Ijumaa, 19 Juni 2026
RAIS SAMIA AMUAPISHA DKT.JOHN ANTONY JINGU MTENDAJI MKUU MPYA WA MAHAKAMA
Matukio katika picha-Uapisho wa Mtendaji Mkuu mpya wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu Ikulu-Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Dkt. John Anthony Jingu kuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Dkt. John Anthony Jingu (kulia) akiapa Kiapo cha Maadili pamoja na Karani wa Baraza la Mawaziri Bw. Francis Petro Mossongo, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na viongozi mbalimbali baada ya kumuapisha Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Dkt. John Anthony Jingu, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Viongozi mbalimbali kwenye picha na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Anthony Jingu (aliyesimama nyuma), Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.
JAJI FAHAMU MTULYA AKABIDHIWA OFISI MAHAKAMA KUU MASJALA NDOGO MBEYA
Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Aliyekuwa
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim
Tiganga, tarehe 17 Juni, 2026 alimkabidhi rasmi Ofisi Jaji Mfawidhi mpya wa
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya baada ya kuripoti katika
kituo chake hicho kipya cha kazi.
Akizungumza
katika hafla ya makabidhiano, Mhe. Tiganga alitoa shukrani zake za dhati kwa
viongozi na watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya na kumpongeza Mhe.
Mtulya kwa kukabidhiwa majukumu hayo na kumtakia heri na mafanikio katika
utekelezaji wa majukumu ya kuiongoza Masjala hiyo ya Mbeya.
Hafla
hiyo ya makabidhiano ya Ofisi ilifanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya, ikihudhuriwa na aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga, Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Mussa Pomo, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi.
Mavis Miti na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Wilaya Mkoa wa Mbeya.
Makabidhiano
hayo yalijikita katika kukabidhi majukumu ya kiutawala, nyaraka mbalimbali za
ofisi, na taarifa muhimu za utendaji kazi, zote zikiwa na lengo la kuhakikisha
mwendelezo wa utoaji wa huduma za kimahakama na usimamizi wa shughuli za
Mahakama katika Masjala Ndogo ya Mbeya.
Kwa
upande wake, Mhe. Mtulya aliahidi kuendesha ofisi hiyo kwa weledi, kuendeleza
ushirikiano baina ya watumishi na kuimarisha upatikanaji wa huduma za haki kwa
wananchi wanaotumia Masjala hiyo ya Mbeya.
Makabidhiano
hayo yanaashiria mwanzo wa awamu mpya ya uongozi katika Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya, huku yakisisitiza dhamira ya kuendeleza ufanisi, uwazi na ubora
katika utoaji wa huduma za Mahakama kwa wananchi.
Jaji Mfawidhi mpya Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya, (kushoto) na aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (kulia) wakikabidhiana Ofisi katika kituo cha Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya.
Jaji Mfawidhi mpya Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya
Mhe. Fahamu Mtulya, (kushoto) na aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (katikati) wakisaini nyaraka za makabidhiano ya Ofisi na kulia ni Jaji waMahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo akishuhudia kitendo hicho.
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti (kulia) akimpa kipande cha keki Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kushoto) ikiwa ni ishara ya kumkaribisha.
Sehemu ya watumishi walioshiriki katika katika hafla hiyo ya makabidhiano ya Ofisi
Sehemu ya watumishi walioshiriki katika katika hafla hiyo ya makabidhiano ya Ofisi
Aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (katikati) akikabidhiwa zawadi na Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti (kushoto).
Aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Joachim Tiganga akikata keki ya kuagwa katika hafla hiyo.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akikata keki ya ukaribisho katika hafla hiyo.
Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akipokelewa na Viongozi na watumishi wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
MASHAURI 48 YA RUFAA ZA MADAI KUSIKILIZWA MBEYA
Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya.
Mahakama ya Rufani ya Tanzania inatarajia
kuendesha Kikao cha usikilizaji wa mashauri 48 ya rufaa za madai katika Masjala Ndogo ya Mbeya kuanzia
tarehe 18 Juni 2026 hadi tarehe 17 Julai, 2026.
Kikao hicho kitakua na jopo moja la Majaji wa
Mahakama ya Rufani wakiongozwa na Jaji wa Rufaa ya Tanzania Mhe. Winifrida
Beatrice Korosso, Majaji wengine katika jopo hilo ni Jaji wa Mahakama ya Rufani
Mhe. Dkt. Mary Calorine Levira na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Agnes Zephania
Mgeyekwa.
Akiwasilisha taarifa katika kikao kilichofanyika
katika ukumbi wa Mahakama Kuu Mbeya, ambacho ni kikao cha maandalizi (Pre-
Session Meeting), Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Mhe. Agatha Chugulu
alieleza kuwa Jumla ya mashauri 48 ya Rufaa za madai yamepangwa kusikilizwa
katika Masjala Ndogo ya Mbeya.
Aidha Mhe. Chugulu aliongeza kuwa, katika kuhakikisha ufanisi wa kikao hicho na kufikiwa kwa malengo yaliyokusudiwa ratiba ya kikao ilitolewa kwa wakati na Hati za kuitwa shaurini za wadaawa kwa ajili ya usikilizwaji wa mashauri zimesambazwa na juhudi za kuwapata wadaawa amabao hawajapatikana zinaendelea.
Naye, Mwenyekiti wa kikao hicho, Jaji wa Rufaa
Mhe. Winifrida Korosso, alihitimisha kwa kuomba ushirikiano baina ya wadau na kusisitiza
kuchunga muda wa kufika mahakamani.
“Lengo letu sote ni kupatikana kwa haki kama
kuna changamoto yoyote wasilisha mapema ili tufikie lengo la kutafuta haki kwa
pamoja ni
matarajio yetu kuwa kutokana na mpango wa kusikiliza mashauri kuandaliwa mapema
pamoja na ufuatiliaji wa karibu wa kila jalada, kikao hiki kitafikia malengo
yaliyokusudiwa,” alisema Mhe. Korosso.
Kikao
hicho kilihudhuriwa pia na Viongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya akiwemo
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya, Jaji wa
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbeya,
Mhe. Tedy Mlimba, Mawakili na Wadau wengine wa Haki Madai.
Mwenyekiti
jopo Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Winifrida
Beatrice Korosso (kulia), akiongoza kikao hicho, kushoto ni Jaji wa Mahakama ya
Rufani Mhe. Agnes Zephania Mgeyekwa.
Viongozi
wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya waliohudhuria kikao hicho, ni Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kulia), Jaji wa
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo (katikati) na Mtendaji wa
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti (kushoto).
Naibu Msajili wa
Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Agatha Chugulu (kushoto) akiwasilisha
taarifa katika kikao hicho na (kulia) ni Hakimu
Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbeya, Mhe. Tedy Mlimba. Ambaye katika kikao
hicho alikaimu nafasi ya Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya.
Sehemu ya Wadau walioshiriki katika kikao hicho hoja mbalimbali kwa makini.
Sehemu ya Wadau walioshiriki katika kikao hicho wakifuatilia kwa makini.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
WATUMISHI KUTOKA CHUO CHA UFUNDI ARUSHA WATEMBELEA MAHAKAMA KUU DIVISHENI YA BIASHARA
Na KEVIN HEZRON-Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Dar es Salaam
Watumishi
kutoka Chuo cha Ufundi Arusha (Arusha Technical
College), jana tarehe 18 Juni, 2026, walitembelea Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara kwa
lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu matumizi ya mifumo ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika usimamizi na utunzaji wa
kumbukumbu.
Akizungumza wakati wa
ziara hiyo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu – Divisheni ya Biashara, Mhe. Kevin Mhina, aliwashauri wageni hao kufanya juhudi za kuhamia
katika mfumo wa utendaji usiotegemea karatasi.
Alieleza kuwa matumizi ya
mifumo ya kidijitali hurahisisha utekelezaji wa shughuli za Taasisi, huongeza ufanisi wa utendaji
kazi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wakati.
Katika ziara hiyo, Afisa TEHAMA Mwandamizi wa Mahakama Kuu –
Divisheni ya Biashara, Bi. Amina Said, aliwasilisha
mada kuhusu Kanzidata ya Hifadhi na Usimamizi wa Nyaraka (Record Centre
Database) iliyobuniwa kwa lengo la kuboresha usimamizi wa majalada
yaliyofungwa.
Aliwaeleza wageni hao
changamoto zilizokuwepo kabla ya kuanzishwa kwa kanzidata hiyo, ikiwemo ugumu
wa kufuatilia maeneo yalipohifadhiwa majalada na ucheleweshaji wa upatikanaji
wa taarifa muhimu.
Aidha, aliwasilisha namna
kanzidata hiyo inavyowezesha usajili wa majalada, utambuzi wa maeneo
yanapohifadhiwa, ufuatiliaji wa Watumishi
wanaochukua majalada kwa matumizi ya muda pamoja na utoaji wa taarifa na ripoti
mbalimbali.
Kanzidata hiyo imeleta
maboresho makubwa katika kuokoa muda, kuongeza ufanisi wa kazi, kupunguza
upotevu wa majalada na kuboresha utoaji wa huduma.
Baada ya kupata
mawasilisho na kushuhudia onesho la matumizi ya kanzidata hiyo, wageni hao walionesha kuvutiwa na ubunifu huo na
kutoa pongezi kwa Mahakama Kuu – Divisheni ya Biashara kwa kutumia TEHAMA
kutatua changamoto za kiutendaji.
Kwa pamoja walieleza kuwa wamejifunza mambo mengi yatakayowasaidia katika kuboresha mifumo ya usimamizi wa kumbukumbu katika Taasisi yao.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Mhe. Kevin Mhina akiwakaribisha Watumishi kutoka Chuo cha Ufundi Arusha.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Mhe. Kevin Mhina akizungumza na wageni kutoka Chuo cha ufundi Arusha. Kushoto kwake, ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Mhe. Susan Kihawa, na Kulia kwake ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Bw. Anatory Kagaruki.
Bi.
Amina Said, Afisa TEHAMA wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, akitoa
wasilisho juu ya matumizi ya kanzidata ya usajili, usimamizi na utunzaji wa
kumbukumbu.
Wageni kutoka Chuo cha ufundi Arusha, wakisikiliza kwa makini mawasilisho yaliyoandaliwa.
Picha
na Iman Kasian, Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.
JAJI MFAWIDHI MPYA DODOMA AKABIDHIWA OFISI
Na ARAPHA RUSHEKE- Mahakama Kuu Dodoma.
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dodoma imeingia katika awamu mpya ya uongozi jana tarehe 18 Juni, 2026, baada ya Jaji Mfawidhi mpya, Mhe. Joachim Tiganga, kukabidhiwa ofisi na mtangulizi wake, Mhe. Dkt. Juliana Masabo, ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama ya Rufani.
Makabidhiano hayo yalijikita katika kukabidhi majukumu ya kiutawala, nyaraka mbalimbali za ofisi, na taarifa muhimu za utendaji kazi, zote zikiwa na lengo la kuhakikisha mwendelezo wa utoaji wa huduma za kimahakama na usimamizi wa shughuli za Mahakama katika Masjala Ndogo hiyo.
Akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano, Mhe. Dkt. Masabo alimpongeza Jaji Tiganga kwa kukabidhiwa majukumu hayo na kumtakia mafanikio katika utekelezaji wake.
“Nitumie fursa hii kumpongeza Mhe. Tiganga, tunaungana nawe kumshkuru mwenyezi Mungu kwa kibali ambacho amekupatia ili uje uhudumu hapa uwatumikie watu wake. Namshukuru pia Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Masaju, kwa imani kubwa ambayo ameionesha kwako na kuona ni muda sahihi kuweza kufanya kazi katika kituo hiki cha Dodoma,” alisema.
Naye Mhe Tiganga aliwashukuru Viongozi na Watumishi wote wa Mahakama Kuu Dodoma kwa mapokezi mazuri aliyoyapata na alisisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa haki kwa Wananchi.
Makabidhiano hayo yanaashiria mwanzo wa awamu mpya ya uongozi katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dodoma, huku yakisisitiza dhamira ya kuendeleza ufanisi, uwazi na ubora katika utoaji wa huduma za Mahakama kwa Wananchi kwa kuzingatia salamu ya Mahakama isemayo Uadilifu,Weredi na Uwajibikaji.
Jaji
wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (wa kwanza kulia)
akikabidhi ofisi kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga,
wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu
Dodoma Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC).
Watumishi
wa Mahakama Kuu Dodoma wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa kumpokea Jaji Mfawidhi
mpya mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Mahakama Kuu Masjala ndogo
Dodoma.
Meza
Kuu ikiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (aliyepo
katikati waliokaa), kulia kwake ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe.
Joachim Tiganga na kushoto kwake ni Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Biswalo
Mganga, ikiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mahakama Kuu Dodoma
waliohudhuria hafla hiyo ya makabidhiano.
Meza
Kuu ikiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (aliyepo
katikati waliokaa), kulia kwake ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe.
Joachim Tiganga na kushoto kwake ni Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Biswalo
Mganga, ikiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma
waliohudhuria hafla hiyo ya makabidhiano.
Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (aliyepo katikati) na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga (kulia) wakisaini nyaraka za makabidhiano. Kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Biswalo Mganga, anayeshughudia zoezi hilo.
Baadhi
ya watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma waliohudhuria hafla hiyo ya makabidhiano.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.
Alhamisi, 18 Juni 2026
TUTEKELEZE MAJUKUMU YETU VEMA; JAJI NGUNYALE
Na MICHAEL RITTE, Mahakama-Bukoba
Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. David Nyanguye amewasihi
watumishi wa Masjala hiyo kuhakikisha kazi za usikilizwaji wa mashauri
zinaendeshwa vema pasipo kukwama na jukumu hilo liambatane na juhudi katika
utendaji wa majukumu ya kila siku kwa kuzingatia Maadili na kanuni za nafasi
husika wanazozitumikia.
Mhe. Ngunyale aliyasema
hayo jana tarehe 17 Juni, 2026 katika Ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba wakati wa makabidhiano ya Ofisi kati yake na aliyekuwa
Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi ambaye ameteuliwa
hivi karibuni kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.
Kabla ya makabidhiano ya
ofisi, kulikuwa na mapokezi ya awali
katika viwanja vya Mahakama hiyo.
Jaji Ngunyale alisema kuwa,
kila mtumishi ana wajibu wa kuhakikisha huduma za utoaji haki zinafanyika kwa
uadilifu na weledi. Huku akisisitiza kuwa, “tujivunie nafasi tulizopewa na
kuzisimamia ipasavyo.”
“Tukifanikiwa kusimamia
majukumu yetu na kuwekeza nguvu na muda katika kazi, itatuletea nafasi thabiti
ya kujengeana uwezo katika kazi na katika majukumu mbalimbali,” amesisitiza
Mhe. Ngunyale.
Ameongeza kuwa, katika
utekelezaji wa majukumu ni muhimu kujali afya, familia zetu na jamii sambamba
na kuwa na ukaribu na kutenga muda na nafasi
kushiriki shughuli za kijamii ambazo kwa namna moja hudumisha afya ya kiakili
na kiutendaji kwa mtumishi.
Alisisistiza kwa kunukuu,
“To be trusted is a greater Compliment than to be loved,” Usemi kutoka kwa
Mwandishi George MacDonald ambao unamaanisha kuwa, ‘Kuaminiwa ni sifa kubwa
kuliko kupendwa.’
Kwa upande wake, aliyekuwa
Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi ambaye kwa sasa
ni Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, aliwasihi watumishi hao kuendelea
kuishi kwa upendo kama walivyoishi naye kipindi akiwa katika nafasi hiyo.
Kadhalika, Mhe. Banzi
amewasihi watumishi hao kuendeleza ushirikiano. Na kuhitimisha kwa kumtakia Mhe.
Ngunyale kila la kheri katika utekelezaji wa majukumu mapya katika Kituo hicho.
Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. David Ngunyale akisalimiana na Watumishi wa Mahakama hiyo alipowasili katika Kituo chake kipya cha kazi jana tarehe 17 Juni, 2026.
Jaji wa Mahakama ya Rufani na aliyekuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Bukoba, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi (kulia) akimkabidhi taarifa ya makabidhiano ya ofisi Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. David Ngunyale.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi (wa pili kushoto) akizungumza jambo wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Bukoba kwa Mhe. David Ngunyale. Wa pili kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. Lillian Itemba na wa kwanza kulia ni Mhe. Ferdinand Kiwonde, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, wakiwa kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu Bukoba.
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. Said Mkasiwa akitoa neno la kumkaribisha Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama hiyo, Mhe. David Ngunyale (wa kwanza kushoto).
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)
WATUMISHI DODOMA WAMPONGEZA NAIBU MSAJILI MPANGULE
Na ARAPHA RUSHEKE, Mahakama Kuu Dodoma.
Kaimu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dodoma, Mhe Biswalo Mganga,
amewaongoza Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma katika hafla fupi ya kumpongeza
Mhe. Zabibu Mpangule, mara baada ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa Naibu Msajili
wa Mahakama Kuu Dodoma.
Hafla
hiyo imefanyika tarehe 17 Juni 2026 katika ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji
Haki (IJC) Dodoma.
Akizungumza
kwa niaba ya watumishi, Mhe. Mganga amempongeza Mhe. Mpangule kwa kuaminiwa na
kupewa nafasi hiyo muhimu, akieleza kuwa uteuzi wake ni matokeo ya utendaji
kazi uliotukuka, uadilifu na kujituma katika kutekeleza majukumu yake.
Kabla
ya uteuzi huo, Mhe. Mpangule alikuwa akihudumu kama Hakimu Mkazi Mfawidhi wa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma ambapo alitoa mchango mkubwa katika utoaji wa
huduma za haki kwa Wananchi.
Kwa
upande wake, Mhe. Mpanguke aliwashukuru Watumishi kwa pongezi zao na kuhahidi
kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uadilifu na kujituma kwa manufaa
ya Mahakama na Wananchi kwa ujumla.
Watumishi
wa Mahakama Kuu Dodoma pamoja na Wilaya zake walimtakiwa kila la kheri katika
majukumu yake mapya.
Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja na kumpatia dhawadi Naibu Msajili mteule (wa nne kutoka kushoto).
JAJI FAHAMU MTULYA AAGWA MUSOMA KUFUATIA UHAMISHO WA KITUO
- Yamkaribisha pia Jaji Kakolaki katika Kituo hicho
Na FRANCISCA SWAI, Mahakama-Musoma
Uongozi
na watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ndogo Musoma wamejumuika kumuaga
Jaji Fahamu Mtulya kufuatia uhamisho wake kwenda Mahakama Kuu Masjala ndogo ya
Mbeya na kumkaribisha Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Edwin
Kakolaki aliyehamia kutokea Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mtwara.
Hafla
ya kumuaga Jaji Mtulya na kumkaribisha Jaji Kakolaki ilifanyika tarehe 14 Juni,
2026 katika Viwanja vya Mahakama Kuu Musoma.
Akizungumza
katika hafla hiyo, Mhe. Mtulya aliwashukuru watumishi na wadau wote wa Mahakama
Musoma kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi chote cha utumishi wake akiwa
Musoma.
Pia,
aliwaasa watumishi kuendelea kufanya kazi kwa umoja na upendo, kuzingatia
maadili ya kazi na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Zaidi alisisitiza umuhimu wa ushirikiano na wadau katika kuhakikisha shughuli
za Mahakama zinafanyika kama inavyopaswa.
Naye
Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Musoma, Mhe.
Edwin Kakolaki aliwashukuru Uongozi, watumishi na wadau wote wa Mahakama Kanda
ya Musoma kwa kumkaribisha na kuahidi kutoa ushirikiano pamoja na kufanya kazi
kwa bidii.
Kwa
upande wao watumishi wa Mahakama Kuu Musoma walimshukuru Jaji Mtulya kwa
uongozi wake thabiti, malezi bora kwa watumishi wa kada zote, kuwa mfano hai wa
mchapakazi, uadilifu, upendo na kujitoa kwake katika kazi, matukio ya kijamii,
kuhamasisha umoja, michezo na utalii wa ndani.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kiserikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Mtambi, Mkuu wa Wilaya Musoma, Mhe. Juma Chikoka pamoja na Wadau mbalimbali wa Mahakama ambao wote kwa pamoja walitoa salamu na zawadi mbalimbali kumshukuru Jaji Mtulya kwa uongozi wake imara uliothibitika kwa uwajibikaji, uadilifu, na mashirikiano mzuri na wadau.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (wa pili kushoto) akijiandaa kukata keki na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Musoma, Mhe. Edwin Kakolaki (katikati)wakati wa hafla ya kumuaga Jaji Mtulya na kumkaribisha Jaji Kakolaki (katikati). Wa kwanza kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Musoma, Mhe. Marlin Komba, wa kwanza kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Musoma, Mhe. Kamazima Idd na wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Mtambi.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Musoma, Mhe.Edwin Kakolaki (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Mtambi (kulia).
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akipokea mkono wa kwaheri kutoka kwa Chama cha Mahakimu na Majaji (TMJA) Tawi la Musoma.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Musoma.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (wa pili kushoto) akiwa ameshika zawadi aliyopatiwa ikiwa ni ishara ya shukrani na kumtakia kheri kutoka kwa Viongozi wa Mahakama Kuu Musoma ambao ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Musoma, Mhe. Omari Kingwele (wa kwanza kushoto), wa pili kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Musoma, Mhe. Monica Ndyekobora na wa kwanza kulia ni Mtendaji wa Mahakama Masjala Ndogo ya Musoma, Bw. Leonard Maufi.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akipokea zawadi ikiwa ni ishara ya mkono wa kwaheri na shukrani kutoka kwa watumishi ambao ni wadau wa utalii Masjala ndogo Musoma.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya hafla ya kumuaga ambao ni watumishi wa Kanda ya Musoma.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau walioshiriki katika hafla ya kumuaga.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (kulia) akipokea mkono wa kwaheri na shukrani kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Musoma, Mhe. Juma Chikoka.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akipokea mkono wa kwaheri na shukrani kutoka wadau wa Mahakama kwa namna alivyokuwa mstari wa mbele kuhamasisha shughuli za utalii wa ndani.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)




















