Na EUNICE LUGIANA, Mahakama-Mwanza
Timu
za Kamba (wanaume na wanawake), Mpira wa Pete na Mpira wa Miguu zimeanza vema michuano
ya Shirikisho la Michezo ya Wizara, Idara, Wakala za Serikali na Ofisi za Wakuu
wa Mikoa (SHIMIWI) inayoendelea kwenye viwanja mbalimbali jijini Mwanza.
Katika
michezo ya siku ya kwanza wanawake walivutana na Ofisi ya Katibu Tawala (RAS) Kagera
na kutoka na ushindi wa bao mbili (2) kwa 0 katika mchezo huo wa vuta nikuvute
Mahakama wanawake walifanikiwa kuvuta mivuto yote miwili na kupata ushindi.
Na
katika siku ya pili Mahakama walivutana dhidi ya Timu ya Wizara Katiba na
Sheria na kufanikiwa kuwavuta mivuto yote miwili hivyo kuondoka na ushindi.
Akizungumza
baada ya mechi hiyo jana tarehe 02 Septemba, 2025, Nahodha Msaidizi wa Timu ya Kamba
Wanawake, Bi. Eva Mapunda alisema siri ya ushindi huo ni mazoezi na ndio maana
wanapata matokeo mazuri.
Aidha,
Nahodha huyo amemuahidi Mtendaji Mkuu wa Mahakama kuwa, watarudi na ushindi
mnono na vikombe, kutokana na malezi mazuri wanayoyapata kambini hapo.
Kwa
upande wa mchezo wa kamba wanaume ambapo siku ya kwanza walivutana na timu
kutoka Viwanda na kufanikiwa kuwavuta mivuto yote miwili kama karatasi na
kujichukulia pointi mbili lakini katika
mchezo wa pili baada ya kuona viwanda walivyovutwa kama karatasi Timu ya Kilimo
waliingia mitini na kutokutokea uwanjani na hivyo kusababisha ushindi.
Katika michezo hiyo ya kamba kwa wanawake na wanaume iliyofanyika katika viwanja vya Furahisha jiji Mwanza timu za Mahakama wameshinda mechi zote mbili katika hatua hii ya makundi.
Nayo
Timu ya Mpira wa Pete ya Mahakama imefanikiwa kushinda katika mchezo wake wa
kwanza kwa kuifunga Timu ya GST magoli 41 kwa 11 katika mchezo uliofanyika
katika viwanja vya CCM Kirumba, Nahodha wa timu hiyo, Akanganyila Theophil alisema
wapinzani hao walikuwa wa kawaida na hivyo kusababisha ushindi huo kupatikana na
kuongeza kuwa wamejiandaa vizuri kwa mechi ijayo ambapo wanatarajia ushindi
mnono.
Katika
mtanange uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mabatini B kati ya Timu
ya Mahakama na Kilimo, kilimo walichokikimbia asubuhi kwenye kamba wanaume
wamekutana nacho kwenye mpira wa miguu kwa kuchabangwa bao mbili kwa nunge,
magoli hayo yalifungwa dakika ya 17 na ya 26 ya kipindi cha pili. Magoli hayo
yote yalifungwa na mchezaji Muhamadi Ghafuru.
Kocha
wa Timu ya Mpira wa Miguu, Spear Dunia Mbwembwe alisema ushindi huo uliopatikana ni salamu za shukrani
kwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Prof. Elisante Ole Gabriel kwa kuwezesha timu
kuishi vizuri kupata malazi mazuri, chakula na mavazi kwa kupindi chote tangu
wamefika kambini hapo na hivyo Kocha huyo kuahidi kurudi na vikombe.
Mashindano ya SHIMIWI yalianza tarehe 01 Septemba, 2025 na yanatarajiwa kufunguliwa rasmi tarehe 06 Septemba 2025. Mahakama ya Tanzania imepeleka jumla ya timu tisa ambazo ni Timu za Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete, Kamba (wanawake na wanaume), Riadha, Baiskeli, Tufe, Karata na Bao.
Kikosi cha Timu ya Mpira wa Miguu cha Mahakama kabla ya mtanange.
Timu ya Kamba Wanaume baada ya mechi dhidi ya Viwanda.
Kikosi cha Timu ya Mpira wa Pete kabla ya mechi kuanza.
Mfungaji wa Timu ya Mahakama akifunga goli.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni