- Yawaelimisha Wadau wa Mahakama umuhimu wa Usuluhishi kupitia Kongamano maalum
Na NAUMI SHEKILINDI, Mahakama-Simiyu
Mahakama
Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Simiyu nayo imeungana pamoja na Mahakama
nyingine nchini kuadhimisha Wiki ya Usuluhishi nchini ambayo iliyoanza tarehe 14
Aprili, 2026 na kufikia tamati tarehe leo tarehe 17 Aprili, 2026.
Katika
Maadhimisho hayo, Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Simiyu imefanikiwa kufanya
kongamano la Usuluhishi tarehe 16 Aprili, 2026 likiongozwa na Kaimu Jaji
Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. Hussein Mtembwa pamoja na wadau mbalimbali wa
Mahakama wakiwemo Watumishi wa Mahakama, Polisi, Taasisi za kibenki, Taasisi ya
Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),
Uhamiaji, Wakala wa Vipimo, TUGHE, Viongozi wa dini na wananchi.
Mhe. Mtembwa alifungua kongamano hilo na
kueleza kuwa lengo la Wiki ya Usuluhishi ni kupunguza muda wa mashauri mahakamani,
kupunguza gharama za mashauri na kuwezesha suluhu ya haraka na ya kirafiki, “Mfano
benki wanapofanya usuluhishi baina ya benki na mteja inajenga mahusiano mema na
ya kirafiki baina ya benki na mteja” amesisitiza Jaji Mtembwa.
Aidha,
Mhe. Mtembwa aliongeza kwa kusema, “Haki sio tu kuhukumu bali pia kusuluhisha,”
alieleza kuwa usuluhishi una mchango mkubwa katika kufikia Dira ya Taifa ya
Maendeleo 2050 kwani amani, usalama na utulivu ndio msingi utakaojenga umoja
ndani ya nchi, vilevile Mahakama imejipanga kukuza dhana ya usuluhishi kama
ilivyo kwenye Ibara ya 107A(2)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
(1977) na kwamba ana imani kongamano hilo litaleta tija kwa jamii.
Naye,
Naibu Msajili Mfawidhi, Mhe. Elimo Daniel Massawe alitoa mada juu ya usuluhishi
wa migogoro ya Tanzania ambapo alieleza maana ya usuluhishi, lengo, faida zake
pamoja na mbinu za kufanya usuluhishi.
Mhe.
Massawe alieleza kwamba, usuluhishi ni sehemu rasmi ya mfumo wa sheria
unaotambuliwa na taratibu za Mahakama nchini, pia ni utaratibu unaowapa
wahusika nafasi ya kusuluhisha mgogoro wao kwa hiari na kwa msaada wa mtu wa
kati asiye na upendeleo, lakini pia mpatanishi sio mtoa uamuzi bali wahusika
ndio wenye mamlaka ya mwisho.
Wakati
wa kuhitimisha kongamano hilo, Kaimu Jaji Mfawidhi alisema kuwa, kongamano hilo
litakua chachu katika kuimarisha usuluhishi na kuwaomba wadau waende kuwa Mabalozi
wa Usuluhishi kabla ya wadaawa kufika
Mahakamani.
Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Simiyu, Mhe. Hussein Mtembwa akifungua Kongamano la Usuluhishi kwa wadau waliohudhuria
kongamano hilo lililofanyika tarehe 16 Aprili, 2026 katika Mahakama hiyo.
Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo Simiyu, Mhe. Elimo Massawe (aliyesimama) akimkaribisha Kaimu Jaji Mfawidhi, Mhe. Hussein Salum Mtembwa (katikati) kuzungumza na wadau wakati wa Kongamano hilo.
Wadau mbalimbali waliohudhuria kongamano wakisikiliza mada kutoka kwa Mhe. Elimo Daniel Massawe, Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Simiyu.
Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Simiyu, Mhe. Hussein Mtembwa (katikati mstari wa mbele ) akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali aliohudhuria Kongamano la Usuluhishi katika Mahakama Kuu Masjala ndogo Simiyu.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Mara)
































.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)