Alhamisi, 2 Mei 2024

UJENZI WA KITUO JUMUISHI LINDI WAIVA

Na Hilaly Lorry – Mahakama, Lindi

Mkandarasi kutoka kampuni ya Rizvi Engineering Ltd amekabidhiwa eneo kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Mradi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Mkoa wa Lindi.

Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni huku yakushuhudiwa na Mkuu wa Kitengo cha Majengo cha Mahakama ya Tanzania Mhandisi Moses Lwiva na Mkandarasi Mshauri Mhandisi Bw. Amri Mumba kutoka kampuni ya Usanifu wa Majengo ya Y & P (T) Ltd na viongozi mbalimbali wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi.

Mwenyekiti wa kikao hicho Bw. Amri Mumba alieleza kuwa ujenzi wa mradi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Lindi utachukua miezi tisa (9) hadi kukamilika na unatarajiwa kuanza rasmi tarehe 09 Mei, 2024 na kukamilika 08 Februari 2025.

Aidha, Bw.  Mumba alisisitiza mambo mbalimbali ikiwemo jinsi ya kuratibu taka zinazozalishwa wakati wa zoezi la ujenzi na kuwataka kutafuta namna bora yakuweza kuziharibu taka hizo ili zisilete madhara kwa watu wanaozunguka eneo hilo la mradi.

Kwa upande wake, Mhandisi Moses Lwiva alimtaka Mkandarasi kujisajili kwa wakala wa usalama na afya mahala pa kazi (OSHA).Vilevile kuzingatia sheria zote za usalama kwa mafundi na watu watakao fika eneo la mradi kwani mradi huo ni wa Benki ya Dunia huku akiwapa angalizo kuwa Benki ya Dunia wanazingatia  usalama mahali pa kazi zaidi.

 Mhandisi Mshauri, Mkandarasi na timu nzima walikubaliana kufanya kazi  kwa ushirikiano usiku na mchana kwa lengo la kuhakikisha kuwa zoeli la ujenzi linakamilika kwa muda waliopewa  ili kuwapunguzia gharama wananchi mkoani Lindi  kufuata huduma za kimahakama hasa Mahakama kuu nje ya Mkoa wao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi.Quip Mbeyela na Hakimu mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe.Consolata Singano pamoja na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Lindi Mhe. Maria Batulaine waliahidi kutoa ushirikiano wa karibu na kufanya mawasiliano na pande zote zinahusika na ujenzi huo kwa lengo la kuhakikisha ujenzi wa mradi huo unakamilika bila mkwamo wowote.

Makabidhiano ya mkataba kwa ajili ya ujenzi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Mkoa wa Lindi kati ya Mkandarasi kutoka Kampuni ya Rizvi Engineering Ltd Bw.Ali Rivzi na Mkuu wa Kitengo cha Majengo Mahakama ya Tanzania Mhandisi Moses Lwiva kutoka Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania.

Mkandarasi kutoka kampuni ya Rizvi Engineering Ltd   akionyeshwa eneo la ujenzi na mipaka yake.

Mkandarasi kutoka kampuni ya Rizvi Engineering Ltd   akionyeshwa eneo la ujenzi na mipaka yake.

Wajumbe wa kikao cha makabadhiano wakifuatia kwa Makini wakati wa kikao.

Mtendji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi.Quip Mbeyela (aliyevaa shati jeupe) wakitoa neno la ukaribisho wakati wa kikao cha makabidhiano ya eneo la mradi wa ujenzi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Mkoa wa Lindi.


Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe.Consolata Singano (aliyevaa gauni jeusi), Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Lindi Mhe.Maria Batulaine (aliyevaa suti) wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kikao hicho

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha -Mahakama) 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni