Na. SHARIFU MOKIWA-Mahakama, Sumbawanga
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Sumbawanga Mhe. Fredrick
Kapela Manyanda amewataka washiriki wa Mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha
kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia ambao ni Mahakimu wa Mahakama za Wilaya, Waendesha
Mashtaka wa Serikali pamoja na Maafisa wa Ustawi wa Jamii kutoka mikoa ya Rukwa
na Katavi kuongeza umakini wanaposhughulikia mashauri ya aina hiyo ili
kuwajengea imani waathirika wanapofika mahakamani.
Mhe.
Manyanda alisema hayo wakati akifungua Mafunzo ya siku tatu kuhusu namna ya kuepuka
kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia (Sexual and Gender
Based Violance-SGBV) Mafunzo hayo yameanza jana tarehe 20 Aprili, 2026 katika ukumbi
wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Sumbawanga.
Mhe.
Manyanda ameongeza kuwa, mafunzo hayo yanalenga kuwasaidia washiriki
kuhakikisha wanaepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia
wakati wa utekelezaji wa majukumu yao.
“Mafunzo
haya yakatumike kuhakikisha kuwa tunaepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa
ukatili wa kijinsia, tutumie lugha ya staha, tuzingatie weledi na tujenge
mazingira ambayo waathirika wanaweza kuwa huru kutoa ushahidi bila kuathiri
kumbukumbu zao,” alisema Mhe. Manyanda
Aidha,
Jaji Manyanda aliongeza kuwa, utoaji wa haki unapaswa kuzingatia utu, usalama na
mazingira rafiki kwa waathirika ili kusaidia upatikanaji wa haki bila kuongeza
maumivu ya kihisia na kisaikolojia.
Mafunzo
hayo yameandaliwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) kwa kushirikiana na
Mahakama ya Tanzania kwa ufadhili wa Irishi
Rule of Law International pamoja na kushirikiana na Mahakama Kuu ya Tanzania
Masjala Ndogo ya Sumbawanga.
Vilevile,
Mafunzo hayo yanawezeshwa na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala
Ndogo ya Sumbawanga, Mhe. Pamela Mazengo kwa kushirikiana na Hakimu Mkazi Mkuu Mahakama
ya Wilaya Momba, Mhe. Raymond Kaswaga.
Mafunzo
hayo yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 22 Aprili, 2026 huku yakilenga kuongeza
ufanisi wa utoaji wa haki na kuimalisha ulinzi kwa waathirika wa ukatili wa
kijinsia katika jamii.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Sumbawanga Mhe. Fredrick
Kapela Manyanda akifungua mafunzo
Sehemu
ya washiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia kwa umakini mada mbalimbali
zinazoendelea kutolewa na wawezeshaji
Washiriki
wa Mafunzo hayo wakiwa kwenye majadiliano ya pamoja wakati wa Mafunzo
Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Sumbawanga, Mhe. Pamela
Mazengo (aliyesimama) akiwasilisha mada wakati wa mafunzo hayo.
Meza
Kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya
Sumbawanga Mhe. Fredrick Kapela Manyanda (katikati) wakiwa kwenye picha ya
pamoja na washiriki wa Mafunzo hayo.
Hakimu
Mkazi Mkuu Mahakama ya Wilaya Momba, Mhe. Raymond Kaswaga (aliyesimama) akiwasilisha mada
wakati wa mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo
Sumbawanga
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)













