Ijumaa, 19 Juni 2026

RAIS SAMIA AMUAPISHA DKT.JOHN ANTONY JINGU MTENDAJI MKUU MPYA WA MAHAKAMA

 Matukio katika picha-Uapisho wa Mtendaji Mkuu mpya wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu Ikulu-Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Dkt. John Anthony Jingu kuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.


Dkt. John Anthony Jingu akila kiapo kuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Dkt. John Anthony Jingu (kulia) akiapa Kiapo cha Maadili pamoja na Karani wa Baraza la Mawaziri Bw. Francis Petro Mossongo, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na viongozi mbalimbali baada ya kumuapisha Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Dkt. John Anthony Jingu, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Viongozi mbalimbali kwenye picha na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Anthony Jingu (aliyesimama nyuma), Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Dkt. John Anthony Jingu (kushoto) pamoja na Mtendaji Mkuu Mstaafu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel mara baada ya hafla ya Uapisho, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Juni, 2026.







JAJI FAHAMU MTULYA AKABIDHIWA OFISI MAHAKAMA KUU MASJALA NDOGO MBEYA

Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya

Aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga, tarehe 17 Juni, 2026 alimkabidhi rasmi Ofisi Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya baada ya kuripoti katika kituo chake hicho kipya cha kazi.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano, Mhe. Tiganga alitoa shukrani zake za dhati kwa viongozi na watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya na kumpongeza Mhe. Mtulya kwa kukabidhiwa majukumu hayo na kumtakia heri na mafanikio katika utekelezaji wa majukumu ya kuiongoza Masjala hiyo ya Mbeya.

Hafla hiyo ya makabidhiano ya Ofisi ilifanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, ikihudhuriwa na aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga, Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti na Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Wilaya Mkoa wa Mbeya.

Makabidhiano hayo yalijikita katika kukabidhi majukumu ya kiutawala, nyaraka mbalimbali za ofisi, na taarifa muhimu za utendaji kazi, zote zikiwa na lengo la kuhakikisha mwendelezo wa utoaji wa huduma za kimahakama na usimamizi wa shughuli za Mahakama katika Masjala Ndogo ya Mbeya.

Kwa upande wake, Mhe. Mtulya aliahidi kuendesha ofisi hiyo kwa weledi, kuendeleza ushirikiano baina ya watumishi na kuimarisha upatikanaji wa huduma za haki kwa wananchi wanaotumia Masjala hiyo ya Mbeya.

Makabidhiano hayo yanaashiria mwanzo wa awamu mpya ya uongozi katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, huku yakisisitiza dhamira ya kuendeleza ufanisi, uwazi na ubora katika utoaji wa huduma za Mahakama kwa wananchi.

Jaji Mfawidhi mpya Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya, (kushoto) na aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (kulia) wakikabidhiana Ofisi katika kituo cha Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya.

Jaji Mfawidhi mpya Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya, (kushoto) na aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (katikati) wakisaini nyaraka za makabidhiano ya Ofisi na kulia ni Jaji waMahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo akishuhudia kitendo hicho.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya katika hafla hiyo 

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti (kulia) akimpa kipande cha keki Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kushoto) ikiwa ni ishara ya kumkaribisha.



Sehemu ya watumishi walioshiriki katika  katika hafla hiyo ya makabidhiano ya Ofisi

Sehemu ya watumishi walioshiriki katika  katika hafla hiyo ya makabidhiano ya Ofisi

Aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (katikati) akikabidhiwa zawadi na Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti (kushoto).

Aliyekuwa Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga akikata keki ya kuagwa katika hafla hiyo.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya akikata keki ya ukaribisho katika hafla hiyo.

Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akipokelewa na Viongozi na watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)

 

MASHAURI 48 YA RUFAA ZA MADAI KUSIKILIZWA MBEYA

Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya.

Mahakama ya Rufani ya Tanzania inatarajia kuendesha Kikao cha usikilizaji wa mashauri 48 ya rufaa za madai katika Masjala Ndogo ya Mbeya kuanzia tarehe 18 Juni 2026 hadi tarehe 17 Julai, 2026.

Kikao hicho kitakua na jopo moja la Majaji wa Mahakama ya Rufani wakiongozwa na Jaji wa Rufaa ya Tanzania Mhe. Winifrida Beatrice Korosso, Majaji wengine katika jopo hilo ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Mary Calorine Levira na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Agnes Zephania Mgeyekwa.

Akiwasilisha taarifa katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu Mbeya, ambacho ni kikao cha maandalizi (Pre- Session Meeting), Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Mhe. Agatha Chugulu alieleza kuwa Jumla ya mashauri 48 ya Rufaa za madai yamepangwa kusikilizwa katika Masjala Ndogo ya Mbeya.

Aidha Mhe. Chugulu aliongeza kuwa, katika kuhakikisha ufanisi wa kikao hicho na kufikiwa kwa malengo yaliyokusudiwa ratiba ya kikao ilitolewa kwa wakati na Hati za kuitwa shaurini za wadaawa kwa ajili ya usikilizwaji wa mashauri zimesambazwa na juhudi za kuwapata wadaawa amabao hawajapatikana zinaendelea.

Naye, Mwenyekiti wa kikao hicho, Jaji wa Rufaa Mhe. Winifrida Korosso, alihitimisha kwa kuomba ushirikiano baina ya wadau na kusisitiza kuchunga muda wa kufika mahakamani.

“Lengo letu sote ni kupatikana kwa haki kama kuna changamoto yoyote wasilisha mapema ili tufikie lengo la kutafuta haki kwa pamoja ni matarajio yetu kuwa kutokana na mpango wa kusikiliza mashauri kuandaliwa mapema pamoja na ufuatiliaji wa karibu wa kila jalada, kikao hiki kitafikia malengo yaliyokusudiwa,” alisema Mhe. Korosso.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Viongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya akiwemo Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya, Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbeya, Mhe. Tedy Mlimba, Mawakili na Wadau wengine wa Haki Madai.

 

Mwenyekiti jopo Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Winifrida Beatrice Korosso (kulia), akiongoza kikao hicho, kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Agnes Zephania Mgeyekwa.

Viongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya waliohudhuria kikao hicho, ni Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (kulia), Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo (katikati) na Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti (kushoto).

Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Agatha Chugulu (kushoto) akiwasilisha taarifa katika kikao hicho na (kulia) ni Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbeya, Mhe. Tedy Mlimba. Ambaye katika kikao hicho alikaimu nafasi ya Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya.

Sehemu ya Wadau walioshiriki katika kikao hicho hoja mbalimbali kwa makini. 

Sehemu ya Wadau walioshiriki katika kikao hicho wakifuatilia kwa makini.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)

 


WATUMISHI KUTOKA CHUO CHA UFUNDI ARUSHA WATEMBELEA MAHAKAMA KUU DIVISHENI YA BIASHARA

Na KEVIN HEZRON-Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Dar es Salaam

Watumishi kutoka Chuo cha Ufundi Arusha (Arusha Technical College), jana tarehe 18 Juni, 2026, walitembelea Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu matumizi ya mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika usimamizi na utunzaji wa kumbukumbu.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu – Divisheni ya Biashara, Mhe. Kevin Mhina, aliwashauri wageni hao kufanya juhudi za kuhamia katika mfumo wa utendaji usiotegemea karatasi.

Alieleza kuwa matumizi ya mifumo ya kidijitali hurahisisha utekelezaji wa shughuli za Taasisi, huongeza ufanisi wa utendaji kazi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wakati.

Katika ziara hiyo,  Afisa TEHAMA Mwandamizi wa Mahakama Kuu – Divisheni ya Biashara, Bi. Amina Said, aliwasilisha mada kuhusu Kanzidata ya Hifadhi na Usimamizi wa Nyaraka (Record Centre Database) iliyobuniwa kwa lengo la kuboresha usimamizi wa majalada yaliyofungwa.

Aliwaeleza wageni hao changamoto zilizokuwepo kabla ya kuanzishwa kwa kanzidata hiyo, ikiwemo ugumu wa kufuatilia maeneo yalipohifadhiwa majalada na ucheleweshaji wa upatikanaji wa taarifa muhimu.

Aidha, aliwasilisha namna kanzidata hiyo inavyowezesha usajili wa majalada, utambuzi wa maeneo yanapohifadhiwa, ufuatiliaji wa Watumishi wanaochukua majalada kwa matumizi ya muda pamoja na utoaji wa taarifa na ripoti mbalimbali.

Kanzidata hiyo imeleta maboresho makubwa katika kuokoa muda, kuongeza ufanisi wa kazi, kupunguza upotevu wa majalada na kuboresha utoaji wa huduma.

Baada ya kupata mawasilisho na kushuhudia onesho la matumizi ya kanzidata hiyo, wageni hao walionesha kuvutiwa na ubunifu huo na kutoa pongezi kwa Mahakama Kuu – Divisheni ya Biashara kwa kutumia TEHAMA kutatua changamoto za kiutendaji.

Kwa pamoja walieleza kuwa wamejifunza mambo mengi yatakayowasaidia katika kuboresha mifumo ya usimamizi wa kumbukumbu katika Taasisi yao.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Mhe. Kevin Mhina akiwakaribisha Watumishi kutoka Chuo cha Ufundi Arusha.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Mhe. Kevin Mhina akizungumza na wageni kutoka Chuo cha ufundi Arusha. Kushoto kwake, ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Mhe. Susan Kihawa,  na Kulia kwake ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Bw. Anatory Kagaruki.

Bi. Amina Said, Afisa TEHAMA wa Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, akitoa wasilisho juu ya matumizi ya kanzidata ya usajili, usimamizi na utunzaji wa kumbukumbu.

Wageni kutoka Chuo cha ufundi Arusha, wakisikiliza kwa makini mawasilisho yaliyoandaliwa.

 

Picha na Iman Kasian, Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.

JAJI MFAWIDHI MPYA DODOMA AKABIDHIWA OFISI

Na ARAPHA RUSHEKE- Mahakama Kuu Dodoma.

Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dodoma imeingia katika awamu mpya ya uongozi jana tarehe 18 Juni, 2026, baada ya Jaji Mfawidhi mpya, Mhe. Joachim Tiganga, kukabidhiwa ofisi na mtangulizi wake, Mhe. Dkt. Juliana Masabo, ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Makabidhiano hayo yalijikita katika kukabidhi majukumu ya kiutawala, nyaraka mbalimbali za ofisi, na taarifa muhimu za utendaji kazi, zote zikiwa na lengo la kuhakikisha mwendelezo wa utoaji wa huduma za kimahakama na usimamizi wa shughuli za Mahakama katika Masjala Ndogo hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano, Mhe. Dkt. Masabo alimpongeza Jaji Tiganga kwa kukabidhiwa majukumu hayo na kumtakia mafanikio katika utekelezaji wake. 

“Nitumie fursa hii kumpongeza Mhe. Tiganga, tunaungana nawe kumshkuru mwenyezi Mungu kwa kibali ambacho amekupatia ili uje uhudumu hapa uwatumikie watu wake. Namshukuru pia Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Masaju, kwa imani kubwa ambayo ameionesha kwako na kuona ni muda sahihi kuweza kufanya kazi katika kituo hiki cha Dodoma,” alisema.

Naye Mhe Tiganga aliwashukuru Viongozi na Watumishi wote wa Mahakama Kuu Dodoma kwa mapokezi mazuri aliyoyapata na alisisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa haki kwa Wananchi.

Makabidhiano hayo yanaashiria mwanzo wa awamu mpya ya uongozi katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dodoma, huku yakisisitiza dhamira ya kuendeleza ufanisi, uwazi na ubora katika utoaji wa huduma za Mahakama kwa Wananchi kwa kuzingatia salamu ya Mahakama isemayo Uadilifu,Weredi na Uwajibikaji.


Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (wa kwanza kulia) akikabidhi ofisi kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga, wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu Dodoma Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC).


 

Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa kumpokea Jaji Mfawidhi mpya mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Mahakama Kuu Masjala ndogo Dodoma.

 


Meza Kuu ikiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (aliyepo katikati waliokaa), kulia kwake ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga na kushoto kwake ni Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Biswalo Mganga, ikiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mahakama Kuu Dodoma waliohudhuria hafla hiyo ya makabidhiano.


 

Meza Kuu ikiongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (aliyepo katikati waliokaa), kulia kwake ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga na kushoto kwake ni Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Biswalo Mganga, ikiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma waliohudhuria hafla hiyo ya makabidhiano.


 

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (aliyepo katikati) na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga (kulia) wakisaini nyaraka za makabidhiano. Kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Biswalo Mganga, anayeshughudia zoezi hilo.


Baadhi ya watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma waliohudhuria hafla hiyo ya makabidhiano.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.

Alhamisi, 18 Juni 2026

TUTEKELEZE MAJUKUMU YETU VEMA; JAJI NGUNYALE

Na MICHAEL RITTE, Mahakama-Bukoba

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. David Nyanguye amewasihi watumishi wa Masjala hiyo kuhakikisha kazi za usikilizwaji wa mashauri zinaendeshwa vema pasipo kukwama na jukumu hilo liambatane na juhudi katika utendaji wa majukumu ya kila siku kwa kuzingatia Maadili na kanuni za nafasi husika wanazozitumikia.

Mhe. Ngunyale aliyasema hayo jana tarehe 17 Juni, 2026 katika Ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba wakati wa makabidhiano ya Ofisi kati yake na aliyekuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi ambaye ameteuliwa hivi karibuni kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Kabla ya makabidhiano ya ofisi, kulikuwa na  mapokezi ya awali katika viwanja vya Mahakama hiyo.

Jaji Ngunyale alisema kuwa, kila mtumishi ana wajibu wa kuhakikisha huduma za utoaji haki zinafanyika kwa uadilifu na weledi. Huku akisisitiza kuwa, “tujivunie nafasi tulizopewa na kuzisimamia ipasavyo.”

“Tukifanikiwa kusimamia majukumu yetu na kuwekeza nguvu na muda katika kazi, itatuletea nafasi thabiti ya kujengeana uwezo katika kazi na katika majukumu mbalimbali,” amesisitiza Mhe. Ngunyale.

Ameongeza kuwa, katika utekelezaji wa majukumu ni muhimu kujali afya, familia zetu na jamii sambamba na kuwa na ukaribu na kutenga muda na  nafasi kushiriki shughuli za kijamii ambazo kwa namna moja hudumisha afya ya kiakili na kiutendaji kwa mtumishi.

Alisisistiza kwa kunukuu, “To be trusted is a greater Compliment than to be loved,” Usemi kutoka kwa Mwandishi George MacDonald ambao unamaanisha kuwa, ‘Kuaminiwa ni sifa kubwa kuliko kupendwa.’

Kwa upande wake, aliyekuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, aliwasihi watumishi hao kuendelea kuishi kwa upendo kama walivyoishi naye kipindi akiwa katika nafasi hiyo.

Kadhalika, Mhe. Banzi amewasihi watumishi hao kuendeleza ushirikiano. Na kuhitimisha kwa kumtakia Mhe. Ngunyale kila la kheri katika utekelezaji wa majukumu mapya katika Kituo hicho.

Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. David Ngunyale akisalimiana na Watumishi wa Mahakama hiyo alipowasili katika Kituo chake kipya cha kazi jana tarehe 17 Juni, 2026. 

Jaji wa Mahakama ya Rufani na aliyekuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Bukoba, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi (kulia) akimkabidhi taarifa ya makabidhiano ya ofisi Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. David Ngunyale.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi (wa pili kulia) akiwa katika picha na Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. David Ngunyale (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. Lillian Itemba (wa kwanza kushoto) na Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. Ferdinand Kiwonde. 

 Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi (wa pili kushoto) akizungumza jambo wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Bukoba kwa Mhe. David Ngunyale. Wa pili kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. Lillian Itemba na wa kwanza kulia ni Mhe. Ferdinand Kiwonde, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, wakiwa kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu Bukoba.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Bukoba, Mhe. Said Mkasiwa akitoa neno la kumkaribisha Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama hiyo, Mhe. David Ngunyale (wa kwanza kushoto).

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)



 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


WATUMISHI DODOMA WAMPONGEZA NAIBU MSAJILI MPANGULE

Na ARAPHA RUSHEKE, Mahakama Kuu Dodoma.

Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dodoma, Mhe Biswalo Mganga, amewaongoza Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma katika hafla fupi ya kumpongeza Mhe. Zabibu Mpangule, mara baada ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Dodoma.

Hafla hiyo imefanyika tarehe 17 Juni 2026 katika ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi, Mhe. Mganga amempongeza Mhe. Mpangule kwa kuaminiwa na kupewa nafasi hiyo muhimu, akieleza kuwa uteuzi wake ni matokeo ya utendaji kazi uliotukuka, uadilifu na kujituma katika kutekeleza majukumu yake.

Kabla ya uteuzi huo, Mhe. Mpangule alikuwa akihudumu kama Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma ambapo alitoa mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za haki kwa Wananchi.

Kwa upande wake, Mhe. Mpanguke aliwashukuru Watumishi kwa pongezi zao na kuhahidi kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uadilifu na kujituma kwa manufaa ya Mahakama na Wananchi kwa ujumla.

Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma pamoja na Wilaya zake walimtakiwa kila la kheri katika majukumu yake mapya.

Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Biswalo Mganga (wa kwanza kushoto) akimkabidhi zawadi Naibu Msajili, Mhe. Zabibu Mpangule, katika hafla ya kumpongeza.

Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja na kumpatia dhawadi  Naibu Msajili mteule (wa nne kutoka kushoto).

 

Naibu Msajili, Mhe. Zabibu Mpangule akikata keki ambayo ameandaliwa katika hafla ya kumpongeza.

Watumishi wa Mahakama Dodoma waliohudhuria hafla hiyo wakiwa katika picha ya pamoja wakifanya ibada kabla ya kuanza hafla hiyo.

Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja mara baada kumpokea Naibu Msajili, Mhe. Zabibu Mpangule, mara baada ya kuwasili kutokea kula kiapo katika Ofisi za Tume ya utumishi wa Mahakama.

 

 

 

JAJI FAHAMU MTULYA AAGWA MUSOMA KUFUATIA UHAMISHO WA KITUO

  • Yamkaribisha pia Jaji Kakolaki katika Kituo hicho

Na FRANCISCA SWAI, Mahakama-Musoma

Uongozi na watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ndogo Musoma wamejumuika kumuaga Jaji Fahamu Mtulya kufuatia uhamisho wake kwenda Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya na kumkaribisha Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Edwin Kakolaki aliyehamia kutokea Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mtwara.

Hafla ya kumuaga Jaji Mtulya na kumkaribisha Jaji Kakolaki ilifanyika tarehe 14 Juni, 2026 katika Viwanja vya Mahakama Kuu Musoma.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mtulya aliwashukuru watumishi na wadau wote wa Mahakama Musoma kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi chote cha utumishi wake akiwa Musoma.

Pia, aliwaasa watumishi kuendelea kufanya kazi kwa umoja na upendo, kuzingatia maadili ya kazi na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Zaidi alisisitiza umuhimu wa ushirikiano na wadau katika kuhakikisha shughuli za Mahakama zinafanyika kama inavyopaswa.

Naye Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Musoma, Mhe. Edwin Kakolaki aliwashukuru Uongozi, watumishi na wadau wote wa Mahakama Kanda ya Musoma kwa kumkaribisha na kuahidi kutoa ushirikiano pamoja na kufanya kazi kwa bidii.

Kwa upande wao watumishi wa Mahakama Kuu Musoma walimshukuru Jaji Mtulya kwa uongozi wake thabiti, malezi bora kwa watumishi wa kada zote, kuwa mfano hai wa mchapakazi, uadilifu, upendo na kujitoa kwake katika kazi, matukio ya kijamii, kuhamasisha umoja, michezo na utalii wa ndani.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kiserikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Mtambi, Mkuu wa Wilaya Musoma, Mhe. Juma Chikoka pamoja na Wadau mbalimbali wa Mahakama ambao wote kwa pamoja walitoa salamu na zawadi mbalimbali kumshukuru Jaji Mtulya kwa uongozi wake imara uliothibitika kwa uwajibikaji, uadilifu, na mashirikiano mzuri na wadau.

 Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (wa pili kushoto) akijiandaa kukata keki na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Musoma, Mhe. Edwin Kakolaki (katikati)wakati wa hafla ya kumuaga Jaji Mtulya na kumkaribisha Jaji Kakolaki (katikati). Wa kwanza kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Musoma, Mhe. Marlin Komba, wa kwanza kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Musoma, Mhe. Kamazima Idd na wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Mtambi.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Musoma, Mhe.Edwin Kakolaki (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Mtambi (kulia).

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akipokea mkono wa kwaheri kutoka kwa Chama cha  Mahakimu na Majaji (TMJA) Tawi la Musoma.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Musoma.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (wa pili kushoto) akiwa ameshika zawadi aliyopatiwa ikiwa ni ishara ya shukrani na kumtakia kheri kutoka kwa Viongozi wa Mahakama Kuu Musoma ambao ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Musoma, Mhe. Omari Kingwele (wa kwanza kushoto), wa pili kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Musoma,  Mhe. Monica Ndyekobora na wa kwanza kulia ni Mtendaji wa Mahakama Masjala Ndogo ya Musoma, Bw. Leonard Maufi.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akipokea zawadi ikiwa ni ishara ya mkono wa kwaheri na shukrani kutoka kwa watumishi ambao ni wadau wa utalii Masjala ndogo Musoma.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya hafla ya kumuaga ambao ni watumishi wa Kanda ya Musoma.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau walioshiriki katika hafla ya kumuaga.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (kulia) akipokea mkono wa kwaheri na shukrani kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Musoma, Mhe. Juma Chikoka.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akipokea mkono wa kwaheri na shukrani kutoka wadau wa Mahakama kwa namna alivyokuwa mstari wa mbele kuhamasisha shughuli za utalii wa ndani.

(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)