Ijumaa, 10 Mei 2019

WAHASIBU NA MAKARANI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

 Sehemu ya watumishi wa Mahakama walioshiriki katika mafunzo ya kutumia mfumo wa kielektroniki wa JSDS II, wakiwa katika picha ya pamoja na waratibu wa mafunzo hayo yalitofanyika katika ukumbi wa habari na mafunzo ya Mahakama walioketi  wa pili kutoka kushoto ni Mhasibu Mkuu wa Mahakama ya Tanzania. Bw. Fanuel Tiibuza, wa pili  kulia ni Mkuu wa idara ya Tehama Mahakama ya Tanzania Bw. Kallege Enock, wa kwanza kushoto ni Mhasibu wa Mahakama Bi. Annastella Natai na wa  kwanza kulia ni Afisa Tehama wa Mahakam ambaye pia ni mwezeshaji wa mafunzo hayo Bw. Athuman Juma.


 Mhasibu Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Bw. Fanuel Tiibuza akielezea faida za mfumo wa JSDS II wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya kutumia mfumo huo. Mafunzo hayo yaliifanyika katika ukumbi wa habari na mafunzo ya Mahakama uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Akifunga mafunzo hayo Bw. Tiibuza amewataka Wahasibu na Makarani kufanya kazi kwa weledi.



Mkuu wa Idara ya Tehama Bw. Kellege Enock akiwashukuru washiriki waliohudhuria mafunzo ya kutumia mfumo wa kielektroniki yaliyofanyika katika ukumbi wa Habari na Mafunzo ya Mahakama uliyopo Jijini Dar es Salaam

 Afisa Tehama Bw. Athumani Juma ambaye pia ni mwezeshaji Mkuu wa mafunzo hayo, akiwaelezeza kwa vitendo sehemu ya washiriki  wa mafunzo hayo jishi mfumo wa JSDS II unavyofanya kazi.


 Mmoja ya washiriki waliohudhuria mafunzo hayo akimuelekeza mshiriki mwenzake kwa vitendo jinsi ya kutumia mfuo huo unavyofanya kazi kama kama wanavyoonekana katika picha.


 .
 Miongoni mwa washiriki wa Mafunzo hayo wakijadiliana jambo wakati mafunzo hayo yakiendelea katika ukumbi wa Habari na Mafunzo ya Mahakama uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam.


Sehemu ya washiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia kwa makini mada iliyokuwa inatolewa, wakati mafunzo hayo yakiendelea katika ukumbi wa Habari na Mahakama uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam.
Afisa Tehama Bw. Athumani Juma ambaye ni mwezeshaji wa mafunzo hayo akitoa Mada wakati mafunzo hayo yakiendelea katika ukumbi wa Habari na Mafunzo uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.
 Mmoja ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwaelezea washiriki wenzake namna mfumo wa JSDSII unavyofanya kazi.


Sehemu ya washiriki wa warsha hiyo, wakimsikiliza kwa makini mtoa mada Bw. Athuman Juma, wakati akiendesha mafunzo hayo.

 Wawezeshaji wa Mafunzo hayo Bw. Samweli Mshote akiwa pamoja na Bw. Athuman Juma wakimsikiliza kwa makini mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo akiwaelezea washiriki wenzake namna mfumo wa JSDS II unavyofanya kazi.
Mmoja ya washiriki wa mafunzo hayo, akielezea kwa kifupi jinsi mfumo huo unavyofanya kazi na namna utakavyo saidia kuongeza ufanisi na hivyo kuisaidia Mahakama kutoa haki kwa wakati.

Mmoja ya watumishi wa Mahakama, akiuliza swali wakati mafunzo ya kutumia mfumo wa JSDS II yakiendelea katika ukumbi wa Habari na mafunzo ya Mahakama uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni