Na Catherine Francis – Mahakama Kuu Songea
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. Yose Mlyambina amewapongeza
watumishi wa Mahakama Kanda ya Songea kwa kuwa na mahusiano mazuri na wadau wa
Mahakama katika utekelezaji wa majukumu yo ya kila siku.
Mhe.
Mlyambina alitoa pongezi hizo hivi karibuni wakati wa kikao cha menejementi cha
robo ya kwanza ya mwaka 2022/2023. Jaji Mfawidhi huyo alisema kuwa amekuwa
akishuhudia mahusiano hayo yakiimarika kila siku kwa Mahakama kushiriki katika
matukio ya kijamii na ya kiserikali kama vile ushiriki kwenye sherehe za mbio
za mwenge.
Alibainisha
kuwa wadau mbalimbali wamekuwa wakishirikiana na Mahakama katika kutoa elimu ya
sheria kwa jamii kwa kutumia njia kadhaakama vile redio zilizopo ndani ya Mkoa
wa Ruvuma pamoja na kushirikiana katika michezo.
Kadhalika,
Mhe. Mlyambina aliwapongeza Mahakimu ambao wameendelea kufanya kazi vizuri kwa
kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ya Mkoa wa Ruvuma, hivyo kufanikiwa
kupunguza mashauri ya mlundikano kwa kiasi kikubwa kutoka 160 mwezi Januari
hadi kufikia mashauri 14 mwezi Septemba. “Hii inaonyesha ni kwa namna gani tumekuwa
mahusiano mazuri kati ya Mahakama na Taasisi nyingine,” alisema.
Vilevile
Mhe. Mlyambina alisema kuwa ili kuweza kuendelea kudumisha mahusiano hayo
mazuri ni vyema watumishi wa Mahakama Songea kujitafakari juu ya utendaji kazi wao,
kwa kujipima wenyewe kama huduma wanayotoa kwa jamii zinaridhisha na pia wapate
nafasi ya kujitathimini kama uwajibikaji wao ni wa uadilifu na unaofuata katiba
ya nchi au wanafanya kazi kwa mazoea.
Jaji
Mfawidhi huyo alisema kuwa kufanya hivyo kutapunguza malalamiko juu huduma
zipatikanazo mahakamani na kurudisha imani kwa jamii yote kwa ujumla kwa kuwa
Mahakama inafanya kazi kwa kufuata nguzo kuu tatu za Mpango Mkakati wa Mahakama
na hii ikiwa Nguzo ya tatu, hivyo hawana budi kuendelea kuiboresha kila siku.
Picha ya pamoja kati ya meza kuu na wajumbe wa kikao.
(Picha
na George Sabinus).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni