Na Magreth Kinabo – Mahakama
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe.Prof. Ibrahim Hamis Juma amewasihi wafanyakazi wa Mahakama ya Tanzania kupitia wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi na wadau wote katika mnyororo wa haki, kutambua kuwa jukumu la utoaji haki ni sehemu muhimu ya maendeleo ya nchi yetu na watu wake.
Akizungumza leo
Juni29, mwaka huu katika mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Mahakama hiyo wa
siku mbili unaoendelea katika ukumbi wa LAPF jijini Dodoma, Jaji Mkuu alisema utekelezaji
wa wajibu
wa wafanyakazi hao ni katika utoaji haki unaimarisha utawala wa
sheria na pia utawala bora.
“Utekelezaji wa wajibu wenu unachangia pia
uwepo wa amani ya nchi, na huimarisha uchumi na ustawi wa Watanzania. Kila mtumishi wa Mahakama atambue kuwa yeye ni sehemu ya mnyororo wa utoaji haki.
Unapotimiza wajibu wako kikamilifu na kwa uadilifu, mnyororo wa haki unakuwa imara na
kufanikisha uwekezaji na pia shughuli za biashara za ndani na za kimataifa,” alisema Prof. Juma.
Aliongeza kwamba hata
watalii wanaongezeka kutokana na kazi nzuri ya Mhe. Samia Suluhu Hassan kupitia
mkakati wa ‘Royal Tour’, wanafurahia kuja Tanzania kutokana na kuwepo kwa amani
ambayo inatokana na watumishi waadilifu katika mnyororo wa utoaji Haki.
Alisema kila mtumishi wa
Mahakama inabidi afahamu mwelekeo na Dira ya Mahakama. Hivyo wajumbe
hamna budi kuendelea kuwaelimisha watumishi wote wapi Mahakama ya Tanzania
inapoelekea.
Aliishukuru Serikali inayoongozwa
na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi inavyowezesha kwa hali na mali na ambavyo
inatoa kipaumbele kwa mahitaji ya Mhimili wa Mahakama, ambapo hivi karibuni
Serikali ya Tanzania imechukua tena Mkopo wa gharama nafuu wa dola za
Kimarekani milioni 90 (zaidi ya bilioni
Tsh 210) kwa ajili ya kuimarisha miundo mbinu ya Mahakama Tanzania kwa mwaka
ujao wa Fedha 2022/23.
“Ni vyema mkafahamu kuwa
katika jitihada za kuhakikisha mfumo matumizi ya fedha ni imara, nimejulishwa
kuwa, katika ujenzi wa vile Vituo 6 Jumuishi, baada ya vipimo vya mwisho
(re-measurement), tumeweza kuokoa zaidi ya bilioni Tsh 3.5. Fedha
zilizobakizwa kwenye ujenzi zimetumika kununulia vitendea kazi vingine ambavyo
vitazidi kumarisha ufanisi wetu katika utoaji haki,’’alisema.
Alisema kutokana na mabadiliko ya kasi ya teknolojia
wafanyakazi
wote wa Mahakama
na wadau wetu, kutokubali
kubaki nje ya Mradi
Mkubwa wa Serikali ukiwepo mradi mkubwa uitwao TANZANIA YA KIDIJITI (Tanzania
Digital Project) iliyoanza mwaka jana (2021).
Alifafanua kwamba ni wajibu wa Mwajiri namna
kutoa huduma kuweka programu za mafunzo endelevu ambayo yatawawezesha wafanyakazi wa kada
zote kuhama kutoka utoaji huduma kwa njia 13 zilizozowekwa hadi kutoa huduma
katika Mahakama ya Kidijiti au Mahakama Mtandao. Huku
akikitaka Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA),
kutafakari mafunzo hayo maalum.
”Katika kutekeleza hili hata
maeneo ya pembezoni yapewe kipaumbele na siyo maeneo ya mijini tu. Ni muhimu
sote tuwe kwenye safari moja na asiwepo atakayeachwa nyuma eti kwa kuwa yuko
kwenye Mahakama ya maeneo ya vijijini, ikiwemo kuwashirikisha wadau kwenye suala hilo, alisisitiza.
Aidha Jaji Mkuu huyo amlimtaka kila mtumishi kutafuta
maarifa ili kuweza kuwa mtumishi bora kwa kuwa hakuna wakati maarifa yanatosha.
Kwa
wale ambao wako karibu na vyuo vya elimu ya juu vinayotoa masomo ya
jioni ni vyema kuanza kuchangamkia fursa hii kuanzia majaji, mahakimu,
watendaji na watumishi wasaidizi.
Jaji Mkuu amewataka watumishi hao kujitokeza siku
ya Sensa tarehe 23 Agosti 2022 ili
kushiriki zoezi la kuhesababiwa.
Jaji Mkuu pia alisema ugonjwa wa UVIKO bado upo kwa viwango
vinavyobadilika hivyo aliwataka wale ambao hawajapata chanjo kuenda kuchanja.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof.
Ibrahim Hamis Juma akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa Baraza Kuu la
Wafanyakazi wa Mahakama ya Tanzania ambao umefunguliwa leo Jijini Dodoma.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel akitoa taarifa
masuala mbalimbali wakati wa mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Mahakama
ya Tanzania ambao umefunguliwa leo Jijini
Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Mahakama ya
Tanzania wakifuatilia kikao ambacho kinaendelea leo Jijini Dodoma.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya Pamoja na wajumbe wa mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Mahakama ya Tanzania kutoka Mahakama ya Rufaa ambao baada ya kufungua kikao hicho leo Jijini Dodoma.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof.
Ibrahim Hamis Juma (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya Pamoja na wajumbe
wa mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi
wa Mahakama ya Tanzania kutoka Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania baada ya kufungua mkutano huo leo Jijini Dodoma. kushoto ni Katibu wa baraza hilo, Bw. Ezra Kyando na kulia ni Katibu Msaidizi Bi. Christina Mlwilo.
(Picha na Vincent Tiganya -Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni