Alhamisi, 15 Aprili 2021

MRADI WA UJENZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA MAHAKAMA WASHIKA KASI

· Wasajili na Watendaji wa Mahakama watembelea mradi huo Dodoma

Na Mary Gwera, Mahakama-Dodoma

Mradi wa ujenzi wa jengo la makao makuu ya Mahakama ya Tanzania unaojengwa katika eneo la ‘NCC Link’ jijini Dodoma unaendelea vizuri.

Akizungumza na baadhi ya Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama waliotembelea mradi huo wa ujenzi jana Aprili 14, 2021, Mhandisi Mkazi kutoka timu ya Washauri Elekezi, Mhandisi Evarist Mushi alisema kuwa Mradi huu unajumuisha ujenzi wa majengo matatu (3) yanayounganishwa na jengo la utawala.

Mhandisi Mushi amesema kuwa mradi huu unajumuisha jengo la Mahakama ya juu ‘Supreme court’ ambapo anaeleza kuwa jengo hili lipo katika hatua ya ‘floor’ ya chini ‘ground floor’ ambapo nguzo zote zimekamilika pamoja na msingi wa jengo hilo.

“Kwa upande wa jengo la Mahakama ya Rufani, lipo katika hatua ya ghorofa ya kwanza ‘first floor’ ambao ‘elevated ground floor, ground floor, basement floor’ na msingi tayari zimekamilika,” alisema Mhandisi Mushi.

Aidha, kwa upande wa jengo la Mahakama Kuu, Mtaalamu huyo amesema kuwa msingi pamoja na ‘floor’ za chini zimeshakamilika ambapo kwa sasa zinafungwa nguzo za kwenda ghorofa ya kwanza ‘first floor’ ya jengo hilo.

Aliongeza kuwa jengo la Makao Makuu ‘HQ’ lipo kwenye hatua ya msingi na maandalizi yote ya chuma yapo tayari.

Kwa mujibu wa Mtaalam huyo ujenzi wa mradi huu ulianza rasmi mwezi Julai, 2020 na unatarajia kukamilika Desemba 2022.

Muonekano wa sehemu za jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania linaloendelea kujengwa jijini Dodoma.

Mhandisi Mkazi kutoka timu ya Washauri Elekezi, Mhandisi Evarist Mushi (mwenye suruali ya kaki) akizungumza na sehemu ya Naibu Wasajili, Watendaji wa Mahakama na Maafisa wengineo wa Mahakama waliotembelea kujionea maendeleo ya Mradi wa ujenzi wa Makao makuu ya Mahakama ya Tanzania.



Maelezo yakitolewa kuhusu maendeleo ya ujenzi.

 

 

 

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni