Jumamosi, 24 Oktoba 2020

BODI YA MAJUZUU YA SHERIA MBIONI KUKAMILIMISHA JUZUU LA 2020

 Na Tawani Salum, Mahakama

Bodi ya Udhamini wa Taarifa ya Majuzuu ya Sheria imeendelea kwa kasi kukamilisha uchambuzi wa maamuzi ya Juzuu la mwaka 2016 na majuzuu ya miaka ya nyuma kuanzia mwaka 2007 na kuendelea na ifikapo mwisho wa mwezi Oktoba mwaka huu inategemea kukamilisha uchapishaji wa juzuu ya sheria ya mwaka huu.

Akizungumza katika  kikao cha Bodi hiyo, kilichofanyika hivi karibuni  katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria  jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi, Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Jacobs Mwambegele alisema kuwa Majuzuu ya mwaka 2007 hadi 2015,2017 ,2018 na 2019 tayari yamewasilishwa  kwa Mzabuni kwa hatua ya mapitio na  uchapishaji.   


Ni mpango wa Bodi na Mahakama kuhakikisha imemaliza kuchapisha Taarifa za Majuzuu ya Sheria ya Mwaka  2007 hadi Mwaka 2020 katika kipindi cha miezi kumi kuanzia mwezi wa nane mwaka huu,” alieleza Mhe. Jaji Mwambegele.

Naye Kaimu Mratibu wa  Bodi ya Udhamini wa Taarifa ya Majuzuu ya Sheria, Mhe. Kifungu Mrisho Kariho alisema kuwa Bodi hiyo imedhamiria kutoa Majuzuu hayo kwa mkupuo kwa kuwa tayari  kipindi kirefu kimepita toka 2006  bila Majuzuu hayo kuwafikia wadau walaji na  kurahisisha tafiti za kisheria  na  kumalizika  kwa Mashauri kwa wakati kupitia   Wahe. Majaji  na Mahakimu.

Mhe. Kariho aliongeza kuwa Majuzuu hayo yatasaidia katika uwasilishwaji wa hoja mpya  za kisheria Mahakamani  kupitia  Mawakili wa Serikali, Mawakili wa Kujitegemea  pamoja na wadau wengine katika fani ya Sheria.

Bodi hiyo ina jumla ya Wajumbe 12, ambao ni Majaji kutoka Mahakama ya Rufani, Majaji wa Mahakama Kuu Tanzania  Bara na Zanzibar, Wawakilishi toka Tanzania Bara na Zanzibar, Katibu na Mratibu wa Bodi hiyo.

Pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini  ya Taarifa ya Majuzuu ya Sheria ambaye pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Jacobs Mwambegele na kulia ni Katibu wa Bodi hiyo, Prof. H.I. Majamba wakiwa katika kikao cha Bodi ya Udhamini  ya Taarifa ya Majuzuu ya Sheria  kilichofanyika hivi karibuni.

Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Udhamini  ya Taarifa ya Majuzuu ya Sheria wakiwa katika kikao hicho, Kulia ni Mhe.Jaji F. Manyanda,  kushoto ni Bi. Nelly Mwasongwe  na katikati ni Bw. H.A. Haji.

Wajumbe wa Bodi ya Udhamini  ya Taarifa ya Majuzuu ya Sheria wa kwanza kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. S.A.  Lila, katikati Ni Jaji wa Mhakama Kuu Zanziabr Mhe. A. Mwampashi na wa kwanza kulia ni ni Kaimu Mratibu wa Bodi hiyo Mhe.Kifungu Mrisho Kariho wakifuatilia kikao hicho.

 

Wajumbe wa Bodi hiyo wakiendelea na majadiliano, kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Ignas Kitusi na kulia ni Prof. Majamba.



 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni