Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya, Mhe. Joachim Tiganga ameongoza hafla
ya uzinduzi wa Majengo Mapya Matatu (3) ya Mahakama za Mwanzo. Majengo hayo matatu
yaliyozinduliwa ni pamoja na Mahakama ya Mwanzo Lupatingatinga wilayani Chunya, Mahakama ya
Mwanzo Ndobo Wilaya ya Kyela na Mahakama ya Mwanzo Madibila Wilaya ya Mbarali.
Hafla
hiyo ilifanyika tarehe 23 Machi, 2026 katika Viwanja vya Mahakama ya Mwanzo
Lupatingatinga wilayani Chunya. Uzinduzi wa Mahakama hizo unalenga kurahisisha
upatikanaji wa haki kwa wananchi, kupunguza umbali wa kufuata huduma za kimahakama
na kuongeza ufanisi katika utoaji wa haki kwa wakati mapema ipasavyo.
Akizungumza
katika hafla hiyo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Tiganga,
aligusia dhima ya Mahakama katika kutoa haki kwa wakati unaostahili bila kuchelewesha
huduma hizo za msingi kwa wananchi.
“Haki ndiyo msingi wa ustawi wa amani na usalama wa
wananchi, na sisi kama Mahakama tumejidhatiti katika utoaji wa haki kwa watu
wote na tuko tayari kufanya hivyo mapema ipasavyo,” alisema Mhe. Tiganga.
Vilevile,
Mhe. Tiganga aliwaasa watumishi wa Mahakama katika Vituo hivyo kuhakikisha
huduma zitakazotolewa zinaakisi hadhi ya Majengo hayo, na kusisitiza umuhimu wa
kutoa huduma bora kwa haki na weledi kwa kuzingatia uadilifu na misingi ya
utumishi wa umma.
Aidha,
aliuomba uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kusaidia upatikanaji wa
viwanja katika kila kata ili kufikia lengo la Mahakama ya Tanzania la kusogeza
huduma za Mahakama karibu zaidi na wananchi.
Kwa
upande wake, mgeni maalum katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe.
Alhaj Baraka Batenga, aliwaasa wananchi kuyatunza na kuyahifadhi Majengo hayo
kwani ni kwa ajili ya kulinda msingi wa amani na kudumisha ustawi wa utoaji
haki kwa wananchi.
“Mahakama ni mali ya wananchi, hivyo ni wajibu wetu
sote kuyalinda na kuyatunza majengo ya Mahakama zetu pamoja na miundombinu yake
kwa ujumla,” alisema Mhe. Batenga.
Naye,
Mbunge wa Jimbo la Lupa, Mhe. Masache Kasaka, alitoa shukrani kwa Mahakama ya
Tanzania kwa kuwezesha kukamilika kwa Majengo hayo ya kisasa, ambayo yatasogeza
huduma za Mahakama karibu na wananchi.
“Suala
la utoaji haki kwa wananchi mapema ipasavyo linaendana sambamba na ukaribu wa
upatikanaji wa huduma za kimahakama,” alisema Mhe. Kasaka.
Hafla
hiyo ilihudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Mahakama Kuu, Kanda za Mbeya na
Songwe, akiwemo Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masijala Ndogo ya Songwe, Mhe.
Gabriel Malata, Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya, Mhe. Mussa Pomo, Naibu Msajili
wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu na Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama
Kuu Masjala Ndogo Songwe Mhe. Joyce Minde.
Wengine
ni Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya, Bi. Mavis Miti, Mtendaji wa
Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Songwe Bw. Sostenes Mayoka na Mahakimu Wakazi wakiongozwa
na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi Laizer.
Aidha,
Uongozi wa Wilaya ya Chunya uliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe. Alhaj
Baraka Batenga, pamoja na Mbunge wa Jimbo la Lupa, Mhe. Masache Kasaka na
viongozi wengine.
.JPG)
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga
akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Majengo Mapya Matatu (3) ya Mahakama
za Mwanzo za Lupatingatinga wilayani Chunya, Mahakama ya Mwanzo Ndobo Wilaya ya
Kyela na Mahakama ya Mwanzo Madibila Wilaya ya Mbarali, tarehe 23 Machi, 2026
katika Viwanja vya Mahakama ya Mwanzo Lupatingatinga wilayani Chunya.
Sehemu ya wananchi waliohudhuria katika hafla hiyo.
Sehemu ya Mahakimu Wakazi Wafawidhi
wa Mahakama za Wilaya na Mkoa wa Mbeya waliohudhuria hafla hiyo ya uzinduzi waliosimama
mbele wakiongoza na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya wilaya Mbeya Mhe. Tedy
Mlimba (watatu kulia)
Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda
ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (Katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na
Viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo, wengine ni Mbunge wa Jimbo la
Lupa Mhe. Masache Kasaka (kulia), Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo
ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (wa pili kulia), Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Mussa
Pomo (wa kwanza kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Alhaj Baraka Batenga (wa pili kushoto).
Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (Katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wananchi waliohudhuria hafla hiyo, wengine ni Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe. Masache Kasaka (kulia), Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (wa pili kulia), Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo (wa kwanza kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Alhaj Baraka Batenga (wa pili kushoto).
Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (Katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama waliohudhuria hafla hiyo, wengine ni Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe. Masache Kasaka (kulia), Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (wa pili kulia), Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo (wa kwanza kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Alhaj Baraka Batenga (wa pili kushoto).
Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (Katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama waliohudhuria hafla hiyo, wengine ni Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe. Masache Kasaka (kulia), Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (wa pili kulia), Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo (wa kwanza kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Alhaj Baraka Batenga (wa pili kushoto).
.JPG)
Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (Katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Wilaya Mkoa wa Mbeya waliohudhuria hafla hiyo, wengine ni Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe. Masache Kasaka (kulia), Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Malata (wa pili kulia), Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo (wa kwanza kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Alhaj Baraka Batenga (wa pili kushoto).
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga akipanda Mti wa Matunda katika viwanja vya Mahakama ya Mwanzo
Lupatingatinga.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (kulia) akikabidhi kibao cha Ufunguzi wa Mahakama ya Mwanzo
Madibila kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbarali Mhe. Emily
Mwambapa.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (kulia) akikabidhi kibao cha Ufunguzi wa Mahakama ya Mwanzo
Ndobo kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Kyela Mhe. Rosta Mofuga.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim
Tiganga (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi Jengo la Mahakama ya
Mwanzo Lupatingatinga pamoja na majengo mengine mawili ya Mahakama za Mwanzo
Ndobo na Madibila.
Kikundi cha ngoma za asili “Dedede” wakitumbuiza
katika hafla hiyo.
Sehemu ya watumishi wa Mahakama waliohudhuria katika hafla hiyo.
Sehemu ya watumishi wa Mahakama waliohudhuria katika hafla hiyo.