Na Lusako Mwang’onda-Mahakama Kuu, Iringa
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustafa Mohamed Siyani amewahimiza Watumishi wa Mahakama kujielekeza katika matumizi ya Teknolojia ya Habari na Maasiliano (TEHAMA) ili kwenda sambamba na maboresho mbalimbali yanayoendelea sasa katika Mahakama ya Tanzania.
Mhe. Siyani ametoa wito huo leo tarehe 30 Mei, 2024 alipokuwa anazungumza na Watumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa.
Amesisitiza kuwa hakuna namna yoyote kwa sasa mtumishi wa Mahakama kutoka Kada yoyote anaweza kufanya kazi mahakamani pasipokuwa na uelewa wa msingi katika masuala ya TEHAMA.
“Kwa sasa Mahakama yetu inaendelea kufanya maboresho mbalimbali ya kiutendaji, maboresho ambayo yanamlazimisha kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa anakuwa na ujuzi wa matumizi ya TEHAMA,” Mhe. Siyani amesema.
Pamoja na kuweka msimamo huo, Jaji Kiongozi amesisitiza nidhamu kazini, uadilifu katika utumishi, weledi kazini, utunzaji wa mazingira na mazoezi kwa ajili ya kuimarisha afya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni