Jumamosi, 25 Januari 2025

JAJI MFAWIDHI MBEYA AWAKARIBISHA WADAU, WANANCHI KWENYE MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA

Na Daniel Sichula Mahakama, Mbeya

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Joachim Charles Tiganga jana tarehe 24 Januari, 2025, akiwa katika Kituo cha Radio cha Rock FM jijini Mbeya aliwakaribishisha wadau washeria pamoja na wananchi wa jiji la Mbeya pamoja na viunga vyake katika uzinduzi wa wiki ya sheria Jumamosi ya tarehe 25 Januari, 2025 katika viwanja vya stand ya Mabasi Kabwe na siku ya kilele itakayofanyika siku ya tarehe 3 Februari 2025 katika viwanja vya Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya.

Katika Maadhimisho ya mwaka 2025 yenye Kauli Mbiu isemayo, “Tanzania ya 2025: Nafasi ya taasisi zinazosimamia haki katika katika kufikia malengo makuu ya dira ya taifa ya maendeleo.” katika uzinduzi wa wiki ya sheria jijini Mbeya utakaoambatana na matembezi ya kilometa nne kutoka viwanja vya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya hadi stendi ya mabasi Kabwe ambapo shughuli nzima ya uzinduzi itafanyika itaongonzwa na Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Juma Homera alisema Jaji Mfawidhi.

Mhe. Tiganga aliwataka wananchi kuwa tayari kwani elimu ya sheria itatolewa maeneo mbalimbali katika jiji la Mbeya ikiwepo Stendi ya mabasi Kabwe, Stendi ya mabasi Mbalizi, Stendi ya Uyole na katika Taasisi mbalimbali za Serikali na ambazo sio za kiserikali.

Akiwa ameambatana na Hakimu Mkazi Mkuu Mhe. Paul Ntumo pamoja Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Mbeya Mhe. Tedy Raphael Mlimba, Mhe. Tiganga alisema “Tunapowakaribisha wadau mbalimbali wa sheria, wananchi wasifikilie ni polisi, magereza, waendesha mashataka au mawakili peke yao hata nyinyi wananchi wa kawaida ni wadau kwani ndiyo mnaoeleta kesi mahakamani na tunawahudumia.”

Aidha, Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya imeendelea na maandalizi kabambe kuelekea wiki ya sheria hadi siku ya kilele cha wiki ya sheria kwa kuendelea kuujulisha umma wa wana Mbeya kwa kufanya matangazo kupitia vipindi mbalimbali vya Radio, mabango pamoja na gari kuzunguka maeneo mbalimbali ya jiji la Mbeya.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Joachim Charles Tiganga (katikati) akiwa na Hakimu Mkazi Mkuu Mhe. Paul Ntumo (wa kwanza kushoto) pamoja Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Mbeya Mhe. Tedy Raphael Mlimba wakiwa Kituo cha Radio cha Rock FM jijini Mbeya.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Joachim Charles Tiganga (akiwa katikati) akijadiliana jambo na sehemu ya wadau kabla ya kuingia Kituo cha Radio cha Rock FM jijini Mbeya.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Joachim Charles Tiganga wakiwa Kituo cha Radio cha Rock FM jijini Mbeya.



 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni