Na. Daniel Sichula-Mahakama, Mbeya
Kaimu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Said Kalunde hivi karibu alifungua
mafunzo ya marekebisho ya kanuni za mirathi kwa Mahakama za Mwanzo za Mwaka
2025 kwa Mahakimu, Maafisa Utumishi na Wahasibu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya.
Mafunzo
hayo yaliendeshwa katika Ukumbi wa Mikutano wa Mahakama Kuu Mbeya kwa kuwajumuisha
watumishi wa kada hizo yamelenga kuwajengea uelewa wa pamoja watumishi hao
wanapokuwa wanashughulikia mashauri ya mirathi.
Akizungumza
wakati wa kufungua mafunzo hayo Mhe. Kalunde aliwashukuru wakufunzi kwa kuandaa
mafunzo hayo kwani yatasaidia katika kuelewa mabadiliko na kuboresha utendaji
kazi katika kushughulikia mashauri ya Mirathi kwa Mahakama za Mwanzo.
“Mafunzo
haya yanaweza kutuonesha tulikotoka na tunako kwenda na hii itasaidia kutujengea
uelewa kwetu sisi sote, na kuweza kutoa elimu hii tutayoipata hapa kwa wengine
huko ili tuweze kusaidia jamii katika suala zima la mirathi,” alisema Mhe. Kalunde
Aidha,
wakufunzi wa mafunzo hayo Mhe. Adriano Julius Mtafya pamoja na Mhe. Mayonga
Manyeresa walisema elimu hiyo kwa washiriki juu ya kanuni mbalimbali za mirathi
zilizoboreshwa na vipengele vyake ni shirikishi hasa kwa wanufaika
“Itasaidia
warithi kuitwa kuthibitisha orodha ya mali na hesabu za warithi, utaratibu wa
kusikiliza mapingamizi, maombi ya kutengua msimamizi wa mirathi, kuongezwa kwa
akaunti maalum za mirathi na maboresho katika usikilizwaji wa mapingamizi na
kufungua mirathi pamoja na ujazaji wa fomu mbalimbali za mirathi,” alisema
Mkufunzi huyo.
Katika
majadiliano washiriki walitoa maoni juu ya maboresho ya kanuni mbalimbali
zilizofanyika katika kushughulikia mashauri ya mirathi pamoja na changomoto
zitakazo jitokeza kutoka kwa wadau mbalimbali.
“Ni
muhimu mafunzo haya yawafikie pia wadau wengine kama vile maofisa wa benki,
ardhi na jamii kwa ujumla ili uendashaji wa mashauri ya mirathi yaweze kutolewa
maamuzi kwa haki na kwa wakati na kuondoa malalamiko kwa wanufaika wa mirathi,”
alisema mmoja wa washiriki.
Akifunga
mafunzo hayo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya Mbeya Mhe. Teddy Mlimba kwa niaba
ya Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya aliwashukuru wakufunzi
kwa elimu ya maboresho ya kanuni mbalimbali za mirathi waliyoitoa na kwa
washiriki wote waliohudhuria mafunzo.
“Kwa
elimu iliyotolewa itatusaidia sana katika uendeshaji wa mashauri ya mirathi
kwenye Mahakama zetu, hivyo basi nawasihi Mahakimu tuwe makini katika uendeshaji
wa mashauri ya mirathi,” alisema Mhe. Mlimba
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Said Kalunde alifungua mafunzo ya marekebisho ya kanuni za mirathi kwa Mahakama za Mwanzo za Mwaka 2025, kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa
Mkufunzi wa mafunzo Mhe. Adriano
Mtafya akitoa elimu juu ya maboresho ya kanuni mbalimbali za mirathi kwa
Mahakama za Mwanzo
Mkufunzi wa Mafunzo hayo Mhe. Mayonga
Manyeresa akielezea maboresho ya matumizi ya fomu za mirathi kwa washiriki
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni