Jumatatu, 27 Januari 2025

MAHAKAMA YA MOTO YATINGA MTAANI KWA GARI MAALUM KUTOA ELIMU YA SHERIA KWA WANANCHI

Na Innocent Kansha – Mahakama, Dodoma.

Maadhimisho ya Wiki ya Sheria kitaifa yanayofanyika jijini Dodoma yaingia siku ya tatu tangu kuzinduliwa rasmi tarehe 25 Januari, 2025 na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete yameshika kasi baada ya Mahakama ya Tanzania kuzindua rasmi programu maalum ya kutoa Elimu ya Sheria na kujibu hoja za wananchi kwenye maeneo mbalimbali yenye mkusanyiko wa Umma kwa vitendo.

Katika kuhakikisha Mahakama inawafikia wananchi wengi zaidi kupitia programu hiyo maalum ya utoaji elimu mtaani leo tarehe 27 January, 2024 Maafisa Mahakama walishiriki kutoa elimu kwa njia ya gari maalum katika maeneo kadhaa ya jiji la Dodoma ikiwemo Mnada Mpya na Soko la Machinga Complex.

Mada mbalimbali zilizowasilishwa na Maafisa hao zilikuwa ni pamoja na matumizi ya TEHAMA katika kuongeza ufanisi wa utoaji haki nchini, Nafasi ya Kituo cha Huduma kwa Mteja katika kuboresha huduma za Mahakama na kuongeza imani kwa Umma, Wosia na umuhimu wake katika kujenga jamii yenye Amani na maendeleo ya Taifa, Warithi na haki za warithi, Taratibu za malipo ya mirathi na pia taratibu za uendeshaji mashauri ya mirathi, ndoa, talaka na kuasili.

Aidha, Maafisa hao wa Mahakama ya Tanzania walijimwaga mtaani kwa wananchi kwa kutoa mada za Mchango wa Maboresho ya Mahakama katika kukuza ustawi wa haki madai na uchumi wa Taifa, Mchango wa Mahakama katika kuboresha na kurekebisha sheria na kanuni ili kurahisisha upatikanaji wa haki madai kwa wakati vilevile, utekelezaji wa amri na tuzo za Mahakama nafasi ya Mahakama katika kuhakikisha haki inafikiwa.

Akitoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya mirathi, ndoa na talaka Mhe. Sifa Jacob amesema, msimamizi wa mirathi huteuliwa na Mahakama kulingana na majadiliano na mapendekezo ya ukoo husika wa marehemu na akasisitiza kuwa jamii inatakiwa kutambua kuwa msimamizi wa mirathi siyo mmiliki wa mali za marehemu kwani msimamizi anawajibu wa kukusanya mali za marehemu, kugawa mali halali za marehemu kwa warithi na kulipa madeni kama yapo kwa mujibu wa utaratibu na pia anaweza kushitakiwa ama kushitaki kama italazimu kufanya hivyo.

“Napenda niwahakikishie ndugu wananchi msimamizi wa mirathi siyo mmiliki wa mali za marehemu kazi zake za msingi akishateuliwa na Mahakama anawajibu wa kuhakikisha wanufaika wa mirathi wanapata mgao unaostahiki kutokana na mali alizoziacha marehemu aidha iwe ni kwa wosia ama bila wosia kadri busara itakavyo iongoza familia husika,” amesema Mhe. Jacob.

Wakati huo huo akitoa elimu kuhusu Matumizi ya TEHAMA mahakamani yanavyorahisisha utoaji wa haki kwa wananchi na kwa wakati Afisa TEHAMA wa Mahakama ya Tanzania Bw. Witness Ndenza amesema, mifumo ya TEHAMA imekuwa msaada mkubwa katika kuharakisha shughuli za utoaji haki kwa kupitia mfumo wa kuratibu mashauri (e- CMS) mathalani upatikanaji wa nakala za hukumu kwa njia ya mtandao, kusajili mashauri, utoaji wa ushahidi wa mashauri mahakamai, malipo ya ada za Mahakama, utambuzi wa mawakili halali na wasio na sifa, kushughulikia taarifa za kiutumishi, mfumo wa kutambua Mahakama mahali zilipotolea huduma, kuongeza uwazi na uwajibikaji wa shughuli za Mahakama na kusaidia kusomana kwa taarifa mbalimbali wakati zinapohitajika kupitia mifumo ya kielektroniki.

“Ni wajibu wa kila mwananchi kujielimisha kutumia mifumo hii ya kimtandao ili kuweza kupunguza gharama za kuendesha mashauri na kuokoa muda ili kupata muda wa kutosha kufanya shughuli za kiuchumi ili kuweza kujiingizia kipatao kwa maakama mifumo imerahisisha shughuli za uendeshaji wa mashauri na kupunguza adha kwa wananchi kufika mahakamani pasipo kuwa na ulazima wa kufanya hivyo,” ameongeza Afisa TEHAMA huyo.

Naye, Afisa Uchumi Idara ya Mipango na Uratibu kutoka Mahakama ya Tanzania Bw. Kisingi Mhando akitoa mada ya Programu ya maboresho ya Mahakama amesema, Mahakama ya Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuboresha utoaji wa huduma za kimahakama hususani ujenzi wa miundombinu ya kutolea huduma ya haki.

“Ujenzi wa majengo ya kisasa kuanzia ngazi za Mahakama ya Mwanzo hadi Mahakama ya Rufani, ukarabati mkubwa wa majengo ya zamani ili kusogeza huduma za utoaji haki karibu zaidi na wananchi, uboreshaji wa mifumo ya kuendeshea mashauri kama ilivyotajwa awali na kuweka mipango mathubuti ya kupunguza na kama siyo kuondoa kabisa mlundikano wa mashauri kwa kushirikiana na wadau wa mnyororo wa haki nchini ili mwananchi aweze kupata haki kwa wakati na pia kuongozwa na Mpango Mkakati ili kufikia malengo na vilevile kutekeleza malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo,” amesema Bw. Mhando.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania, Mhe. Denice Mlashani amesema, Kituo hicho kimeanzishwa ili kuwasaidi wananchi kutoa mrejesho wa huduma wanazopata kutoka mahakamani kwa kuwasilisha maoni, pongezi, malalamiko ya namna huduma za Mahakama zinavyotolewa kwa wananchi. Kituo kinafanya kazi masaa 24 siku saba za wiki kupokea na kuchakata maoni ya wananchi juu ya huduma za Mahakama na hatua stahiki huchukuliwa kurekebisha dosari na kasoro zilizobainishwa na mteja kwa wakati.

“Hii inasaidia zaidi wananchi watapata fursa ya kutoa mrejesho wa huduma wanazopokea kupitia maoni yao. Maoni yatakayotolewa yatatumika kama mtaji wa kuboresha utoaji haki nchini,” ametanabaisha Mhe Mlashani.

Kwa upande Mwingine, akitoa mada ya Mchango wa Mahakama katika kuboresha na kurekebisha sheria na kanuni ili kurahisisha upatikanaji wa haki madai kwa wakati Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Maktaba ya Mahakama ya Tanzania Mhe. Kifungu Mrisho Kariho amesema, Mahakama ya Tanzania kupitia Kamati ya Jaji Mkuu ya mapitio ya kanuni imefanya kazi nyingi za kumshauri Jaji Mkuu na kurekebisha baadhi ya kanuni za uendeshaji wa mashauri ya madai mathalani kupitia mchako huo Mahakama imeweza kupunguza hatua za uendeshaji wa mashauri ya madai kutoka hatua 38 za awali hadi hatua 21 ili kuharakisha utoaji haki kwa wananchi.

“Na pia kuna kanuni za uendeshaji wa mashauri ya madai madogo zilizoanza kufanya kazi mwaka 2023, kwa sababu zinaenda tofauti na zile kanuni za madai ya kawaida yanayoendeshwa na Mahakama, unaweza kuwa unamdai mtu milioni mia tano au mia tatu ukatumia kanuni hizi ambapo kesi yako ikasikilizwa ndani ya miezi mitano au mwezi mmoja na ukapata haki yako,” ameongeza Mhe. Kariho.

