Na EVA LESHANGE, Mahakama-Singida
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Singida, Mhe. Ayoub Mwenda leo
tarehe 30 Machi, 2026 amewasili mkoani Singida ikiwa ni mara ya kwanza baada ya
kupata uteuzi huo hivi karibuni wa kuiongoza Kanda hiyo mpya ya Mahakama Kuu.
Akiwa
katika hafla ya ukaribisho wake alipata nafasi ya kusikiliza taarifa fupi ya
utekelezaji iliyosomwa na Afisa Utumishi Mwandamizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi
Singida, Bi. Eva James Leshange.
Mara
baada ya kupokea taarifa hiyo, Mhe. Mwenda amewapongeza Viongozi na watumishi wote
wa Mahakama Mkoa wa Singida kwa kazi nzuri wanayoifanya hasa katika
usikilizwaji wa mashauri kwani hadi kufikia tarehe 27 Machi, 2026 Mkoa wa
Singida haukuwa na shauri la mlundikano.
Aidha,
Jaji Mfawidhi huyo amewashukuru watumishi kwa mapokezi mazuri na kuona
watumishi wana ari na nguvu ya kufanikisha malengo ya Mpango Mkakati wa
Mahakama.
“Nawashukuru
sana viongozi na watumishi kwa ujumla kwa mapokezi mazuri na hongereni sana kwa
kufanya kazi kwa bidii na ushiriano mkubwa hususan katika usikilizwaji wa
mashauri ni kiashiria watu wanafanya kazi kwa ushirikiano,” amesema.
Vilevile
amewasisitiza watumishi kuendela kuwa na nidhamu kwani, Mahakama inapokea
wateja ambao wameumizwa na wanahitaji msaada hivyo wasaidiwe kuhudumiwa kwa
heshima, pia amesisitiza kufanya kazi katika timu pasipo kuangalia vyeo ili
kusiwe na mkwamo katika kutekeleza majukumu ya kila siku.
Baada
ya kuzungumza na watumishi alipata wasaa wa kwenda kutembelea jengo jipya la
Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Singida na kufanya ukaguzi wa vyumba vya
ofisi na kuona hatua ilipofikiwa.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Singida, Mhe. Ayoub Mwenda (wa kwanza kushoto) akisalimiana na watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida alipowasili ofisini hapo leo tarehe 30 Machi, 2026.
Afisa Utumishi Mwandamizi Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, Bi. Eva Leshange akiwasilisha taarifa ya utekelezaji majukumu mbele ya Mhe. Ayoub Mwenda, Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda Ya Singida (hayupo katika picha) leo tarehe 30 Machi, 2026 alipowasili katika Mahakama hiyo.
Sehemu ya watumishi waliohudhuria hafla fupi ya ukaribisho wa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda mpya ya Singida.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Singida, Mhe. Ayoub Mwenda akikagua jengo jipya la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Singida.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)












.jpg)













