Na. MWINGA MPOLI – Mahakama, Mbeya
Mashauri
ya Rufaa 48 ya Ardhi, Kazi na Ndoa yanatarajiwa kumalizika katika kikao cha
Uendeshaji wa Mashauri (session) katika Masjala Ndogo ya Mahakama ya Rufani ya
Tanzania mkoani Mbeya.
Kikao
hicho kinachoendeshwa na Jopo la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufani, kikiongozwa
na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Rehema K. Mkuye ambaye ameambatana na Jaji
wa Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Eliezer M. Feleshi na Jaji wa Mahakama ya
Rufani Mhe. Dkt. Deo J. Nangela, wakisaidiwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya
Rufani Mhe. Daudi P. Kinywafu pamoja na watumishi wengine wa Mahakama ya Rufani.
Akiongea
katika kikao cha mapokezi, Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Mkuye aliushukuru
uongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya unaongozwa na Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim C. Tiganga kwa maandalizi na
mapokezi mazuri. Alifafanua kuwa, ushirikiano kutoka kwa wadau na wahusika,
utawezesha umalizaji wa mashauri hayo kama ilivyopangwa.
“Tunawashukuru
sana kwa mapokezi na maandalizi mazuri ya kikao hiki kwa hakika tumefarijika
sana na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu tunaamini kuwa mashauri haya yote
tutayasikiliza bila kikwazo chochote,” alisema Mhe. Mkuye.
Kwa
upande wake, Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Charles
Tiganga ameahidi kutoa ushirikiano kwa kipindi chote ambacho Waheshimiwa hao
watakuwepo Masjala Ndogo ya Mbeya kuendesha usikilizaji wa mashauri hayo ya
Mahakama ya Rufani.
Kikao
cha usikilizaji wa Mashauri hayo kimeanza jana tarehe 27 Aprili, 2026 na
kinatarajiwa kuhitimishwa tarehe 22 Mei, 2026.
Mwenyekiti
wa jopo la Majaji ambaye pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Rehema K. Mkuye
akisaini katika kitabu cha wageni mara tu baada ya kuwasili Mahakama Kuu Masjala
Ndogo Mbeya.
Jopo
la Majaji watatu likiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Rehema K. Mkuye
wakiwa pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Mbeya wakisaini kitabu
cha wageni mara baada ya kuwasili Masjala Ndogo Mbeya.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga (aliyesimama) akitoa neno la ukaribisho kwa waheshimiwa Majaji hao mara baada ya kuwapokea.
Jopo la Majaji watatu likiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Rehema K. Mkuye wakisalimiana na Majaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Pamoja na watumishi mbalimbali.
Jopo
la Majaji watatu likiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Rehema K. Mkuye
wakisalimiana na Majaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Pamoja na watumishi mbalimbali.
Naibu
Msajili wa Mahakama ya Rufani Mhe. Daudi kinywafu (wa pili kushoto kushoto),
Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo Mbeya Mhe. Aziza Temu (kulia),
Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo Mbeya Mhe. Judith lyimo (wa kwanza
kulia) na Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti
wakishiriki mapokezi hayo.
Jopo
la Majaji watatu likiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Rehema K. Mkuye
wakisalimiana na Majaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Pamoja na watumishi mbalimbali.
Jopo
la Majaji watatu likiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Rehema K. Mkuye
wakisalimiana na Majaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Pamoja na watumishi mbalimbali.
