Mhe. Kariho amesema kwa kutumia kanuni hizo mdaawa anatakiwa kufungua madai yake ndani ya siku saba na anayekujibu atafanya hivyo ndani ya siku saba lakini baada ya kusikilizwa madai hayo Hakimu hatakiwi kukaa zaidi ya siku 30 kabla hajatoa uamuzi wa madai hayo. Na pia Kanuni hizo zinaruhu maombi ya mdomo kusikilizwa hapo hapo wakati yamewasilishwa na mleta maombi. Vilevile, Kanuni hizo zimeondoa mbinu za kiufundi wakati wa uendeshaji wa mashauri madogo ya madai. Kanuni hizo zinalenga mashauri ya kuanzia milioni mia moja kushuka chini au kupanda juu hasa kwa masahuri ya madai madogo.

“Ukifungua shauri la madai kwa njia hiyo utakuwa unaepuka zile taratibu za kawaida za madai zinazoongozwa na sheria Madai Sura namba 33 ambazo zimefanyiwa marekebisho mwaka 2022 tunawashauri wananchi kuzitumia Kanuni hizi ambazo zimerahisisha uendeshaji wa mashauri ya madai,” amesema Mhe. Kariho.

Msimamizi wa Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania, Mhe. Denice Mlashani akitoa mada kwa wananchi wa eneo la Mnada Mpya jijini Dodoma.

Msimamizi wa Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania, Mhe. Denice Mlashani akitoa mada kwa wananchi wa eneo la Mnada Mpya jijini Dodoma.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maktaba ya Mahakama ya Tanzania Mhe. Kifungu Mrisho Kariho akitoa machapisho yenye taarifa mbalimbali za Mahakama kwa wananchi waliopata elimu ya kisheria.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maktaba ya Mahakama ya Tanzania Mhe. Kifungu Mrisho Kariho akitoa machapisho yenye taarifa mbalimbali za Mahakama kwa wananchi waliopata elimu ya kisheria.


Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maktaba ya Mahakama ya Tanzania Mhe. Kifungu Mrisho Kariho akitoa machapisho yenye taarifa mbalimbali za Mahakama kwa wananchi waliopata elimu ya kisheria.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maktaba ya Mahakama ya Tanzania Mhe. Kifungu Mrisho Kariho akitoa machapisho yenye taarifa mbalimbali za Mahakama kwa wananchi waliopata elimu ya kisheria.


Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maktaba ya Mahakama ya Tanzania Mhe. Kifungu Mrisho Kariho akitoa machapisho yenye taarifa mbalimbali za Mahakama kwa wananchi waliopata elimu ya kisheria.



Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maktaba ya Mahakama ya Tanzania Mhe. Kifungu Mrisho Kariho akitoa machapisho yenye taarifa mbalimbali za Mahakama kwa wananchi waliopata elimu ya kisheria.

Mwananchi wakisoma vipeperushi vya Mahakama walivyopatia kwa ajili ya kujielimisha kuhusu masuala shughuli mbalimbali zitolewazo na Mahakama ya Tanzania.

Mwananchi wakisoma vipeperushi vya Mahakama walivyopatia kwa ajili ya kujielimisha kuhusu masuala shughuli mbalimbali zitolewazo na Mahakama ya Tanzania.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maktaba ya Mahakama ya Tanzania Mhe. Kifungu Mrisho Kariho akitoa machapisho yenye taarifa mbalimbali za Mahakama kwa wananchi waliopata elimu ya kisheria.

Afisa TEHAMA wa Mahakama ya Tanzania Bw. Witness Ndenza akimuelekeza mwananchi mara baada ya kumkabidhi machapisho mbalimbali yenye taarifa za Mahakama.

Wananchi wakisoma vipeperushi vya Mahakama walivyopatia kwa ajili ya kujielimisha kuhusu masuala shughuli mbalimbali zitolewazo na Mahakama ya Tanzania.

Sehemu ya Wananchi wakiwasiliza Maafisa Mahakama watoa elimu katika wiki ya maadhimisho ya sheria nchini kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya Wananchi wakiwasiliza Maafisa Mahakama watoa elimu katika wiki ya maadhimisho ya sheria nchini kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya Wananchi wakiwasiliza Maafisa Mahakama watoa elimu katika wiki ya maadhimisho ya sheria nchini kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya Wananchi wakiwasiliza Maafisa Mahakama watoa elimu katika wiki ya maadhimisho ya sheria nchini kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Maafisa wa Mahakama ya Tanzania waliotoa elimu mtaani wakiwa kwenye chombo ya fundi wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Sheria kitaifa yanayofanyika jijini Dodoma.

(Picha na Innocent Kansha - Mahakama -Dodoma)

    

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni