wala polisi pekee kwa kuwa vyombo hivyo vyote haviwi sehemu na wakati ambapo matukio hayo ya kihalifu yanatokea hivyo, wadau wote wanapaswa kuungana na kufanya kazi kwa pamoja kama ambavyo viungo katika mwili vinavyofanya kazi kwa pamoja na kutegemeana.

“Kesi ya jinai inaanza kwenye jamii huko tukio linapotokea, inaenda kwenye vyombo vya uchunguzi iwe ni Polisi, ni Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, ni Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, inaenda Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, hatimaye kama kuna ushahidi inaenda mahakamani, na waliohusika kumkamata mshukiwa wanakuja kutoa ushahidi mahakamani kama amepatikana na hatia anarudi gerezani kwa ajili ya reform, utaona kwamba huu mnyororo ni mpana ni mnyororo mrefu lakini mnyororo imara, ” ameeleza Mhe. Masaju.

Katika hatua nyingine, amesema kuwa, ni vema kukawa na mtiririko mzuri wa kimfumo wa usimamizi wa mashauri ya jinai  ili kuondoa changamoto zinazokwamisha mashauri kumalizika na kuongeza kuwa Mahakama haiwezi kuwa na ufanisi wa asilimia 100, ikiwa hatua zilizotangulia hazifanyi kazi mapema ipasavyo na kwa ufanisi na kwamba kunaweza kuwa na Mahakama yenye uwezo wa kusikiliza Mashauri Majaji na Mahakimu wenye uwezo lakini kama uchunguzi haujakamilika au kuwepo kwa changamoto yoyote shauri haliwezi kuendelea.

 “Mahakama haiwezi kuwa na ufanisi wa asilimia 100 ikiwa hatua zilizotangulia Mahakama hazifanyi kazi mapema ipasavyo na kwa ufanisi. Tunaweza kuwa na Mahakama yenye uwezo wa kusikiliza mashauri, Majaji na Mahakimu wenye uwezo, na mifumo ya kielektroniki au miundombinu, lakini pia ni waadilifu. Lakini kama uchunguzi haujakamilika, jalada halijawasilishwa, mashahidi hawapatikani, maelezo hayajakamilika, hati za mashtaka zina kasoro, mshtakiwa hajaletwa mahakamani, au nyaraka muhimu hazijafikishwa mahakamani mapema, katika mtiririko kama huu kesi haiwezi kwenda mbele, hivyo ni vema kukawa na ile systematic flow ya criminal justice ya case management ili kuondoa hizo changamoto” amesisitiza Jaji Mkuu.

Akizungumza kuhusu uwajibikaji na kujituma, Mhe. Masaju amesema kuwa, kila Taasisi ya Haki Jinai inapaswa kuwajibika ipasavyo ili kuondoa ucheleweshaji wa mashauri bila kusubiri shauri lifike mahakamani huku akirejea Ibara ya 25 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inasisitiza juu ya uwajibikaji na kujituma katika kila kazi kwa kufahamu chanzo cha kukwama kwa shauri, wapi lilipofikia katika utekelezaji, imefikia hatua zipi za ushahidi, jambo litakalosaidia mnyororo mzima wa haki jinai kufanya kazi vizuri.

Kadhalika, Mhe. Masaju amewakumbusha wadau wa Haki Jinai kwamba, mfumo unahitaji ushirikiano thabiti, mawasiliano ya karibu na uratibu mzuri ambayo ndio nguzo ya mafanikio hivyo, taasisi zote zifanye kazi bila kujitenga.

“Ni vyema tukumbuke kuwa, mfumo wetu wa haki jinai unahitaji ushirikiano thabiti (cooperation), mawasiliano ya karibu (communication), na uratibu mzuri (coordination). Hivi vitu vitatu yaani Cooperation, Communication, and Coordination ndivyo nguzo kuu za mafanikio yetu katika usimamizi wa haki jinai. Kama taasisi moja inafanya kazi kwa kujitenga au bila kutoa taarifa kwa nyingine, ni wazi kuwa, kutakuwa na kukwama kwa mashauri au kuchelewa kwa haki,” amesisitiza Jaji Mkuu.

Kadhalika, Mhe. Masaju amezitaka Taasisi za mnyororo wa Haki Jinai kuzingatia matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na kuhakikisha mifumo inasomana ili kurahisisha mchakato mzima wa kuhakikisha haki inapatikana mapema ipasavyo bila kucheleweshwa na sababu zisizo na msingi.

Akihitimisha hotuba yake. Mhe. Masaju amezitaka Taasisi za mnyororo wa Haki Jinai kuchukua tahadhari juu ya uwepo wa mvua za El nino kwa kuhakikisha wanaweka miundombinu imara itakayowawezesha kufanya kazi pindi mvua hizo zitakapoanza kunyesha.


Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Majaji, Viongozi na Watumishi wa Mahakama pamoja na Wadau wa Haki Jinai wakati wa Mkutano wa Mahakama na Wadau wa Haki Kuhusu Ushirikiano na Mahusiano katika Utekelezaji Majukumu ya Utoaji Haki Mahakamani uliofanyika tarehe 17 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Aliyeketi kushoto ni Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Amir Mruma na kulia ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju akitoa hotuba ya kufunga Mkutano wa Mahakama na Wadau wa Haki Kuhusu Ushirikiano na Mahusiano katika Utekelezaji Majukumu ya Utoaji Haki Mahakamani uliofanyika tarehe 17 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Baadhi ya Viongozi, Watumishi wa Mahakama pamoja na Wadau wa Haki Jinai wakisikiliza hotuba ya Jaji Mkuu alipokuwa akifunga Mkutano wa Mahakama na Wadau wa Haki Kuhusu Ushirikiano na Mahusiano katika Utekelezaji Majukumu ya Utoaji Haki Mahakamani uliofanyika tarehe 17 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Amir Mruma akitoa neno wakati wa kufunga 
Mkutano wa Mahakama na Wadau wa Haki Kuhusu Ushirikiano na Mahusiano katika Utekelezaji Majukumu ya Utoaji Haki Mahakamani uliofanyika tarehe 17 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya akitoa taarifa ya utekelezaji wa mikakati kwa upande wa Mahakama wakati wa 
Mkutano kati ya Mahakama na Wadau wa Haki Kuhusu Ushirikiano na Mahusiano katika Utekelezaji Majukumu ya Utoaji Haki Mahakamani uliofanyika tarehe 17 Septemba, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)