Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Menejimenti
ya Mahakama Masjala Ndogo ya Mbeya hivi karibuni ilifanya kikao cha tathmini ya
utendaji kazi kwa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2025/2026, kwa lengo la kupitia
utekelezaji wa majukumu ya kimahakama, kiutawala pamoja na kuweka mikakati ya
kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za haki kwa wananchi.
Kikao
hicho kiliongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Fahamu Mtulya, na kuwakutanisha Majaji, viongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo
ya Mbeya, Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Wilaya za Masjala Ndogo ya Mbeya
pamoja na Maafisa mbalimbali kutoka katika Mahakama hizo.
Aidha, kila
Mahakama iliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu yake kwa robo ya nne,
zikijumuisha usimamizi wa rasilimali watu, matumizi ya fedha, manunuzi na
ugavi, hali ya mashauri, upimaji wa utendaji kazi pamoja na utoaji wa motisha
kwa watumishi.
Akizungumza
wakati wa kikao hicho, Mhe. Mtulya alisisitiza umuhimu wa kuzingatia usawa
katika kuwathamini watumishi ili kuongeza ari ya kazi na kuimarisha utendaji
katika Mahakama zote za Masjala hiyo.
“Katika
kuboresha utendaji kazi, nasisitiza kuwepo na usawa wa utoaji wa stahiki na
motisha kwa watumishi wa mahakama zote katika Masjala nzima ya Mbeya, kuanzia
Mahakama Kuu hadi Mahakama za Mwanzo,” alisema Mhe. Mtulya.
Taarifa
zilizowasilishwa zilionesha mafanikio mbalimbali mathalani kusikiliza na
umalizaji wa mashauri yaliyopangwa, matumizi bora ya fedha kwa kuzingatia
vipaumbele vya ofisi, kupunguza msongamano wa wafungwa na Mahabusu magerezani
kupitia usikilizaji wa mashauri na kuendelea kudumisha ushirikiano mzuri na
wadau wa Mahakama,
Aidha, kikao
hicho pia kilibaini changamoto mbalimbali zinazohitaji kufanyiwa kazi, miongoni
mwa changamoto hizo ni uchakavu wa vyombo vya usafiri unaosababisha kuongezeka
kwa gharama za matengenezo, uchakavu wa majengo hususan Mahakama za Mwanzo,
ufinyu wa bajeti pamoja na upungufu wa watumishi.
Mwenyekiti alisisitiza umuhimu wa kuendeleza usimamizi madhubuti wa rasilimali zilizopo,
kuimarisha uwajibikaji na kuendelea kushirikiana katika kutafuta suluhisho la
changamoto zilizojitokeza ili kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za Mahakama
na kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya
Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiongoza kikao hicho cha menejimenti, wengine ni
Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo (kulia) na kushoto
ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Bi. Mavis Fransis Miti.
Naibu Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe.
Zawadi Laizer akiwasilisha taarifa ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya.
Sehemu ya washiriki katika kikao hicho wakimfuatilia
kwa makini Mwenyekiti wa kikao hicho Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (hayupo pichani).
Sehemu ya washiriki katika kikao hicho wakimfuatilia
kwa makini Mwenyekiti wa kikao hicho Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (hayupo pichani).
Sehemu ya washiriki katika kikao hicho wakimfuatilia
kwa makini Mwenyekiti wa kikao hicho Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (hayupo pichani).
Sehemu ya washiriki katika kikao hicho wakimfuatilia kwa makini Mwenyekiti wa kikao hicho Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (hayupo pichani).
Afisa Utumishi Mahakama ya Wilaya Mbeya Bi. Odilia Mapunda
(katikati) akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa Mahakama ya Wilaya na
Mahakama za Mwanzo.






























