Jumatatu, 7 Mei 2018

JAJI MKUU AFUNGUA MAFUNZO ELEKEZI KWA MAJAJI WAPYA

Na Mary Gwera

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amewataka Majaji wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania kufanya kazi kwa kiwango cha juu kwani wananchi wana matarajio makubwa na matokeo ya kazi zao.

Alisema hayo mapema Mei 07 alipokuwa akifungua Mafunzo Elekezi ya Waheshimiwa Majaji wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania katika Kituo cha Mafunzo kilichopo katika eneo la Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu-Dar es Salaam.

“Mafunzo haya yamekuja wakati muafaka, wakati ambao Mahakama ya Tanzania ipo katika maboresho mbalimbali, hivyo ni vyema ninyi Majaji kupitia utendaji kazi wenu mtumike kubadili taswira ya Mahakama,” alisema Mhe. Jaji Mkuu.

Mhe. Jaji Mkuu alisema kuwa lengo la Mafunzo hayo kwa Waheshimiwa Majaji wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania ni kuwapa miongozo na taratibu mbalimbali katika ufanyaji kazi ya Ujaji.

“Mafunzo haya endelevu yanayotolewa na Mahakama kwa kushirikiana na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto ni muhimu katika utendaji kazi kwani baadhi ya Majaji walioteuliwa wametoka sehemu mbalimbali hivyo ni vyema kuwafunza ili kuwa na uelewa wa pamoja katika utendaji kazi,” alifafanua Mhe. Jaji Mkuu.

Mhe. Jaji Mkuu pia amewataka Wahe. Majaji kufanya kazi kwa kuzingatia pia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025.

Mafunzo hayo yalioshirikisha jumla ya Majaji wapya 14, 12 kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania na wawili (2) kutoka Mahakama Kuu-Zanzibar yatafanyika kwa muda ya Wiki tatu, na katika mafunzo hayo mada mbalimbali zitatolewa ikiwa ni pamoja na Matumizi ya TEHAMA Mahakamani, Makosa ya Kimtandao nk.

Mafunzo haya yanaendeshwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto chini ya ufadhili wa fedha za Mradi wa Benki ya Dunia.


Jaji Mkuu wa Tanzania , Mhe. Profesa Ibrahim   Juma  akifungua mafunzo elekezi ya wiki ya tatu   kwa  ajili  ya  majaji wapya  yaliyoanza  leo kwenye  Kituo  cha  Mafunzo , kilichopo katika   Mahakama ya Hakimu Mkazi  Kisutu, jijini Dar e s Salaam.
Baadhi  ya Majaji wapya  wa Mahakama Kuu  wakimsikiliza  Jaji  Mkuu (hayupo pichani   wakati  ufunguzi wa mafunzo elekezi ya wiki tatu    yaliyoanza  leo  kwenye  Kituo  cha  Mafunzo , kilichopo katika   Mahakama ya Hakimu Mkazi  Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Baadhi  ya Majaji wapya  wa Mahakama Kuu  wa kimsikiliza  (Jaji  Mkuu ,ambaye  hayupo pichani     wakati  ufunguzi wa mafunzo elekezi ya wiki tatu    yaliyoanza  leo  kwenye  Kituo  cha  Mafunzo , kilichopo katika   Mahakama ya Hakimu Mkazi  Kisutu, jijini Dar e s Salaam.

Jaji  Kiongozi wa Mahakama Kuu  ya Tanzania, Mhe. Ferdinand  Wambali   akitoa neno leo  kwa Majaji wapya  wakati ufunguzi wa mafunzo elekezi  ya wiki tatu yaliyoanza leo kwenye  Kituo  cha  Mafunzo , kilichopo katika   Mahakama ya Hakimu Mkazi  Kisutu, jijini Dar e s Salaam.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim  Juma  (katikati)akiwa katika  picha  ya pamoja  mara baada  ya kufungua mafunzo elekezi kwa  ajili  ya  Majaji wapya  yaliyoanza leo   kwenye  Kituo  cha  Mafunzo , kilichopo katika   Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar e s Salaam.
Meza Kuu katika picha ya pamoja na Majaji wapya wa Mahakama Kuu-Zanzibar (waliosimama)
 

Meza kuu ikiwa katika picha ya pamoja na Wasajili, Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama (waliosimama).

Mkuu wa Chuo cha Uongozi  cha  Mahakama(IJA) Mhe.  Jaji Dkt .Paul Kihwelo akizungumza jambo katika mafunzo elekezi   wiki tatu kwa  ajili  ya  majaji wapya  yayoanza   leo kwenye  Kituo  cha  Mafunzo , kilichopo katika   Mahakama ya Hakimu Mkazi  Kisutu, jijini Dar e s Salaam.
Majaji wapya wakiwa katika  mafunzo  elekezi ya wiki tatu yaliyoanza leo  kwenye Kituo cha Mafunzo, Kilichopo Katika Mahakama ya Kisutu jijini  Dar es Salaam.

Majaji wapya wakiwa katika  mafunzo  elekezi  ya wiki tatu yaliyoanza leo  kwenye Kituo cha Mafunzo, Kilichopo Katika Mahakama ya Kisutu jijini  Dar es Salaam.

Meza Kuu katika ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Idara ya Mafunzo Mahakama ya Tanzania (waliosimama)
  (Picha na Magreth Kinabo)
.









Hakuna maoni:

Chapisha Maoni