Ijumaa, 11 Julai 2025

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ATEMBELEA BANDA LA MAHAKAMA MAONESHO YA 77

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro leo tarehe 11 Julai 2025 ametembelea Banda la Mahakama katika maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.

Mhe. Dkt. Ndumbaro akiwa kwenye mabanda hayo alijionea watumishi wa Mahakama wanaotoa elimu kwa Wananchi mbalimbali wanaofika kupewa elimu hiyo ya kisheria na taratibu mbalimbali za uendeshaji wa shughuli za kimahakama.

“Mimi nimekuwa mdau na mpiga debe wa maboresho ya shughuli za Mahakama kwa mda mrefu na nitaendelea kufanya hivyo kwani Mahakama ni chombo chetu sote, vilevile niwapongeze kwa kazi kubwa mnayofanya ya kutoa elimu kwa umma hili ni jambo jema sana,” amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Itakumbukwa kwamba, maonesho hayo yatahitimishwa tarehe 13 Julai, 2025 na Waziri huyo akatoa rai kwa wananchi mbalimbali kuendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), 2025 yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.





































(PICHA NA INNOCENT KANSHA - Mahakama 77)



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni