Jumatano, 15 Julai 2026

JAJI MFAWIDHI MANYARA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MAHAKAMA

Na. CHRISTOPHER MSAGATI- Mahakama, Manyara

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi amefanya ziara ya Ukaguzi katika Mahakama zilizopo Wilayani Mbulu na Hanang’ na kuwasisitiza watumishi kufanya kazi kwa uadilifu, ueledi na uwajibikaji ili kuhakikisha malengo ya Mahakama yanatimia ipasavyo.

Hii ni ziara ya kwanza ya ukaguzi kwa Mhe. Dkt. Mambi tangu ahamie Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara kama Jaji Mfawidhi akitokea Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Tabora ambapo pia alikuwa Jaji Mfawidhi.

Akizungumza na watumishi katika Mahakama ya Wilaya ya Mbulu, Mhe. Dkt. Mambi aliwaasa watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na nidhamu wanapokuwa ofisini na hata wanapokuwa nje ya Ofisi.

“sisi watumishi wa Mahakama tunapaswa kuishi kwa nidhamu kuanzia ofisini na hata tunapokuwa nje ya Ofisi zetu, tunatarajiwa kuwa vioo vya jamii kwa wadaawa wetu na watu wote tunaowahudumia. Kwa misingi hii, maadili na nidhamu lazima vitutawale popote tutakapokuwa”, alisema Mhe. Dkt. Mambi.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na Mahakimu wa vituo vilivyokaguliwa, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava aliwasisitiza Mahakimu kuhakikisha kuwa wanahuisha taarifa za mashauri yao kwenye mfumo kila siku bila kukosa na kuhakikisha kuwa wanatoa nakala za Hukumu ipasavyo.

“Katika kipindi hiki cha matumizi makubwa ya TEHAMA, hatutarajii kuona kuwa tuna madeni ya kuhuisha mashauri katika mfumo rasmi uliowekwa hivyo ninawasihi mlichukulie suala hili kwa uzito wa hali ya juu. Vilevile hatutarajii tukifika katika magereza yetu tukutane na mfungwa ambaye analalamika kukosa nakala ya hukumu katika zama hizi”, alisema Mhe. Mnzava.

Kwa upande wa Wilaya ya Mbulu, Mahakama zilizokaguliwa ni Mahakama ya Wilaya Mbulu, Mahakama za Mwanzo Daudi, Dongobesh, Haydom na Gereza lililopo wilayani Mbulu.

Kwa upande wa Wilaya ya Hanang, Mahakama ambazo zilikaguliwa ni Mahakama ya Wilaya ya Hanang, Mahakama za Mwanzo Katesh, Bassotu na Endasak pamoja na mradi wa ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Hanang ambao unaendelea kwa sasa.

Katika hatua nyingine, Mhe. Dkt. Mambi alifanikiwa kufika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbulu na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu pamoja na kamati ya Wilaya ya Ulinzi na usalama, ambapo Mkuu wa Wilaya huyo aliahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Mahakama hususan kusaidia upatikanaji wa viwanja kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama na upatikanaji wa hati za viwanja hivyo.

Aidha, Mhe. Dkt. Mambi alitumia pia ziara hiyo kutambulisha viongozi wapya wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara ambao ni yeye mwenyewe pamoja na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava ambaye awali alikuwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara.

Pia katika ziara hiyo, viongozi wengine walioambatana nao ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu anayehudumu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara Mhe. Mariam Lusewa pamoja na Mtendaji wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Bi. Nyanzobe Hemedi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (aliyesimama) akizungumza na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbulu (hawapo pichani) katika ziara ya Ukaguzi iliyofanyika wilayani hapo, kushoto ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava na kulia ni Naibu Msajili anayehudumu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara Mhe Mariam Lusewa.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa kwanza kulia) akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, aliyekaa mbele ni Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa tatu kushoto) akiendelea na zoezi la ukaguzi katika Mradi wa Ujenzi katika Mahakama ya Wilaya ya Hanang.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi akisalimiana na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Hanang mara baada ya kufika kituoni hapo kwa ajili ya Ukaguzi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi akiongoza zoezi la ukaguzi katika Mahakama ya Mwanzo Bassotu wilayani Hanang.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Haydom iliyopo Wilayani Mbulu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wanne kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara pamoja na viongozi waandamizi wa Gereza la Wilaya ya Mbulu mara baaada ya kufanya Ukaguzi Gerezani hapo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa tatu kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Hanang.


Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara, Mhe. Charles Mnzava (aliyesimama) akichangia neno wakati walipo mtemebelea Ofisini Mkuu wa Wilaya ya Mbulu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (aliyesimama katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Dongobesh wilayani Mbulu.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha-Mahakama)

 

KATIBU MKUU WIZARA YA KATIBA NA SHERIA AJITAMBULISHA RASMI KWA JAJI MKUU

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju, leo tarehe 15 Julai, 2026 amepokea ugeni wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe, aliyefika ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma kwa ajili ya kujitambulisha.

Dkt. Shekalaghe amesema kuwa lengo la kukutana na Jaji Mkuu ni kujitambulisha rasmi kwake, kufuatia kuteuliwa kwake hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kushika nafasi hiyo. 

"Mhe. Jaji Mkuu, nimefika kujitambulisha kwako rasmi kwa nafasi yako kama Kiongozi Mkuu katika Mhimili huu wa Mahakama. Lakini pia kama kuna lolote niweze kupokea maelekezo. Ndilo lengo hasa kubwa kwa nini nimefika hapa," ameeleza Katibu Mkuu huyo.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe (aliyesimama) akijitambulisha mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 15 Julai, 2026 ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji
 
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju leo (kulia) akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe aliyemtembelea Jaji Mkuu leo tarehe 15 Julai, 2026 ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (aliyeketi mbele) akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe (wa kwanza kulia kwa Jaji Mkuu) wakati alipomtembelea Jaji Mkuu leo tarehe 15 Julai, 2026 kwa lengo la kujitambulia. Wa kwanza kushoto kwa Jaji Mkuu ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, wa kwanza kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu, kushoto kwa Jaji Kiongozi ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya, anayefuatia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Katibu wa Jaji Mkuu, Mhe. Venance Mlingi, anayefuatia ni Katibu wa Jaji Kiongozi, Mhe. Mussa Hamza .

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (kushoto), Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya (katikati) na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Katibu wa Jaji Mkuu, Mhe. Venance Mlingi wakifuatilia mazungumzo wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe alipomtembelea Jaji Mkuu ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.


Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe alipomtembelea Jaji Mkuu ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma leo tarehe 15 Julai, 2026.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (kulia) akimuonesha Dkt. Shekalaghe (katikati) picha za ukutani za Majaji Wakuu waliopita (hawapo katika picha) wakati Katibu Mkuu huyo alipomtembelea Jaji Mkuu ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe  alipomtembelea Jaji Mkuu ofisini kwake Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma leo tarehe 15 Julai, 2026.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (wa kwanza kushoto), Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu (wa pili kulia), Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya na wa pili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (kulia) akimuaga Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe mara baada ya kujitambulisha kwa Jaji Mkuu leo tarehe 15 Julai, 2026. 
















Jumanne, 14 Julai 2026

TANZANIA JUDICIARY DELEGATION IN KOREA FOR JUDICIAL COOPERATION

By FAUSTINE KAPAMA-Judiciary, monitoring from Dar es Salaam

A section of Justices of the Court of Appeal and Judges of the High Court of Tanzania is in Korea for a visit aimed at advancing judicial experiences through international cooperation.

The delegation of Tanzania Judiciary is led by Court of Appeal Justice and Principal of the Institute of Judicial Administration (IJA), Hon. Paul Kihwelo. Other Justices of Appeal are Hon. Issa Maige, Hon. Gerson Mdemu and Hon. Dr. Juliana Massabo.

High Court of Tanzania Judges in the list are Hon. Fahamu Mtulya, Hon. Danstan Ndunguru, Hon Dr. Lilian Mongela and Hon. Kevin Mhina. On July 13, 2026, the delegation attended the launch of the Judicial Capacity Building Programme, hosted by the Judicial Research and Training Institute (JRTI) of the Republic of Korea.

The launch was also attended by Ambassador -Designate of the United Republic of Tanzania to the Republic of Korea, His Excellence Noel Emmanuel Kaganda, to further strengthen economic and judicial cooperation between the two nations

The progremme serves as a valuable platform for exchanging best practices in digital courts, artificial intelligence, electronic case management and judicial administration to strengthen access to justice and judicial efficiency.

Speaking during the occasion, Justice Kihwelo noted that, such second edition reflects the growing partnership between Tanzania and the Republic of Korea and their shared commitment to modern, technology-driven judicial system.

On his part, Ambassador Kaganda thanked the JRTI and the Republic of Korea for their continued support, emphasizing the programme's important role in strengthening judicial institutions and advancing the rule of law.

According to the programme, yesterday dated July 13, 2026, the Judiciary of Tanzania delegation was taken through the ‘Judicial System of Korea’ and visited the Yonsei University Law School.

Today dated July 14, 2026, the delegation will have three sessions which include ‘E-Litigation System in Korean Courts (Civil Cases)’, ‘Introduction to the E-Criminal Litigation System’ and the ‘Current State and Future Prospects of AI in Judicial Education.’

The programme also shows that on Wednesday dated July 15, 2026, the delegation will be taken through the ‘Use of AI in the Korean Judiciary’ and later be transferred to the Seoul Southern District Court for a meeting with the Chief Judge.

On Thursday dated July 16, 2026, the delegation will visit the Supreme Court of Korea and have a meeting with the representative from the National Court Administration and later in the afternoon they will move to the JRTI for other issues.


A group photo comprising Justices of the Court of Appeal and Judges of the High Court of Tanzania who are in Korea for the second visit.


A group picture comprising of Justices of the Court of Appeal of Tanzania and other judicual officers who were in Korea for the first visit.

 

 

"TUMIENI TAALUMA ZENU KULINDA UHURU NA MASLAHI YA TAIFA," RAIS SAMIA AWAASA MAWAKILI WA SERIKALI


 Matukio katika picha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) AICC- Arusha, Tarehe 13 Julai, 2026. 
Mkutano huo umehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) kwenye Ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa (AICC) jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.

Mawakili wa Serikali pamoja na Wadau wengine wa Sheria wakiwa katika Hafla ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali (TPBA) kwenye ukumbi
wa  Mikutano wa Kimataifa (AICC) jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026 ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alikuwa Mgeni Rasmi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na  baadhi ya Viongozi wa Sekta ya Sheria. Walioketi wa pili kulia ni Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju, wa pili  kushoto ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, wa kwanza kushoto ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Said Johari na wa kwanza kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Gabriel Makalla.

Matukio katika picha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) AICC- Arusha, Tarehe 13 Julai, 2026. 


Jumatatu, 13 Julai 2026

TIMU ZA MAHAKAMA SPORTS KIGOMA, REDIO JOY ZASAKATA KABUMBU

  • Zaibuka kwa sare ya goli mbili kwa mbili
  • Mahakama Sports Kigoma azindua Jezi mpya

Na AIDAN ROBERT, Mahakama-Kigoma

Kapteni wa Timu ya Mahakama Sports Kigoma, Bw. Omary Magege ameongoza Kikosi cha Mpira wa Miguu kilichochuana vikali na Timu ya Redio Joy ya Mkoani humo katika Mechi ya kirafiki baina ya timu hizo iliyolenga kuzindua Jezi/Sare mpya za Timu ya Mahakama sambamba na kudumisha mahusiano na wadau.

Mechi hiyo ilifanyika tarehe 11 Julai, 2026 katika uwanja wa Kajuna uliopo katika Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Kocha wa Timu ya Mpira ya Mahakama Kigoma, Bw. Ramadhani Kufakunoga, alisema, “Tunawashukuru Viongozi wetu wa Mahakama Kigoma, kuona Timu hii inastahili jezi mpya pamoja na vifaa vingine kwa ajili ya mechi mbalimbali ambazo zinaendelea. Uwepo wa vifaa hivi vya michezo kwa Wachezaji ni motisha kubwa sana inayoungwa mkono na Timu hii pamoja na Mashabiki wetu.”

Kabla ya Mechi hiyo, Bw. Kufakunoga aliwataka Wachezaji wa Timu ya Mahakama kucheza kwa upendo na kujiamini ili kuonesha weledi katika mpira wao bila kusababisha majeraha kwa Timu pinzani.

Hata hivyo aliwatia shime kuwa, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma, Bw. Yusuph Kasuka, ambaye ndio Mdhamini Mkuu wa timu hiyo ameahidi kufanya makubwa yanayoleta motisha katika michezo, hivyo waendelee kuvitumia vipaji vyao ili kuileta Mahakama pamoja na wananchi.

Na kwa upande wake, Mkurugenzi wa Redio Joy Kigoma, Bw. Mwenge Muyombi, alisema kuwa, “Mechi hii ni ya kuimarisha mahusiano hivyo chezeni kwa furaha, hii ni sehemu ya kujenga afya zaidi, pia kujiandaa na mashindano mengine ya kirafiki yanayokuja, hivyo tunategemea burudani nzuri sana, nawatakia mpira mwema.”

Aidha, mechi hiyo iliendelea kwa mchuano mkali ambapo mpaka dakika ya 65, Timu ya Mahakama ilikuwa inaongoza, hata hivyo, Wachezaji wa Mahakama walionesha uimara mkubwa ambapo baadae kibao ikiligeuka kwa Timu ya Redio Joy kujitutumua na kujibu mapigo kwa wapinzani wao na kuiwezesha mechi hiyo kutoka sare ya mbili kwa mbili.

Ushindi huo kwa timu zote mbili ilikuwa ni kipimo kizuri ambapo Makocha wa Timu zote mbili, walibaini wapi wakaboreshe ili kuendelea kuwa na Timu bora zaidi katika mechi zijazo.

Watumishi wa Mahakama na Redio Joy walijumuika na wananchi waliojitokeza katika mechi hiyo, ambapo walionesha kufurahia mchezo huo kwani ulisheheni utulivu na weledi wa kucheza mpira kwa malengo ya mmoja wapo kuwa mshindi ingawa mizani ililingana kwa matokeo ya sare.


Kikosi cha Timu ya Mahakama Sports Kigoma kikiwa katika uzi mpya wa jezi iliyozinduliwa katika Mechi yao na Timu ya  Redio Joy Kigoma.


Kapteni wa Timu ya Mahakama Sports Kigoma, Bw. Omary Magege akitoa neno baada ya dakika 45 kutamatika, wakiongoza kwa goli moja dhidi ya wapinzani wao Timu ya Redio Joy Kigoma.

Mkurugenzi wa Redio Joy Kigoma, Bw.Mwenge Muyombi akisalimiana na  Wachezaji wa Timu zote mbili ya Mahakama Sports Kigoma na ya Redio Joy mara baada ya kutoa neno kwa Wachezaji wote wa Timu hizo.


Kikosi cha Timu ya Redio Joy Kigoma kikiwa maridadi kwa ajili ya mchezo wa kirafiki na Timu ya Mahakama Kigoma,  mechi iliyopigwa katika uwanja wa Kajuna Kigoma.


Sehemu ya Mashabiki wa Timu ya Redio Joy wakifuatilia Mchezo uliokuwa ukiendelea katika Uwanja wa Kajuna uliopo katika Manispaa ya Kigoma Ujiji.


Sehemu ya Mashabiki na Watumishi wa Timu ya Mahakama  wakifuatilia Mchezo uliokuwa ukiendelea katika Uwanja wa Kajuna uliopo katika Manispaa ya Kigoma Ujiji.


Sehemu ya wananchi wakifuatilia mchezo uliokuwa ukiendelea katika Uwanja wa Kajuna uliopo katika Manispaa ya Kigoma Ujiji.

 

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)

 

 

 

 

 

MAHAKAMA YA WILAYA UBUNGO YATIMIZA MIAKA MIWILI BILA MLUNDIKANO WA MASHAURI

Na EUNICE LUGIANA, Mahakama-Dar es Salaam

Mahakama ya Wilaya Ubungo imefanya kikao cha tathmini ya miaka miwili tangu kufunguliwa kwake ambapo kaulimbiu ya kikao hicho ilikuwa Mahakama ya Wilaya Ubungo bila mashauri ya mlundikano (two years without backlog cases).

Kikao hicho kilifanyika tarehe 10 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mahakama wa wazi wa Mahakama hiyo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Ubungo, Mhe. Tumsifu Barnabas alisema kauli mbiu hiyo ililenga kutokuwepo kabisa kwa Mashauri ya Mlundikano na kwa sasa wametimiza miaka miwili pasipokuwa na mashauri ya Mlundikano.

Mhe. Barnabas alisema kuwa, dhumuni la kikao hicho ni kutathmini utendaji kazi, mafanikio, changamoto na pia kufahamiana na watumishi wapya waliohamia katika Mahakama hiyo kutoka vituo mbalimbali.

Aliwasisitizia Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Ubungo na Mahakama zake za Mwanzo kutimiza lengo la kaulimbiu ya Mahakama na kufanyia kazi kwa kufuata kauli mbiu ya Uadilifu, Weledi na Uwajibikaji.

Aidha, Mfawidhi huo amesema, muitikio wa wananchi katika Mahakama hiyo umekuwa Mkubwa sana na ndio maana mashauri yanayofunguliwa ni mengi. Kwa kipindi cha mwaka 2024 hadi 2026 ni zaidi ya mashauri 5000 yamefunguliwa.

Katika kikao hicho, elimu kuhusu Mahakama SACCOS ilitolewa ambapo Meneja Mikopo wa Mahakama SACCOS, Bw. Godfrey Lulenga aliwaeleza faida za Chama hicho ambazo ni pamoja na kuweka akiba lakini pia kukopesha, ambapo kuna mikopo ya aina nne.

Bw. Lulenga alitaja mikopo hiyo kuwa ni Anza Maisha; ambapo alisema ni aina ya mkopo ambao mtumishi wa ajira mpya anakopeshwa ili kujikimu na Maisha, kuna mkopo wa dharura, mkopo wa maendeleo na mkopo wa sikukuu na kwamba Mahakama SACCOS wana mgawanyo wa riba.

Sambamba na kikao hicho watumishi hao walipata wasaa wa kukata keki ya upendo wa kusherehekea miaka miwili ya Mahakama hiyo.

Kikao hicho kilihudhuriwa na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Ubungo, Mahakama ya Mwanzo Kimara, Mahakama ya Mwanzo Kwembe na Mahakama ya Mwanzo Sinza/Manzese.

Mahakama ya Wilaya Ubungo ilianza kufanya shughuli za kimahakama tarehe 17 Mei, 2024.


Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Ubungo, Mhe. Tumsifu Barnabas  akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tathmini ya miaka miwili ya Mahakama ya Wilaya Ubungo kilichofanyika tarehe 10 Julai, 2026 kwenye ukumbi wa Mahakama hiyo.

 Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Ubungo wakifungua kikao kwa dua.

Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Ubungo wakiwa katika picha ya pamoja na wakijiandaa kukata keki ya upendo na ishara ya kuadhimisha miaka miwili ya Mahakama hiyo.

Meneja Mikopo wa Mahakama SACCOS, 
Bw. Godfrey Lulenga akielezea faida na mikopo inayopatikana Mahakama SACCOS wakati wa Kikao cha Tathmini ya miaka miwili ya Mahakama ya Wilaya Ubungo.

Keki ya kusherehekea Maadhimisho ya miaka miwili ya Mahakama ya Wilaya Ubungo.


(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)