Alhamisi, 1 Juni 2023

JAJI MAKUNGU ATEULIWA KUWA JAJI MAHAKAMA YA AFRIKA MASHARIKI

Na Mwandishi wetu

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Omar Othman Makungu ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki, Divisheni ya Rufani.

Uteuzi huo ambao umefanyika mjini Bujumbura, Burundi katika Mkutano wa Marais wa Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki Uliofanyika jana tarehe 31 Mei, 2023.

Mkutano huo ulifanyika kujadili mambo mbalimbali, ikiwemo suala la usalama Mashariki wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Majaji wengine walioteuliwa ni Mhe.Anita Mugeni kutoka Rwanda anayekuwa Makamu Rais wa Mahakama hiyo na Mhe. Kayembe Rene kutoka DRC ambaye anakuwa Jaji wa Mahakama katika Divisheni ya Awali.

Uteuzi wa Mhe. Makungu na Mhe. Mugeni utaanza rasmi tarehe 20 Juni, 2023, huku uteuzi wa Mhe. Kayembe umeanza jana tarehe 31, 2023.

Mhe. Makungu amewahi kuwa Jaji Mkuu wa Zanzibar kabla ya kuteliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania.


Mhe. Omar Othman Makungu.

JAJI DKT. MONGELA AKABIDHIWA MIKOBA KANDA YA MOSHI

Na Paul Pascal – Mahakama Kuu-Moshi

Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Moshi, Mhe. Dkt. Lilian Mongela amekabidhiwa rasmi ofisi na mtangulizi wake, Mhe. Dkt. Juliana Massabo ambaye amehamishiwa Dodoma kuwa Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo. 

Hafla ya makabidhiano hayo ilifanyika jana tarehe 31/05/2023 katika ukumbi wa wazi wa Mahakama Kuu Moshi na kushuhudiwa na Wajumbe wa Menejimenti wa Kanda hiyo kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi na za Wilaya za Rombo, Moshi, Siha, Hai, Mwanga na Same.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mhe. Dkt. Massabo ameainisha mafanikio yaliyopatikana katika uongozi wake ambayo ni pamoja na kuondoa mlundikano wa mashauri ya muda mrefu, kujenga ushirikiano imara na wadau wa Mahakama katika Kanda hiyo na kuleta upendo na ushirikiano baina ya watumishi.

“Katika kipindi cha miezi tisa niliyoongoza hapa Moshi vilevile tumeweza kufanya jitihada za kutumia TEHAMA kwa asilimia 100,” alisema Mhe.Dkt. Massabo.

Kadhalika, Jaji Massabo ameainisha baadhi ya changamoto zinazoikabili Kanda ya Moshi ambazo ni pamoja na upungufu wa watumishi, uchakavu wa baadhi ya Mahakama hususani Mahakama za Mwanzo na nyingine.

Kwa upande wake, Jaji Mhe. Dkt. Mongela amemshukuru mtangulizi wake, Mhe. Dkt. Massabo huku akieleza kuwa yote aliyoeleza atayatumia kama funguo za kufungulia milango ya Kanda ya Moshi.

 “Mhe. Massabo ninakushukuru kwa hotuba nzuri ambayo kwangu naomba iwe ndio funguo zangu kwa milango ya Kanda ya Moshi. Vilevile niwaombe Viongozi wenzangu katika Kanda hii ule ushirikiano uliokuwepo kwa dada yangu Massabo niombe muuhamishie kwangu ili mambo yaendelee tena kwa kasi zaidi,” alisema Jaji Dkt. Mongela.


Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Moshi, Mhe. Dkt. Lilian Mongela (kushoto) akipokea nyaraka mbalimbali za Ofisi kutoka kwa mtangulizi wake aliyekuwa Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo, Mhe. Dkt. Juliana Massabo. Hafla ya makabidhiano ya ofisi ilifanyika jana tarehe 31 Mei, 2023 katika ukumbi wa wazi wa Mahakama Kuu Moshi.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Moshi, Mhe. Dkt. Lilian Mongela akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuripoti Kituoni hapo. 

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Moshi, Mhe. Dkt. Lilian Mongela akizungumza jambao wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi ya Kanda hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Massabo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Moshi, Mhe. Dkt.  Lilian Mongela (kushoto) na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Mhe. Adrian Kilimi (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Mtendaji Mahakama Kuu Kanda Moshi, Bw. Donald Makawia (aliyesimama kushoto) na Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Mhe. Omary Kingwele aliyesimama kulia).

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Massabo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Moshi, Mhe. Dkt. Lilian Mongela (kushoto) na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Mhe. Adrian Kilimi (kulia) pamoja na Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Na Mahakama za Wilaya-Kanda Ya Moshi. 

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Massabo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Moshi, Mhe. Dkt. Lilian Mongela (kushoto) na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Mhe. Adrian Kilimi (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Wasaidizi wa Sheria wa Majaji mara baada ya hafla fupi ya makabidhiano ya ofisi ya Mahakama Kuu Kanda ya Moshi.

Meza Kuu katika picha ya pamoja na Mtendaji Wa Mahakama Kanda ya Moshi na Maafisa Tawala Utumishi wa Kanda hiyo.

(Taarifa hii imehaririwa na Mary Gwera, Mahakama)


Jumatano, 31 Mei 2023

MAJAJI MBEYA WAJITOSA KWENYE MAZOEZI

Na Mwinga Mpoli- Mahakama Kuu, Mbeya

Mahakama Mkoa wa Mbeya imezindua programu maalum itakayowashirikisha watumishi wa kada zote, wakiwemo Majaji kushiriki katika mazoezi ya viungo ili kujenga afya bora na ushupavu, hatua itakayosaidia kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Programu hiyo ilizinduliwa hivi karibuni ambapo Majaji, viongozi waamdamizi na watumshi kwa ujumla walishiriki kwenye mazoezi ya michezo mbalimbali, ikiwemo kukimbia, mpira wa miguu na mpira wa pete.

Akizungumza katika ufunguzi wa mazoezi hayo, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. James Karayemaha aliwapongeza watumishi kwa kushiriki kwa wingi kwani mazoezi ni afya.

“Kwa hakika, mazoezi ni afya na hii inaongeza ari na nguvu hata katika utendaji wetu wa kazi, hivyo kutufanya tuweze kuepuka magonjwa yasiyo ya kuambukiza,” alisisitiza Mhe. Karayemaha.

Naye Mtendaji wa Mahakama Kuu Mbeya, Bw. Teoford Ndomba alisema atahakikisha vifaa vyote vinavyohitajika vinapatikana kwa wakati ili kuwapa watumishi nguvu ya mazoezi. Alisema atahakikisha  mwalimu wa mazoezi anapatikana.

Kwa upande wao, watumishi wa Mahakama walionyesha kufurahia programu hiyo ya mazoezi na kuahidi kushiriki bila kukosa kwa kuzingatia ratiba endelevu itakayotolewa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda Mbeya, Mhe. Dastan Ndunguru akiongoza mazoezi.
Sehemu ya watumishi wa Mahakama katika mazoezi wakiongozwa na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Victoria Nongwa (kushoto) wakishiriki kwenye mazoezi. Katikati ni Jaji wa Mahakama Kuu katika Kanda hiyo, Mhe. David Ngunyale.
Watumishi (juu na chini) wakiwa katika mazoezi.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama.



WATUMISHI MAHAKAMA MBEYA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU AFYA YA AKILI

Na Mwinga Mpoli, Mahakama Kuu Mbeya

Watumishi wa Mahakama Mkoa wa Mbeya wamepatiwa mafunzo ya afya ya akili ili kuboresha huduma wanazotoa kwa wateja kwa makundi yote.

Mafunzo hayo yalizinduliwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Dastan Ndunguru hivi karibuni ambayo yalifanyika katika ukumbi wa Mahakama hiyo.

“Matatizo ya afya ya akili hayachagui, mtu yeyote anaweza kuyapata. Sisi kama taasisi tunafaidika na mafunzo haya kwa sababu afya ya akili ni kila kitu. Tukijiangalia hapa tunajiona tuna akili, lakini tukipimwa tunaweza kujikuta wote tuna matatizo,” alieleza.

Kwa upande wake, Jaji wa Mahakama Kuu Mbeya ambae ni mratibu wa mafunzo, Mhe. David Ngunyale alisema kuwa kutokuwa na utulivu wa kiakili kunaweza kuathiri familia, mwajiri, wananchi na nafsi pia, hivyo ni vema kuwa na mafunzo hayo ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali.

Jaji mwingine anayehudumu katika Mahakama hiyo, Mhe. Victoria Nongwa, akizungumza wakati ana ahirisha mafunzo hayo alisisitiza watu kujipenda na kupunguza matarijio makubwa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Dastan Ndunguru akizungumza wakati anafungua mafunzo hayo.
Msaikolojia, Bi Betuna Mwamboneke akieleza jambo.

Majaji wa Mahakama Kuu Mbeya na viongozi wengine waandamizi wakiwa katika mafunzo hayo.

Watumishi wa Mahakama Mbeya (juu na chini) wakifuatilia mafunzo.


(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama)

Jumanne, 30 Mei 2023

WATUMISHI MAHAKAMA YA KAZI WAPATA ELIMU KUHUSU AFYA YA AKILI

Na Mwanaidi Msekwa-Mahakama Kazi

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina hivi karibuni alishiriki katika zoezi la utoaji elimu kuhusu Afya ya Akili lililoongozwa na Msaikolojia kutoka Sally International Hospital, Bi. Eva Msaki.

Mafunzo hayo yalihudhuriwa na washiriki 32, wakiwemo Majaji, viongozi na watumishi wa Mahakama hiyo ambayo yalifanyika katika Ukumbi wa Mikutano. Bi Msaki alifafanua kwa kina maana ya afya ya akili, visababishi na sababu zinazopelekea mtu kupata ugonjwa wa akili.

Katika mada yake, Msaikolojia huyo aliweza kutaja tabia na mtindo wa maisha utakaomwezesha mtumishi kuepukana na ugonjwa huo, ikiwemo kuzingatia ulaji wa mlo kamili na kufanya mazoezi mara kwa mara. Pia alisisitiza kuwa mazingira na jamii inayomzunguka mtu ni kisababishi kikubwa cha kupata ugonjwa wa akili.

Vile vile, Bi. Msaki alieleza njia za kukabiliana na ugonjwa wa afya ya akili, huku aliruhusu watumishi kuuliza maswali mbalimbali ambayo yalijibiwa vema.

Akichangia mada hiyo, Mhe. Dkt. Mlyambina aliwaeleza watumishi kujitambua na kujua kwamba wote wana akili, hivyo inawapasa kujiamini katika kutekeza majukumu yao.

Akizungumza wakati wa kuahirisha mafunzo hayo, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, Mhe. Biswalo Mganga alimshukuru Bi. Msaki kwa kutoa mada hiyo nzuri na aliwasisitiza watumishi kufuatilia elimu hiyo.

Alimuomba Mtaalamu huyo kurudi tena na kutoa mada hiyo kwa undani ili kuwawezesha wafanyakazi kupata maarifa ya namna ya kuwahudumia wadau.

Utoaji wa elimu hiyo ni mwendelezo wa mafunzo yanayoendelea kutolewa kwa wadau na watumishi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi yakisimamiwa na Kamati ya Elimu ya Ndani.

Katika hatua nyingine, aliyekuwa Mtendaji katika Divisheni hiyo, Bw. Samson Mashalla alitumia nafasi hiyo kuwaaga watumishi baada ya kuhamishiwa katika Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke. Amewashukuru watumishi hao kwa ushirikiano waliompa katika kipindi chote alipokuwa akihudumu kwenye Mahakama hiyo.

Msaikolojia kutoka Sally International Hospital, Bi. Eva Msaki (juu na chini) akitoa elimu ya afya ya akili.

Viongozi na watumishi wakifuatilia darasa.

 Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, Mhe. Biswalo Mganga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na aliyekuwa Mtendaji wa Mahakama hivyo, Bw. Samson Mashalla (kulia), Bi Eva Msaki (kushoto) na watumishi wengine.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama)

MASHAURI 35 YA RUFANI KUSIKILIZWA MKOANI KIGOMA KWA WIKI TATU

Na Aidan Robert-Mahakama -Kigoma

Jumla ya mashauri 35 ya Rufani yatasikilizwa katika kipindi cha wiki tatu kwenye kikao kilichoanza jana mkoani Kigoma cha Majaji watatu wa Mahakama ya Rufani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana Mjini Kigoma na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Mhe. Daines Lyimo kati ya mashauri hayo ya Jinai ni 12, madai 12 na mashauri ya maombi ni 11.

Alisema kuwa kikao hicho kimepanga kuhakikisha  kinasikiliza mashauri 3 hadi 4 na kuyamalizwa kwa kila siku.

Aidha mashauri yote yatasikilizwa kwa muda wa wiki tatu mfululuzo, kuanzia leo tarehe 29 Mei, 2023 mpaka tarehe 16 June, 2023.

Aidha Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani alisema hii ni mara ya tatu kwa Mkoa wa Kigoma kupangiwa kikao hiki toka mahakama ya rufani kuzinduliwa mnamo Mei, 2021, ambapo kwa mara ya kwanza ilizinduliwa Rasmi na Mhe. Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahimu Hamis Juma, toka kuanzishwa mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Kigoma.

Alisema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati ya Mahakama ya Tanzania wa  kuhakikisha inamaliza mashauri mengi zaidi katika kanda zote kwani Majaji wamejipanga vyema na kikazi zaidi ili kuwapa watanzania haki kwa wakati ili waendelee na shughuli zao za kujenga uchumi wa nchi bila kupoteza muda mahakamani.

Kwa upande wake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe Lameck Mlacha, alisema Mahakama hiyo inayoa miundombinu ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA) ambayo itawasaidia Majaji hao kwa ajili ya kufanikisha vikao vyao.

Jopo hilo la Majaji wa Rufani ambalo linaongozwa na Mhe. Jaji, Stella Mugasha,(Mwenyekiti)  pamoja  na  Mhe. Jaji Barke  Sehel, na Mhe. Abrahaman Mwampashi  limewasili na kupokelewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe Lameck Mlacha akishirikiana na Watumishi wa Kanda ya Kigoma .

Majaji wa Mahakama ya Rufani  Jaji, Stella Mugasha,(katikati)  kiwa na  Mhe. Jaji Barke  Sehel(kushoto), na Mhe. Abrahaman Mwampashi(kulia) wakijadiliana jambo kabla ya kuanza kusikiliza mashauri ya Rufani jana Mjini Kigoma.
Jaji wa Rufaa Mhe. Stella Mugasha , ambaye ni Mwenyekiti wa kikao cha kusikiliza mashauri ya rufani mkoani Kigoma akiwa amekati katika ofisi yake mara baada ya kupokelewa Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma kwaajili ya kikao cha Mahakama hiyo kilichopangwa kuanza hii jana Tarehe 29, Mei, 2023.
Wakili Bw.Gabriel Kabuguzi, akijiandaa kuingia katika ukumbi wa Mahakama kuu Kanda ya Kigoma kuwawakilisha wateja wake katika mashauri ya jana yatakayo sikilizwa mahakama kuanza asubuhi ya jana Tarehe29, Mei,2023
Wakili  Bw.Sadick Aliki, akiwa katika ukumbi wa Mahakama Kuu kanda ya Kigoma akisubiri kuanza kwa kikao cha Rufaa jana tarehe29, Mei, 2023.

 Mawakili na waendesha Mashitaka wa Serikali wakielekea kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma kwa ajili ya kufuatilia mashauri ya Rufani yaliyoanza jana tarehe 29 Mei 2023.

 

JAJI DKT. NDIKA AZINDUA TOLEO LA TATU MFUMO WA KUTUNZA MAAMUZI

Na. Innocent Kansha-Mahakama

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, Mhe. Dkt. Gerald Ndika jana tarehe 29 Mei, 2023 amezindua Tovuti toleo la tatu la mfumo maalumu wa kutunza maamuzi ya kimahakama ujulikanao kama TanzLII wenye kauli mbiu isemayo ufikiaji na upatikanaji bure wa Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania kwa njia ya Mtandao “TanzLII - Access Court Decisions and Laws of Tanzania for Free”.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke Mkoa wa Dar es Salaam na kuhudhuriwa na machampioni wa mfumo huo, wakiwemo Majaji wa Mahakama wa Mahakama ya Rufani na wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Makatibu wa Sheria wa Majaji na Wakutubi, Mhe. Dkt. Ndika alisema kuwa ni furusa muhimu kuzindua mfumo huo mpya unaofanya kazi kwa takribani miaka tano sasa kwa ufanisi mkubwa.

“Natambua kuwa mfumo huu tunaouzindua leo ulioboreshwa wenye muonekano mpya ni toleo la tatu wenye uwezo wa kufanya kazi nyingi zaidi ikilinganishwa na ule wa awali na sasa tutaanza kutumia toleo hili la mfumo unaotumia lugha mbili kwa maana ya Kiswahili na Kiingereza hapo awali tulikuwa tukitumia mfumo wa kiingereza pekee”, alisema Mhe. Dkt. Ndika

Mhe. Dkt. Ndika aliongeza kuwa, mfumo huo sasa unamuonekano wa kuvutia sana, unaweza pia kupatikana kupitia simu janja ya kiganjani tofauti na ule mfumo ulipita ilikuwa sio rahisi kwa watumiaji kutumia kupitia simu ya mkononi.

“Mfumo huu mpya ni rafiki kwa mtumiaji unatoa fursa kwa mtu yeyote kuyafikia maamuzi ya kimahakama kwa njia nyepesi na unatoa matokeo sahihi zaidi kwa mtumiaji yaani mtafiti anayetafuta taarifa fulani za kimaamuzi ama kisheria, unatoa matokea sahihi na kwa haraka binafsi nimeshautumia”, alifafanua Jaji Dkt. Ndika.

Jaji Dkt. Ndika alitanabaisha kuwa, mfumo huo unasifa ya kipekee, unatumia kiungo maalum “hyperlink” unayomwezesha mtafiti kufanya kazi kutoka dirisha moja hadi jingine wakati wa utafiti kwa njia rahisi zaidi. Tofauti na mfumo uliopita haukuwa na kiunganishi hicho.

“Kupitia mfumo huu mpya utasaidia kutunganisha na kuboresha mahusiano ya Mahakama za kikanda kama vile Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariaki na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kwenye eneo la maamuzi na sheria mbalimbali zilizotungwa”, aliongeza Mhe. Dkt. Ndika

Aidha, mfumo huo hautaishia kwa wataalum wa sheria na watafiti bali unalenga hasa kumnufaisha mwananchi wa kawaidi ambaye atataka kupata nakala ya maamuzi ama sheria iliyokwisha pakiwa kwenye mfumo huo bila kutumia gharama, muda na kumuondolea usumbufu.

Awali, akisoma histori fupi ya maendeleo ya matumizi ya mfumo wa TanzLII kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, Jaji wa Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Manyara, Mhe. John Kahyoza alisema, ushirikianao na mahusiano mema baina ya Mahakama ya Tanzania na Chuo Kikuu cha Cape Town Afrika ya Kusini yamekuwa na tija kwa kuimarisha matumizi ya mfumo huo wa kutunza maamuzi ya kimahakama TanzLII na kutengeneza namna bora ya ufikiaji na upatikanaji bure wa Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania kwa njia ya Mtandao.

Mhe. Kahyoza alisema kuwa, kwa kipindi chote Mahakama imeendelea kuchukua utaalam na uzoefu wa namna bora ya kuendesha na kuratibu maendeleo endelevu ya mfumo wa TanzLII hadi sasa unapoziduliwa mfumo huo wa toleo la tatu.

“Natambua jitihada za wadau wote SafLII, AfricnLII, Chuo Kikuu cha Cape Town Afrika ya Kusini na Mahakama ya Tanzania licha ya changamoto tumeendelea kushirikiana na tumeweza kuimarisha mfumo huu wa kutunza maamuzi yaani TanzLII”, alisema Jaji Kahyoza

Mhe. Kahyoza aliondeza kuwa, mfumo huo unawawezesha Majaji, Mahakimu, wanafunzi wa sheria wanataaluma ya sheria, mawakili na wananchi wa kawaida ufikiaji na upatikanaji bure wa maamuzi, sheria na kanuni za Tanzania kwa njia ya mtandao na kuifanya kuwa njia ya ufuatiliaji na usimamizi kwa viongozi wa Mahakama na uora wa mfumo umethibitisha kuwa kiungo muhimu kwa utawala wa sheria nchini.

Sambamba na uzinduzi wa mfumo TanzLII, Mahakama ya Tanzania imeingia makubaliano ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Cape Town Afrika ya Kusini wenye lengo kuendeleza juhudi za kuboresha mfumo maalumu wa kutunza maamuzi ya kimahakama TanzLII na kutengeneza namna bora ya ufikiaji na upatikanaji bure wa Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania kwa njia ya Mtandao “TanzLII - Access Court Decisions and Laws of Tanzania for Free”.

Makubaliano hayo yamesainiwa jana tarehe 29 Mei, 2023 Mahakama Kuu Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke jijini Dar es salaam kati ya Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma kwa upande wa Mahakama ya Tanzania pamoja na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva. Huku utiwaji saini huo ukishudiwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika, jana tarehe 29 Mei, 2029 amezindua toleo la tatu la tovuti mpya ya mfumo wa kutunza maamuzi ya kimahakama wenye lengo la kuboresha ufikiaji na upatikanaji bure wa Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania kwa njia ya Mtandao “TanzLII - Access Court Decisions and Laws of Tanzania for Free”,  katika hafla iliyofanyika Mahakama Kuu Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke jijini Dar es salaam. 


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Manyara na Championi wa mfumo wa TanzLII Mhe. John Kahyoza (wa kwanza kulia) akitoa historia fupi ya mfumo huo wakati wa uzinduzi wa toleo la Tatu la mfumo huo, kushoto ni Kaimu Mkuu wa huduma za Maktaba ya Tanzania, Mhe. Kifungu Mrisho.


Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na wa Mahakama Kuu (walioketi mstari wa mbele) waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa tovuti ya kutunza maamuzi TanzLII toleo la Tatu sambamba na utiaji saini makubaliano ya ushirikiano wa lengo la kuboresha ufikiaji na upatikanaji bure wa Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania kwa njia ya Mtandao “TanzLII - Access Court Decisions and Laws of Tanzania for Free”, wakimsikiliza Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Manyara Mhe. John Kahyoza (hayupo pichani) akitoa historia fupi ya mchakato wa uanzishwaji wa mfumo wa kutunza maamuzi TanzLII wakati wa hafla hiyo.


Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika (wa nne kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya Majaji walishiriki hafla hiyo, wengine ni Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Jacobs Mwambegele (wa pili kushoto), Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa tatu kulia), Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Manyara Mhe. John Kahyoza (wa kwanza kulia), Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Temeke (IJC) Mhe. Asina Omari (wa pili kulia), Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Iringa Mhe. Said Kalunde (wa kwanza skushoto) pamoja na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (wa nne kushoto) akiwa na Meneja Mradi wa sheria Africa Bi. Morina Chindia (wa tatu kushoto).
 
Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika (wa sita kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya machampioni wa mfumo wa kutunza maamuzi ya kimahaka TanzLII wengine katika picho hiyo ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma (wa tano kulia) na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (wa saba kushoto)   walishiriki hafla hiyo.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma (kulia)kwa upande wa Mahakama ya Tanzania akitia saini makubaliano ya ushirikiano ya kuimarisha mfumo wa kutunza maamuzi ya kimahakama pamoja na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (kushoto). Huku utiwaji saini huo ukishudiwa na  Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika, jana tarehe 29 Mei, 2029 katika hafla iliyofanyika Mahakama Kuu Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke jijini Dar es salaam. 


Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma (kulia) na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (kushoto) kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town Afrika ya kusini, akionyesha hati zililzosainiwa za kukubali mashirikiano hayo.


Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma (kulia) akibalisha hati za makubaliano mara baada ya kutia saini na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (kushoto) kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town Afrika ya kusini, nyuma yao ni Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika aliyeshuhudia utiaji wa saini makubaliano hayo.


Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva ( kushoto) akiwa na Meneja Mradi wa sheria Africa Bi. Morina Chindia (Kulia) wakifuatilia shughuli hiyo.

(Picha na Innocent Kansha-Mahakama)
 

Jumatatu, 29 Mei 2023

MAHAKAMA YA TANZANIA, CHUO KIKUU CAPE TOWN KUSHIRIKIANA KUBORESHA MFUMO WA KUTUNZA MAAMUZI

Na. Innocent Kansha-Mahakama

Mahakama ya Tanzania imeingia makubaliano ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Cape Town Afrika ya Kusini wenye lengo kuendeleza juhudi za kuboresha mfumo maalumu wa kutunza maamuzi ya kimahakama TanzLII na kutengeneza namna bora ya ufikiaji na upatikanaji bure wa Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania kwa njia ya Mtandao “TanzLII - Access Court Decisions and Laws of Tanzania for Free”.

Makubaliano hayo yamesainiwa leo tarehe 29 Mei, 2023 Mahakama Kuu Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke jijini Dar es salaam kati ya Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma kwa upande wa Mahakama ya Tanzania pamoja na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva. Huku utiwaji saini huo ukishudiwa na  Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika.

Tukio hilo lilienda sambamba uzinduzi wa Tovuti ya TanzLII iliyofanyiwa uboreshaji mkubwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika.

Habari picha na matukio mbalimbali yaliyojili katika shughuli hiyo.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma (kulia)kwa upande wa Mahakama ya Tanzania akitia saini makubaliano ya ushirikiano ya kuimarisha mfumo wa kutunza maamuzi ya kimahakama pamoja na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (kushoto). Huku utiwaji saini huo ukishudiwa na  Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika, leo tarehe 29 Mei, 2029 katika hafla iliyofanyika Mahakama Kuu Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke jijini Dar es salaam. 

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika, leo tarehe 29 Mei, 2029 amezindua toleo la tatu la tovuti mpya ya mfumo wa kutunza maamuzi ya kimahakama wenye lengo la kuboresha ufikiaji na upatikanaji bure wa Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania kwa njia ya Mtandao “TanzLII - Access Court Decisions and Laws of Tanzania for Free”,  katika hafla iliyofanyika Mahakama Kuu Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke jijini Dar es salaam. 

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma (kulia) akibalisha hati za makubaliano mara baada ya kutia saini na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (kushoto) kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town Afrika ya kusini, nyuma yao ni Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika aliyeshuhudia utiaji wa saini makubaliano hayo.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma (kulia) na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (kushoto) kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town Afrika ya kusini, akionyesha hati zililzosainiwa za kukubali mashirikiano hayo.

Majaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na wa Mahakama Kuu (walioketi mstari wa mbele) waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa tovuti ya kutunza maamuzi TanzLII toleo la Tatu sambamba na utiaji saini makubaliano ya ushirikiano wa lengo la kuboresha ufikiaji na upatikanaji bure wa Maamuzi, Sheria na Kanuni za Tanzania kwa njia ya Mtandao “TanzLII - Access Court Decisions and Laws of Tanzania for Free”, wakimsikiliza Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Manyara Mhe. John Kahyoza (hayupo pichani) akitoa historia fupi ya mchakato wa uanzishwaji wa mfumo wa kutunza maamuzi TanzLII wakati wa hafla hiyo.



Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika (wa nne kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya Majaji walishiriki hafla hiyo, wengine ni Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Jacobs Mwambegele (wa pili kushoto), Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa tatu kulia), Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Manyara Mhe. John Kahyoza (wa kwanza kulia), Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Temeke (IJC) Mhe. Asina Omari (wa pili kulia), Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Iringa Mhe. Said Kalunde (wa kwanza skushoto) pamoja na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (wa nne kushoto) akiwa na Meneja Mradi wa sheria Africa Bi. Morina Chindia (wa tatu kushoto).
 

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na Kamishina wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Dkt. Gerald Ndika (wa sita kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya machampioni wa mfumo wa kutunza maamuzi ya kimahaka TanzLII wengine katika picho hiyo ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Wilbert Martin Chuma (wa tano kulia) na Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva (wa saba kushoto)   walishiriki hafla hiyo.


 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Manyara na Championi wa mfumo wa TanzLII Mhe. John Kahyoza (wa kwanza kulia) akitoa historia fupi ya mfumo huo wakati wa uzinduzi wa toleo la Tatu la mfumo huo, kushoto ni Kaimu Mkuu wa huduma za Maktaba ya Tanzania, Mhe. Kifungu Mrisho.


Mkurugenzi wa AfricanLII Bi. Mariya Badeva ( kushoto) akiwa na Meneja Mradi wa sheria Africa Bi. Morina Chindia (Kulia) wakifuatilia shughuli hiyo.

(Picha na Innocent Kansha-Mahakama)
 



Ijumaa, 26 Mei 2023

WADAU WA MAHAKAMA MOROGORO WASTAAJABISHWA NA MABORESHO; WASIFU JITIHADA ZA MAHAKAMA

Na Evelina Odemba – Mahakama Morogoro

Wananchi waliofika kupata huduma katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Morogoro wamepongeza jitihada za Mhimili huo kufuatia maboresho makubwa yaliyofanyika kwa upande wa utoaji haki na miundombinu yake.

Pongezi hizo zilitolewa jana tarehe 25 Mei, 2023 wakati wa kipindi cha elimu kinachotolewa katika Kituo hicho kuanzia Jumatatu mpaka Alhamisi ya kila wiki ambapo ndani ya wiki hii mada kubwa ilikuwa ni maboresho yanayofanywa na Mahakama ikiwemo mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Akizungumza wakati wa kutoa elimu kwa wateja hao hivi karibuni, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Livin Lyakinana aliwaeleza kuwa Mahakama imeboresha mifumo yake ili kuweza kumsaidia mteja kupata haki kwa wakati.

“Sasa hivi mteja anaweza kukaa nyumbani kwake na akafuatilia kesi yake mahakamani kwa njia ya mtandao, hii inampunguzia mwananchi gharama za kulipia usafiri ili kumfikisha mahakamani” alieleza Mhe. Lyakinana.

Aidha Mhe. Lyakinana aliwaelekeza kwamba, kwa sasa Mahakama imeanzisha mfumo mpya wa ‘Sema na Mahakama’ ambao unampa mteja uhuru wa kutoa malalamiko, maoni na mapendekezo yake ili kuisaidia Mahakama kuboresha huduma zake bila kuingilia uhuru wake.

Elimu hiyo imetolewa kuanzia terehe 23 Mei, 2023 hadi tarehe 25 Mei, 2023 ambapo sanjari na kufundishwa kuhusu maboresho hayo pia walipata fursa ya kutembelea  moja ya kumbi za Mahakama ya Wazi (Open Court) zilizoko katika jengo hilo ambapo walijionea namna ukumbi huo ulivyojengwa kisasa na baada ya kuingia ndani ya ukumbi huo hawakusita kuonesha mshangao na kuimwagia sifa Serikali na Uongozi wa Mahakama kwa kuboresha miundombinu ya maeneo ya Utoaji Haki.


Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Livin Lyakinana 
(kulia) akitoa elimu kwa wananchi waliofika kupata huduma katika Mahakama hiyo jana tarehe 25 Mei, 2023.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Livin Lyakinana akiendelea kutoa elimu kwa wananchi (hawapo katika picha) kuhusu mada ya Maboresho ya Mahakama.
Wananchi wakimsikiliza Mhe. Lyakinana (hayupo katika picha).
Wananchi waliofika kupata huduma ya Mahakama katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki 9IJC) Morogoro wakisikiliza mada inayotolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Livin Lyakinana (hayupo katika picha).

Muonekano wa jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Morogoro.

(Habari hii imehaririwa na Mary Gwera, Mahakama)