Na. CHRISTOPHER MSAGATI- Mahakama, Manyara
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam
Mambi amefanya ziara ya Ukaguzi katika Mahakama zilizopo Wilayani Mbulu na Hanang’
na kuwasisitiza watumishi kufanya kazi kwa uadilifu, ueledi na uwajibikaji ili
kuhakikisha malengo ya Mahakama yanatimia ipasavyo.
Hii
ni ziara ya kwanza ya ukaguzi kwa Mhe. Dkt. Mambi tangu ahamie Mahakama Kuu,
Masjala Ndogo ya Manyara kama Jaji Mfawidhi akitokea Mahakama Kuu Masjala Ndogo
ya Tabora ambapo pia alikuwa Jaji Mfawidhi.
Akizungumza
na watumishi katika Mahakama ya Wilaya ya Mbulu, Mhe. Dkt. Mambi aliwaasa
watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na nidhamu wanapokuwa ofisini na hata
wanapokuwa nje ya Ofisi.
“sisi
watumishi wa Mahakama tunapaswa kuishi kwa nidhamu kuanzia ofisini na hata tunapokuwa
nje ya Ofisi zetu, tunatarajiwa kuwa vioo vya jamii kwa wadaawa wetu na watu
wote tunaowahudumia. Kwa misingi hii, maadili na nidhamu lazima vitutawale
popote tutakapokuwa”, alisema Mhe. Dkt. Mambi.
Akizungumza
kwa nyakati tofauti na Mahakimu wa vituo vilivyokaguliwa, Naibu Msajili wa
Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava aliwasisitiza
Mahakimu kuhakikisha kuwa wanahuisha taarifa za mashauri yao kwenye mfumo kila
siku bila kukosa na kuhakikisha kuwa wanatoa nakala za Hukumu ipasavyo.
“Katika
kipindi hiki cha matumizi makubwa ya TEHAMA, hatutarajii kuona kuwa tuna madeni
ya kuhuisha mashauri katika mfumo rasmi uliowekwa hivyo ninawasihi mlichukulie
suala hili kwa uzito wa hali ya juu. Vilevile hatutarajii tukifika katika
magereza yetu tukutane na mfungwa ambaye analalamika kukosa nakala ya hukumu
katika zama hizi”, alisema Mhe. Mnzava.
Kwa
upande wa Wilaya ya Mbulu, Mahakama zilizokaguliwa ni Mahakama ya Wilaya Mbulu,
Mahakama za Mwanzo Daudi, Dongobesh, Haydom na Gereza lililopo wilayani Mbulu.
Kwa
upande wa Wilaya ya Hanang, Mahakama ambazo zilikaguliwa ni Mahakama ya Wilaya
ya Hanang, Mahakama za Mwanzo Katesh, Bassotu na Endasak pamoja na mradi wa
ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Hanang ambao unaendelea kwa sasa.
Katika
hatua nyingine, Mhe. Dkt. Mambi alifanikiwa kufika katika Ofisi ya Mkuu wa
Wilaya ya Mbulu na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael
Semindu pamoja na kamati ya Wilaya ya Ulinzi na usalama, ambapo Mkuu wa Wilaya
huyo aliahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Mahakama hususan kusaidia
upatikanaji wa viwanja kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama na upatikanaji wa hati
za viwanja hivyo.
Aidha,
Mhe. Dkt. Mambi alitumia pia ziara hiyo kutambulisha viongozi wapya wa Mahakama
Kuu Masjala Ndogo ya Manyara ambao ni yeye mwenyewe pamoja na Naibu Msajili wa
Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava ambaye awali alikuwa
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara.
Pia
katika ziara hiyo, viongozi wengine walioambatana nao ni Naibu Msajili wa
Mahakama Kuu anayehudumu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara Mhe. Mariam
Lusewa pamoja na Mtendaji wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Bi.
Nyanzobe Hemedi.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi
(aliyesimama) akizungumza na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbulu (hawapo
pichani) katika ziara ya Ukaguzi iliyofanyika wilayani hapo, kushoto ni Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava na kulia
ni Naibu Msajili anayehudumu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara Mhe Mariam
Lusewa.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa kwanza kulia) akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, aliyekaa mbele ni Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa tatu
kushoto) akiendelea na zoezi la ukaguzi katika Mradi wa Ujenzi katika Mahakama
ya Wilaya ya Hanang.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi
akisalimiana na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Hanang mara baada ya kufika
kituoni hapo kwa ajili ya Ukaguzi.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi akiongoza
zoezi la ukaguzi katika Mahakama ya Mwanzo Bassotu wilayani Hanang.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa pili
kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Haydom
iliyopo Wilayani Mbulu.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wanne
kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Mahakama Kuu, Masjala
Ndogo ya Manyara pamoja na viongozi waandamizi wa Gereza la Wilaya ya Mbulu
mara baaada ya kufanya Ukaguzi Gerezani hapo.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa tatu
kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya
Hanang.
Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara, Mhe. Charles Mnzava (aliyesimama)
akichangia neno wakati walipo mtemebelea Ofisini Mkuu wa Wilaya ya Mbulu.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi
(aliyesimama katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya
Mwanzo Dongobesh wilayani Mbulu.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha-Mahakama)




































