Na. MWINGA MPOLI – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga
amekutana na wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama Mkoa wa Mbeya na kufanya nao
mazungumzo kuhusu masuala muhimu ya kazi ikiwemo nidhamu, uadilifu, matumizi ya
mfumo mpya wa kusajili mashauri pamoja na utunzaji wa vielelezo.
Ameyasema
hayo wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa
mikutano wa Mahakama Kuu Mbeya. Mhe Tiganga alisisitiza kuwa, maadili ya
utumishi wa umma na nidhamu kazini ndiyo msingi wa kazi za Mahakama. Aliongeza
kuwa, utunzaji sahihi wa nyaraka na vielelezo ni jambo la msingi katika kuhakikisha
haki inatolewa kwa wananchi bila vikwazo.
“Ni
vizuri kuusoma mfumo wa kusajili mashauri na kuufanyia kazi, lakini pia
tuongeze nidhamu na maadili kazini. Tunapaswa kuhakikisha tunatunza kumbukumbu
vizuri pamoja na vielelezo ili kutokwamisha zoezi zima la utoaji haki kwa
wananchi.” alisema Mhe. Tiganga
Naye,
Hakimu Mkazi Mkuu kutoka Kurungenzi ya usimamizi, ukaguzi, Maadili na
ufuatiliaji wa huduma za kimahakama kutoka Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania Mhe.
Mohamed Siliti alipata fursa ya kuongea na watumishi hao kwa njia ya mtandao.
Akitoa
elimu juu ya utunzaji wa kumbukumbu za Mahakama Mhe. Mohamed Siliti aliwaasa
watunza kumbukumbu hao kutimiza wajibu wao na kuepuka kutumia lugha zisizo za
staha na nzuri kwa wateja.
Kupitia
kikao kazi hicho kiliweka maazimio na kukubaliana kufanya kazi kwa ushirikiano
na weledi mkubwa huku wakizingatia maadili na nidhamu kufuatia kanuni na
taratibu za utumishi wa umma.
Kikao
hicho kilihudhuriwa na Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Aziza
Temu, Mtendaji wa Mahakama Bi Mavis Miti, Maafisa Utumishi pamoja na wasaidizi
wa kumbukumbu Mahakama Mkoa wa Mbeya.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga (katikati)
akiongoza kikao kazi hicho cha wasaidizi wa kumbukumbu na nyaraka (kulia) ni Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu na kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda
ya Mbeya Bi. Marvis Miti.
Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu akitolea ufafanuzi sehemu ya mambo yaliyojadiliwa kwenye kikao hicho.
Mmoja
wa wajumbe akizungumza jambo katika kikao hicho Msaidizi wa
Kumbukumbu Mahakama Kuu Mbeya Bi. Isabela Osiah
Mmoja
wa wajumbe akizungumza jambo katika kikao hicho Msaidizi wa Kumbukumbu Mahakama
ya wilaya Mbeya Bi. Queen Mapunda.
Sehemu ya Maafisa
Utumishi Mahakama Mbeya walioshiriki kikao kazi hicho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni