Jumatatu, 13 Aprili 2026

WIKI YA USULUHISHI YAANZA KUADHIMISHWA MKOANI MBEYA

Na. MWINGA MPOLI – Mahakama, Mbeya

Katika kuadhimisha Wiki ya Usuluhishi nchini Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya imeungana na Kanda zingine nchini kuadhimisha wiki ya Usuluhishi kuanzia tarehe 13 Aprili, 2026 hadi tarehe 17 Aprili, 2026 yenye kaulimbiu isemayo, “Kutumia Njia Mbadala ya Utatuzi wa Migogoro kama Mbinu Inayopendelewa ya Kutatua Migogoro nchini Tanzania”.

Katika maadhimisho hayo Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga, Naibu Wasajili pamoja na Mahakimu wameweka mkakati wa kupokea na kusajili migogoro mbalimbali ihusuyo ardhi, ndoa na madai ya kawaida na kuwapangia wasuluhishi wenye nyenzo za usuluhishi kwa ajili ya kuitatua migogoro hiyo.

Mbali na hilo Uongozi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya umeweka dawati maalumu la kupokea migogoro katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya pamoja na kuandaa vyumba maalumu vitakavyotumika kufanya usuluhishi.

 Wananchi wote waliokuwa wamejitokeza walianza kwa kupatiwa elimu ya usuluhishi na misingi yake, ambapo wananchi walipata nafasi ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi wa kina juu ya masuala mbalimbali ya kisheria yanayohusu usuluhishi wa migogoro.

Sehemu ya watumishi na Mawakili wa Serikali wanaoshiriki katika maadhimisho hayo


Sehemu ya watumishi na Mawakili wa Serikali wanaoshiriki katika maadhimisho hayo

 Hakimu Mkazi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Adriano Mtafya akitoa elimu ihusuyo usuluhishi na misingi yake kwa wananchi (hawapo pichani)

Wananchi waliofika mahakamani wakipatiwa elimu aliyesimama ni Hakimu Mkazi Mahakama ya Wilaya Mbeya Mhe. Paul Rupia.

Wananchi waliofika mahakamani wakipatiwa elimu ya usuluhishi inayoadhimishwa Kanda ya Mbeya.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni